Matajiri wanaoishi mikoa ya mbali ikiwemo Mara, Mwanza, Arusha, Kilomanjaro, Dar es salaam walitumia kigezo cha jamii ya kimasai kuishi Ngorongoro kuingiza hifadhini mamilioni ya ngombe hivyo kuathiri uhifadhi.
Hii ni baada ya serikali kudhibiti mifugo kuingia katika hifadhi nyingine ikiwemo seregeti.
Matajiri hao kwa sasa wanatumia nguvu ya fedha na kuwapa kikundi kidogo cha wamasai ili wakatae kuondoka Ngorongoro kwa kuwa wnaajua itakula kwao, kwa sababu itakuwa maajabu na hao matajiri wanaomiliki migodi, viwanda, na mabasi wakipewa ekari mbili msomera.
Wingi wa wanyama wa kufugwa umesababisha magonjwa mengi kwa wanyama pori, na vifo vya wanyama pori kwa sasa vimekithiri Ngorongoro kutokana na kurundikana kwa mifugo toka kanda ya ziwa, Mbeya, Lindi, na baadhi ya maeneo ya Tanga na kilimanjaro.
Wale wafugaji wa asili kabisa ya Ngorongoro wote wameondoka kwenda Msomera, Tanga, wamebaki vibarua wa matajiri hao ambao sasa wanasababisha vurugu mbugani.
Pia soma: