Maswali na ushauri kwa Malinzi

Mh, hujajibu swali, tunaomba utupe mifano, in nchi zipi? Unajua unaua Mpira kabisaaa

ahsante Yombayomba.
Fanya jitihada uwasiliane na Alhaj Maigari (NFA President Nigeria) au Nyantaki (FA President wa Ghana),ukitaka mbali zaidi wasiliana na KNVB (FA ya Holland) au muulize Danny Jordan akwambie FA ya South Africa wana plan nini.Mipango ya Greg Dyke Chairman English FA umeisikia majuzi.
Mandate ya TFF kikatiba ni "to develop,promote and control" the game of Association football in Tanzania,iweje useme TFF inaua mpira kwa kuandaa a comprehensive youth football development plan.Rais Kikwete kila akikutana na TFF huwa anatuambia nini.Kazi aliyoifanya Lawrence Mulindwa Uganda unaijua?
 
Last edited by a moderator:

Mh Rais inawezekana sisi tuna taarfa Nusu juu ya hii Youth Football Dvlp Plan itakayokuwa chini ya TFF Direct...kama kuna makarabrasha ambayo ni Public Ofisini kwako tunaomba Utuwekee humu tuyapitie kidogo...
Lakini tunaelewa hili ni suala la Private zaidi kama alivyosema Yombayomba...TFF Ikianza kudili moja kwa moja na uendeshaji wa soka mgongano wa maslahi lazima utokee tu..Angalia mfano wale wachezaji wa maboresho mliowachagua timu ya Taifa na kuwaweka kule Tukuyu...tunasoma kwenye magazeti kocha amewakataa wote..
Huko Nje mfano England Club zote zina Misingi imara ya timu za vijana, si Sunderland mh Kikwete aliwatembelea alipokuwa huko kikazi..??
 
Last edited by a moderator:

Na nakubaliana na wewe Ndugu Malinzi mmiliki wa mpira ni TFF hivyo hata sera ya youth development lazima iandaliwe na TFF tena kiustadi na ndio ishirikishe wadau wengine kama vilabu, vyama vya mpira vya mkoa, mashirika n.k, lakini mpango mzima lazima uratibiwe na usimamiwe na shirikisho hatuwezi kuwa na youth development holela holela kama ilivyo sasa lazima kuwe na mission na vision na kuwe na msimamizi mkuu wa mpango huo ambaye lazima iwe ni TFF, naunga mkono mnachotaka kufanya it is good idea wasiwasi wangu ni mipango yenu kwenye utekelezaji tu, maana kuna hitaji la gharama na maamuzi magumu,mfano tu wa haya maamuzi magumu yalitakiwa yaanze na timu za ligi kuu TFF iwe serious kuwa huna timu za vijana kuanzia under 20 hadi under 15 huruhusiwi kushiriki ligi na hapa iwe serious kweli kweli ikiwa ni pamoja na kuzitembelea hizo timu na kuzitafutia udhamini kwa kushirikiana na vilabu.
 

Ahsante MKALIKENYA kwa kuelewa hii dhana.Tatizo letu kubwa tulio wengi ni kutaka twende mbinguni bila kufa kwanza!Unapataje timu nzuri ya Taifa ambayo wachezaji waki pata call up na kuingia kambini wanacheza mpira unaofanana kama hukuweka utaratibu wa kitaifa wa kuwafundisha mpira wa awali na wa vijana? Nani ataratibu haya mafunzo kitaifa kama sio TFF?
 
