Mateso ya magerezani yanawasaidia wafungwa kujirekebisha?

Mateso ya magerezani yanawasaidia wafungwa kujirekebisha?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Inasemekana, magereza ya Tanzania ni tofauti sana na ya Ulaya na nchi zingine "zilizostaarabika". Mfungwa wa Ulaya hukoseshwa uhuru tu wakati wa Tanzania hunyimwa karibia kila kitu: uhuru na mahitaji mengine muhimu ya kumwezesha kuishi kama binadamu wa kawaida.

Inasekana, magereza ya Tanzania ni kama mahali pa kuwakomolea watu. Kuna wafungwa wengi wanaodaiwa kufungwa kwa uonevu.

Inasemekana, magereza ya Tanzania hayazingatii haki za binadamu. Hata mfungwa anapowasili gerezani kwa mara ya kwanza, hukaguliwa kwa namna isiyozingatia utu. Huvuliwa nguo zote na kuamriwa kuruka kichura. Inamaanisha Serikali imeshindwa kununua vifaa vya kisasa vya kukagulia wafungwa kistaarabu?

Inasekana, magerezani kumejaa uonevu baina ya wafungwa na wafungwa, n.k.

Inasemekana, viongozi mbalimbali wameshatembelea magerezani na kusikiliza malalamiko ya wafungwa lakini malalamiko yao huwa kama yanayoishia hewani. Hayafamyiwi kazi.

Inasekana, mahalli wanakolala wafungwa ni pabaya sana. Magodoro ni machache kuliko idadi ya wafungwa.

Kwa ufupi, mbali na magereza kumpokonya mfungwa uhuru wake, jambo ambalo ni sahihi kama mahakama itajiridhisha kuwa anastahili hiyo adhabu, pia ni kama maeneo ya mateso.

Hayo mateso yanawasaidia wafungwa kujirekebisha au yanawafanya kuwa sugu?
 
Kwetu sisi ulimwengu wa tatu inaonesha haisaidii bali inaongeza tatizo.

Kuna shahidi kadhaa niwewahi zisikia zinazoonesha asilimia flani ya wahalifu wanaokamatwa, huwa ni wale waliotoka jera.

Hivyo, kwa nadharia hiyo, inaashiria huenda kule hawatendewi vema au hawapewi mafunzo chanya yanayojitosheleza.
 
Gerezani kubaya
Kule pasikie tu.
Unapangiwa muda wa Kulala na kujigeuza upande.
Dadeki kule usiende
Yote ayo kasolo muda wa kulala tu vingine vyote Sababu ni umasikini. Magereza yanaidadi kubwa ya wafungwa kuliko uwezo wa gereza.
 
Inasemekana, magereza ya Tanzania ni tofauti sana na ya Ulaya na nchi zingine "zilizostaarabika". Mfungwa wa Ulaya hukoseshwa uhuru tu wakati wa Tanzania hunyimwa karibia kila kitu: uhuru na mahitaji mengine muhimu ya kumwezesha kuishi kama binadamu wa kawaida...
Unaweza kuingia na hakili timamu ukaludi dishi na una weza kuingia dishi ukaludi timamu

Magereza yetu ni ya kinyama Sana huko nako ndiko mashoga huzaliwa
 
Japo uzi wako umetawaliwa na neno inasemekana ila nikuulize wewe swali rahisi tu,

Sikuombei mabaya ila mfano wewe ukifungwa na ukayakuta hayo mateso huko Jela,je utajirekebisha au utarudia tena kufanya makosa ili urudishwe huko tena?
 
Katika pitapita zangu siku moja nlikutana na afande mmoja mwenye "ka cheo" kidogo pale magereza.

Kwenye stori za hapa na pale nkawa nampa mtazamo wangu kua wafungwa wangetumiwa na serikali kama nguvu kazi in this essence; wapewe vile vibarua vinavyotokana na mirafi mbalimbali ya serikali mfano kutengeneza barabara n.k.

lakini, while at it, kama kibarua analipwa lets say 4000, bas buku iende serikalini, buku 2 irudi magereza kurekebisha mazingira ya wafungwa na buku awekewe mfungwa kwenye commisary yake imsaidie lets say kununua vitu kama sabuni, na pia hata ka mtaji siku atakayotoka ili apate pa kuanzia.

Yule jamaa bila aibu akaniambia, magereza ni sehem ya kurekebisha tabia na sio kumpa mtu mtaji au kumpa maisha bora.

Moyoni nkasema, hata wewe pia n mfungwa tu maana hata nyumba mnazokaa zimeoza lakn hamlalamiki.
Nkasepa zangu.
 
Wafungwa ni wengi kuliko facilities ilo haliepukiki. Kunagereza moja lipo Rwanda capacity ya gereza ni 400, mpaka sasa kunawafungwa 3450. Gereza limezidiwa mara 800%
Serikali iboreshe magereza kwanini kuwalaza wafungwa pamoja.
Au iangalie namna nyingine ya kuadhibu watu bila kuwapeleka wakaishi magerezani
 
Nguvu za wafungwa ni Aset kubwa Kwa Taifa letu!hasa JKT na jeshi la magereza!!

Walishe vizuri watibu magonjwa wapigishe kazi mchana na usiku muda wa kulala masaa matano tu ,muda wote kazi za uzalishaji!!

Watafungiwa JP's ili kuwamonitor watatembea mtaani kufanya kazi za usafi,kulima,kuuza kama machinga n.k!!

Wata suply maziwa kitaa na na mashuleni,maofisini kwa Bei ya kawaida!

Wata suplya nyanya vitunguu n.k

Wafungwa na jkt ni asset sana!!

Subirini niwe Rais wa Tanganyika nitawaonesha kazi ilivyo!!
 
Back
Top Bottom