MATOKEO ya Kidato cha Nne a mjadala wa kuboresha Kufaulu

MATOKEO ya Kidato cha Nne a mjadala wa kuboresha Kufaulu

Mwaka jana mlisema hivohivo..vijana zaidi ya asilimia 70 walipata Div 0 na IV.
 
Hii ni aibu kwa taifa la Tanzania na wananchi wake kuwa na tabaka la watu wenye Elimu na uelewa wa namna hii!. Je, ni kweli shule za Kata ndo chanzo cha yote haya!!!! au walimu wa VODA FASTA ndo chanzo cha haya! au zamani watu walikuwa wakiiba sana mitihani na mwaka huu wamezibitiwa wizi??? au morali ya waalimu haipo katika suala zima la ufundishaji kama ilivyokuwa enzi zile hasa kwa shule za Serikali????
Maswali haya na mengine yanahitaji majibu na ufumbuzi, Tutafute suluhisho la hili, Nini kifanyike kuondokana na tatizo hili???.
Hapo chini ni Matokeo hayo kwa kifupi yakionyesha Idadi kwa kila daraja na asilimia zake.

Daraja I - 5,363 1.5% Daraja la II 9,942 Asilimia 2.8% Daraja la III 25,083 Asilimia 7.1% Daraja la IV 136,633 Asilimia 38.9% Daraja la 0 174,193 Asilimia 49.6% na Jumla ya wanafunzi 351,214 walifanya mtihani huo.
NB: Kwa kifupi, Daraja la Kwanza hadi la Tatu ni asilimia 11.5 tu na madaraja ya Nne na la Zero (o) yanachukua asilimia 38.9 na aslimia 49.6 sawia. Hii inaashiria nini kwa Taifa la Tanzania?? na hata
Waziri wa elimu sijasikia akitoa tamko na wala Mhe. Dr. Dr. Jk yuko inje ya nchi wala hashitushwi na hali hii anaona ni kawaida tu! Kwani Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana kwa mfumo huu wa kuwa na tabaka la watu wa aina hii ambao watakuja kuwa Madaktari Mhimbili, Bugando, KCMC na watakuwa Specilist wa Ubongo na mifumo ya fahamu!!!!.​

Nakumbuka mwaka jana Prof. Maghembe alijinadi kwamba shule za kata zinaongoza kwa kufanya vizuri! sasa hali halisi ndio inaonekana. hii ni kutokana na kuwekeza katika ujinga na ubangaizaji, badala ya kuwekeza katika maendeleo ya kweli ya elimu. project nzima ya elimu imekaa kibabaishaji. na ukiikosoa serikali inakuja juu. siku zote Haki elimu imekuwa at loggerheads na serikali, kisa wanakosoa mno! Interest ya serikali sio kuleta maendeleo ya kweli ya elimu, bali kujikusanyia sifa - sijui za nini.

ukiangalia shule za kata, project ile ilikuwa ni ya voda fasta, ili mafanikio yaonekane JK akiwa madarakani. hakuna kitu kama hicho. mafanikio ya kweli ya elimu yangeanza kuonekana kuanzia miaka 5 na kuendelea. yaani kama JK angekuwa serious katika elimu toka awamu ya kwanza, sasa hivi ndio tungeanza kuona matunda, kidogo kidogo. lakini yeye anataka matokeo palepale. sawa tu na katika mpira. badala ya kuleta mabadiliko ya kweli ya football kwa kuanzia kuwekeza kwa vijana wa umri mdogo, anatumia gharama kubwa sana kwa timu iliyopo sasa ili avune sifa zake.

Unashangaa JK yupo kimya? siku hizi amegundua ka mtindo. anaminya kimyaa. si umeona la Dowans?
 
Shule za Msingi za serikali sasa hivi ni mbaya mno kitaaluma, kimazingira. Tusitarajie miujiza watoto hawa wanapofika sekondari ambako nako hali ni hiyohiyo. Acheni watu wafanye biashara ya ELIMU kwanza.
 
Inabidi shule binafsi zifutwe...

