Maswali yenye Utata Kifo cha Balozi C. Mushi. Nini kipo nyuma yake?

Maswali yenye Utata Kifo cha Balozi C. Mushi. Nini kipo nyuma yake?

Mtu Asiyejulikana

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2017
Posts
2,254
Reaction score
5,161
KUTOKA KWA MALISA GJ

Nimejiuliza maswali kadhaa nikakosa majibu;

1. Balozi Mushi alikua anajiendesha mwenyewe? Tena usiku wa manane? Protocal za kidiplomasia zinasemaje, Balozi anapokua na safari binafsi? Je alikua peke yake?

2. Kama ajali ni uso kwa uso means lori lilikua linatoka ielekeo wa Segera na Balozi alikua anaenda uelekeo wa lori lilipotoka. Kama ndivyo hayo makaa ya mawe yalitoka wapi? Tanga, Kilimanjaro, Arusha hata nchi jirani ya Kenya hakuna makaa ya mawe. Makaa ya mawe yapo Mbeya, Rukwa na sehemu za Njombe. Kenya wanatumia makaa ya mawe kuendesha mitambo yao ya viwanda, lakini wanayachukua Mbeya (Kiwira). Hakuna lori linalotoka na makaa ya mawe Kenya kuja Tanzania, bali malori yanayotoka na makaa ya mawe Tanzania kwenda Kenya. Kwahiyo kama Lori lilikua limebeba makaa ya mawe it means lilikua linaenda uelekeo mmoja na Balozi Mushi. Sasa ilikuwaje wagongane uso kwa uso?

3. Gari iliteketea na Balozi Mushi aliungua kiasi cha kutotambulika. Ndugu walimtambua kwa nguo zake. Je hizo nguo zilipatikana sehemu gani ya gari? Ni moto gani unaweza kuchoma gari ikateketea, lakini nguo zikabaki?

4. Inadaiwa mashuhuda walijua ni Balozi Mushi baada ya kuingiza namba za gari kwenye mifumo ya TRA ndipo ikaonesha mmiliki ni Celestine Mushi. Hizo namba walizionaje kama gari iliteketea?

5. Kwanini usiku huo wa ajali kuna ujumbe ulizunguka sana kwenye mitandao ya kijamii, ukisema aliyepata ajali ni mwanamke lakini gari ni ya Balozi Mushi? Nani aliandika ujumbe huo? Lengo lake lilikua nini? Kuiandaa kisaikolojia familia ya Mushi au?

6. Ajali imetokea Mkata, Handeni Vijijini. Wakazi wake wamepata wapi "exposure" ya kuingiza namba kwenye system za TRA ili kumjua mmiliki wa gari? Je huwa wanafanya hivyo kwenye ajali zote au ni hii tu?

7. Kwanini mamlaka za serikali zilikimbilia kutoa pole kabla ya mwili haujafanyiwa uchunguzi. Je ingebainika kuwa sio Balozi Mushi bali alimwazima mtu gari yake, serikali ingefanyaje na ilishatoa salamu za rambirambi?

Anyway; Mungu ampumzishe kwa amani Mhe.Balozi Celestine Mushi. Laa ko oforo mangi.!
 
Yale yale ya Imran Kombe,

Huyu balozi kama kweli alikuwa na kesi ya ubakaji huko ughaibuni ndio maana akakimbilia nyumbani,aliisha kuwa "compromised"sasa inawezekana waliotaka ku "mrecruit"waliona Bora wamuondoe,au Kuna Siri alivujisha,Idara ikaona huyu hafai Tena,Bora atulizwe milele.

Kwa idara yetu,ambayo ipo bize kuiba kura,na kuilinda ccm,nchi haipo salama,Nina hakika,wanadiplimasia wetu wengi,wapo compromised sana,wanavujisha Siri za nchi,kwa kujua ama kutokujua!!

Sasa sijuhi ni kwa kiwango gani,nchi yetu na systems zipo penetrated.
 
Yale yale ya Imran Kombe,
Huyu balozi kama kweli alikuwa na kesi ya ubakaji huko ughaibuni ndio maana akakimbilia nyumbani,aliisha kuwa "compromised"sasa inawezekana waliotaka ku "mrecruit"waliona Bora wamuondoe,au Kuna Siri alivujisha,Idara ikaona huyu hafai Tena,Bora atulizwe milele.
Kwa idara yetu,ambayo ipo bize kuiba kura,na kuilinda ccm,nchi haipo salama,Nina hakika,wanadiplimasia wetu wengi,wapo compromised sana,wanavujisha Siri za nchi,kwa kujua ama kutokujua!!
Sasa sijuhi ni kwa kiwango gani,nchi yetu na systems zipo penetrated.
Mabalozi wana siri gani za nchi za kuvujisha? Labda kama na yeye alikuwa ni mtu wa idara pia. Wanaokuwa compromised ni watu wanaoujua hizo siri. Sasa jiulize ni nani hao.
 
Gari iliteketea na Balozi Mushi aliungua kiasi cha kutotambulika. Ndugu walimtambua kwa nguo zake. Je hizo nguo zilipatikana sehemu gani ya gari? Ni moto gani unaweza kuchoma gari ik
Atakuwa alihusika JPM, si bule,

Maana viloba na mauwaji ni yeye hakuna mwingine!

Eeh Mungu, uirehemu nchi yetu na ccm uifute na watu wake
 
Mabalozi wana siri gani za nchi za kuvujisha? Labda kama na yeye alikuwa ni mtu wa idara pia. Wanaokuwa compromised ni watu wanaoujua hizo siri. Sasa jiulize ni nani hao.

As far as wanawakilisha nchi lazima wawe na siri nyingi za Taifa letu zihusuzo uchumi, usalama na ustawi wetu.

Tatizo langu ni moja; pamoja na siri zote hizi mbona tunazidi kuwa maskini kama nchi na tegemezi? Hizo strategic information zinatumikaje?
 
Back
Top Bottom