Maswali kuhusu Taulo za Kike zinazotolewa bure

Maswali kuhusu Taulo za Kike zinazotolewa bure

Kwa uelewa wangu mdogo naamini wanafanya hivyo kwa sababu kama tatu hivi,

1. Kutoa mrejesho kwa jamii / Taasisi zilizotoa pesa kufadhili zoezi hili.

2. Kuongeza uelewa wa jamii kuhusu tatizo lililopo hasa kwa wanafunzi walio katika mazingira magumu.

3. Kuvutia zaidi taasisi / jamii kuchangia zaidi ili taulo hizi zifikie walengwa wengi zaidi.
Kwanini wanagawa mara moja tu kwenye shule husika na hawarudi tena kuwapa mwenzi unaofuata?
 
Kuna familia hazina uwezo wa kununua chakula Sasa watakuwa wanawaza kuhusu taulo kweli?
 
WANAWAKE WADADA WENGI SAIVI WANAENDA MP ZAO KWA MIEZ MITATU ANAEZA KUONA MARA MOJA AU AKAONA KWA MWEZ MARA MBILI HADI TATU AU ASIONE KABISAAA. SASA HILI NALO JANGA KWA AFYA YA WAKE ZETU DADA ZETU.
Je nini sababu na lipi suluhisho?
 
Kwanini wanagawa mara moja tu kwenye shule husika na hawarudi tena kuwapa mwenzi unaofuata?
Mkuu unahitaji elimu zaidi kugusu haya mambo.

Kwa uelewa wangu 'mdogo' nafahamu kua tarehe za mwishoni mwa mwezi wa tano kila mwaka hua na maadhimisho ya Hedhi salama (MHH) ndio maana utaona kama wanagawa mwezi mmoja tu. Ila kuna watu / taasisi zinaendelea kugawa hata baada ya maadhimisho hayo, tatizo linakuja kwenye coverage ya media kwenye ugawaji huo unakua tofauti kidogo.

Pia kwenye shule mara nyingi hua wanagawa taulo ambazo zinaweza kutumika zaidi ya mara moja (washable / reusable pads) hivyo mtoto akipata mara moja anaweza kutumia hata miaka mitatu ijayo.
 
Je, wanaogawa Pedi za Kike lengo lao huwa ni lipi?

Je, huwarudia waliowapa na kuwapa tena?

Je, ni kweli wazazi wanashindwa nunua pedi za 1500-3000 mara moja kwa mwezi?

Je, serikali ina mpango gani katika kuhusishwa kwenye huo ugawaji?

Je, wahusika sio kwamba wanataka watumia wasichana kupata pesa kutoka kwa wafadhiri?

Kwanini wawarekodi wanaopewa msaada?

Kwanini wanalia kuwa Kodi iondolewe wakati wao wanakuja ziuza kwa bei zile zile?

Je, tujiandaeje kama taifa ili tuweze ondoa hilo tatizo?
Dah... ubarikiwe sana hata jana mimi nliona mahali yule dad wa LAVY PAD kule njombe kwenye shule moja eti ana Gawa bure huku akiwa amezungukwa na wana habari nlijiuliza maswali mengi sana .... ivi nikweli sisi wazazi tumeshindwa kuwanunulia wane tu pedi za 3000 kwa mwezi au kuna jambo nyuma ya hizi drama
 
Dah... ubarikiwe sana hata jana mimi nliona mahali yule dad wa LAVY PAD kule njombe kwenye shule moja eti ana Gawande bure huku akiwa amezungukwa na wana habari nlijiuliza maswali mengi sana .... ivi nikweli sisi wazazi tumeshindwa kuwanunuloa wanetu pedi za 3000 kwa mwezi au kuja jambo nyuma ya hizi drama
Kuna wakati aliondolewa kodi ili zishuke bei, badala yake akauza bei ile ile. Serikali ikaamua rudisha kodi akalalamika.

Yule pale anasaka hela za wazungu
 
Back
Top Bottom