@ Tuko, Sioni kama hilo linaweza kuwa suluhisho! Mie hapa kwenye hoja yako hiyo kama shule za binafsi zinafaulisha kuliko serikali ni kwa nini?? je zinawaalimu ambao wako motivated!!, mazingira ya kusoma na kufundishia yako condusive, na mambo mengine kibao!. Lakini je Shule za Kata au Serikali zinawaalimu???, zina mazingira condusive kama ya shule za private???, au kama ni mishahara private wanapesa nyingi kuliko serikali!!???. Kufuta shule hizo hakuwazi kuwa suluhisho.
Kwani mkono wako ukijaa au ukashika mavi unaukata au unausafisha na kuendelea na kazi zake??
 
Sababu za kufeli zipo nyingi kama walivyosema wenzetu. Lakini jambo moja la msingi ni kuwa hizo shule za KATA ambazo zimechangia sana kufeli HAZIKUWA NA WALIMU. Kuna baadhi ya maeneo tumepata taarifa za vyombo vya habari kuwa kulikuwa na mwalimu MMOJA, WAWILI, AU WATATU TU. Tulitegemea nini katika mazingira kama hayo? Jambo la pili ni kuwa hao walimu wa shule za kata walikuwa ni wale WASIO NA UJUZI. Wengi wao walipata mafunzo ya miezi mitatu ambayo hata English Course mwanafunzi angekuwa hajafaulu bado.

Matatizo hayo chanzo chake ni kwenye awamu ya TATU YA BWANA BEN. Ben alikuwa mpango wa MEM wa shule za msingi bila kujua kama shule hizo baadaye zitakuja kutoa wanafunzi wa SEKONDARI. Walimu walipaswa kuandaliwa na awamu ya Mkapa ili watumike kwenye serikali ya awamu ya NNE ya JK junior. Tunazalisha taifa la walioshindwa, taifa watu wasioweza na hilo ni JANGA jipya kwetu wenyewe maana tunaanda vijana watakao kuja kuleta matatizo kwenye jamii yetu. TUNAANDAA KUFELI KWA TAIFA ZIMA!
 
.....
ukiangalia shule za kata, project ile ilikuwa ni ya voda fasta, ili mafanikio yaonekane JK akiwa madarakani. hakuna kitu kama hicho. mafanikio ya kweli ya elimu yangeanza kuonekana kuanzia miaka 5 na kuendelea. yaani kama JK angekuwa serious katika elimu toka awamu ya kwanza, sasa hivi ndio tungeanza kuona matunda, kidogo kidogo. lakini yeye anataka matokeo palepale. sawa tu na katika mpira. badala ya kuleta mabadiliko ya kweli ya football kwa kuanzia kuwekeza kwa vijana wa umri mdogo, anatumia gharama kubwa sana kwa timu iliyopo sasa ili avune sifa zake.

Unashangaa JK yupo kimya? siku hizi amegundua ka mtindo. anaminya kimyaa. si umeona la Dowans?

Sie kama sehemu ya jamii, hatuwezi kumuachia JK na mrithi wake KAWAMBWA watuletee mageuzi ya ELIMU Tanzania tunahitaji kufanya kazi ya ZIADA! ikibidi kufanya hayo yanayofanywa na nchi za Kiarabu TUNISIA na EGPTY kwa sasa, taifa hili ni letu na tutaendelea kuwepo hapa mpaka mwenyezi mungu atuchukue! then tunahitaji kufanya maamuzi a firm decision on what do we need our education should be like na si vinginevyo.
 
Najiuliza sipati majibu
- Shule za kata zinasimamiwa na Wizara ya Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa
-Shule za zamani kama azania, tambaza, ilboru, msalato, etc the like, zinasimamiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi stadi
-Baraza la mitihani linasimamiwa na wizara ya elimu

Kituko kingine
Mfano DAR ES SALAAM
-Shule za secondary za kata na zile rasmi za zamani (za o-level tu) nyingi mno. pengine zaidi ya 30- kupitia MEMM wamejenga shule nyingi sana za O-level, chanika almost kila street in shule ya kata.
-High school zilizopo ukiondoa Kibasila zote ni zile zile zilizoko eneo la upanga - Jangwani, Zanaki, Azania, Tambaza.


