Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 87
JK ameshatangaza kuwa mwaka huu ni mwaka wa siasa,na kama ndio hivyo tutegemee tusichokipenda hivi karibuni.Mimi nashangaa kashfa kibao hazijashughulikiwa yet bado mtu anaongoza kwa asilimia 70 we are not serious.
Hata kama sensization ya mambo ya siasa imefanyika matokeo haya yanaonyesha kuwa uelewa wa watanzania bado ni zero kwani hawajaweza kupambanua sifa dhabiti za kiongozi.
Kashfa ya ndege ya Rais, kashfa ya Rada, Meremeta, wizi wa BOT, Kagoda, Deep Green Finance, Richmond, IPTL, Kiwira, mabomu ya mbagala, ufujaji wa hela halmashauri, matumizi makubwa ya serikali inluding magari ya kifahari yanayotumika hivyo,bila kusahau safari za JK ambazo hazijaonyesha tija yoyote kwa Taifa nk.
Yaani yote hayo hapo juu hayajatolewa maelezo ya kina kwa wananchi kutosheleza kiu yao,isitoshe JK hajaonyesha uongozi wa dhati kukabiliana na mambo hayo yet anapata asimia 70 na chama kinaonekana kuwa karibu na wananchi,huu si usanii huu.
Haya ndiyo mambo yatakayoendelea kuanzia sasa mpaka wakati wa uchaguzi kuwabrain wash wadanganyika wasahau yale yote yaliyotokea huko nyuma.Kazi kubwa ipo kuwaelimisha wadanganyika walio wengi ili kuepukana na utapeli huu wa kisiasa ambao sasa umeanza kufanyiwa kazi.
hayo ni maoni yako ukiwa kama kada wa ccm tuondolee uchafu wako kwenye jf , kiwete nani anmuhitaji kwenye taifa hili labda ccm wasiyo ona mbali kama wewe
upuuzi mtupu! 😕
kipi alichokifanya kikwete tangu aingine madarakani kinachostahili apate 70%!? 😕 Juhudi zake za kutetea mafisadi wa epa, richmond, kiwira etc!?
...tena wangeuliza kama hao waulizwaji kama wanafahamu ni kitu gani kinachompa chati JK.ndiyo hivyo mojwapo ya maswali ambayo wangetupa tuelewe ni kuwa ni wangapi wana jiconsider kuwa ni mashabiki au wanachama wa CCM..
Sijakuelewa mzee unaongelea kuhusu nini hapa na pia kuna nini kama watu wakivaa kofia hata kumi??Hivi ni lini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi itakemea huu upuuzi na ujinga unaoendelezwa na shule za chekechea pamoja na za msingi na za sekondari kuwavika majoho na kofia watoto wanaomaliza shule hizo kwamba eti watoto hao ni "graduates"?
Watoto hao watakapomaliza vyuo vikuu wavalishwa nini? Nikumbuka wakati sisi tukiwa Chuo Kikuu, miaka ya 1960s, hata undergraduates hawakuwa wanavaa kofia!!!!!!!!!!!
Leo synovate wamekutana na wanahabari na kutangaza matokeo ya utafiti wao kuhusu hali ya taifa. Wametaja kuwa Kikwete anaongoza kwa kuwa na asilimia 70 akifutiwa na Freeman Mbowe mwenye asilimia 10, akiwa ametangulia kidogo Lipumba. Hii ni katika nafasi ya urais.
Kwa upande wa vyama matokeo yanaonyesha kwamba CCM iko karibu zaidi na wananchi kwa asilimia 70 ikifuatiwa na CHADEMA yenye asilimia 14.
......ndiyohiyo
Baba- synovate ni nini? NGO?? or what ?? na Board of Directors ni akina nani?
- utafiti kuhusu hali taifa maana yake nini?
- ubora wa mbunge umepimwa kwa vigezo vipi?
- Jerry Silaa ni diwani au mbunge?
- sample size mbona inatia shaka? watu 2,000 (elfu mbili!)
- ukaribu na wananchi unapimwaje?
naomba maelezo zaidi kwa mwenye nayo - this looks like a Y2K bug!
na idadi kubwa ya watanzania wanaipenda na kuitukuza CCM(hata kama sio wanachama).naunga mkono matokeo ya utafiti huu kwani yanaegemea kwenye ukweli ingawa ukweli unauma)....sasa kama wananchi waliulizwa 90% walikuwa wanachama wa CCM, unategemea nini?
Hapa mseme tu mnataka Jerry Silaa asikike au ajulikane. Anakuwaje mbunge maarufu wakati wala si mbunge na bado hajatangaza anagombea na kama ametangaza ni kwenye forum ipi na hao watanzania 1000 wa nchi nzima wamepataje taarifa?Leo synovate wamekutana na wanahabari na kutangaza matokeo ya utafiti wao kuhusu hali ya taifa. Wametaja kuwa Kikwete anaongoza kwa kuwa na asilimia 70 akifutiwa na Freeman Mbowe mwenye asilimia 10, akiwa ametangulia kidogo Lipumba. Hii ni katika nafasi ya urais.
Katika bunge utafiti wao unaonyesha kwamba Zitto Kabwe ndiye mbunge bora kuliko wote akifuatiwa na Anna Kilango. Katika matokeo hayo Mbunge mwingine bora anayetajwa ni Jerry Silaa ambaye ni diwani wa ukonga. Utafiti huo unasema kwamba wananchi wapatao elfu mbili waliohojiwa kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wamemtaja diwani huyo kuwa anachapa kazi kwa kiwango kikubwa na wakiamini kwamba ni mbunge. Katika utafiti huo Dr Slaa anatajwa kuwa nyuma.
Kwa upande wa vyama matokeo yanaonyesha kwamba CCM iko karibu zaidi na wananchi kwa asilimia 70 ikifuatiwa na CHADEMA yenye asilimia 14.
......ndiyohiyo
...waislamu wana matatizo! mbona mkapa hakuwahi kufanyiwa kura za maoni???Na Tiganya Vincent-MAELEZO
Asilimia 75 ya watanzania waliohojiwa na Shirika lisilokuwa la kiserikali linajihusisha na utafiti wa masuala ya siasa, uchumi na kijamii wameonyesha kuwa wangependa Rais Jakaya Mrisho Kikwete andelelee kuongoza Tanzania mara baada ya uchaguzi Mkuu mwisho mwa mwaka huu.
Hatua hiyo inafuatia watanzania 2000 waliohojiwa kutoka sehemu mbalimbali kumkubali kuwa Rais Kikwete anastahili kuchaguliwa tena kuwa Kiongozi Mkuu wa Tanzania.
Takwimu hizo zilitolewa jana jijini Dar es salaam na Meneja wa Utafiti wa Vyombo vya Habari na Umma kutoka Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Synovate Tanzania Abdallah Gunda alipokuwa anatoa matokeo ya utafiti wa hali ya demokrasia hapa nchini.
Alisema kuwa asilimia hizo ni zaidi ya theluthi mbili ya Watanzania ambao walihojiwa kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania.
Katika utafiti huo Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alipata asilimia 10 wakati Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi alipata asilimia 9.
Gunda aliongeza kuwa Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP) , Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe na Dkt Salim Ahmed Salim walipa asilimia moja kwa kila mmoja wao ya Watanzania wenye uwezo kupiga kura wakipenda kuwa wanafaa kuwa Rais.
Meneja huyo alisema kuwa katika utafiti wao asilimia mbili ya wahoojiwa wote walisema kuwa wasingependa kueleza nani wangependa awe Rais wakati asilimia mbili nyingine hawajui wa kumchagua.
Aidha katika utafiti huo Chama cha Mapinduzi kilioneka kuwa watu wengi walio karibu nacho kwa kuapa asilimia 70, CHADEMA asilimia 17, CUF asilimia 9, NCCR-Mageuzi kuwa na asilimia 2 huku TLP na UDP zikiwa na asilimia moja kila kimoja.
Source Michuzi Blog
Ni rubbish si utafiti wala ndugu yake utafiti. Ni ile wao wanaita propaganda.Leo synovate wamekutana na wanahabari na kutangaza matokeo ya utafiti wao kuhusu hali ya taifa. Wametaja kuwa Kikwete anaongoza kwa kuwa na asilimia 70 akifutiwa na Freeman Mbowe mwenye asilimia 10, akiwa ametangulia kidogo Lipumba. Hii ni katika nafasi ya urais.
Katika bunge utafiti wao unaonyesha kwamba Zitto Kabwe ndiye mbunge bora kuliko wote akifuatiwa na Anna Kilango. Katika matokeo hayo Mbunge mwingine bora anayetajwa ni Jerry Silaa ambaye ni diwani wa ukonga. Utafiti huo unasema kwamba wananchi wapatao elfu mbili waliohojiwa kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wamemtaja diwani huyo kuwa anachapa kazi kwa kiwango kikubwa na wakiamini kwamba ni mbunge. Katika utafiti huo Dr Slaa anatajwa kuwa nyuma.
Kwa upande wa vyama matokeo yanaonyesha kwamba CCM iko karibu zaidi na wananchi kwa asilimia 70 ikifuatiwa na CHADEMA yenye asilimia 14.
......ndiyohiyo