LBL: Pyramid Scheme Inayowatapeli Watu kwa Kisingizio cha Uwekezaji

LBL: Pyramid Scheme Inayowatapeli Watu kwa Kisingizio cha Uwekezaji

Status
Not open for further replies.

Mshangazi dot com

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
1,345
Reaction score
3,503
Kwanini watanzania wengi wanatapeliwa na Ponzi schemes kama LBL Tanzania?
Nini chanzo cha watu kutokupenda kufanya tafiti na kutafuta taarifa kabla ya kuinvest pesa.

Hakuna kampuni inayoitwa LBL Advertising Media LTD ambayo imesajiliwa Tanzania, ila kuna Kampuni yenye jina sawia imesajiliwa uingereza na raia wa marekani anaitwa Challis (see image). Hapa Tanzania kuna makampuni zaidi ya kumi yenye majina ya kufanana na hilo ambayo yamesajiliwa hivi karibuni. Kama kuna watu wa Brela humu wafanye uchunguzi yakinifu kuhusu uhusiano wa hizi kampuni.

TAHADHARI: Najua umeshawishiwa na kuona watu wanapata pesa, ila huu ni utapeli, kama umeweka pesa yako huko itoe chap, la sivyo soon utalambwa.

Nawasilisha!

Screenshot 2025-01-17 at 13.29.44.png
Screenshot 2025-01-17 at 13.39.13.png
Screenshot 2025-01-17 at 12.30.57.png

=====

Maelezo ya ziada kuhus utapeli unaofanywa na kampuni hiyo

Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko la makampuni yanayodai kutoa fursa za uwekezaji wa mtandaoni, lakini kwa uhalisia ni matapeli wa hali ya juu. Moja ya makampuni haya ni, ambalo limekuwa likiwahadaa watu kwa mfumo wa Pyramid Scheme — utapeli wa kifedha unaojificha chini ya kivuli cha uwekezaji.

LBL ni Pyramid Scheme, Si Uwekezaji wa Kweli
LBL linadanganya watu kuwa wanaweza kupata faida kubwa kwa kuwekeza kiasi kidogo cha pesa na kuwashawishi wengine kujiunga. Mfumo wake unategemea kusajili watu wapya ambao hulipa pesa zao kwa wale waliowatangulia badala ya kufanya biashara halali. Hii ni tabia ya kawaida ya Pyramid Scheme, ambapo faida inapatikana tu endapo watu wapya wataendelea kuingia kwenye mfumo.

Mbinu wanazotumia Kutapeli watu
  1. Ahadi za Faida Kubwa kwa Muda Mfupi — Wanadanganya kuwa unaweza kuongeza pesa zako kwa haraka bila juhudi yoyote.
  2. Motisha kwa Kusajili Watu Wengine — Ili upate “faida,” unalazimika kuwaleta watu wengine, jambo linalothibitisha kuwa si biashara halali.
  3. Matumizi ya Ushuhuda wa Uongo — Wanatumia video na picha za watu wakidai kuwa wamepata mafanikio, ilhali ni sehemu ya mbinu za kushawishi watu zaidi.
  4. Hakuna Bidhaa Halisi Inayouzwa — Biashara yoyote halali lazima iwe na bidhaa au huduma inayoeleweka. LBL haifanyi hivyo, inaendeshwa kwa mfumo wa mlolongo wa udanganyifu.
Kwa nini LBL ni Hatari?
  • Mfumo wake hudumu kwa muda mfupi kabla ya kuanguka na watu kupoteza pesa zao.
  • Walioko juu tu ndio hunufaika, lakini wanachama wapya huishia kulia baada ya kuliwa pesa zao.
  • Serikali nyingi zimekuwa zikifungia makampuni ya aina hii kwa sababu ni kosa la jinai kuendesha Pyramid Scheme.
USIJINGE! CHUKUA HATUA MAPEMA
Ikiwa umeshawahi kushawishiwa kujiunga na LBL, usiweke pesa zako hata kidogo. Ikiwa tayari umeshaingia, tafuta namna ya kutoka mapema kabla hujapoteza zaidi. Onyo watu wengine kuhusu utapeli huu ili tusiruhusu matapeli kuendelea kueneza hadaa zao.