Katika hali hii, kama nilivyo wasikia watu wakihoji, Je baraza la mitihani linaweza kuwa fair katika kutoa alama kati ya shule za kata (zisizo na vifaa na walimu waliobobea na zilizo chini ya Tamisemi) na shule za secondary zilizo chini ya wizara ya elimu ilhali yenyewe iko chini ya wizara hiyo hiyo?

Kwa nini serikali isijenge angalau high school mbili au moja iliyokamilika kila wilaya?
Nakubaliana na wazo hilo badala ya kujenga mashule katika kila kata kungekua na shule kubwa na zenye madarasa ya kutosha katika kila wilaya au TARAFA hii ya kila kata naona kwa nchi yetu bado itasumbua sana hasa kwa suala la miundo mbinu upatikanaji wa waalimu pamoja na maabara na vifaa vya maabara pia fedha za kuziendeshea hizi shule kwasababu kutakua hakuna faida yeyote mmejenga shule nyingi halafu wanafunzi wanafeli kwa kuwa shule hazina waalimu na hazijitoshelezi kimiundombinu pia kipato cha waalimu ni kidogo na hawana nyumba za kuishi serikali ingekaa chini na kuliangalia upya hilo either wabadilishe mfumo kwenda kwenye tarafa au wilaya wajenge shule kwa level hiyo!
 
Sababu za kufeli zipo nyingi kama walivyosema wenzetu. Lakini jambo moja la msingi ni kuwa hizo shule za KATA ambazo zimechangia sana kufeli HAZIKUWA NA WALIMU. Kuna baadhi ya maeneo tumepata taarifa za vyombo vya habari kuwa kulikuwa na mwalimu MMOJA, WAWILI, AU WATATU TU. Tulitegemea nini katika mazingira kama hayo? Jambo la pili ni kuwa hao walimu wa shule za kata walikuwa ni wale WASIO NA UJUZI. Wengi wao walipata mafunzo ya miezi mitatu ambayo hata English Course mwanafunzi angekuwa hajafaulu bado.

Matatizo hayo chanzo chake ni kwenye awamu ya TATU YA BWANA BEN. Ben alikuwa mpango wa MEM wa shule za msingi bila kujua kama shule hizo baadaye zitakuja kutoa wanafunzi wa SEKONDARI. Walimu walipaswa kuandaliwa na awamu ya Mkapa ili watumike kwenye serikali ya awamu ya NNE ya JK junior. Tunazalisha taifa la walioshindwa, taifa watu wasioweza na hilo ni JANGA jipya kwetu wenyewe maana tunaanda vijana watakao kuja kuleta matatizo kwenye jamii yetu. TUNAANDAA KUFELI KWA TAIFA ZIMA!

Mzalendo mkuu unasema kweli! na ni kweli tupu
 
@ Tuko, Sioni kama hilo linaweza kuwa suluhisho! Mie hapa kwenye hoja yako hiyo kama shule za binafsi zinafaulisha kuliko serikali ni kwa nini?? je zinawaalimu ambao wako motivated!!, mazingira ya kusoma na kufundishia yako condusive, na mambo mengine kibao!. Lakini je Shule za Kata au Serikali zinawaalimu???, zina mazingira condusive kama ya shule za private???, au kama ni mishahara private wanapesa nyingi kuliko serikali!!???. Kufuta shule hizo hakuwazi kuwa suluhisho.
Kwani mkono wako ukijaa au ukashika mavi unaukata au unausafisha na kuendelea na kazi zake??

Mtoto wa mwalimu anasoma private, mtoto wa mwenyekiti wa bodi ya shule anasoma private, mtoto wa diwani anasoma private, mtoto wa afisa mtendaji (kata) anasoma private, mtoto wa katibu tarafa anasoma private, mtoto wa afisa elimu, na wa mkuu wa wilaya, na wa mkurugenzi wanasoma private. Watoto wa wakurugenzi wote wizarani, wa katibu mkuu, wa makamishna, na wa waziri, wanasoma private.

