Matibabu ya Lissu: Wasiojulikana na maswali yasiyojibika

Matibabu ya Lissu: Wasiojulikana na maswali yasiyojibika

Paskali, mwanzoni nilidhani na wewe huwajui "Wasiojulikana" na Wasiojulikana. Lakini nimeacha imani hiyo. Unawajua wote wa aina mbili na ndo maana unakimbilia kukosoa thread yangu badala ya kujikita na maswali niliyouliza.
Mkuu Baija, nchi inaongozwa kama familia, hata wewe ukiwa nyumbani, kama mtoto wa kiume unaejitambua, siku mama yenu amesafiri kwenda kijijini kwao kusalimia, huku nyuma baba akaingiza mgeni, na ukamuona. Kumbe yule mgeni aliacha chumbani kwa baba nguo yeke fulani, bila baba kujua, ama kwa kusahau kwa bahati mbaya ama kwa makusudi ili mwenye nyumba ajue hayuko peke yake.

Mama aliporudi, kukaibuka ugomvi mkubwa kati ya baba na mama kuhusu hiyo nguo imetoka wapi na imeachwa na nani?.

Baba kamwambia mama hamjui mwenye nguo hiyo wala hajui imeingiaje,labda watoto au msichana wa kazi alijichanganya.

Kwa vile wewe uliona picha nzima, jee utamweleza mama ukweli wa ulichoona?.

Hiyo ndio essence ya wasiojulikana hawa
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Kama baba amesema hajui nguo imefikaje, who are you kusema imefikaje?.

Kama yule aliyemshikia Nape bastola naye hajulikani mpaka leo anatafutwa na polisi, what are the chances kuwabaini julikana wa Lissu?.

Wana familia bora, wanamwamini baba mwenye nyumba, hata kama wewe ulimuona mgeni wa baba, lakini hukumshuhudia wakati akiivua hiyo nguo na kuiacha uvunguni mwa kitanda chumbani kwa baba, hivyo kama baba kasema hajui, then it migh be true, baba hajui, na hiyo nguo iliachwa siku nyingi nyuma na mgeni mwingine ambaye hata wewe hukumuona.
P
Hivyo nilitoa angalizo hili
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Kwenye hili la kuwabaini wasiojulikana wa Tundu Lissu, serikali yetu imeshindwa, nilisema humu, kwa vile tupo watu wenye uwezo kuisaidia serikali yetu iweze kuwabaini, nikauliza jee tujitolee tuu kuwabaini na kuwataja, kuisaidia serikali yetu au tuisubiri, serikali iseme imeshindwa ndipo isaidiwe?.

WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums

P .
 
Nimekosa usingizi nikaamua nianzishe thread hii.

Tujiulize, hivi Spika Ndugai anaposema Tundu Lissu hawezi kuhudumiwa na bunge katika matibabu yake kwa sababu alikiuka taratibu za kwenda kutibiwa nje, ana msingi gani katika hoja yake, ikiwa:

- Baada ya Tundu Lissu kupigwa risasi na kufikishwa hospitali hadi kwenda Nairobi, alikuwa hajitambui wala kufanya maamuzi yoyote kuhusu maisha yake!!

- Je, anaadhibiwa kwa kupoteza fahamu?

- Ikiwa ni CHADEMA au familia yake walifanya maamuzi haya, kwani yanamhusu nini Lissu na haki zake ikiwa Chadema na Familia siyo wabunge? Kwa nini serikali isiwachukulie hatua Chadema na familia kwa kumtorosha mbunge wake bila ridhaa ya bunge/serikali?

- Nakumbuka kusoma salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais kwenda kwa Lissu na familia baada ya tukio; je kwa salaam hizo si Rais alitaka Lissu apone? Angeponaje bila kwenda hospitali?

- Nakumbuka mmoja wa madaktari waliomtibu Lissu Dodoma ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya. Kama Lissu angepelekwa DSM kama Ndugai anavyodai, si Katibu Mkuu huyu huyu ndiye angetoa kibali cha Lissu kwenda nje?

- Hivi hospitali ya Muhimbili ni majengo au ni wataalam ambao sasa ndo hawa waliomtibu Lissu huko Dodoma na bahati nzuri sasa Dodoma ndiyo DSM ya taifa?

