Maswali kwa mkurugenzi wa HESLB ndugu Badru

Maswali kwa mkurugenzi wa HESLB ndugu Badru

Je kwanini bodi haiwapi wanachuo hela za mwaka wa kwanza ambao wapo mwaka wa pili.
Hii inatokea kwawale waliokata rufaa wakapangiwa lakini hawajapewa. Nini tatizo
Mwaka wa kwanza hukuwa na mkataba nao. Mkataba unasoma tangu pale uliposainiwa. Wanafanya hivi kwa sababu hela hazitoshelezi kutimiza kila kitu.
Mwenyewe mwaka wa kwanza sikupewa mkopo
 
Mkuu pole ila umeandika kwa hisia sana bila kuzingatia kuwa yawezekana shida ipo chuoni kwenu.

1. Amini kuna vyuo vinachukua fedha alafu vinafanya kuizungusha kwanza alafu lawama zinaangukia HESLB

2. Amini kuna vyuo vinachelewesha sana kuwasilisha majina yaliyosainiwa HESLB hivyo fedha nayo haitoki

3. Amini kuna vyuo vinachelewesha kutuma taarifa za matokeo ya wanufaika hasa wanaoendelea na masomo nayo inachangia fedha kuto kutoka kwa wakati.

Sidhani kama chuo kikikamilisha mambo yote yanayotakiwa kuwasilishwa HESLB fedha itachelewa kutoka tena kwa chuo kimoja au viwili ni ngumu sana labda kwa vyuo vyote na hapo ni labda fedha hamna.

Angalia pande zote Mkuu, ni vizuri uzi wako ungeuandika kama kuhoji na ungetaja chuo na mazingira sio lawama kwa wahusika alafu ukute wala hawahusiki na huu uzembe, watakuona mjinga.

Ila Mkuu pole sana!.
Nimemwambia tatizo litakuwa chuo. Mimi natoa mfano wa Tumaini ya DSM hawa jamaa wana Loan Officer mmoja kijana kijana hivi yuko very smart na anawajibika. Yuko friendly hana misifa ya uongozi na uungu mtu kama maofisa wetu vyuo vingine hata ukiona chats zake WhatsApp na wenye shida utaona.

Huwa nikitaka kujua hela kama zimekuja namuuliza jamaa yangu anasoma pale, mara zote wao ndio wanatangulia kusaini na kupokea hela. Chuo kikiamua kuwahisha hayo matokeo na taarifa fedha zinawahi. Sisi kuna muda hela ilizingua watu wakaacha kutumia uongozi wa shule uliokuwa una ubabaishaji na officer miyeyusho wakaenda HESLB kwenyewe, kumbe hela zishatoka muda tu. Muda mwingine tatizo ni chuo alafu wanafunzi wasio na uelewa wakilishwa maneno na loan officer wanalaumu HESLB.
 
Mkuu ulichosema Ni kweli, lakini kwa tukio la Sasa pesa haijawekwa vyuo vyote. Watu wamesin Ni wiki ya pili Sasa lakini pesa hamna.
Vyuo vyote gani havijapewa hela. SMS nimepokea ila sijasaini, wengine wote sijasikia malalamiko kwamba hakuna hela. Hata marafiki zangu vyuo vingine sijasikia malalamiko hawana hela kabisa. Huwezi generalize ukasema vyuo vyote havijapewa hela.

Alafu ujue kitendo cha kutumiwa SMS ujue hela imepelekwa CRDB tiyari. Na kabla hujatumiwa SMS ujue anayechelewesha ni chuo kutuma matokeo na taarifa za wanafunzi. Ndio maana vyuo vinapata SMS nyakati tofauti.

Hatuwezi kuwa na uhakika kama ni bodi hawajatoa hela, au chuo chako wamefanya upuuzi. Rais kashasema wale kwa urefu wa kamba yao
 
Vyuo vyote gani havijapewa hela. SMS nimepokea ila sijasaini, wengine wote sijasikia malalamiko kwamba hakuna hela. Hata marafiki zangu vyuo vingine sijasikia malalamiko hawana hela kabisa. Huwezi generalize ukasema vyuo vyote havijapewa hela.

Alafu ujue kitendo cha kutumiwa SMS ujue hela imepelekwa CRDB tiyari. Na kabla hujatumiwa SMS ujue anayechelewesha ni chuo kutuma matokeo na taarifa za wanafunzi. Ndio maana vyuo vinapata SMS nyakati tofauti.

Hatuwezi kuwa na uhakika kama ni bodi hawajatoa hela, au chuo chako wamefanya upuuzi. Rais kashasema wale kwa urefu wa kamba yao
Hii nguvu unayo itumia hapa na wakati wa kulipa deni ui tumie sawa mkuu
 
Hii nguvu unayo itumia hapa na wakati wa kulipa deni ui tumie sawa mkuu
Kulipa deni sio hisani wala jambo la kupongezwa. Ukiwa na ethics na morals unalipa bila hata kukumbushwa. Wenye akili za kijambazi ndio wanaona ni big deal kukwepa madeni
 
Nimemwambia tatizo litakuwa chuo. Mimi natoa mfano wa Tumaini ya DSM hawa jamaa wana Loan Officer mmoja kijana kijana hivi yuko very smart na anawajibika. Yuko friendly hana misifa ya uongozi na uungu mtu kama maofisa wetu vyuo vingine hata ukiona chats zake WhatsApp na wenye shida utaona.

Huwa nikitaka kujua hela kama zimekuja namuuliza jamaa yangu anasoma pale, mara zote wao ndio wanatangulia kusaini na kupokea hela. Chuo kikiamua kuwahisha hayo matokeo na taarifa fedha zinawahi. Sisi kuna muda hela ilizingua watu wakaacha kutumia uongozi wa shule uliokuwa una ubabaishaji na officer miyeyusho wakaenda HESLB kwenyewe, kumbe hela zishatoka muda tu. Muda mwingine tatizo ni chuo alafu wanafunzi wasio na uelewa wakilishwa maneno na loan officer wanalaumu HESLB.
JE KAMA MTU AMESAINI ZAIDI YA WIKI TATU HAPEWI FEDHA TATIZO LIPO KWA CHUO AU HESLB?
 
Hio bodi ni mzigo kwa taifa , madudu ni mengi sana na hawana wa kuwawajibisha .
 
JE KAMA MTU AMESAINI ZAIDI YA WIKI TATU HAPEWI FEDHA TATIZO LIPO KWA CHUO AU HESLB?
Tatizo sio heslb tatizo ni vyuo ...kama leo nme fatilia issue kama iyo kwa kijana chuo cha Tumaini makumira...Bodi wame daima pesa zisha wekwa ila ni kwamba chuo chenyewe kime tumia fixed account kuweka izo pesa za wanafunzi ivyo ina bidi wasubiri adi tar 1 mwezi wa 2 ndo wapatiwe pesa zao ..vyuo vina tumia pesa za wanafunzi kujipatia faida
 
Back
Top Bottom