Mataifa 50 kukutana Uswisi kujadili amani ya Ukraine na Urusi

Mataifa 50 kukutana Uswisi kujadili amani ya Ukraine na Urusi

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Uswisi inaratajia kuwaalika washiriki zaidi ya 160 kutoka mataifa mbalimbali katika mkutano utakaolenga kuleta amani na upatanishi wa Ukraine na Russia.

Mkutano huo unatarajia kufanyika kwa siku mbili kuanzia Juni 15 hadi 16 katika Hoteli ya Bürgenstock Hotel nchini humo.Taarifa iliyotolewa na Idara ya Mamlaka ya Mambo ya Nje ya Uswisi ilieleza kuwa waalikwa hao ni wanachama kutoka mataifa saba yenye nguvu kubwa ya uchumi (G7), G20, Umoja wa Ulaya (EU) Nchi wanachama wa Brics isipokuwa Russia.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, waalikwa wengine ni mashirika mbambali ya kimataifa na kidini.

“Hii itakuwa ni jitihada za tano kunurusu hali ya amani kati ya Russia na Ukraine. Wageni watatoka pia mataifa ya Afrika Kusini, Misri, Senegal, Congo-Brazzaville, Comoro, Zambia na Uganda ambao wataongozwa na Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa,” ilieleza taarifa hiyo.
 
Fikiria kama sio Ujinga ni nini?? Mhusika mkuu ni Russia halafu hayupo hapo sasa hao si wanakutana kunywa chai nankuondoka mana vikwazo vyao ngoma imewabumia uwanja wa vita wanachakazwa sana sasa waitane wanywe chai wapige picha waondoke muda huo Majeshi ya Urusi yatakua Kyiv.
 
Fikiria kama sio Ujinga ni nini?? Mhusika mkuu ni Russia halafu hayupo hapo sasa hao si wanakutana kunywa chai nankuondoka mana vikwazo vyao ngoma imewabumia uwanja wa vita wanachakazwa sana sasa waitane wanywe chai wapige picha waondoke muda huo Majeshi ya Urusi yatakua Kyiv.
Ukifikiria nje ya box utagundua huo mkutano utakuwa na nia ya kufanya mazungumzo na Brics kuishawishi iachane na Russia. Yaani huo mkutano ni kati ya NATO na BRICS - Russia
 
Fikiria kama sio Ujinga ni nini?? Mhusika mkuu ni Russia halafu hayupo hapo sasa hao si wanakutana kunywa chai nankuondoka mana vikwazo vyao ngoma imewabumia uwanja wa vita wanachakazwa sana sasa waitane wanywe chai wapige picha waondoke muda huo Majeshi ya Urusi yatakua Kyiv.
Na Papa alimwambia Ukraine sio vibaya kupandisha bendera "nyeupe" wakambishia
 
Uswisi inaratajia kuwaalika washiriki zaidi ya 160 kutoka mataifa mbalimbali katika mkutano utakaolenga kuleta amani na upatanishi wa Ukraine na Russia.

Mkutano huo unatarajia kufanyika kwa siku mbili kuanzia Juni 15 hadi 16 katika Hoteli ya Bürgenstock Hotel nchini humo.Taarifa iliyotolewa na Idara ya Mamlaka ya Mambo ya Nje ya Uswisi ilieleza kuwa waalikwa hao ni wanachama kutoka mataifa saba yenye nguvu kubwa ya uchumi (G7), G20, Umoja wa Ulaya (EU) Nchi wanachama wa Brics isipokuwa Russia.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, waalikwa wengine ni mashirika mbambali ya kimataifa na kidini.

“Hii itakuwa ni jitihada za tano kunurusu hali ya amani kati ya Russia na Ukraine. Wageni watatoka pia mataifa ya Afrika Kusini, Misri, Senegal, Congo-Brazzaville, Comoro, Zambia na Uganda ambao wataongozwa na Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa,” ilieleza taarifa hiyo.
😁😁😁😁😁 bila Putin kuwepo hicho ni kikoba tu.
 
Bendera nyeupe maana yake kutaka Amani na kujua kwamba mgogoro wao hautamalizwa Kwa vita Bali Kwa mazungumzo,.

Ndio nakuambia bendera nyeupe haitosaidia kitu, kwamba waachie nchi ichukuliwe kisa bendera nyeupe, wewe kwa akili zako unawaza mvamiwe na nchi jirani ichukue Tanzania kisa bendera nyeupe.....
Natumai hautakua ustaadhi maana ndio wanaaminishana huu ujinga.
 
Ndio nakuambia bendera nyeupe haitosaidia kitu, kwamba waachie nchi ichukuliwe kisa bendera nyeupe, wewe kwa akili zako unawaza mvamiwe na nchi jirani ichukue Tanzania kisa bendera nyeupe.....
Natumai hautakua ustaadhi maana ndio wanaaminishana huu ujinga.
Unapofanya mazungumzo na mtu mwingine inamaanisha nchi kuchukuliwa?? Unapofanya mazungumzo ina maana ni jinsi gani mnatatua kilicho sababisha vita.
Tuchukulie hutaki mazungumzo, je hiyo vita unayopigana inakusaidia kitu ikiwa kupigwa Una pigwa na Ardhi inatekwa. Kwa hiyo hapa unaopata hasara mara mbili ya kupigwa na Ardhi kutekwa.
Wakati Bendera nyeupe utaokoa maisha ya Askari wako na miundo mbinu nchi.
Makaburu SA walikubaliana na Hilo
 
Huo utakuwa siyo mkutano wa kupatanisha.kwa nini mhusika anaondolewa? Kwa nini tz hatujaalikwa?.Mama anavyopenda kisafiri lazima ajipeleke
 
Back
Top Bottom