Ng'wanamalundi
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,203
- 1,422
Hivi inaingia akilini kwamba mtu ana ng'ombe wake Mwanza, Dar au Mara na Arusha awapeleke ng'ombe wake hao akamkabidhi Mmasai asiyemfahamu wala ili amchungie? Ningeelewa kama huyo tajiri angemwajiri huyo Mmasai amchungie ng'ombe wake hapo hapo aishipo yeye tajiri; sawa na watu wa Dar walivyokuwa wakiajiri Masai walinde makazi yao.Matajiri wanaoishi mikoa ya mbali ikiwemo Mara, Mwanza, Arusha, Kilomanjaro, Dar es salaam walitumia kigezo cha jamii ya kimasai kuishi Ngorongoro kuingiza hifadhini mamilioni ya ngombe hivyo kuathiri uhifadhi.
Hii ni baada ya serikali kudhibiti mifugo kuingia katika hifadhi nyingine ikiwemo seregeti.
Matajiri hao kwa sasa wanatumia nguvu ya fedha na kuwapa kikundi kidogo cha wamasai ili wakatae kuondoka Ngorongoro kwa kuwa wnaajua itakula kwao, kwa sababu itakuwa maajabu na hao matajiri wanaomiliki migodi, viwanda, na mabasi wakipewa ekari mbili msomera.
Wingi wa wanyama wa kufugwa umesababisha magonjwa mengi kwa wanyama pori, na vifo vya wanyama pori kwa sasa vimekithiri Ngorongoro kutokana na kurundikana kwa mifugo toka kanda ya ziwa, Mbeya, Lindi, na baadhi ya maeneo ya Tanga na kilimanjaro.
Wale wafugaji wa asili kabisa ya Ngorongoro wote wameondoka kwenda Msomera, Tanga, wamebaki vibarua wa matajiri hao ambao sasa wanasababisha vurugu mbugani.
Pia soma:
- Kuelekea 2025 - Wamasai Ngorongoro wamechoka kunyang’anywa ardhi yao na kupewa Mwarabu, Wameamua liwalo na liwe
- Masai hawana ardhi, Rais Samia anawapenda
- CHADEMA na Wakenya wana maslahi gani kwenye vurugu zinazoendelea Ngorogoro?
- Kuelekea 2025 - Njama: Vituo vyote vya kupigia kura Jimbo la Ngorongoro vimefutwa, ila watu bado wapo na Jimbo bado lipo
- Wamasai wa Ngorongoro Wametendewa Uharamia Dhidi ya Utu, Wasaidiwe
- Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi: Kaya 1,373 zenye Watu 8,364 zimeshahama Ngorongoro kufikia Aprili 2024
- Wamasai na Ngorongoro: Siasa ya Maendeleo ya Vitu au ya Watu?