Kikao kinafanywa na hawa 'wadau' wa elimu kuboresha shule za serikali. Unadhani zaidi ya kuongea, utekelezaji na ufuatiliaji utakuwepo hapo? Fikiria kuwa watoto wa 'wadau' hawa wangekuwa wanasoma kwenye hizi shule zisizo na madawati, vitabu wala walimu, huoni wangeguswa kidogo kuziboresha. Ongea na mwalimu yeyote wa primary au sekondari leo, anakuambia mi sina mda wa kufatafata mitoto ya watu, aandike asiandike, afaulu asifaulu, shauriyake. Ukimuuliza na mwanao je, anasema mwanangu anasoma St nini sijui. Uzalendo haupo. Shule za private zifutwe, tubanane humohumo. watoto wetu sisi walalahoi wakalie tofali moja na watoto wa waziri.
 
Hii ni aibu kwa taifa la Tanzania na wananchi wake kuwa na tabaka la watu wenye Elimu na uelewa wa namna hii!. Je, ni kweli shule za Kata ndo chanzo cha yote haya!!!! au walimu wa VODA FASTA ndo chanzo cha haya! au zamani watu walikuwa wakiiba sana mitihani na mwaka huu wamezibitiwa wizi??? au morali ya waalimu haipo katika suala zima la ufundishaji kama ilivyokuwa enzi zile hasa kwa shule za Serikali????
Maswali haya na mengine yanahitaji majibu na ufumbuzi, Tutafute suluhisho la hili, Nini kifanyike kuondokana na tatizo hili???.
Hapo chini ni Matokeo hayo kwa kifupi yakionyesha Idadi kwa kila daraja na asilimia zake.

Daraja I - 5,363 1.5% Daraja la II 9,942 Asilimia 2.8% Daraja la III 25,083 Asilimia 7.1% Daraja la IV 136,633 Asilimia 38.9% Daraja la 0 174,193 Asilimia 49.6% na Jumla ya wanafunzi 351,214 walifanya mtihani huo.
NB: Kwa kifupi, Daraja la Kwanza hadi la Tatu ni asilimia 11.5 tu na madaraja ya Nne na la Zero (o) yanachukua asilimia 38.9 na aslimia 49.6 sawia. Hii inaashiria nini kwa Taifa la Tanzania?? na hata
Waziri wa elimu sijasikia akitoa tamko na wala Mhe. Dr. Dr. Jk yuko inje ya nchi wala hashitushwi na hali hii anaona ni kawaida tu! Kwani Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana kwa mfumo huu wa kuwa na tabaka la watu wa aina hii ambao watakuja kuwa Madaktari Mhimbili, Bugando, KCMC na watakuwa Specilist wa Ubongo na mifumo ya fahamu!!!!.​

Hili ni janga la kitaifa, taifa lisilokuwa na wajuzi ni taifa la vibarua na makuli, kwa takwimu hizi zaidi ya 85% ya watahiniwa wote wanaingia kwenye jeshi la vibarua na makuli au hata vibaka na majambazi. Ni aibu kwa rais, ni aibu kwa waziri, ni aibu kwa wazazi.... ni aibu kwa mfumo mzima wa utawala.
Na kibaya zaidi wanafunzi walioko kwenye kundi la wataalam watarajiwa (division I & II) zaidi ya 99% ni wale waliosoma shule za binafsi ambazo wenzangu na mimi hawawezi kumudu kulipia gharama za kupeleka watoto wao hapo.

