Master J: 99% ya wasanii wa bongo ni 'mateja'

Master J: 99% ya wasanii wa bongo ni 'mateja'

nilikuwa morogoro siku moja hivi, nimepanga lodge ya kawaida tu, nikasikia makelele reception kutoka nione nini, nikakuta Chid Benz, aisee, ni teja kabisa hadi anavoongea, ila cha ajabu, yupo na mwanamke wamekaa naye hapo karibia wiki, ila inavyoonyesha wote yeye na mwanamke ni mateja, ila mwanamke anatoka mambo safi na ni kama anamlea. anatia huruma mno. ni mgomvi dakika moja, sasa nilikuta anamgombeza dada wa reception na dada hajibu chochote, anadai amelipa pesa siku mbili kumbe hajalipa wala nini, na mwanamke anayeonekana alimpa hela alipe reception au sijui nini amesimama mlangoni na taulo tu anashangaa ugomvi. madawa ni kitu hatari mno.
 
Bangi inaandamwa sana, kuna waheshimiwa wengi tu wanaivuta, tatizo linakuja pale uhuni/utovu wa maadili wa mtu binafsi unapohusishwa na kuvuta bangi, hii si sawa. Zamani muziki ulionekeana ni uhuni kwa sababu kuna wahuni waliokuwa wananfanya muziki, ila baadae ikaonekena ni ajira.
 
Bangi inaandamwa sana, kuna waheshimiwa wengi tu wanaivuta, tatizo linakuja pale uhuni/utovu wa maadili wa mtu binafsi unapohusishwa na kuvuta bangi, hii si sawa. Zamani muziki ulionekeana ni uhuni kwa sababu kuna wahuni waliokuwa wananfanya muziki, ila baadae ikaonekena ni ajira.
Kwa hiyo sasa wasanii bado wanavuta au wameacha mkuu?
 
Master anasema ukweli 100%. Serikali isipochukua hatua, kizazi cha vijana kitaangamia ktk taifa hili.
Bangi ipo toka zamani, hawajaangamia wakina mandojo na domo kaya, wakina Suma lee, wahangamie hawa ambao hela haikauki na bangi kama sigara kwao..
Mnataka sholo mwamba avute Sports au zile za mia winston sijui. Acheni hizo. Bangi ni safi tu. Serikali iwafungulie tu milango ya kazi hawa vijana.
 
Wako na hali gani mkuu? Ndio maana sober houses zinazidi kuongezeka ktk nchi hii.

Kuna siku nilidamka kwenda Muhimbili nikakutana na kijiji kizima cha mateja wanaenda kupigwa sindano za kuondoa bangi mwilini. Nilishangaa sana. Siku zote bangi inaonekana kuwa ni kitu kibaya kwanini sasa wasanii wanalazimisha kula bangi? Haya masanii yana akili ndogo sana.
Wamekuwa kama wazee madawa na bangi sio nzuri ...Huyo Dullayo kabaki kichwa tu.
 
Wajikite zaidi kwenye kudhibiti upatikanaji.
Polisi wanajua bangi zinapouzwa hata zinapolimwa, vijiwe vya bangi mtaani vinajulikana wazi lakini hawachukui hatua yoyote maana na wao wanafaidika.
 
Wajikite zaidi kwenye kudhibiti upatikanaji.
Polisi wanajua bangi zinapouzwa hata zinapolimwa, vijiwe vya bangi mtaani vinajulikana wazi lakini hawachukui hatua yoyote maana na wao wanafaidika.
Hili haliwezekani hadi Yesu atakaporudi. Polisi ni zaidi ya mbwa. Kuna rafiki yangu mmoja polisi kipindi naishi Kinondoni siku akiishiwa hela utamuona anapita kwa wauza bangi na cocaine akikusanya hela halafu anawaachia waendelee kuwaharibu vijana.
 
Wamekuwa kama wazee madawa na bangi sio nzuri ...Huyo Dullayo kabaki kichwa tu.
Mungu awafanyie wepesi wahudhuria kliniki ya matibabu ya uteja kule Muhimbili watapona nakurejea kwenye kazi zao.
 
Bangi ipo toka zamani, hawajaangamia wakina mandojo na domo kaya, wakina Suma lee, wahangamie hawa ambao hela haikauki na bangi kama sigara kwao..
Mnataka sholo mwamba avute Sports au zile za mia winston sijui. Acheni hizo. Bangi ni safi tu. Serikali iwafungulie tu milango ya kazi hawa vijana.
Nilikuwa sijakupata mkuu. Kumbe wewe unashabikia bangi? Itakuwa wewe ama ni msanii au ni muuzaji wa bangi. sio bure!
 
Hili haliwezekani hadi Yesu atakaporudi. Polisi ni zaidi ya mbwa. Kuna rafiki yangu mmoja polisi kipindi naishi Kinondoni siku akiishiwa hela utamuona anapita kwa wauza bangi na cocaine akikusanya hela halafu anawaachia waendelee kuwaharibu vijana.
Kwa mtindo huo kudeal na wavuta bangi ni kupoteza muda
 
Naijua bangi vizuri toka nimeanza itumia bangi huu mwaka wa 22, niamin mm huwez kuvuta bang kama bangi alafu ukafanya mambo ya kijinga kwanza ukivuta unakuwa very smart hata kwenye kuongea utaongea kwa tahadhar sana na point sana....kama kichwa mbovu utakuwa unacheka sana hata kwenye jambo dogo... Nazungumzia bang kama bang na sio mtu umevuta bang anaenda kunywa pombe muda huo huo sigara kinachofuata lazima udate na ufanye mambo ya hovyo
 
Back
Top Bottom