Matokeo Law School yafanyiwa ukarabati

Matokeo Law School yafanyiwa ukarabati

Watu wamekuwa vilaza. Tuache kulalamika.
Vilaza LST ila vipanga vyuo watokavyo? Hebu fikiri kwa sauti....angalia hoja za wahanga hao na sio jibu la pamoja lisilo na msingi kwa malalamiko tajwa
 
Safari ya kudai haki haijawahi kuwa rahisi.

Tulipo kumeundwa tume ambayo composition yake ni suala jingine.

Cha kushangaza kutokea kwenye website ya matokeo ya LST cohort 33 kuna ukarabati mpya!

Awali kulikuwa na cases za marks dash (-) kwenye somo moja mtu kafaulu na dash (-) kwenye somo jingine mtu kafeli.


View attachment 2385998

Maajabu ya Mussa. Ghafla na punde tu, wamebadilisha!

Sasa hivi kwenye dash (-) mtu kafeli wamebadili kwa kuindoa dash na kuwa "F". Hii ni mpya!

View attachment 2386000

Bila shaka wangali wana shauriana cha kufanya kwenye dash (-) mtu kafaulu iweje.

Tunaendelea ku monitor kila hatua wanayofanya.

Hili, hadi mbivu na mbichi zijulikane.

Watanzania hasa wanafunzi wanapenda dezo sana na mteremko sana! Watu wamefeli badala wajipange kurudia mitihani wanakwenda kushitaki kwa wanasiasa !

Hivi hata form four wakiwa wanafeli hatutashangaa wakilalamika na ikaundwa tume!

Wanasiasa wanataka watu wajinga wajinga wasio na vigezo mtaani ili wawatawale vizuri......
 
Watanzania hasa wanafunzi wanapenda dezo sana na mteremko sana! Watu wamefeli badala wajipange kurudia mitihani wanakwenda kushitaki kwa wanasiasa !

Hivi hata form four wakiwa wanafeli hatutashangaa wakilalamika na ikaundwa tume!

Wanasiasa wanataka watu wajinga wajinga wasio na vigezo mtaani ili wawatawale vizuri......

Kwani wewe ni mmoja wa wanafunzi hao?

Miaka nenda rudi malalamiko haya yapo.

Wewe hujawahi kusikia wanafunzi kufelishwa?
 
Hao walimu wamekuwa wakifanya mambo ya hovyo makusudi kuwakomoa wanafunzi, wakijua hakuna mwanafunzi atakayelalamika kwani matokeo mabaya yamekuwa ndio tabia yao miaka yote.

Sasa haya malalamiko ya wakati huu ndio yamewaamsha usingizini, hawakutegemea; matokeo yake wanakurupuka kufanya jambo bila kujua jambo hilo hilo walishalifanya mwanzo tofauti, hawa wanazidi kujitega.

Huu ni uthibitisho mwingine usioacha shaka, matokeo ya wanafunzi hapo LST huchezewa kwa makusudi na walimu wajuaji wasiojali, huku kisingizio chao siku zote kikiwa wanafunzi walipotoka hawakuandaliwa vizuri.

Ikiwa wanafunzi ambao ni wafanyakazi wa taasisi za umma wakiongoza kwa ufaulu, sijui wao waliandaliwa vizuri vyuo gani walipotoka tofauti na wanafunzi wengine wa hapo LST.

NI kawaida kwa waonevu kudhani maisha yataendelea hivyo hivyo Hadi kurudi Messiah mara ya pili. Wasijue hayapo marefu yasiyokuwa na mwisho.
 
Mkuu nawashauri endeleeni kupambania suala hili, naamini litasaidia sana hata katika vyuo vingine ambapo lecturers huwa na imani ya kushikilia hatma ya maisha ya wanafunzi wao.

Aluta continua na kelele za chura ni nadra kumteteresha mtu.
 
Back
Top Bottom