Kama ningekuwa Rais wa nchi hii ningefanya yafuatayo:
  • Watendaji wa wizara ya elimu wote wapatikane kwa kuajiriwa na waajiriwe kupitia mfumo ulio wazi na ambao hautakuwa na chembechembe ya upendeleo ili kusudi wanaoajiriwa kusimamia elimu wawe ni wale tu ambao wanauwezo na ujuzi unaostahili
  • Ningetangaza kuwa Ualima ni "rare profession" na kumfanya mwalimu kuwa mfanyakazi wa serikali anayelipwa masulufu bora zaidi kuliko wote
  • Waziri wa elimu awe wa kuajiriwa---- yaani natangaza nafasi ya waziri wa elimu kwa yeyote anayeweza na namfanyia usairi na kuangalia historia yake ya utumishi, akishapatikana namteua kuwa mbunge kwa sababu katiba yetu inasema ili mtu awe waziri anatakiwa awe mbunge.
 
Mtoto wa mwalimu anasoma private, mtoto wa mwenyekiti wa bodi ya shule anasoma private, mtoto wa diwani anasoma private, mtoto wa afisa mtendaji (kata) anasoma private, mtoto wa katibu tarafa anasoma private, mtoto wa afisa elimu, na wa mkuu wa wilaya, na wa mkurugenzi wanasoma private. Watoto wa wakurugenzi wote wizarani, wa katibu mkuu, wa makamishna, na wa waziri, wanasoma private.

Kikao kinafanywa na hawa 'wadau' wa elimu kuboresha shule za serikali. Unadhani zaidi ya kuongea, utekelezaji na ufuatiliaji utakuwepo hapo? Fikiria kuwa watoto wa 'wadau' hawa wangekuwa wanasoma kwenye hizi shule zisizo na madawati, vitabu wala walimu, huoni wangeguswa kidogo kuziboresha. Ongea na mwalimu yeyote wa primary au sekondari leo, anakuambia mi sina mda wa kufatafata mitoto ya watu, aandike asiandike, afaulu asifaulu, shauriyake. Ukimuuliza na mwanao je, anasema mwanangu anasoma St nini sijui. Uzalendo haupo. Shule za private zifutwe, tubanane humohumo. watoto wetu sisi walalahoi wakalie tofali moja na watoto wa waziri.

Ni kweli uliyosema, ila hoja inabakia pale pale tu je ukizifuta shule za akina KAYUMBA zitaboreka??? hapa uta create anaza loop hole nyingine ya kupeleka watoto nje ya nchi kumbuka enzi ya Uganda na Kenya kwenda kutafuta elimu bora (kujua kuongea kiingereza) ndo walichukulia elimu bora! hii nayo ilikuwa aibu kwa taifa kwani watoto wote wa kipindi hicho hata wimbo wa Taifa walikuwa hawaujui, unategemea uzalendo utatoka wapi?? Tuziache shule za Private ila tufanye shule za serikali ziwe ndo the best school kwa kuangalia wapi chanzo cha tatizo (a root causes of the problem) na tulishughulikie hilo tatizo.
 
Kwa swala hili jamani naungana na aliyesema kuwa serikali inapaswa kuangalia kwa makini swala la walimu kwa shule za kata. Mazingira ya maisha yaboreshwe, walimu waongezwe na vifaa muhimu viwepo. Pili kuwepo na ushirikiano mzuri kati ya wazazi na waalimu katika kutunza mwanafunzi kielimu. Kama Dowans wanaweza lipwa fasta basi walimu wapewe zana zao waingie mzigoni alafu halmashauri husika ziweke mikakati ya kuwasaidia walimu wa kata ili nao wajisikie. Niliona district council moja Uganda wana walipa posho walimu wao tofauti na mshahara mdoogo wanaolipwa na serikali.
 
Baada ya kugundua kuwa wasomi ndio wanatoa changamoto, inawezekana kabisa serikali hii ya CCM imeamua kuzalisha kizazi cha wajinga ili iendelee kutawala, personally sikuona sababu ya msingi ya kufuta mitihani ya kidato cha II na hiki ndicho tulichovuna
 
Ghafla nimekumbuka wimbo wa Mjomba Mrisho Mpoto kuna sehemu anasema "Tukitaka kufukuza tuwafukuze wote, majengo tufugie kuku, labda ndio tunaloliweza!".........
 
