Maswali na ushauri kwa Malinzi


mkuu hilo ni jukum la vilabu, sema vilabu vyetu viko busy na siasa badala ya kuendeleza mpira
 
mkuu hilo ni jukum la vilabu, sema vilabu vyetu viko busy na siasa badala ya kuendeleza mpira

sio hili tu komeka,jingine ni kuwa vilabu vyetu,hasa hivyo vinavyoitwa vikubwa wanachama wake hawana subira,wanataka ushindi wa leo leo,washinde makombe,wamfunge mpinzani wa jadi,basi hiyo tosha,ukiwaambia wawekeze kwa vijana (kama wanavyofanya Al ahly Misri) hawakuelewi,matokeo yake ni kusajili wageni walioiva tayari kwa kuwatafutia ushindi.
 
Last edited by a moderator:

hilo ki kweli mheshimiwa mi biinafsi nakuonea huruma sana jinsi unavyoendesha mpira kwny mazingira magumu km hya coz duniani kote vilabu ndyo vinanafanya timu ya taifa kuwa bora kwa mfano huwezi kuzungumzia mafanikio ya timu ya taifa ya ivory coast bila kuizunngumzia asec memosa vile vile huwez kuzungumzia mafanikio ya spain bila kuzungumzia Barcelona vile vile ujerumani na bayern Munich pamoja ghana na libety professional so utaona kwa staili hii ni ngumu kufikia mafanikio ya kweli ya kimpira ukichanganya na kukosa exposure na kutojjitambua kwa wachezajii wetu(rejea ishu ya kapombe na boban) ukichanganya na udhaifu Wa ligi yetu ( mechi chache sana 26?????) bado na rushwa na upangaji matokeo ndyooo kabsa soka letu liinazidi kuzama
 
Last edited by a moderator:
Imezoeleka Tz kuwa ni kichwa cha wenda wazimu ktk soka na cha ajab zaidi Ukweli wa maneno haya bado timu za mpira zinauthibitisha.Licha ya jitihada kadhaa za TFF ,serikali,Vilabu na taasisi mbalimbali ktk kuibua vipaji vya vijana tatzo bado vipaji vinavopatikana haviendelezwe,nafkir tutaungana kuwa tatizo ni umaskini.Sasa bas mh. kunahaja ya kuwa na mifumo tofauti inayoendana na uhalisia ulivo sasa bas pendekezo langu ni hili,TFF UNDENI TIMU ZA VIJANA ZA KUDUM ANGALAU MBILI AU PENGINE HATA MOJA NA IINGIZENI KTK MIKIKI MIKIKI YA LIGI KUU pana faida nyingi za kufanya hivo.Au vp mzee wangu.
 
Malinzi,

Rejea habari za Yanga kukataliwa kupeleka timu ya vijana, nauomba uongozi wa TFF utoe ufafanuzi, ni wapi ilipoandikwa kuwa timu iwakilishwe na nani? Kama nia ni kukuza soka la ukanda huu, basi hii ni kitu cha ajabu saana, nia na dhamira ya Yanga ilitakiwa kuungwa mkono, kwani ilikuwa inatoa nafasi kuwajenga vijana kwa ajili ya baadae, ambayo ni faida kwa Yanga na Taifa stars. Pili imeandikwa kuwa MUSOKE ana uliza kwa nini Maximo haendi? Hivi ni busara kweli yeye apangie timu nanani awe mwalimu? Mbona hakuwapangia Harambee Stars mwalimu wa kuipeleka Lesotho? Kuna ubaya gani kwa Yanga kuanza kumjenga Nsajigwa kuwa kocha?

Kama sera yako ni kuinua vijana, imekuwaje TFF mkubaliane na kusalimu amri kwa kitu ambacho hakipo kwenye sheria? Huu ni udhaifu mkubwa mno, na wala hausaidii kujenga soka la CECAFA.
 
Jamali Malinzi
natamani kujua aina ya wadau..wafadhili na washirika wa karinu wa tff na mipango yao
mikataba ambayo iliingia tff..mikataba ambayo imeingia tff ..na mikataba ambayo itaingia tff katika kukuza soka letu
 
Last edited by a moderator:
Ongereni kwa mahandalizi mazuri kwa timu ya taiga ingawa wachezaji wametuangusha
 
Malinzi
Naomba nitoe ushauri wangu kwa ajili ya kukuza mpira wa Tanzania
1. Kwanza idadi ya timu za premier ziongezeke ili wachezaji wacheze mechi nyingi zaidi
2. Kuanzishwe ligi nyingine ya timu za vijana za vilabu vyote vinavyoshiriki ligi kuu na ligi daraja la kwanza na ligi hiyo iende sambamba na ligi kuu
3. Uongozi wa TFF utafute wadhamini na kuwe na makato ya asilimia flani katika mechi zote za premier ili kuendesha ligi ya vijana
4. Kuwe na mkakati maalumu wa kupandisha vijana kwenye premier kila mwaka kwenye usajili wa vilabu hii itatuwezesha kupata timu bora ya taifa na yenye uzalendo.
Naomba niambie kati ya haya lipi linawezekana na lipi haliwezekani na kwa sababu zipi mkuu?
 
Jamal Malinzi mkimuachia Musonye wa CECAFA ipo siku atawaambia lzm team ya Tanzania inapocheza michuano fulani mkuu wa msafara awe Waziri Mkuu!
Kupeleka team B lilikuwa ni jambo la kuungwa mkono na kila mpenda michezo maana kwa sasa hawa akina Canavaro wamezeeka wawapishe vijana wapate uzoefu!!
Kama Rais wa soka la Tanzania ndiyo kauli ya Musonye haipingwi?
 
