kalukamise
JF-Expert Member
- May 4, 2011
- 683
- 191
Public sympathy kwa kitu gani ambacho kakifanya against public interest? Kwani hatua walizochukuliwa public inaona hazikustahili? Ni kama umemuattack huyu mama bure. Kwa logic sioni kama kuna lolote kakosea. Watoto wamechemka, tatizo linajulikana limeanzia serikalini na walimu wake thats all.
pokea like zangu miaPasco hivi NECTA kazi yao ni kufundisha au kutaini wanafunzi? Ukiangalia vyombo vyote vya habari vinaiangalia NECTA kama wao ndio wenye sababu ya wanafunzi kufeli bila kuangalia nani mwenye wajibu wa kuwaandaa wanafunzi hao yaani Commissioner wa elimu. NECTA walaumiwe kama walitunga mtihani ambao hautokani na "syllabus" inayotumika.
gfsonwin, amini huyu Pasco analo lake binafsi juu ya maneno yake. hoja yake nitaikubali ikiwa tu serikali kupitia wasimamizi wa mitaala ya elimu ya sekondari wakisema kuwa baraza la mitihani lilitunga mtihani ambao haukufanan na walichopaswa/ takiwa kitunga. huyu Pasco anachanganya mambo, eti ni kosa kwa CEO wa baraza la mitihani kuingia na script ya mtahiniwa kwenye chombo cha habari eti alitakiwa kuja na copy, kwani ameacha original pale TBC?.. na anaposema ni siri siri ikiwa kwanani? anataka kutuambia CEO wa baraza la mitihani hatakiwi kushika original scripts za watahiniwa?. hawa wanao lalamika leo kuwa ndalichako a-resign walishindwa kuelewa umuhimu wa madai ya mbatia juzi kuwa Tanzani haina mtaala mmoja uliopitishwa kwaajili ya elimu. walikaa kimya. leo ndo wanajona wanauchungu .. uchungu wanautoa wapi?. hivi ikiwa mtaala walio nao baraza , ni tofauti na wewe gfsonwin unachofindishia, tena tofauti na ule mimi kindimbajuu ninaofundishia huku kiraracha . sasa huu mtihani utakao tungwa na baraza wanafunzi watafaulu vipi? kwamaana hata waliofaulu ni wamefaulu kwa kubahatisha .: haya matokea yalikuwa tayari zaidi ya wiki na ndo yamemfanya Mushi ajihuzuru kule taasisi ya elimupokea like zangu mia
mkuu tatizo la watanzania ni akili fupi na mitazamo yetu ya maneno mengi kumbe pumba tupu.
yaani watu wanaona kwamba NECTA ndiye mkosaji waksahau NECTA ni test administrator tu ambaye hausiki kwa lolote lile zaid ya kuatibu mitihani bad enough hata watunzi wa mitihani sio wao ni waalimu wenyewe, na hata kusahihisha ni waalimu wenyewe kuhusu kuyapanga ni jopo la mratibu wa elimu tena kulingana na matokeo ya usahihishaji sasa hapa necta inahusika vipi??
tena kwa ujinga na umbumbu wetu, eti mtu anasema mama ndalichako anatafuta public sympathy ...................my foot kwa kitu gani??
wakaulize ofisi ya maktaba inaidhinisha vitabu vyenye ubora gani kwa hawa wanfunzi, waulize mamlaka ya elimu inaratibu vipi ubora wa elimu wa taifa hili kuanzia kwenye mitaala hadi uwezeshwaji kisera. waulize wizara ahusika inasmamia vipi ubora wa elimu y nchi hh kuanzia kwenye miundo mbinu hadi malipo kwa watumish waalimu.
mamlaka ya elimu inachangisha sh ngapi kwa mwaka?? je imewah kusema inatrain waalimu wawe bora?? kuna kozi gani ambazo mwl anakwenda za capacity building zaid ya kukalia ujuzi aliofundishwa na pro Mbise na Katabaro toka akiwa chuo?? tizama mabadiliko ya kisayansi je yanakuwa kulingana na elimu yetu?? je nani anayejali??
kiukweli serikali inamengi ya kujibu hapa, mtihani wa biology ndo kabisaa wanafunzi hawajaufanya wengi wao walitoka kwa kukusanya karaatasi bila kujaza, wakachora na messi wafikiri Necta hapa inahusikaje??
serikali irudi kwa waalimu ituulize tatizo ni nini nasi tutawaambia tatizo lilipo.
Upo sahihi kabisa mimi siku naamini kabla ya kutupia lawama Serikali na Walimu lazima tuangalie Wazazi na Wanafunzi wamefanya nini? sio siri utandawazi umetumaliza sana tena sana, Wazazi wamewaacha tu watoto wafanye wanavyotaka, kila siku watoto wanashinda kwenye mitandao, mwalimu anafundisha dent anasikiliza mziki kwenye simu.
Nachokiamini mimi hata serikali iwalipe walimu mshahara wa milioni, na hata walimu wafundishe namna gani kama Wanafunzi na wazazi wataendelea na life style ya kujiachia tusitegemee kabisa elimu ya nchi hii kupanda.
Miaka ya tisini na mwanzoni mwa miaka ya 2000 hakukuwa na walimu wengi kama ilivyo sasa lakini ufaulu ulikuwa mzuri tu, mimi nimesoma advance shule ambayo haikuwa na mwalimu hata mmoja lakini katika darasa letu hakuna aliyefeli kwa kuwa tulikuwa tunajituma wenyewe bila kutegemea mwalimu wala serikali
sitegemei TBC kummuhoji lolote kwa manufaa ya taifa!sanasana anauza sura tu.kama ana guts aje hapa JF kwenye wananchi wenye ujuzi wa mambo!