Short and Clear: TATIZO LA WANAFUNZI KUFELI NI CCM; NAMNA YA KUIONDOA TATIZO NI KUIONDOA CCM MADARAKANI

Haingii akilini CCM wanaondoa mtihani wa Form II the mtu anfika form four bila kufanya mtihani hat mmoja. mwisho wa siku unategemea nini?
Haingii akili kuona shule nyingi hazina waalimu na serikali ya CCM haitaki vijana waliomaliza vyou mwaka huu na kuwachukua wachache eti serikali haina Pesa, wana pesa za kugawa bure wakati wa uchagu na kulipa makampuni hewa ya mifukoni mwa watu kama Dowans n.k. ila hawana pesa za kuwlipa waalimu na kuwajengea manyumba.

Hii haiwezekani na hali hii ikiendelea kwa miaka kama miwili au mitatu watu wageuka na kuwa kam Tunisia

 
Short and Clear: TATIZO LA WANAFUNZI KUFELI NI CCM; NAMNA YA KUIONDOA TATIZO NI KUIONDOA CCM MADARAKANI

Haingii akilini CCM wanaondoa mtihani wa Form II the mtu anfika form four bila kufanya mtihani hat mmoja. mwisho wa siku unategemea nini?
Haingii akili kuona shule nyingi hazina waalimu na serikali ya CCM haitaki vijana waliomaliza vyou mwaka huu na kuwachukua wachache eti serikali haina Pesa, wana pesa za kugawa bure wakati wa uchagu na kulipa makampuni hewa ya mifukoni mwa watu kama Dowans n.k. ila hawana pesa za kuwlipa waalimu na kuwajengea manyumba.

Hii haiwezekani na hali hii ikiendelea kwa miaka kama miwili au mitatu watu wageuka na kuwa kam Tunisia


Nime-underline kuonyesha msisitizo na nimekugongea senksi!
 
serikali imetelekeza sekta ya elimu,hivyo hata matokeo ya mwaka haikuwa kitu cha kushangaza kwa watu wanaofuatilia kinachoendelea kwenye sekta hiyo.
mimi nashauri serikali ifanye yafuatayo;
1.iboreshe maslahi walimu.
2.kuajiri walimu wenye sifa stahiki.
3.kuboresha shule zote za serikali kwa kiwango cha kutoa taaluma kama shule za private.
4.kuwepo na sheria ya kuwabana viongozi/watu wote watoto wao wasome shule za hapa nchini.
5.mtihani wa kidato cha pili kupewa kipaumbele kwa wanafunzi kwenda cha tatu.
6.kujenga nyumba za walimu na kuzingatia miundombinu ya barabara,umeme,maji,n.k.kama kigezo cha kuwafanya waishi nyumba hizo.
 
Short and Clear: TATIZO LA WANAFUNZI KUFELI NI CCM; NAMNA YA KUIONDOA TATIZO NI KUIONDOA CCM MADARAKANI

Haingii akilini CCM wanaondoa mtihani wa Form II the mtu anfika form four bila kufanya mtihani hat mmoja. mwisho wa siku unategemea nini?
Haingii akili kuona shule nyingi hazina waalimu na serikali ya CCM haitaki vijana waliomaliza vyou mwaka huu na kuwachukua wachache eti serikali haina Pesa, wana pesa za kugawa bure wakati wa uchagu na kulipa makampuni hewa ya mifukoni mwa watu kama Dowans n.k. ila hawana pesa za kuwlipa waalimu na kuwajengea manyumba.

Hii haiwezekani na hali hii ikiendelea kwa miaka kama miwili au mitatu watu wageuka na kuwa kam Tunisia


Nakuunga mkono mkuu. Mfumo mzima wa elimu umewekwa mateka na CCM. Ata mitihani inasahihishiwa kwenye shule za mafisadi. Mfano f2 imekuwa ikisahihishwa kwa Mchungaji Rwakatare mara nyingi tu. Anafaidika yeye na walimu wanatoka kapa.
 
Back
Top Bottom