Matibabu ya Lissu: Wasiojulikana na maswali yasiyojibika

Matibabu ya Lissu: Wasiojulikana na maswali yasiyojibika

Baija Bolobi

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2009
Posts
1,093
Reaction score
1,733
Nimekosa usingizi nikaamua nianzishe thread hii.

Tujiulize, hivi Spika Ndugai anaposema Tundu Lissu hawezi kuhudumiwa na bunge katika matibabu yake kwa sababu alikiuka taratibu za kwenda kutibiwa nje, ana msingi gani katika hoja yake, ikiwa:

- Baada ya Tundu Lissu kupigwa risasi na kufikishwa hospitali hadi kwenda Nairobi, alikuwa hajitambui wala kufanya maamuzi yoyote kuhusu maisha yake!!

- Je, anaadhibiwa kwa kupoteza fahamu?

- Ikiwa ni CHADEMA au familia yake walifanya maamuzi haya, kwani yanamhusu nini Lissu na haki zake ikiwa Chadema na Familia siyo wabunge? Kwa nini serikali isiwachukulie hatua Chadema na familia kwa kumtorosha mbunge wake bila ridhaa ya bunge/serikali?

- Nakumbuka kusoma salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais kwenda kwa Lissu na familia baada ya tukio; je kwa salaam hizo si Rais alitaka Lissu apone? Angeponaje bila kwenda hospitali?

- Nakumbuka mmoja wa madaktari waliomtibu Lissu Dodoma ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya. Kama Lissu angepelekwa DSM kama Ndugai anavyodai, si Katibu Mkuu huyu huyu ndiye angetoa kibali cha Lissu kwenda nje?

- Hivi hospitali ya Muhimbili ni majengo au ni wataalam ambao sasa ndo hawa waliomtibu Lissu huko Dodoma na bahati nzuri sasa Dodoma ndiyo DSM ya taifa?

- Kwanini serikali inaonekana kujibambikizia kesi hii mbaya mbele ya umma? Kumnyima matibabu, kukataa uchunguzi wa ndani na wa nje, kung'oa CCTV camera, kuzuia watu wasimuombee, kuzuia watu wasivae t-shirt za Lissu, kumtukana hata kama ni mgonjwa, n.k. Mbona hizi ni dalili za serikali yetu kujibambikizia kesi? Nilidhani mwenye jinai mjanja huwa anakuwa wa kwazna kufika kilioni.

- Kwanini serikali inalikuza mno suala hili? Kwa nini haijifunzi kutokana na historia, kwamba, mambo yaliyofumbiwa macho na serikali iliyopita, serikali hii imeyafukua na kuyachukulia hatua? Nani ataizuia serikali ijayo kuyafukua haya?
 
Baija, heading ingekuwa, matibabu ya Lissu, maswali yasiyojibika, na sio wasiojulikana!.

Kama ni kuwahusu wasiojulikana, wako wa aina mbili.
1. Wasiojulikana
2. 'Wasiojulikana'
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums
P.

Paskali, mwanzoni nilidhani na wewe huwajui "Wasiojulikana" na Wasiojulikana. Lakini nimeacha imani hiyo. Unawajua wote wa aina mbili na ndo maana unakimbilia kukosoa thread yangu badala ya kujikita na maswali niliyouliza. Na kisa cha serikali kukataa wachunguzi huru (wa nje au ndani), ni kwa sababu inajua kina Paskali tayari wanawajua waliohusika. Kuwajua si lazima ushiriki matendo yao, bali wako wanaowajua watu kwa kuwa victims wao kama wewe. Watu kama wewe mlipata fursa ya kukutana nao na kuonywa kutowasema. Ndo maana dana dana zako zimezidi sana. Kila wakati unaanzisha thread unazodai ni "nutro" ili "kunyutrolize" wenye kiu ya kuwajua.

