Makoye Matale
JF-Expert Member
- May 2, 2011
- 6,491
- 2,104
Salaam kwenu WanaJF.
Zimesalia siku chache kufikia mpambano mwingine wa watani wa jadi Simba na Yanga. Yapo mabishano mengi yanayojitokeza hasa katika kipindi hiki, kila upande ukijinasibu kuwa ni bora kuliko upande mwingine. Hata hivyo matokeo ya uwanjani huwa hayafuati mapenzi au hata majigambo ya kila upande, matokeo hutokea kulingana na uwezo wa kila timu.
Nimejaribu kupitia wavuti na blogu mbalimbali, sikufanikiwa kupata matokeo ya watani hawa wa jadi isipokuwa katika blogu ya BIN ZUBEIRY, nimefanikiwa kupata matokeo yote ya watani hawa tangu waanze kuingia katika mapambano ya ligi daraja la kwanza (sasa Ligi Kuu), kombe la Muungano na mapambano mengine mfano CECAFA, TUSKER n. k. Nimeandaa muhtasari wa matokeo hayo katika format ya pdf. Naomba sasa nitoe dondoo chache zitokanazo na matokeo hayo.
1. Yanga ndiyo timu ya kwanza kuifunga Simba hapo tarehe 07/06/1965 pale ipoibugiza Simba bao 1-0 mfungaji akiwa ni Mawazo Shomvi katika dakika ya 15 ya mchezo.
2. Yanga ndiyo timu ya kwanza kuibamiza Simba kichapo cha paka mwizi cha 5-0 hapo tarehe 01/06/1968. Kwa kipindi cha takribani miaka 9 hivi Simba ilikuwa ikijipanga kulipa kisasi hicho na ilipofika tarehe 19/07/1977 iliibamiza Yanga kipigo kikali zaidi cha 6-0.
3. Abdallah Kibadeni wa Simba ndiye mchezaji pekee aliyeweza kupiga bao 3 (hat trick) katika mapambano ya watani siku ya kifo cha karne cha Yanga cha bao 6-0 siku ya tarehe 19/07/1977. Kipigo hiki hakijalipwa na Yanga hadi leo.
4. Simba kwa mara nyingine tena iliibamiza Yanga kipigo kikali cha bao 5-0 siku ya tarehe 06/05/2012. Kipigo hiki ni malipo kwa Yanga kwa kipigo kama hicho cha tarehe 01/06/1968.
5. Hadi sasa watani Simba na Yanga wamecheza mapambano 109. Mapambano 30 yaliisha kwa sare au suluhu bila kutambiana. Yanga imefanikiwa kushinda mapambano 43 huku Simba ikitamba katika mapambano 36. Hadi sasa Simba inadaiwa na Yanga mapambano 7 ya kushinda.
6. Hadi sasa Yanga imefanikiwa kuifunga Simba mabao 140 huku Simba ikizifumania nyavu za Yanga mara 132. Simba inadaiwa na Yanga mabao 8.
7. Takwimu katika vipengele 5 & 6 hapo juu zinaungwa mkono na mataji ya ubingwa wa ligi kuu ambapo Yanga imefanikiwa kuchukua ubingwa mara 24 huku Simba ikishinda mataji mara 18.
Taarifa ndani ya jedwali ni nyingi, naomba niishie hapa ili kutoa nafasi kwa wachangiaji wengine kuzichambua.
Chanzo: BIN ZUBEIRY - MAPAMBANO YOOOOTE YA WATANI WA JADI, SIMBA NA YANGA KABLA YA PAMBANO LA KESHO | BIN ZUBEIRY
DISCLAIMER: Makoye Matale hatahusika kwa njia moja ama nyingine na madhara yoyote yatakayompata shabiki au msomaji yeyote wa post hii kwa mfano msongo, shinikizo la damu, kiharusi, kifo cha ghafla, kifafa, kizunguzungu, kuhara na kuhara damu n.k. yatokayo na kuujua ukweli huu.