Last edited by a moderator:

Mheshimiwa Rais mimi napenda kujua kocha msaidizi wa Taifa Stars Salum Mayanga na yule wa makipa Patrick Mwangata walipatikanaje na vigezo vilivyotumika then nikipata jibu ya hili kuna kitu nataka kushare na wewe pamoja na wadau wengine humu?
 

pachanya let me make this clear:
1.Mpango wa maboresho wa TFF hauku feli hata kidogo,on the contrary umefanikiwa sana.Yako mambo Mwl Nooij halazimiki kuyatamka hadharani kuhusu wale vijana,wapo na wanaendelea na mafunzo,kumbuka Afcon qualifiers awali ilikuwa ziwe Septemba na sio May,mipango ya TFF ya awali ililenga hapo.
2.Unasema youth development ni jukumu la private sector,private sector ipi duniani ulisikia imenunua mipira laki tano size 3 ikaisambaza shule zote za msingi nchi nzima,ni private sector ipi duniani ulisikia imeajiri na kulipa mshahara wa mwalimu mmoja wa mpira kila shule ya msingi nchi nzima? Ndio maana ninasema TFF tutabuni na kuratibu mpango huu,utekelezwaji utafanywa na wadau wote ikiwemo Serikali (Hasa Tamisemi,wizara ya elimu na wizara ya michezo),mashirika ya umma na binafsi,NGO,mimi,wewe,media,familia ya mpira vikiwemo vilabu nk
 
Last edited by a moderator:

Ndugu Rais kuna kauli umekuwa unairudia sana kwamba yapo mambo ambayo mwalimu hawezi ya kuyatamka hadharani mimi hii kauli inanipa mashaka kidogo sababu kama mambo hayo ni ya kiufundi nachelea kuamini ni kitu gani cha ufundi kwa maendeleo ya soka na hao vijana eti ni siri? hii football ya wap ya kiintelijensia kwenye mipango ya soka la vijana na ata mipango ya senior timu, nani anafanya hivyo duniani? ukienda Barcelona pale LA MASIA mpango mzima wa kuendeleza vijana na senior timu unafahamika sasa huku kwetu napata mshangao kuona kuna mambo yanayohusu soka (mchezo unaochezwa hadharani) eti ni siri....TUNAELEKEA KUBAYA HII NI SIASA KWENYE MPIRA.
 

Mh Malinzi,

Kwanza naomba uniwie radhi kwa neno nitakalotumia, ukweli hujatutendea hali, na ni dharau kubwa kwa majibu uliyotoa hapa. Sisi hatukukuomba ufungue hii link? leo unaulizwa mswali muhimu, unajibu kama unaongea na mabaunza? its so sill, kwa mtu kama wewe kujibu namna hii. Niwie radhi kwa kauri hii.

Yaani tukitaka kujua unachotaka kufanya tuwafate akina Alhaj Maigari (NFA President Nigeria) au Nyantaki (FA President wa Ghana), na KNVB (FA ya Holland) na Danny Jorda, au tumuulize Mh Jakaya Kikwete kawaambia nini????????????????

Unachotakiwa ni kutueleza ni vipi TFF, itakavyoshiriki kwenye hizi academy, hiki ndio tunatakiwa tujue na tujadili.
 

Yombayomba ulitaka nikupe mifano ya nchi ambazo zina national youth development programmes,nimekupa hizo,kuna ubaya kufanya hivyo?
 
Last edited by a moderator:
Yombayomba ulitaka nikupe mifano ya nchi ambazo zina national youth development programmes,nimekupa hizo,kuna ubaya kufanya hivyo?

Ndugu Rais kuna kauli umekuwa unairudia sana kwamba yapo mambo ambayo mwalimu hawezi ya kuyatamka hadharani mimi hii kauli inanipa mashaka kidogo sababu kama mambo hayo ni ya kiufundi nachelea kuamini ni kitu gani cha ufundi kwa maendeleo ya soka na hao vijana eti ni siri? hii football ya wap ya kiintelijensia kwenye mipango ya soka la vijana na ata mipango ya senior timu, nani anafanya hivyo duniani? ukienda Barcelona pale LA MASIA mpango mzima wa kuendeleza vijana na senior timu unafahamika sasa huku kwetu napata mshangao kuona kuna mambo yanayohusu soka (mchezo unaochezwa hadharani) eti ni siri....TUNAELEKEA KUBAYA HII NI SIASA KWENYE MPIRA.
 
