MATAGA nayo yanaisoma namba πŸ˜‚

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
SEPTEMBER 2020

#Jamaa: Lissu ni kibaraka wa mabeberu. Amepewa pesa na mabeberu kuja kuharibu amani ya Tanzania. Magufuli tano tena.!

#Mimi: Bro hiyo sio siasa. Jadili issues acha kuattack personalities.

#Jamaa: Na wewe kashakugawia pesa za mashoga alizopewa? Mtapata tabu sana mwaka huu. Magufuli Tano tena.!

#Mimi: mi nadhani siasa ni sawa na njia ya kwenda Arusha. Mmoja akapita Bagamoyo na mwingine akapita Chalize. Hakuna sababu ya kumchukia mwenzio au kumtukana kwa sababu amechagua njia tofauti na wewe. Ni ushamba.

#Jamaa: Mtateseka sana bro. Una akili nyingi lakini sijui unafanya nini huko upinzani. Hawawezi kukutumia. Hao ni vibaraka wa mabeberu achana nao, njoo CCM fursa zipo kibao.

#Mimi: Bro upinzani ni umuhimu. Unasaidia kuibua mawazo mbadala na yanafanyiwa kazi. Upinzani unapigia kelele kero zilizopo kwenye jamii na zinatatuliwa. Upinzani ni "watchdog" wa serikali kwenye utendaji.

#Jamaa: Labda "watchdog" wa mabeberu. Serikali ya JPM haihitaji watchdog. Kila kitu kinaenda kama kinavyotakiwa kuwa. Magufuli tano tena.!

JANUARY 2021

#Jamaa: Bro mambo vp? Kaka yetu mkubwa amekamatwa tangu Oktoba mwaka jana hajapewa dhamana. Alituhumiwa kupewa rushwa na wazabuni waliokua wameomba tenda ofisini kwao lakini kesi imebadilishwa kuwa uhujumu uchumi. Akaunti zake zote zimefungwa, mke na watoto wanateseka sana wameshindwa kwenda hata shule. Akaunti zote wamezifreeze. Tusaidie kulisemea hili kaka. Nipigie nikupe more details.

#Mimi: Kaka, serikali ya JPM haihitaji watchdog. Inafanya mambo vile yanavyotakiwa kuwa. Magufuli tano tena.!

Malisa GJ
 
#2020 jamani tumejenga madarasa nchi nzima tumetekeleza #2021 wanafunzi wanakaa chini huku wakiimba ngonjera
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
 
#mimi. Sawa ila yakikufika usije kulia humu.

Simba zee 33 .mlizoea uhuni uhuni wa dj Sasa hakuna shotkat.

#mimi.. weee zee wewe shetani Hana rafiki Lia na waliao Sasa siku likikufika tutalia na wewe Kama faraja.

Simba zee 33. Mchuma janga hula na wakwao.

#mimi . Aksante mkuu kila la heri.

Mwezi June 2021.

Simba zee 33 jamani huu utawala huu najuta kuupigia debe Yani no yumba yangu wameibomoa bila malipo eti kupisha ujenzi wa barabara Sasa kwanini wasitulipe na sheria zipo.

#mimi.. mchuma janga hula na wakwao.🀣🀣🀣🀣🀣🀣
 
Mkuu hilo ni dua la kuku hallimpati mwewe
Viongozi wote wa CCM tunatembelea vieitee!!
Unaijua vieite wewe!
 

Attachments

  • IMG_20210101_160453.jpg
    73.6 KB · Views: 1
  • IMG_20210112_150518.jpg
    86.3 KB · Views: 1
Mwambie huyo wakuchungawakoo, sisi hatuko tayari kuruhusu ndoa za jinsia moja kufungwa kwenyumba za ibada ilimisaada ijeee
 
Wewe ulimpigia debe yule mzee wa kiki na miujiza yakutengenezwa na mabeberu halafu akagazwa kweupeee
 
Cha ajabu walimu hamuwalipi malimbikizo yao mishahara hamuwaongezi mafuta mtaani Lita moja ya kula ni 4800 bado makato ya helsb ila walimu mnawamudu Sana.
 
Huu upuuzi umeuleta humu kwa nn
Atujuwani ila wewe bonge la mshikaji wangu nimecheka sana b4 sija ondoka kwenye hii dunia ninatamani sana tuonane πŸ˜‚
 
πŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½
 
Naomba kuonyeshwa mahali CCM wanaponunulia mafuta ya kula jamani wenzetu Bei Yao sio Kama yetu πŸ˜‰πŸ˜‰πŸ˜‰
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…