Massanza: Simba ni tawi la Yanga

Massanza: Simba ni tawi la Yanga

SIMBA NI YANGA B

Baada ya kikosi cha Simba Sc, kuruhusu kichapo cha mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya mtani wake Yanga Sc, Afisa Habari wa Singida Fountain Gate, Hussein Massanza ameibuka na kusema kuwa ni rasmi kuwa watanzania na wanasoka watakua wameitambua Yanga B kwenye soka la ‘bongo’ ni timu gani.

Massanza amesema kuwa kumekuwa na kauli nyingi zinazosema kuwa Singida FG ni Yanga B kila wanapopoteza mchezo dhidi ya Yanga hivyo ameeleza kuwa Simba nayo imepoteza mchezao kwa goli nyingi ambazo wao kama Singida hawajahi kufungwa na Yanga hivyo basi Simba ndiyo Yanga B.

“Sasa nadhani Yanga B mmeiona, sisi huwa tunasingiziwa tu, maana tukipoteza mchezo dhidi ya Yanga tunaitwa Yanga B, je hawa waliopoteza kwa idadi ya goli 5-1 tuwaite vipi?,” amesema Massanza.

Hamsa [emoji113] 5 G
Ni kweli brother amezungumza Kwenye hii clip 👇🏿


View: https://m.youtube.com/watch?v=fFNq09L1HMk
 
Naskia ndo wanamsakama mwenyekiti kuwa kawasaliti
Sasa si wamtimue huyo Mwenyekiti wao!! Kwa nini wamuonee Robertinho ambaye walikuwa wanampangia mpaka kikosi cha wachezaji wa kuanza!!!!
 
Wameanza na hii

BREAKING NEWS

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari vimeripoti Wachezaji watano wa Simba Sc akiwemo Enock Inonga na Clatous Chota Chama wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi yao baada ya kufungwa na Yanga SC mabao 5-1 siku ya Jumapili.

Wachezaji hao wanatuhumiwa kuihujumu timu kitendo kilichopelekea kupoteza kwa idadi kubwa ya mabao

Maamuzi hayo yamefanyika katika kikao cha bodi ya Wakurugenzi ya Simba kilichofanyika jana jijini Dar es salaam na Wachezaji hao watakua nje ya kambi ya timu mpaka hapo maamuzi mengine yatakapofanyika

Chanzo hicho kimesema huwenda leo klabu ya Simba ikatoa taarifa ya wazi kwa Umma juu ya maamuzi waliyofikia kuhusu wachezaji hao au wasitoe ila wahusika wamepewa taarifa

Maamuzi mengine yaliyofikiwa na bodi ni kufutwa kazi kwa kocha mkuu Robertinho, msaidizi wake pamoja na kocha wa viungo.

#Futbalplanetupdates
 
SIMBA NI YANGA B

Baada ya kikosi cha Simba Sc, kuruhusu kichapo cha mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya mtani wake Yanga Sc, Afisa Habari wa Singida Fountain Gate...
Aache uhuni wanajua walichokifanya.

Waache timu zisshindane kwa soka sio ushawishi unaosababisha wachezaji wanauza mechi.

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Simba ni Yanga bila shaka.ilianzishwa kutoka ndani ya Yanga.sawa Adamu na Hawa.
Pan Africa Yanga C.
Nyota nyekundu ni Yanga B(II)
 
Simba ni Yanga bila shaka.ilianzishwa kutoka ndani ya Yanga.sawa Adamu na Hawa.
Pan Africa Yanga C.
Nyota nyekundu ni Yanga B(II)
Ngoja wakusikie vijana wa mudi
 
Nyie watu wiki hii mmetuweza,haya bhn tambeni wananchi hamna namna[emoji24]
 
Back
Top Bottom