Matokeo ya mchujo TAKUKURU: Let's be honest with each other

Matokeo ya mchujo TAKUKURU: Let's be honest with each other

Shikamoo Mkurugenzi Mkuu Salum Hamduni

Mimi ni kijana niliyekuwa miongoni mwa vijana tuliofanya Usaili tarehe 8 January, 2022 na majibu yametoka juzi. Ulitokea mkanganyiko ambapo jina langu lilitoka kwenye list ya WACHUNGUZI WACHUNGUZI (waombaji wenye Degree) wakati mimi niliomba nafasi ya WACHUNGUZI WASAIDIZI (maana nina Diploma).

Kutokana na mkanganyiko huo,niliambiwa na Wasimamizi nifanye Mtihani wa Wachunguzi Wasaidizi lakini nikitumia namba ya Mtihani niliyopewa kwenye list ya WACHUNGUZI.

Na kwa kuwa sikuwa peke yangu niliochanganywa nafasi, tuliambiwa na Wasimamizi kwamba Mitihani yetu itawekwa Pending kusubiri maelekezo mengine.

Licha ya kuamini kwamba nilifanya vizuri Mtihani ule, jina langu halijatoka pamoja na majina ya wengine wote tuliokumbwa na kadhia ya kuchanganywa nafasi tulizoomba, hivyo tunaamini mkanganyiko uliojitokeza ndio uliosababisha majina yetu yasitoke.

Kwa HESHIMA NA TAADHIMA, tunakuomba Mkurugenzi Mkuu ufuatilie suala hilo.

Ubarikiwe sana
Nitafatilia kijana ,
Pole sana.
 
Same to me. Kuna ambaye niliwasiliana nae na alinitumia hadi screenshot ya msg za kigogo anaewapigania watoto wawili. Niliumia sana, basi tu ndio vile utafanyaje. Yaani sisi tulienda Dom kufanya Aptitude test halafu wengine wamekaa makwao wanaperuzi kwenye pages za umbea Instagram na mwisho wa siku wana nafasi za kazi tayari.
Usiwalaumu watoto wa vigogo mlaumu baba ako kwanini hakuwa kigogo?
 
inasktsha sna hawapo list ya written (officers) but wapo kwnye oral

View attachment 2120480
Hongereni Takukuru kwa mchujo wenu.Mmekaa muda wote na pdf kumbe mnaona aibu jinsi ya kulitoa sababu ya watu wenu mliopachika washenz nyie.Na hawa ndio wenye nafasi za kazi wao walikuwa home wanaperuzi kwenye simu wkt wengine wanapoteza nauli kwenda Dodoma.Mkuu kwa haraka haraka nimeona majina saba humo hapo ni kwa kuangalia juujuu alf kumbuka kuna majina yalijirudia kwenye pdf utagundua nafasi zilikuwa na watu kabla ya usaili
 
Naanza kwa kusema, poleni mliokosa na hongereni mlioona majina.

Ila tukisema tuangalie uhalisia, naweza sema TAKUKURU haijawatendea haki waliofanya usaili ule. To be fair, why wasingetoa majina na marks kila mmoja alizopata, huku wakiainisha cut-off points?

Tuachane na lile swala la baadhi ya majina kujirudia zaidi ya mara moja, hivi, how can we measure the transparency of the process?

Wametumia muda mwingi kuandaa haya majina, ila bado wamechemka pakubwa, maana mpangilio sio mzuri na unamakosa kibao.

Jumanne ya tarehe 04/01/2022 kuna dogo aliniombaga ushauri juu ya hizi application. Kilichokuwa kinamsumbua ni kwamba kuna mzee alimwambia mpaka kufikia ile siku (jumanne), nafasi zilizokuwa zimebaki wazi for everyone zilikuwa 10 out of 200 ( upande wa afisa uchunguzi).

So aliambiwa na yule Mzee atoe around 4 million ili aweze kupatiwa nafasi, na alikuwa guaranteed kupata as long as jina lake lilikuwepo kwenye list ya walioitwa kufanya mtihani hata kama hatoenda Dom kwenye pepa ya mchujo. Me nilichomshauri ni kwamba asitoe hiyo hela, aende tu kufanya mtihani wa mchujo.

Ila am sure now atakuwa anajilaumu kuniskiliza, maana ile hela uwezo wa kulipa alikuwa nao. Even kwa upande wangu baada ya kuona namna results zilivyorudi, napata hisia kuna possibility yule Mzee alikuwa anajua anachokiongea, something is smelling fishy here.