- Kwanini serikali inaonekana kujibambikizia kesi hii mbaya mbele ya umma? Kumnyima matibabu, kukataa uchunguzi wa ndani na wa nje, kung'oa CCTV camera, kuzuia watu wasimuombee, kuzuia watu wasivae t-shirt za Lissu, kumtukana hata kama ni mgonjwa, n.k. Mbona hizi ni dalili za serikali yetu kujibambikizia kesi? Nilidhani mwenye jinai mjanja huwa anakuwa wa kwazna kufika kilioni.

- Kwanini serikali inalikuza mno suala hili? Kwa nini haijifunzi kutokana na historia, kwamba, mambo yaliyofumbiwa macho na serikali iliyopita, serikali hii imeyafukua na kuyachukulia hatua? Nani ataizuia serikali ijayo kuyafukua haya?
Mkuu maswali yako ni magumu katika kipindi hiki tunachopitia.
 
Sawa mkuu P.
Sasa hapo ndipo 'u-nutro' unapoondoka.
Kuomba nisiulizwe kuhusu jambo fulani, hakuondoi neutrality yangu, kwa sababu neutrality inapaswa iwe visible, na sisi waandishi tunapaswa kuwa impartial wakati wote, kwa sababu impartiality ni moja ya misingi ya maadili ya fani yetu, msingi mkuu ni truthfulness, objectivity, impartiality na balancing.
P
 
Ivi unajua kilichomkuta boby wine? Alipotaka kwenda usa kwa matibabu unajua serikali ilimzuia? Kwann cctv zilitolewa? Mpaka hapa hujamjua muhusika ni nani??

Naomba nikuulize...

Ivi hao wasiojulikana wangempiga magu walau risasi mbili unadhan wasingekua wamekamatwa mpaka leo?

Kwa kifupi muhusika mkuu ni JIWE na alitaka lissu aondoke duniani, sasa iweje aruhusu atibiwe?
 
Hapa ndipo chanzo cha watu tunaofahamu msimamo wako wa awali tunakubaliana kabisa kwamba umetiishwa na umetii na imebakia kujiita uko neutral in reality, inasikitisha sana.
Kwa vile ya Dodoma niliomba niyaache, tuyaache. Msimamo wa mtu hukaa ndani yake, na hakuna anayejua msimamo wa mtu yoyote kuliko yeye mwenyewe, mimi naendelea kusisitiza humu kuwa niko neutral nikiegemea kwenye ukweli siku zote.

Kitu ambacho nakiri, ni kuwa pia sio kila ukweli nitausema, najifanyia self censorship ukweli huu ndio usemwe na ukweli mwingine is best if kept out kwa kutokusemwa.
Swali la Morality: Je ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa? - JamiiForums
P
 
Miongoni mwa mambo ambayo Serikali hii imefeli kwa asilimia zote, mojawapo ni hili shambulio la Lissu.

Wenye akili hapa mtameza tu bila kuhitaji kutafuniwa sana.
 
Imefeli sana kwa sababu haijakubali kusikiliza mawazo, maoni, ushauri wa watu tofauti kuhusu jambo hili.

Ni kweli serikali inashindwa kujinasua kwenye hii lawama?

Hapo ndipo ilipofeli, na hadi muda huu ni vigumu kujinasua kwenye hii lawama.

Kuna mdau hapo juu kagusia kuwa, hata kama ni mhalifu ni vyema uwahi/uwe wa kwanza kufika kwenye mazishi na uwe wa kwanza kushirikiana na wahanga ili uweze kuwapoteza wale wote wanaoweza kukudhania kuwa wewe ndio adui.

Badala yake imekuwa kinyume kabisa kwa serikali kuhusu hili jambo ambapo ndio inajichimbia kwenye shimo la lawama na sasa kina kishakuwa kirefu, kuibuka kwenye hiki kina na kuwa safe ni majaliwa.
 
pascal bwana mwachie thread yake
Kidu, kwani kuna mtu ameshika thread ya mtu?. Kwa sasa, issue ya matibabu ya Lissu, has nothing to do na wasiojulikana, it had hapo mwanzo, na kumpeleka Nairobi, was the right thing. Lakini from Nairobi to Belgium is something else na Bunge kutomtibia is something tena.
P
 
Ha ha pasco anajibu kupitia thread zake, sawa kabisa
 
Nimekosa usingizi nikaamua nianzishe thread hii.