View attachment 3225058
 
Hii ni pyramid scheme nzuri sana ukianza nayo itakapokufa utavukana sana Mimi binafsi Nimeanza nayo Kwa kuweka 1089k sasa Nina mwezi wa nne navuna 36000 kila siku ni almost 4.3 ikifa Leo sina hasara
 
Intern utakula zako elfu Tano....then ukitoka hapo utaambiwa uchague kiasi Cha kuwekeza kuanzia 50k Hadi 540k
Mimi sikushawishiwa na mtu niliona tangazo you tube nikasema ngoja nikaangalie Kuna Nini huko,,,nilivyomaliza intern nilivyoona nimepata 5k nikawa Sina habari nayo....wakawa wananilazimisha niitoe ....ilikaa km week 3 ndio nikaitoa nikajiunga bando....ila kilichonishangaza kwenye kutoa ela system haikuruhusu Moja Kwa Moja kutoa ela ni mpaka sijui nani aidhinishe.....nikawauliza km hii kampuni ni kubwa km mnavyosema ipo nje ya nchi na ndani ya nchi kwanini msiruhusu system yenyewe ikampa access mtu kutoa ela yake sijui bila kupitia sijui Kwa nani.....walivuojibu kwa ubabaifu nikazoom nikaona Hawa wasanii na Mimi mwenyewe msanii nikaachana nao....hio ilikuwa mwaka Jana kama mwezi wa nane ivi
 
Kwanini watanzania wengi wanatapeliwa na Ponzi schemes kama LBL Tanzania?
Nini channzo cha watu kutokupenda kufanya tafiti na kutafuta taarifa kabla ya kuinvest pesa.

Hakuna kampuni inayoitwa LBL Advertising Media LTD ambayo imesajiliwa Tanzania, ila kuna Kampuni yenye jina sawia imesajiliwa uingereza na raia wa marekani anaitwa Challis (see image). Hapa Tanzania kuna makampuni zaidi ya kumi yenye majina ya kufanana na hilo ambayo yamesajiliwa hivi karibuni. Kama kuna watu wa Brela humu wafanye uchunguzi yakinifu kuhusu uhusiano wa hizi kampuni.

TAHADHARI: Najua umeshawishiwa na kuona watu wanapata pesa, ila huu ni utapeli, kama umeweka pesa yako huko itoe chap, la sivyo soon utalambwa.

Nawasilisha!
Shortcut is always the longest way you were not going
 
Kwanini watanzania wengi wanatapeliwa na Ponzi schemes kama LBL Tanzania?
Nini channzo cha watu kutokupenda kufanya tafiti na kutafuta taarifa kabla ya kuinvest pesa.

Hakuna kampuni inayoitwa LBL Advertising Media LTD ambayo imesajiliwa Tanzania, ila kuna Kampuni yenye jina sawia imesajiliwa uingereza na raia wa marekani anaitwa Challis (see image). Hapa Tanzania kuna makampuni zaidi ya kumi yenye majina ya kufanana na hilo ambayo yamesajiliwa hivi karibuni. Kama kuna watu wa Brela humu wafanye uchunguzi yakinifu kuhusu uhusiano wa hizi kampuni.

TAHADHARI: Najua umeshawishiwa na kuona watu wanapata pesa, ila huu ni utapeli, kama umeweka pesa yako huko itoe chap, la sivyo soon utalambwa.

Nawasilisha!
HAHAHAHAHA hivi mtu ananunua udongo kwenye kijiko laki tano bado unaumiza kichwa kwa ajili yake kweli?? hebu tumia huo ubongo hata kukatia gogo wakati unapanga mipango ya jioni utafanya nini kwa maendeleo yako binafsi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom