matamshi kiinglish tunayakosea kwa kurithishana

matamshi kiinglish tunayakosea kwa kurithishana

kingereza cha jiji la liverpool na cha london matamshi yao kwenye neno moja pia hutofautiana,sijui hapo tunaliweka vp suala hili
hizo tofauti za kijografia zaweza tofautisha matamshi ya lugha kama ilivyo hata hapa Tanzania , kuna standard English ambayo hutumika kwenye Oxford Advanced Learners Dictionary na lugha hiyo inatoa mwongozo wa matamshi kifonoljia na pia inatofautisha neno kwa matamshi ya Kimarekani na Uingereza
 
Emmanuel ni Emanyuel..

socio-economic watu huyamka sosho-evonomic ila hutamkwa sosio-Economic..

nikashangaa hata neno sociology halitamkwi sosholoj bali sosioloj wakati social inabaki kuwa sosho(OXFORD ADVANCED LEARNERS DICTIONARY)
 
hizo tofauti za kijografia
zaweza tofautisha matamshi ya lugha kama ilivyo hata hapa Tanzania ,
kuna standard English ambayo hutumika kwenye Oxford Advanced Learners
Dictionary na lugha hiyo inatoa mwongozo wa matamshi kifonoljia na pia
inatofautisha neno kwa matamshi ya Kimarekani na Uingereza

mi naona hyo kitu kuiepuka kabisa ni ngumu mno,ingekuwa tatizo labda kama matamshi hayo yanaleta maana nyingne zaidi kiasi cha kuhatarisha uelewano wa mazungumzo hayo
 
vipi kuhusu chwingam Chewing gum or Bubble Gum ,Banzooka

Wengi husema ni Deep! nitakupigia instead ku beep
 
'debt' watz wengi wanatamka debti!
Kwa mujibu wa dictionary debt inaandikwa det hivyo' b' kutosikika kabisa! kiukweli baada ya kuchunguza maneno mengi ya kiinglish unaweza jihurumia jinsi tunavyokosea
 
mi naona hyo kitu kuiepuka kabisa ni ngumu mno,ingekuwa tatizo labda kama matamshi hayo yanaleta maana nyingne zaidi kiasi cha kuhatarisha uelewano wa mazungumzo hayo

japo ni ngumu kuepuka kabisa sababu ni lugha ya pili, lakini ni vyema kujitahidi kujifunza usahihi wa lugha husika ili kuepusha kutoelewana kunakoweza jitokeza wakati wa mawasiliano ,sababu kutamka neno tofauti yaweza badilisha maana
 
Kwa mujibu wa dictionary debt inaandikwa det hivyo' b' kutosikika kabisa! kiukweli baada ya kuchunguza maneno mengi ya kiinglish unaweza jihurumia jinsi tunavyokosea

Hasa ukikaa na wasiowatz ndiyo utangundua makosa mengi tunayofanya ktk kutamka maneno. Nadhani Mjerumani alitumia broken english wakati anatutawala. Wakatuathiri matamshi.

Tatizo kubwa lipo kwa walimu hivyo makosa yanaendelezwa.
 
Kuna mtangazaji radio one anaitwa julius njole ana matamshi mabaya ya majina mbali mbali. Mfano damascus=damasikakasi. baghdad=bagidadi. new york=nyu yoku. Anaboa kweli
 
Kwa mashabiki wenzangu wa mpira,,, neno possesion lina tofauti kubwa na position!! Ila ki boli boli mnaweza shikana mashati,Ee bwana eeh!tatizo ni boli position bwana,ukimwambia amekosea 90% wanakushangaa.


hapo neno sahihi ni possession. yaani inaposemwa ball possession ni umiliki wa mpira.
 
neno question - tunatamka kweshen badala ya kwes'shen
'' consumer - '' konshuma
badala ya konsyuma
'' producer - '' prodyuza badala ya prodyusa
'' assume - '' ashum
badala ya asum au asyum
'' every - '' evere " evri

hayo ni maneno machache katika mengi ambayo nimeshuhudia yakiendelea kukosewa siku hadi siku hadi na walimu wa lugha husika.Mimi nilikua mmoja wa waathirika tokana na aina ya shule nilizosoma ,japo namshukuru Mungu baada ya kufika A level nilisoma Kiingereza katika Combination yangu na kusoma topic ya phonology inayohusisha matamshi ya lugha na kanuni zake ndipo nikagundua nilipokua nakosea na wengine wengi wamekua wakikosea.

Mwenye uelewa wa maneno mengine ya english ambayo ameyasikia yakikosewa na wa Tz ni vyema ayaweke ili tuboreshe lugha kidogo kimatamshi angalau.

Zunguka-zunguka weeeeeeee halafu baadae tutarudi hapa

Lugha ni sauti za nasibu zilizozuka na kukubalika kutumika kwenye jamii bila makubaliano ya watu maalum
 
kweli english wito hata neno nililozoea la basic naambiwa siwi sahihi nikitamka bezik.
 
Liverpool wanaitamkaje "birthday" na London wanaitamkaje "birthday"?

muulize hernandez chicharito,mchezaji wa man u anavyopata shida kumwelewa wayne root ingawa yupo nae kwenye timu kwa miaka kibao
 
Back
Top Bottom