Elections 2010 MATOKEO ya kura za awali CCM August 1, 2010

Elections 2010 MATOKEO ya kura za awali CCM August 1, 2010

Kama taarifa hizi ni sahihi, mbona wilaya/jimbo la Kyela lina wanachama wachache sana? Sasa hao wanachama milioni 4 ambao CCM huwa inatutambia kila siku wako wapi?

Margin ni kubwa sana! Hapo hata kama CC wana kinyongo na mshindi sioni kama wanaweza kuwa na jeuri ya kukata jina la mshindi aliyeongoza.

Rafiki yangu Mwakalinga kama ana nia ya kujaribu tena 2015 anahitaji kuanza mikakati ya ushindi kuanzia mwakani mwezi Januari.

Nimekubali maneno ya Dr. Mwakyembe aliyoyasema siku anahojiwa na Mwanakijiji kuhusu juhudi za Lowassa kujisafisha. Alisema kwamba watu wataaibika, kama huo ndio ushindi wenyewe basi alikuwa na haki ya kutamka hivyo.

Kama msajili wa vyama angekuwa anahakiki wanachama idadi kamili ingejulikana wazi, unaweza kuta CHADEMA, CUF wana wanachama sawa na CCM au hata kuizidi tena kwa mbali
 
Mkakati uliokuwepo ulikuwa Prof Mwandosya, Dr Mwakyembe, Mpesya, Mwambalaswa, Zambi na Hilda Ngoye wasirudi Bungeni, lakini wote wameshinda na ndipo hapo ilipo furaha ya wananchi wa Mbeya
 
whatever happened:

Karamagi atarudi kugombea:

Kamala atarudi kugombea:

Chiligati atarudi kugombea:
 
whatever happened:

Karamagi atarudi kugombea:

Kamala atarudi kugombea:

Chiligati atarudi kugombea:

Siyo ajabu Mkuu kwa sababu Chama kina wenyewe. Na hilo litakuwa jambo jema kwa wapenda maendeleo.

Kule kwenu imekuwaje?
 
Nilitaka nipige kelele zote hapa lakini ..............ngoja niwe mpole.

Ingekuwa vingine, naamini kuwa kambi ya Mwakalinga wangefanya kila wawezacho kutukana na kunyanyasa walioshindwa.

Ushauri tu kwa Mwakalinga, next time, tafuta kampeni meneja, afisa mawasiliano na viongozi wazuri wa kufanya kampeni. Cha zaidi sana, mambo ya kutumia surrogate wako kutukana watu ambao hamuwafahamu (kwa vile tu wamepost hapa JF) sio mazuri na mwisho wake sio mzuri. Mlijikusanyia maadui wengi kuliko inavyotakiwa.

Ni hivyo tu

Mkuu Solomon umenena jambo hili kiungwana.
Awali nampongeza sana Dr Mwakyembe kwa kumgararagaza George Mwakalinga,kama nilivyosema awali the better man has won.
Pili somo kwa Mheshimiwa George ni kuwa careful kayika kuchagua makda wake.Ukiwa na makada wasioleweka basi huhitaji maadui, maana hao wamefanya kazi kubwa kukumaliza kisiasa
Kikaragosi no1 ni yule Afande Samwel, ambaye licha ya kutoeleweka, majigambo, tambo kejeli, matusi na dharau ndio ilikuwa election manifesto yake hapa JF.Sidhani kama George Mwakalinga alimtuma kufanya hivyo, lakini kwa vile hakuvizuia damage yake tumeiona.
Ujumbe ulikuwa unafika verbatim, na kwa watu wa sehemu ile Kyela ,Tukuyu etc, mtu wa aina hiyo anachukiwa sana licha ya pesa yake(sse ikwifuna!)
Ushuri wa bure kwa George ni utakapo gombea 2015 lengo liwe utawafanyia nini wananchi ukipata ubunge , na si kumchafua incumbent.Unaweza kuanza sasa(leo probably) kwa kutoa kompyuta mashuleni, kujenga visima kwa maji salama etc
 
Nimedokezwa kuwa Bendera (jimbo mojawapo la Korogwe) na Mwapachu (Tanga mjini) wamepigwa chini. Pia kuna tetesi kwamba Bendera amezimia baada ya kupewa matokeo

Hizi habari siyo rasmi (tutajaribu kuzifuatilia).
 