Ndugu yangu Paskali, maisha ya mtu hayahitaji balancing, neutrality wala partisanship. Kuwa hivyo ni sawa na kuwa upande wa wasiojulikana. Haiwezekani kuwa watu hawa hawajulikani. Kuna aliyeagiza, aliyeona inaagizwa, aliyetekeleza, aliyeona inatekelezwa, na anayejifanya hakuona wala kusikia. Hawa ni wengi mno kuwaficha. Hata kama Tundu Lissu ni jambazi, mhaini, jangiri, na gaidi - angepelekwa mahakamani akahukumiwa na sote tukashuhudia akitundikwa risasi hadharani kulipia uovu wake.
 
kina Paskali tayari wanawajua waliohusika. Kuwajua si lazima ushiriki matendo yao, bali wako wanaowajua watu kwa kuwa victims wao kama wewe. Watu kama wewe mlipata fursa ya kukutana nao na kuonywa kutowasema. Ndo maana dana dana zako zimezidi sana. Kila wakati unaanzisha thread unazodai ni "nutro" ili "kunyutrolize" wenye kiu ya kuwajua.
😳😳😳😳
 
Ndugu yangu Paskali, maisha ya mtu hayahitaji balancing, neutrality wala partisanship. Kuwa hivyo ni sawa na kuwa upande wa wasiojulikana. Haiwezekani kuwa watu hawa hawajulikani. Kuna aliyeagiza, aliyeona inaagizwa, aliyetekeleza, aliyeona inatekelezwa, na anayejifanya hakuona wala kusikia. Hawa ni wengi mno kuwaficha. Hata kama Tundu Lissu ni jambazi, mhaini, jangiri, na gaidi - angepelekwa mahakamani akahukumiwa na sote tukashuhudia akitundikwa risasi hadharani kulipia uovu wake.
Hoja yako inafikirisha sana mkuu
 
Nimekosa usingizi nikaamua nianzishe thread hii.

Tujiulize, hivi Spika Ndugai anaposema Tundu Lissu hawezi kuhudumiwa na bunge katika matibabu yake kwa sababu alikiuka taratibu za kwenda kutibiwa nje, ana msingi gani katika hoja yake, ikiwa:

- Baada ya Tundu Lissu kupigwa risasi na kufikishwa hospitali hadi kwenda Nairobi, alikuwa hajitambui wala kufanya maamuzi yoyote kuhusu maisha yake!!

- Je, anaadhibiwa kwa kupoteza fahamu?

- Ikiwa ni CHADEMA au familia yake walifanya maamuzi haya, kwani yanamhusu nini Lissu na haki zake ikiwa Chadema na Familia siyo wabunge? Kwa nini serikali isiwachukulie hatua Chadema na familia kwa kumtorosha mbunge wake bila ridhaa ya bunge/serikali?

- Nakumbuka kusoma salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais kwenda kwa Lissu na familia baada ya tukio; je kwa salaam hizo si Rais alitaka Lissu apone? Angeponaje bila kwenda hospitali?

- Nakumbuka mmoja wa madaktari waliomtibu Lissu Dodoma ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya. Kama Lissu angepelekwa DSM kama Ndugai anavyodai, si Katibu Mkuu huyu huyu ndiye angetoa kibali cha Lissu kwenda nje?

- Hivi hospitali ya Muhimbili ni majengo au ni wataalam ambao sasa ndo hawa waliomtibu Lissu huko Dodoma na bahati nzuri sasa Dodoma ndiyo DSM ya taifa?

- Kwanini serikali inaonekana kujibambikizia kesi hii mbaya mbele ya umma? Kumnyima matibabu, kukataa uchunguzi wa ndani na wa nje, kung'oa CCTV camera, kuzuia watu wasimuombee, kuzuia watu wasivae t-shirt za Lissu, kumtukana hata kama ni mgonjwa, n.k. Mbona hizi ni dalili za serikali yetu kujibambikizia kesi? Nilidhani mwenye jinai mjanja huwa anakuwa wa kwazna kufika kilioni.

- Kwanini serikali inalikuza mno suala hili? Kwa nini haijifunzi kutokana na historia, kwamba, mambo yaliyofumbiwa macho na serikali iliyopita, serikali hii imeyafukua na kuyachukulia hatua? Nani ataizuia serikali ijayo kuyafukua haya?
Aisee
 
Wauwaji na muuaji mkuu tunawajua. Kwanza muuaji ni kichaa, kwahiyo hata mahakamani akifikishwa atasema yeye ni kichaa, na akipimwa naimani watamkuta na ukichaa. Tumuombee tu kwa Mungu Lissu.
 
Hili suala la Lisu litaanza kushughulikiwa rasmi magufuli "akitoka" madarakani. Sijatumia neno akimaliza muda wake manake wote tunajua kwamba anaweza kumaliza muda wake ila asitoke madarakani. Kwahiyo tumuombe Mungu ili magufuli atoke madarakani mapema
 
Back
Top Bottom