Anyway, kuna 3 questions ninazo:

1. Nasikia kwenye paper waliandika number, why takukuru wametumia nguvu kubwa kuconvert numbers into majina, wakati ilikuwa simple kurudisha results kwa number?

2. Cut-off point ilikuwa ngapi na ufaulu ulikuwaje?

3. Why hawaja-display attained marks za participants wote?
Tuachane na lile swala la baadhi ya majina kujirudia zaidi ya mara moja, hivi, how can we measure the transparency of the process?
 
Mkuu, kuna wazuri wengi pengine zaidi ya huyo ulonaye karibu. Ni mazingira magumu wanapitia yanayowanyima fursa ya kuajiriwa kwa kufuata taratibu na misingi tulojiwekea. Uovu unaozungumzia hapa upo, yes upo, tena kwenye hizi hizi taasisi ambazo pengine tunaziamini hazina makando kando. Nchi hii inahitaji uponyaji kwenye mambo mengi sana.
Nakuelewa sana mkuu. Uovu upo, upo sana na upo sehemu nyingi sana. Nimezungumzia huyu dogo kwamba yuko vizuri kwa sababu niko naye nafanya naye kazi. Kwamba wapo wazuri kumzidi yeye hao siwajui maana sijafanya nao kazi so siwezi kuwazungumzia
 
Hatuwezi tukawa tunafanya mizaha katika maswala haya kila Mtanzania mwenyesifa ya kuitumikia nchi yake katika nafasi mbalimbali provided amefata taratibu basi naaitumikie nchi sio mizahamizaha hii halafu tunatazama tuu
 
Na ukiwaambia watu ooh mara watu walivyowengi msingepita wote mara sjui nini humo sio hao tu nimeona kama saba yamechomekwa.Na ndio sababu pdf ilitoka na majina bila namba wala maksi
Ukiona mtu anatoa majibu hayo ujue upo walakini
 
Aptitude test karibia zote wanandika number sioni haja ya kulalamika,

Pili kutotoa no na kuleta majina kama ni mtu ulie soma excel ni kazi ya dk tuu wala hutoki jasho ya matakoni.

Ajira kama hizi ni kutoa matangazo ya kuleta lawama bora wangekuwa wanajiliwa kimia kimia mtoto wa fulani na fulani sijui msaafu fulani rahisi tu.
 
Aptitude test karibia zote wanandika number sioni haja ya kulalamika,

Pili kutotoa no na kuleta majina kama ni mtu ulie soma excel ni kazi ya dk tuu wala hutoki jasho ya matakoni.

Ajira kama hizi ni kutoa matangazo ya kuleta lawama bora wangekuwa wanajiliwa kimia kimia mtoto wa fulani na fulani sijui msaafu fulani rahisi tu.
[emoji706]
 
Aptitude test karibia zote wanandika number sioni haja ya kulalamika,

Pili kutotoa no na kuleta majina kama ni mtu ulie soma excel ni kazi ya dk tuu wala hutoki jasho ya matakoni.

Ajira kama hizi ni kutoa matangazo ya kuleta lawama bora wangekuwa wanajiliwa kimia kimia mtoto wa fulani na fulani sijui msaafu fulani rahisi tu.
Mbona nchi ina watu wa ovyo kama wewe ,hoja kuu ni kwamba kwanini mtu akuwepo kwenye written lakini jina limetoka kwenye oral ?
 
Tuwe tu wakweli, hata ingekua wewe uko pale takukuru ungeweza mpa mtu mwingine nafasi wakati mdogo wako hana kazi?

Hata hivyo kama huyo mtu ana milion 4 aitumie kufanya mishe nyingine.

Dunia haiko fair.
Unaona nyingi hio million 4?

Ukiingizwa kwenye payroll ya 1.3M with increments na michongo itakayodumu kwa lifetime kuna mda gani hio pesa itakuwa isharudi? Maisha ni magumu mtaani aisee!

Maisha ya kubangaiza sio kabisa yani ndio mwisho unakuja kuwa baba ambaye hueleweki hata kuendesha familia ni mtihani. Msilete dharau hata mie ningekuwa na hela ya kuhonga hio kazi ningelipa niipate tu!

Kazi zinanunuliwa siku nyingi tu mbona .Sema sahizi mambo yamezidi kuwa tight ndio maana taarifa zina leak. Zile zama za sijui una mjomba ataandika kamemo hakuna sahizi ni pesa tu inaongea.
 
Back
Top Bottom