Kama nilivyoahidi:

NAMPA HONGERA DR. MWAKYEMBE KWA KUSHINDA KURA ZA MAONI HUKO KYELA.

Ninaamini safari hii ukirudi bungeni, utakuwa mkali zaidi kwani utafahamu kuwa Mwakalinga yupo pembeni.

Ila ombea Mungu asihamie CHADEMA maana mpambano utakuwa mkali zaidi na Dr. Slaa akiwa na Mwakalinga.

Hatimaye sasa itakuwa rahisi kumwambia Mwakalinga ahamie CHADEMA.

Yote tisa, kumi ni DR. SLAA FOR PRESIDENT 2010.

Sikonge vipi, pia ningependa mdau mmoja aweke matokeo yote kwenye post moja maana kufuatilia post zote inakuwa issue
 
Habari za kufutwa matokeo ya Kawe si kweli..Kippi Warioba ameshinda.
 
whatever happened:

Karamagi atarudi kugombea:

Kamala atarudi kugombea:

Chiligati atarudi kugombea:

Mkuu what is so special in them, Do they have a divine right to be Parliamentarians? Mmmona naona kama ni Kihiyo, mwingine kila mtu anajua, Captain Chiligati ni mtu wa maana lakini amjishushia hadhi kwa kusema wongo mbele ya watu na kuonesha kuwa chame chake kina maana zaidi kuliko nchi yake. Ni jambo jema kama wakiwa nje ya bunge,they are of no help.
 
Mimi kuna kitu sifahamu hapo ndani ya kijani....

1) Nilisikia katika chaguzi hizi za awali, washindi watatu wanapitishwa kwenda vikao vya juu ndani ya kijani
kujadiliwa and then jina moja litatolewe kama mteule wa jimbo fulani ( katika ubunge )

Kama ni kweli, then hao vigogo walioshindwa kwenye nafasi za kwanza na labda wameangukia nafasi ya pili
au ya tatu -- kwa mimi naona kama mambo yatabadilika huko mbele ???
 
Nimesikia kupitia Clouds FM kwamba Dr. Batilda Buriani ameshinda Arusha mjini, mwenye data zaidi atumwagie.
 
Haya matokeo ni mazuri-yanaleta mabadiliko ktk nyanja ya kisiasa-ila ngoja chimwaga iamue-uone watu watakavyoenda chadema kwa uraisi saana.
 
Inabidi watangaze matokeo kulingana na kura za maoni-wakijifanya kubadilisha tu kama walivyozoea wamekwisha!!
 
Mliokuwa mkijiita makamanda wa ufisadi kama vlie Selelii,Shelukindo,karibuni sana CHADEMA,Mlango uko wazi...
 
Ushuri wa bure kwa George ni utakapo gombea 2015 lengo liwe utawafanyia nini wananchi ukipata ubunge , na si kumchafua incumbent.Unaweza kuanza sasa(leo probably) kwa kutoa kompyuta mashuleni, kujenga visima kwa maji salama etc
Ni ushauri mzuri hizo kompyuta alizoahidi anaweza kuzitoa leo kuliko kusubiri tena wakati wa kampeni 2015.
 
Kamanda atapewa wilaya kama kawaida-c wanapewa waliostaafu na sana sana wa jeshi la polisi? Ndo staili yenyewe iliyopo hapa!! Mimi namuomba mungu anipe uzima 2015 ili magufuli awe president uone watu wanavyoresign kazi hata kabala hajafika ikulu!! Ahahaaa
 
HONGERA MWAKYEMBE KWA USHINDI wa jimbo la KYELA.

La muhimu mwaka huu ni DR. SLAA AWE RAIS WA TANZANIA.
Chonde chonde ndugu yangu usije ukamponza kipenzi chetu Slaa kama ulivyomponza mwakalinga kwa kuanzisha kampeni za matusi, hala hala jicho na mti.
 
Back
Top Bottom