Maswali na ushauri kwa Malinzi

Umegonga msumari mahali pake,kusema kweli zipo gharama za mchezo ambazo zinapaswa kuwa fixed na sio kutegemea mapato ya siku hiyo.
Mheshimiwa Rais kuna maswali nimekuuliza hapo juu...Tangu jana usiku....Kama haitojali naomba unijibu mkuu....
 

hoja yako MKALIKENYA ni ya msingi club vs country ni mgongano wa dunia nzima,hata uingereza wanalia na hili jambo.Upande mmoja unasema Kipre tcheche na hamis tambwe wanawazibia nafasi john bocco na jerry tegete,upande wa pili unasema bila twite,kiiza na owino ligi hainogi,kama Federation lazima utafute balance,swali ni je huo uwiano ni wachezaji wangapi wa nje? Mmoja,wawili,watano au kumi?na kigezo ni kipi? Wadau tusaidiane katika hili maana TFF ni waratibu na wasimamizi tu, ligi ni ya watanzania wote.
 
Last edited by a moderator:

Nadhani wachezaji wa5 wa kigeni wanatosha ila sheria iwe wa3 katika mechi 1. Ila kwa kimataifa wawatumie wote tu.
 
Last edited by a moderator:

Balantanda:
1. Ni kweli makato ya milangoni formula yake nakiri ina utata,tutaifanyia kazi,vilabu kupata chini ya 50% ya mapato si haki.Wao ndio wavuja jasho.
2.Mkataba wa AzamTv pamoja na mikataba mingine ni vyema siku za usoni vilabu vikashiriki tena kwa uwazi.TFF haina chanzo kikubwa cha mapato zaidi ya ligi lakini huwezi kuamini loyalty /mrahaba ambayo TFF inalipwa tokana na mapato ya milangoni ni zero/sifuri % percent,unaweza kuamini?Mambo haya inabidi yaongeleke kwa uwazi.

2.
 
Last edited by a moderator:
Nadhani wachezaji wa5 wa kigeni wanatosha ila sheria iwe wa3 katika mechi 1. Ila kwa kimataifa wawatumie wote tu.

Hapo nitapishana na wewe,what is the point klabu iingie gharama kumsajili mchezaji kwa mamilioni halafu iambiwe akae benchi?
 
Hapo nitapishana na wewe,what is the point klabu iingie gharama kumsajili mchezaji kwa mamilioni halafu iambiwe akae benchi?

Lengo la azimio la bagamoyo lilikuwa kuongea wachezaji wazawa kupata kucheza zaidi. Sasa wakipunguzwa wakatakiwa kucheza wa3 kwa kila mechi basi nao watakupunguza kusajili pia n mwisho wa siku wazawa watapata nafasi
 
Asante kwa majibu mazuri....Jitahidi utekeleze hiyo dhamira yako ya Uwazi katika Mikataba , ukifanya hivyo utakuwa Mkombozi wa kweli wa Soka la Tanzania. Pia suala la makato kwa Vilabu ni la kulizingatia sana....Haiwezekani Timu zinaintiza milioni 160 halafu zenyewe zinapata milioni 40 kila moja na nusu ya Mapato hayo inakatwa na kugawanywa kwa watu ambao kwangu mimi naona hawastahili.....Mfano ni DRFA....

Pia TFF ibuni vyanzo vingine vya mapato badala ya kutegemea mapato ya mechi ama Misaada ya FIFA....TFF wawe na wadhamini wao ambao watasaidia kuongeza Kipato...Jaribuni Kujenga viwanja vyenu wenyewe na kufungua miradi/vitega uchumi mfano Hostel ama TFF House ambayo itakuwa na vyumba vitakavyokodishwa kwa wafanyabiashara...Pia Jezi za Timu ya Taifa zianze kuzalishwa na TFF na kuuzwa kwa wapenzi wa Soka hivyo kuiingizia mapato TFF....

Kingine jitahidini muifanye Ligi yetu iwe na sura ya Kulipwa zaidi badala ya Ridhaa....Tukiwa na Ligi ya Kulipwa itakuwa ni hatua nzuri kuelekea mafanikio ya Soka letu...Tuwe na Ligi ya aina ya PSL ya RSA....Klabu zihimizwe kuingia katika mfumo wa Kampuni badala ya kumilikiwa na wanachama kama ilivyo sasa. Pia mliangalie vizuri suala la kupunguza Idadi ya wachezaji wa Kimataifa kutoka watano mpaka watatu, binafsi sioni sababu ya kuwapunguza kwani uwepo wao unaleta changamoto kwa wachezaji wazawa na wao kupata hamasa ya kutafuta timu nje ya nchi tofauti na sasa ambapo wachezaji wengi wazawa kwao kuchezea Simba ama Yanga ndio malengo yao....

Si vibaya kwenye Kamati zako ukawa unawakumbuka baadhi ya Members wa JF ambao nina uhakika watakua msaada mkubwa sana kwako licha ya kwamba wengi wao wanatumia majina ya vificho, cha msingi ni kuwasiliana na Invisible au Maxence Melo wataona namna ya kukusaidia.
 
Nmependa hii thread.ushauri wangu ni kuwa fanyeni kazi Kwa ushirikiano epukeni majungu yanayoenezwa juu yenu km la ukabila.nadhani umefafanua vema
 
Punguza wahaya pale karume mzee, tafuta majitu ya kazi soka liendelee, pia usilete siasa kwenye soka, mfano kwa lowasa ulikuwa una mdai nini mpaka ukaenda na vyombo vya habari nyumbani kwake,
my take #kuwa serias_piga _kazi
 
Balantanda naomba unitumie email jamalmalinzi@yahoo.com au nipigie au ni sms 0754815543
 
Last edited by a moderator:
Rais wetu wa TFF kuna hili la kufanya sherehe za miaka 50 nimeliona hapa Jf je lina ukweli kiasi gani, kama ni kweli lina faida/tija gani kwa Soka la Bongo na mwisho Bajeti yake ni kiasi gani?
 
huyu muhaya huyu anapenda sana show off
 
Lengo la azimio la bagamoyo lilikuwa kuongea wachezaji wazawa kupata kucheza zaidi. Sasa wakipunguzwa wakatakiwa kucheza wa3 kwa kila mechi basi nao watakupunguza kusajili pia n mwisho wa siku wazawa watapata nafasi

Kwani hizo nafasi za wazawa ziko Simba, Azam na Yanga tu? Mi nadhani tujiulize maswali mawili:

1. Ni kwa nini hatutoi nje wachezaji wetu wengi mpaka tuzing'ang'anie Simba na Yanga?

2. Katika ligi yenye wachezaji 420 ni kwa nini 20 wa kigeni wawe tishio kwa timu yetu ya taifa kwamba wanaziba nafasi? Ni wapi tumepotea njia?

3. Je, ni kweli kwamba ligi yetu ikiwa na wachezaji wa ndani tu ndio itakuwa bora?

4. Tunalotazamaje suala la mvuto wa ligi yetu nje ya nchi hasa pale tutakapoondoa wachezaji wa kigeni?

Maoni binafsi.

TFF itazame viwango vya waamuzi.

Udhamini wa uhakika kwa timu zote ndio mwarobaini wa ligi yetu na si wachezaji wa kigeni

Idadi ya timu katika ligi ni ndogo mno na haitoi bingwa halisi.

Timu za JKT zipunguzwe hata kama ni kwa kutingiwa sheria. Zinapunguza hamasa (hazima mashabiki) na ushindani kwenye ligi (ni vichaka vya kugawa pointi kwa wakubwa). Zibaki timu zinazoleta changamoto kama Ruvu Shooting na JKT Ruvu. Kuna nyingine zinakuja tena, Mlale, Kanembo yaani balaa tupu.

Ni mtazamo wangu mh. Jamal Malinzi
 
Last edited by a moderator:
huyu muhaya huyu anapenda sana show off

Mkuu Kigogo, JF imesheheni kila kitu hata kama ni udaku, jukwaa lipo; utani, jokes & gossips, jukwaa lipo pia. Hapa tunataka maswali na ushauri kwa Hon. Jamal Malinzi, tusihafifishe ubora wa uzi huu. Lengo letu ni kujenga mpira wetu kupitia mawazo ya GT's. Kama una utani na Rais unaweza kuanzisha uzi katika jukwaa husika. Hapa hekima, heshima na upendo vitawale. Vijembe, matusi and the like; NO!
 
Last edited by a moderator:
Malinzi,

Rejea mjadala kuhusu timu ya Taifa, mawazo yangu ni kama ifuatavyo

1) kwanza ili kujua ni mfumo au utaratibu gani tuufuate katika kuijenga timu yetu ya taifa, mimi nakuomba kwa kuwa umemteua mtu mfulani kuwa msaidizi au mshauri wako wa mambo ya mpira, hivyo natumaini huyu mtu analipwa na TFF. sasa huyu mtu nakuomba umpe kazi afanye utafiti yakinifu wa nchi zote za Taifa za Africa, ambazo timu zao zimekuwa na mafanikio. Aaandike ripoti na kuiwakilisha kwako, na wewe kama itawezekana uishushe hapa, hii itatusaidia kutupa mwanga na kujua ni mfumo upi tunaweza kutumia. Pia hapa unawezaq kupata watu ambao wanaweza kufanya kazi na huyu jamaa kwa kupeana malengo, nani ashughulikie nchi hii, na mwingine hii.

Tujiulize nchi kama Rwanda, Burkina farso, na Uganda mbona zimeweza kuwa na timu nzuri katika muda mfupi? Hata Zimbambwe , tumeona juzi walivyoweza kufanya vizuri achilia mbali Libya pamoja na matatizo yote.

2) Idadi ya wachezaji wa kigeni.
Hili swala ni kweli limeathiri kwa kiasi kikubwa nchi kama UK, lakini kwa upande mwingine hakuna ukweli, tujiulize ni tangu lini wachezaji wa kigeni wameanza kufurika kwenye timu za England? Na je kabla ya hapo timu ya Taifa za UK , na hasa England zimekuwa na mafanikio? Jibu utakuta si kweli. Tatizo la UK, na England per se, mfumo wa ufundishaji kutoka academy ni dhaifu mno, hebu tazama tu vipaji ambavyo huzalishwa na academy ya Ajax amsterdam ulinganishe na wachezaji wa Engaland, wengi wao ni media tu ndo imekuwa ikiwakuza.

Tukija kwa hapa kwetu, wachezaji hawa wa kigeni wameongeza saana ushindani na kuifanya ligi yetu kuwa kivutio hata kwa jirani zetu. Kitu kinachoweza kufanywa ni kuwa timu iruhusiwe kusajiri si zaidi ya wacheza 5, lakini uwanjani isichezeshe zaidi ya wachezaji watatu kwa wakati mmoja.
 
MKUU MALINZI

VIPI KUHUSU ITC YA GEORGE MTEMAHANJI tangu mwaka jana mpaka leo kimya ameshindwa kujiunga na timu na kuanza kucheza mpira ITALY na USWISSI, Vipi mkuu au ndio mpaka ailipie hapo TFF ndio atapewa ITC




 
Hapo nitapishana na wewe,what is the point klabu iingie gharama kumsajili mchezaji kwa mamilioni halafu iambiwe akae benchi?
Jamal Malinzi

kama unapinga wazo hili naona hata ukipewa wazo la kuhakikisha kila timu ina chezesha wachezaji wawili wa Under 20 kwenye ligi pia utaipinga, ila ukweli ni kwamba wakati unatakiw aufike ligi yetu wacheze Vijana na sio wazee.
 
Last edited by a moderator:
Kwani hizo nafasi za wazawa ziko Simba, Azam na Yanga tu? Mi nadhani tujiulize maswali mawili:

1. Ni kwa nini hatutoi nje wachezaji wetu wengi mpaka tuzing'ang'anie Simba na Yanga?

Ni mtazamo wangu mh. Jamal Malinzi


Hatutaka kutoa wachezaji nje kwa kuwa hakuna mtu atayekuja kusajili VIKONGWE kupeleka Ulaya , ni wakati sasa timu zipewe ulazima wa kuchezesha Vijana kwenye Mechi za Ligi Kuu.

n ahilo la wageni mimi lina nitia Aibu hasa timu yangu Yanga kila siku inasajili VIKONGWE, hongera simba kwa kusajili vijana wakigeni na kuwauza inapotekea nafasi.
 
Mokoyo kwa vyovyote vile tutaongeza timu za premier league na kuanzisha mashindano mapya ili vijana wetu wapate angalao mechi 40 za kucheza kwa mwaka.Mabadiliko haya yatakuja msimu ujao.
Jamal Malinzi

kwahili twende taratibu,
tuongeze zifike 16 then 18 then 20. na sio haraka haraka.

pia isije ikawa mambo ya kuwa mwaka huu hakuna kushuka daraja, hatutaki kusikia hili ni bora kuboresha ligi daraja la kwanza na kuhakikisha badala ya kupanda watu wawili wapande wanne lakini kushuka wawili kila mwaka ni lazima.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…