Jamal Malinzi
Pongezi kwako binafsi na Team yetu kw akuifunga Zimbabwe!Waingereza wao wana msemo wao "W" is "W" yaani win is a win haijalishi umeshindaje!

Sikuweza kuona mechi hii kwani nilisafiri kwenda kijijini kwetu Ipinda-Kyela kwenye harusi ya Gaudence Mwaikimba(Azam)aliye funga harusi siku Stars inacheza!

Mechi ijayo kule Zimbabwe inachezwa mji gani na lini Rais wa TFF?Nataka nikaone mechi hiyo!
 
Last edited by a moderator:
Mwambie Gaudence kuwa Malinzi anauliza mbona hujamwalika?
zimbabwe vs Tanzania,National stadium Harare,kick,off15hrs,1st june 2015,karibu.
 
Mwambie Gaudence kuwa Malinzi anauliza mbona hujamwalika?
zimbabwe vs Tanzania,National stadium Harare,kick,off15hrs,1st june 2015,karibu.

Salamu zako kwa Mwaikimba zitafika na nashukuru sana kwa maelezo ya wapina muda wa mchezo wetu!

Nitakuwepo Harare siku 1 kabla ya mechi na naanza kuona mwanga kidogo wa matumaini kwenye team yetu regardles matokeo ya mechi hii ya Harare!
 
mkuu Jamal Malinzi, nina maswali mawili siku ya leo
1. Tunafahamu fika ligi ya mabingwa wa mikoa inaendelea katika vituo 3 kama sijakosea, kituo cha mbeya, hapa Morogoro nilipo na kule Mwanza, je kuna jitihada gani za makusudi katika kuangalia upatikanaji wa vipaji kupitia michuano hii? binafsi nimeshuhudia mechi zote za hapa Morogoro, na nimeona Taifa lina hazina kubwa ya vipaji katika soka, je kuna maofisa wa TFF waliopo katika vituo hivi kuspot talent au ndio hii michuano mikubwa itapita hivi hivi
2. kwanini WEBSITE ya TFF haijapa kipaumbele hii michuano ya mabingwa wa mikoa katika eneo la upashanaji habari , nimepitia website ya TFF mara nyingi sijaona updates za matokeo ya mechi hizi kutoka vituo mbalimbali, sijaona picha kama wanavyofanya ktk mechi zengine na cha mwisho kikubwa zaidi sijaona misimamo ya timu katika vituo hivyo vitatu, je kukosekana kwa taarifa hizi muhimu si kuwanyima wadau wa mpira habari muhimu? maana hata vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti kwa uchache sana juu ya michuano hii, na mpaka sasa sijaona gazeti lolote lililotoa misimamo ya timu katika vituo mbalimbali
ni hayo tuu kwasasa mkuu
 
Last edited by a moderator:
Mheshimiwa malinzi sisi wazanzibari kilio chetu kipo pale pale,suala la michezo si la muungano kwa nini mutuwakilishe?tunahitaji kuiona znz ikipeperusha bendera yake everywhere sio somewhere and other places not,ni muda sasa wa kuelewana friendly sio muda wa kufanyiana udikteta,na hyo ni miongoni mwa ahadi zako ulipokuja znz
 

FIFA haitambui kuwa kuna nchi ya Zanzibari, hivyo ongezeni bidii kudai serikali Tatu mtapata Kila kitu.
 
Mwambie Gaudence kuwa Malinzi anauliza mbona hujamwalika?
zimbabwe vs Tanzania,National stadium Harare,kick,off15hrs,1st june 2015,karibu.

Mwaikimba Alitunyima Uhondo Sie tulioshindwa Kufika Ipinda-Mbeya..By the way Namtakia Maisha mema ya Ndoa na Mkewe (Rukia-was my school mate)..
 

Attachments

  • 1400955891606.jpg
    69.1 KB · Views: 255
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…