Zimesalia siku chache kufikia mpambano mwingine wa watani wa jadi Simba na Yanga. Yapo mabishano mengi yanayojitokeza hasa katika kipindi hiki, kila upande ukijinasibu kuwa ni bora kuliko upande mwingine. Hata hivyo matokeo ya uwanjani huwa hayafuati mapenzi au hata majigambo ya kila upande, matokeo hutokea kulingana na uwezo wa kila timu.
Nimejaribu kupitia wavuti na blogu mbalimbali, sikufanikiwa kupata matokeo ya watani hawa wa jadi isipokuwa katika blogu ya BIN ZUBEIRY, nimefanikiwa kupata matokeo yote ya watani hawa tangu waanze kuingia katika mapambano ya ligi daraja la kwanza (sasa Ligi Kuu), kombe la Muungano na mapambano mengine mfano CECAFA, TUSKER n. k. Nimeandaa muhtasari wa matokeo hayo katika format ya pdf. Naomba sasa nitoe dondoo chache zitokanazo na matokeo hayo.
1. Yanga ndiyo timu ya kwanza kuifunga Simba hapo tarehe 07/06/1965 pale ipoibugiza Simba bao 1-0 mfungaji akiwa ni Mawazo Shomvi katika dakika ya 15 ya mchezo.
2. Yanga ndiyo timu ya kwanza kuibamiza Simba kichapo cha paka mwizi cha 5-0 hapo tarehe 01/06/1968. Kwa kipindi cha takribani miaka 9 hivi Simba ilikuwa ikijipanga kulipa kisasi hicho na ilipofika tarehe 19/07/1977 iliibamiza Yanga kipigo kikali zaidi cha 6-0.
3. Abdallah Kibadeni wa Simba ndiye mchezaji pekee aliyeweza kupiga bao 3 (hat trick) katika mapambano ya watani siku ya kifo cha karne cha Yanga cha bao 6-0 siku ya tarehe 19/07/1977. Kipigo hiki hakijalipwa na Yanga hadi leo.
4. Simba kwa mara nyingine tena iliibamiza Yanga kipigo kikali cha bao 5-0 siku ya tarehe 06/05/2012. Kipigo hiki ni malipo kwa Yanga kwa kipigo kama hicho cha tarehe 01/06/1968.
5. Hadi sasa watani Simba na Yanga wamecheza mapambano 109. Mapambano 30 yaliisha kwa sare au suluhu bila kutambiana. Yanga imefanikiwa kushinda mapambano 43 huku Simba ikitamba katika mapambano 36. Hadi sasa Simba inadaiwa na Yanga mapambano 7 ya kushinda.
6. Hadi sasa Yanga imefanikiwa kuifunga Simba mabao 140 huku Simba ikizifumania nyavu za Yanga mara 132. Simba inadaiwa na Yanga mabao 8.
7. Takwimu katika vipengele 5 & 6 hapo juu zinaungwa mkono na mataji ya ubingwa wa ligi kuu ambapo Yanga imefanikiwa kuchukua ubingwa mara 24 huku Simba ikishinda mataji mara 18.
Taarifa ndani ya jedwali ni nyingi, naomba niishie hapa ili kutoa nafasi kwa wachangiaji wengine kuzichambua.
Chanzo: BIN ZUBEIRY - MAPAMBANO YOOOOTE YA WATANI WA JADI, SIMBA NA YANGA KABLA YA PAMBANO LA KESHO | BIN ZUBEIRY
DISCLAIMER: Makoye Matale hatahusika kwa njia moja ama nyingine na madhara yoyote yatakayompata shabiki au msomaji yeyote wa post hii kwa mfano msongo, shinikizo la damu, kiharusi, kifo cha ghafla, kifafa, kizunguzungu, kuhara na kuhara damu n.k. yatokayo na kuujua ukweli huu.
Attachments
Last edited by a moderator: