Maswali na ushauri kwa Malinzi

Kandukamo 1 wakimataifa Kipaji Halisi nini hasa kinaongelewa hapa? Lini TFF ilitoa tamko la kukubali ku host? Lini CECAFA walitoa orodha ya vilabu shiriki? maana wao ndo wenye mandate.Tuwe tuna deal na facts please.
 
Last edited by a moderator:

elezea wapi tumefeli na nini yalikuwa matarajio yako.Program zetu kwa kulingana na kipato cha TFF tumeziweka wazi na zinajulikana.U17 mwaka 2017 Madagascar tunaandaa kikosi sasa cha U15,U17 2019 fainali za Afrika tumeomba uenyeji na kikosi tunaanza na U13 June.Pia kila mkoa kuwa na youth program tumeanza.Sasa tumefeli nini?Kama ni mkakati wa muda mfupi ni maboresho Taifa stars na matunda mnayaona.
 
Nawe unaamini kuwa huu uzi upo kwa ajili ya kujenga soka letu,huu uzi ni ghiriba tu kutupoteza maboya sisi mashabiki wa mpira.Mpira wetu unaporomoka kama shilingi ya Tanzania

kyumana usitarajie kuvuna pale ambapo hukupanda.Structure (mfumo) wa mpira wa nchi hii unaujua? Mchana mwema.
 
Last edited by a moderator:

Hayo matunda yako wapi? Wengine tunaona miba tu, kila Taifa tars inapokanyaga inachomwa.

Hizo zingine zote ni porojo.

Ile turf uliyopeleka kwenu Kagera kwanini usiipeleke Mkwakwani au kwengine?

Na Mkandarasi ni yupi? ni yuleyule aliyeweka viwanja vingine kabla na mwenye uzoefu tayari au ni mtoto wa shangazi?
 
Jamal Malinzi kwanza nikupongeze kwa muda ambao umekaa madarakan manake toka ushinde sijawah kukupa hongera.

well nije kwenye swala langu la msingi,
1. majuzi nimeskia eti wantaka kukupindua umeshindwa kuendesha TFF na tuhuma kibao nikaorodheshewa. Jaman naomba nipe jibu kweli unakubaliana na hoja kwamba umeshindwa kuiongoza TFF?

2. JE ni kweli kwamba TFF imeshindwa kusimamia hali halisi ya uendeshwaji wa ligi hasa kipengele cha baadhi ya timu kuruhusiwa kuhujumu nyingine ili zife kisoka? simaanishi tuhuma dhidi ya Mbeya City manake mjuaj wa mpira atajua kwamba ile haikuwa timu bali ulingo wa siasa. mpira hauchezwi kwa kelele za makofi kama kwenye majukwaa ya siasa, mpira ni ufundi.
apa naongelea timu nyingine ambazo ni nzuri hapa nchini lkn zinahujumiwa
 
Last edited by a moderator:

faiza foxy FIFA wana taratibu zao ,nyasi bandia kabla hazijawekea kuna commitments inabidi zifanywe na wamiliki wa viwanja.Nyamagana na Kaitaba wamiliki ni Halmashauri na ndio maana umekuwepo urahisi wa kukubaliana na FIFA.Next target ni Moshi uwanja wa St George wauza mitumba wakitoa nafasi maana nao ni wa Halmashauri.Uwanja wa uhuru na Gombani ni mali ya Serikali huko nako makubaliano na FIFA yalifikiwa kirahisi.Fanya uchunguzi kidogo kuhusu umiliki wa mkwakwani na viwanja vingine ili tushauriane nini kifanyike.
National team kote duniani huwa haijengwi kwa mipango zimamoto huwa ni gradual development,kuwa na subira.
 
Last edited by a moderator:

@gfsowin Katiba zetu zimepunguza mianya ya wakorofi wachache kutibua utulivu kwenye vyama vya mpira.Ndio maana kipindi kile waliojaribu kumwondoa Mh Rage madarakani walikwama.
Hili la timu kuhujumiwa linahusisha upangaji matokeo yaani match fixing.Hili tunalipiga vita na likibainika adhabu ni wahusika kufungiwa maisha
 
Last edited by a moderator:
ahasante sana kwa majibu yako mazuri japo nimebaki na maswali kibao
ngoja kwanza nije kaunta ya juu nikuambie tujadiliane
BTW unakubaliana na hoja kwamba wafadhili wa timu huwa wanahujumu timu pinzani?
mfano mimi ni mwanachama wa Yanga hadi Tibo (salam zangu kwake mwll wangu) analijua hilo. Ila sasa kuna dhana imejengeka miongoni mwa wapinzani wetu simba kwamba Manji nia yake ilikuwa kuiua timu ya simba na ndio mana kila mchezaj ambaye simba ilitaka kumsajili basi MANJI hutia mkono wake na kumchukua huyo mchezaj.

