Matukio ya kukumbukwa mwaka 2004

Matukio ya kukumbukwa mwaka 2004

Lethergo

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2023
Posts
6,534
Reaction score
11,421
Huu uzi unahusu matukio yoyote yaliyotokea mwaka 2004, basi na wewe mwanajukwaa andika hapa tukio lolote lililotokea mwaka 2004.

Mimi nitaanza na tukio la shindano la kutafuta vipaji vya waimbaji mwaka 2004 lililotambulika km East Afrika Coca Cola Pop Stars Talent Search Competition, ili ni tukio lililohusisha kusaka vipaji vya waimbaji mbalimbali, nakumbuka kipindi hicho tulikua tunafuatilia kipindi mida ya jioni jioni kwenye Luninga (Televisheni) km nitakua sijasahau ilikua ni ITV, baadae mwisho wa shindano wakaibuka washindi watatu ambao ni Witness Mwaijage 'Witness' (Bad Gear), Langa Kileo 'Langa' (RIP) & Sarah Kaisi 'Shaa'.

Baada ya ushindi huo washindi hao wa Coca Cola Pop stars Talent Search Competition wakaunda kundi lililotambuliwa km 'Wakilisha' ikiwa ni muungano wa majina yao ya kisanii yaani Witness, Langa na Shaa, meneja wa kundi hilo alikua anaitwa Daniel Kiondo na wakaachia kibao chao cha kwanza kilichoitwa 'HOI'.

Baadae wakaachia kibao kingine cha pili kikali kilichokwenda kwa jina la 'Kiswanglish'. Baada ya hapo mwaka uliofuatia kundi hilo likafika tamati rasmi na kila mmoja akaanza kufanya kazi zake peke yake.

Shaa akaelekea zake Washington DC kuendelea na masomo. Huku Langa' yeye akaanza kuachia vibao vyake vikitanguliwa na kibao cha kwanza kilichoitwa 'Matawi ya Juu' kule 'Witness' akitoa kibao chake cha kwanza kilichoitwa 'Kichekesho' na pia kupita kwenye kolabo ya kushiriki kwenye kibao cha Fid Q kilichoitwa 'Zero'.

Baadae Witness na Langa waliungana wakaunda kundi lililoitwa 'Wakili' ambalo pia halikudumu muda mrefu sana.
 
Tukio lingine la kukumbukwa mwaka 2004 ni lile la kibao cha wimbo unaohusu masuala mazima ya Virus vya Ukimwi na Ukimwi kilichotambulika km 'Usione Soo, Sema Nae', kibao hicho kilifanywa na wasanii wa kipindi hicho ambao walikua wanatamba sana kimuziki kuanzia kwenye redio mpaka kwenye Televisheni, wasanii hao wakiwa chini ya Ishi Organization in Tanzania iliyoendesha Ishi Campaign ambapo wasanii hao waliunda kundi lililofahamika km 'Ishi Stars'.

Kundi hilo lilisheheni wasanii wakali wa kipindi hicho km vile Pauline Zongo, Stara Thomas, Banana Zoro, Benjamin wa Mambo Jambo, Mr Paul, Solo Thang, Raha P, Dataz, Patricia,

Huku chorus ya wimbo huo ikiimba :

Usione soo sema naye, kuhuusu kusubiri, kuwa mwaminifu au tumia kondom. (Don’t be shy. Talk with your partner about abstinence, being faithful, or using a condom).”
F7GzV3bWMAEEgvu.jpg
 
Tukio lingine la kukumbukwa mwaka 2004 ni lile la kibao cha wimbo unaohusu masuala mazima ya Virus vya Ukimwi na Ukimwi kilichotambulika km 'Usione Soo, Sema Nae', kibao hicho kilifanywa na wasanii wa kipindi hicho ambao walikua wanatamba sana kimuziki kuanzia kwenye redio mpaka kwenye Televisheni, wasanii hao wakiwa chini ya Ishi Organization in Tanzania iliyoendesha Ishi Campaign ambapo wasanii hao waliunda kundi lililofahamika km 'Ishi Stars'.

Kundi hilo lilisheheni wasanii wakali wa kipindi hicho km vile Pauline Zongo, Stara Thomas, Banana Zoro, Benjamin wa Mambo Jambo, Mr Paul, Solo Thang, Raha P, Dataz, Patricia,

Huku chorus ya wimbo huo ikiimba :

Usione soo sema naye, kuhuusu kusubiri, kuwa mwaminifu au tumia kondom. (Don’t be shy. Talk with your partner about abstinence, being faithful, or using a condom).”
View attachment 3131178
Aah Washikaji zangu eeh sukari imeingia shubiri uwazi tuuweke mbele usione sooo, tuongee kuhusu subira.. washikaji msione soo.. tuongee kuhusu kinga.. washikaji msione soo

Aah usione soo sema nae...


Hii nimekumbuka sasa kipindi watu walikua wanakwenda na moto huko Iringa, watakuja kusimulia wenyewe wenye story zao za Njombe, Makete & Mafinga
 
Tukio lingine la kukumbukwa mwaka 2004 ni lile la kibao cha wimbo unaohusu masuala mazima ya Virus vya Ukimwi na Ukimwi kilichotambulika km 'Usione Soo, Sema Nae', kibao hicho kilifanywa na wasanii wa kipindi hicho ambao walikua wanatamba sana kimuziki kuanzia kwenye redio mpaka kwenye Televisheni, wasanii hao wakiwa chini ya Ishi Organization in Tanzania iliyoendesha Ishi Campaign ambapo wasanii hao waliunda kundi lililofahamika km 'Ishi Stars'.

Kundi hilo lilisheheni wasanii wakali wa kipindi hicho km vile Pauline Zongo, Stara Thomas, Banana Zoro, Benjamin wa Mambo Jambo, Mr Paul, Solo Thang, Raha P, Dataz, Patricia,

Huku chorus ya wimbo huo ikiimba :

Usione soo sema naye, kuhuusu kusubiri, kuwa mwaminifu au tumia kondom. (Don’t be shy. Talk with your partner about abstinence, being faithful, or using a condom).”
View attachment 3131178
Hii ndio yenyewe sasa, umenikumbusha mbali sana.

Enzi hizo shule ya msingi, huo wimbo ulikuwa unapigwa kila siku saa 2 asubuhi Radio One, nilikuwa naupenda mno!

Baada ya hapo ndio majarida ya FEMA yakaanza kutoka, akina Amabilis Batamula na Anko Josh.
 
Back
Top Bottom