Last edited by a moderator:
Mheshimiwa Rais
Nina swali moja kwako

Naipenda sana nchi yangu, naipenda sana Timu ya Taifa langu, Naupenda mpira wa Tanzania

Tokea umeingia madarakan mambo yamekua mabaya zaid kwenye timu ya taifa, Sikumbuki kama Taifa Stars imewahi kushinda tokea uwe madaraka

Je Tatizo n nini?
 
Mr President Malinzi

Nimesoma kwa masikitiko makubwa saana jinsi swala la Yanga kupeleka timu ya vijana lilivyokuwa handled na TFF baada ya maagizo ya katibu wa CECAFA, Mr MUSOKE.

1) Mashindano yamepangwa katika wakati mgumu, kwa timu washiriki
2) Kama nia na lengo ni kuibua wachezaji, sasa kosa la Ynga ni lipi?
3) Inamuhusu nini MUSOKE kusema haiwezekani Yanga ije na kocha mwingine?

Rejea yote haya, ni fedheha kubwa jinsi TFF ilivyolishughulikia hili swala.

Afisa wa TFF, aliyeshiriki kutoa uamuzi na kuwapeleka AZAM, anastahili kusimamishwa kazi au Ajiuzulu, haiwezekani ifike Musoke aanze kuamua jinsi ya uendeshaji na ujenzi wa soka katika taifa letu.

Hii ni aibu kwa nchi, wewe kama Rais wa TFF, onyesha kutokubali kuingiliwa katika masuala ambayo hayana sheria.
 

km ulikuwa hujui mkuu kombe la cexafa Ni mradi WA musonye na wenzake kupiga hela ndyo maana walikuwa wanang'ang'ania yanga wapeleke kikosi kamili ,musonye na wenzake hawajawah kuwa na vision ya kuuendeleza mpira WA Africa mashariki zaidi ya kuwaza natumbo Yao.we hujiuliz mashindano Yana zaidi ya miaka 50 lkn bado yanaendeshwa kwa staili ya bonanza ilipaswa wayaboreshe kwa timu kucheza nyunban na ugenini ,nwaka WA ngapi huu nchi wanachama WA cecafa hawashiriki afcon? Wakina musonye wala hawastuki na kuwaita wanachama kupanga mikakati wenyewe wana option moja ya mabonanza wapige hela basi.....simba na yanga yalivyo mabogus wala hayastuki kuwa yanatumiwa
 
Ndala fc pelekeni timu kwenye mashindano acheni ujinga wenu!

EPL imeisha watu moja kwa moja wakaunganisha kujiunga na timu Zao za taifa kwenda world cup,

world cup imeisha wachezaji wamerudi moja kwa moja kwenda kwenye pre season kujiandaa na ligi wiki ijayo, hakuna mapumziko ni kazi tuu kwa kwenda mbelee!


Mkipewa muda wa kupumzika ndio yale yale ya ngassa kwenda kucheza film za ngono!

Kombe la kagame litumieni kufanya mazoezi!

cc komeka
Yombayomba
Jamali Malinzi
Malafyale
 
Last edited by a moderator:
Ndala fc pelekeni timu kwenye mashindano acheni ujinga wenu!

EPL imeisha watu moja kwa moja wakaunganisha kujiunga na timu Zao za taifa kwenda world cup,

world cup imeisha wachezaji wamerudi moja kwa moja kwenda kwenye pre season kujiandaa na ligi wiki ijayo, hakuna mapumziko ni kazi tuu kwa kwenda mbelee!


Mkipewa muda wa kupumzika ndio yale yale ya ngassa kwenda kucheza film za ngono!

Kombe la kagame litumieni kufanya mazoezi!

cc komeka
Yombayomba
Jamali Malinzi
Malafyale
 
Last edited by a moderator:
by Jamal Malinzi;
MLUGU umejenga hoja za msingi,umesikika



Mhh na wewe Jamali Malinzi unaunga mkono hicho kinachoelezwa hapo????
Seriously????

Au kwa sababu ni yanga?
 
Last edited by a moderator:
daaah! me na swali nje ya tz, ni kombe gani linaongoza kwa pesa nyingi kati ya kombe la dunia, na uefa?
 

Nadhani hujui unachoongea au kuandika, unashangilia Taifa lako kuingiliwa katika miiko ya uongozi kisa wewe huipendi Yanga. Hapa swala si yanga ni udhaifu katika uongozi wa CECAFA.
 
Nadhani hujui unachoongea au kuandika, unashangilia Taifa lako kuingiliwa katika miiko ya uongozi kisa wewe huipendi Yanga. Hapa swala si yanga ni udhaifu katika uongozi wa CECAFA.

Ni udhaifu pia wa uongozi wa TFF. 'Mtu akikuambia jambo la kipumbavu, nawe ukalikubali, anakudharau' (J. K.Nyerere, n.d.). CECAFA wamewaambia jambo la kipumbavu TFF kuwa Yanga hawana sifa ya kushiriki mashindano eti kwa sababu wanapeleka kikosi B huku TFF wakijua fika kuwa wale ni wachezaji halali wa Yanga. Kwa kitendo cha TFF kukubali upumbavu ule, CECAFA imewadharau kana kwamba TFF haina viongozi ndiyo maana CECAFA iliwataka TFF wawaandikie barua Yanga na wao kukaa pembeni nje ya tatizo. Nashangaa ni kwa nini viongozi wa TFF hawajaomba radhi hadi sasa kwa kukubali upumbavu ule. CC. Jamal Malinzi (Mkuu una utetezi gani katika hili?).
 
Last edited by a moderator:

CC. Jamal Malinzi (Mkuu tunasubiri majibu yako, tunahitaji kuona watu wakiwajibishwa ili kurejesha heshima iliyonajisiwa na Musonye).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…