Simba wakaona njia sahihi kwao ni kwenda kuloga hivyo wale wachezaj wakitua yanga yaani wanakuwa ahawaeleweki na kiwango kile walichokuwa nacho kinakosekana tena.

mimi nilichojiuliza ivi ni kweli haya yanatokea? kama ndio nyie kama TFF na hasa wewe kama raisi unafanya nini kuhakikisha timu hazihujumiani, pili ushirikina kwenye mpira unakomeshwa?

nalisema la ushirikina kwasbb ninao uhakika mfano simba wako radhi waloge Yanga iendelee kuwa mteja wao lkn wao hawajal hata kama watafungwa na timu ya daraja 3.....................ushahidi wa huu ushirikina na waganga wao upo na najua unalijua hili. je wewe unalisemeaje hili?
 
Kandukamo 1 wakimataifa Kipaji Halisi nini hasa kinaongelewa hapa? Lini TFF ilitoa tamko la kukubali ku host? Lini CECAFA walitoa orodha ya vilabu shiriki? maana wao ndo wenye mandate.Tuwe tuna deal na facts please.
Jamal Malinzi nasubiri hilo tamko kuwa mmekubali kagame cecafa ifanyike hapa niweke ushahidi wa aliosema musonye khs yanga na tz..pale sports view hotel kigali...na amahoro stadium...
Nakukubali sana rais..ila sipendi uyumbe wala uyumbishwe...
 
Last edited by a moderator:

Nashangaa TFF wanapiga faini watu kufanya vitendo vya ushirikina uwanjani halafu wanaruhusu wanaosali kwa dini zao, ushirikina ni Imani kama Imani zingine na kwenye soka la bongo hakuna asiyeloga na some time matokeo ya Imani hizi yanaonekana. So naamini si vibaya kutumia ulozi katika soka ni mbinu za ushindi kama mbinu zingine
 
Reactions: tyc
Jamal Malinzi nasubiri hilo tamko kuwa mmekubali kagame cecafa ifanyike hapa niweke ushahidi wa aliosema musonye khs yanga na tz..pale sports view hotel kigali...na amahoro stadium...
Nakukubali sana rais..ila sipendi uyumbe wala uyumbishwe...

lito bro nimekumiss sana
Pia nimependa sana swali lako kwa Jamal Malinzi kuhusu kagame cup
 
Last edited by a moderator:
Jamal Malinzi hivinTaifa Stars siku hizi ni Mzizima United?Taifa Stars yetu ni Team ya Mkoa wa Dar?Ili uchaguliwe team hii sasa ni lzm ucheze mpira Dar au uwe affiliated na team ya Dar?

Tumekuvumilia sana ww na huyu Mholanzi uliye mleta ambayo hajashinda hata game moja ya maana!Team yetu imekuwa team ya hovyo hovyo kabisa na mtasingizia kuwa hatumuingilii kocha!!

Amri Kiemba anaitwa Stars akafanye nn?U p u u zi mtupu team hii
 
Last edited by a moderator:
mbona tff hamtoi rufaa ya yanga kuhusu ajibu aliecheza wakati ana kadi nne za njano?
 

Anaita wachezaji wazee wanaokaa benchi kina Kiemba, Cannavaro, Kazimoto, Dilunga hata Vitalisi Mayanga 19 years wa Stand hamjamuona? kamuntu wa Ruvu?
Stars siku hizi inachosha na haina mvuto wachezaji wale wale hawajitumi, wamefanya Stars kijiwe cha kupokea posho
 
Last edited by a moderator:

Huyu Jamal Malinzi naona anatuchezea sasa!Kuna vijana mikoani kibao wanaweza chezea team hii!Tuna Lugano Mwangama wa Prison au yule kipa wa Majimaji!

Hii bi team ya Mkoa wa Dar
 
Last edited by a moderator:
kweli kuna makosa madogo madogo kuchagua taifa stars wanachagua kwa wachezaji wazoefu lakini wangechagua kidogo wachanga wapate uzoefu
 
Lakini mh J malinzi hebu utueleze kanuni iliotumika mchezaji Ajibu aliokuwa na adhabu ya kadi za njano na akapewa kibali kucheza leo mnakurupuka kumpa jery muro adhabu
 
Lakini mh J malinzi hebu utueleze kanuni iliotumika mchezaji Ajibu aliokuwa na adhabu ya kadi za njano na akapewa kibali kucheza leo mnakurupuka kumpa jery muro adhabu

hilo hajibu hatamuandike vipi hawezi kujibu kama lilivyo jina la ajibu
 

gfsonwin!!!! msalie Mtume tafadhali!
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…