Tujiulize, hivi Spika Ndugai anaposema Tundu Lissu hawezi kuhudumiwa na bunge katika matibabu yake kwa sababu alikiuka taratibu za kwenda kutibiwa nje, ana msingi gani katika hoja yake, ikiwa:

- Baada ya Tundu Lissu kupigwa risasi na kufikishwa hospitali hadi kwenda Nairobi, alikuwa hajitambui wala kufanya maamuzi yoyote kuhusu maisha yake!!

- Je, anaadhibiwa kwa kupoteza fahamu?

- Ikiwa ni CHADEMA au familia yake walifanya maamuzi haya, kwani yanamhusu nini Lissu na haki zake ikiwa Chadema na Familia siyo wabunge? Kwa nini serikali isiwachukulie hatua Chadema na familia kwa kumtorosha mbunge wake bila ridhaa ya bunge/serikali?

- Nakumbuka kusoma salaam za pole kutoka kwa Mheshimiwa Rais kwenda kwa Lissu na familia baada ya tukio; je kwa salaam hizo si Rais alitaka Lissu apone? Angeponaje bila kwenda hospitali?

- Nakumbuka mmoja wa madaktari waliomtibu Lissu Dodoma ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya. Kama Lissu angepelekwa DSM kama Ndugai anavyodai, si Katibu Mkuu huyu huyu ndiye angetoa kibali cha Lissu kwenda nje?

- Hivi hospitali ya Muhimbili ni majengo au ni wataalam ambao sasa ndo hawa waliomtibu Lissu huko Dodoma na bahati nzuri sasa Dodoma ndiyo DSM ya taifa?

- Kwanini serikali inaonekana kujibambikizia kesi hii mbaya mbele ya umma? Kumnyima matibabu, kukataa uchunguzi wa ndani na wa nje, kung'oa CCTV camera, kuzuia watu wasimuombee, kuzuia watu wasivae t-shirt za Lissu, kumtukana hata kama ni mgonjwa, n.k. Mbona hizi ni dalili za serikali yetu kujibambikizia kesi? Nilidhani mwenye jinai mjanja huwa anakuwa wa kwazna kufika kilioni.

- Kwanini serikali inalikuza mno suala hili? Kwa nini haijifunzi kutokana na historia, kwamba, mambo yaliyofumbiwa macho na serikali iliyopita, serikali hii imeyafukua na kuyachukulia hatua? Nani ataizuia serikali ijayo kuyafukua haya?
Huu ukoo wa wauwaji hawana uwezo wa kujibu maswali haya....
Kinachonishangaza zaidi ni hii hali inayojidhihirisha kuwa hata ndani ya mifumo yetu ya kiusalama hakuna watu wanaosimamia na kuamini katika haki. Maana kama wapo hata wachache, wanapaswa kuanza angalau hata kidogokidogo kufagia huu uozo uliotamalaki katika nchi yetu.
 
Kidu, kwani kuna mtu ameshika thread ya mtu?. Kwa sasa, issue ya matibabu ya Lissu, has nothing to do na wasiojulikana, it had hapo mwanzo, na kumpeleka Nairobi, was the right thing. Lakini from Nairobi to Belgium is something else na Bunge kutomtibia is something tena.
P
Hapo unaonekana un Derail-spin. Uko powerful such that wasomaji watahamia kwako, wakati mtoa mada research yake itakosa data.
 
Nadhani amemumiss mno bungeni na siku akitia mguu pale bungeni kiti kitakuwa cha moto
 
Mimi sijitahidi kuwa neutral bali niko neutral in reality!.
P
Pascal Mayalla unadhani kuwa neutral ni jambo sahihi katika maisha? Kuna wakati unaweza kuwa neutral ikiwa haki imetawala katika mchezo. Katika mazingira ambayo haki hakuna unapokuwa neutral ni sawa na kukubali ayafanyayo huyo anayeinajisi haki na hiyo ni sawa na kuwa upande wake. Katika mazingira ambayo simba anamtesa swala, unaposema upo neutral lazima swala atakulaumu kuwa umechagua upande wa mtesi wake. Najua una psychic power, unaweza kutusaidia yale tusiyoyaona kwa macho yetu ila hii neutrality yako mimi siielewi mkuu.
 
Back
Top Bottom