Lethergo
JF-Expert Member
- Aug 7, 2023
- 6,534
- 11,421
Huu uzi unahusu matukio yoyote yaliyotokea mwaka 2004, basi na wewe mwanajukwaa andika hapa tukio lolote lililotokea mwaka 2004.
Mimi nitaanza na tukio la shindano la kutafuta vipaji vya waimbaji mwaka 2004 lililotambulika km East Afrika Coca Cola Pop Stars Talent Search Competition, ili ni tukio lililohusisha kusaka vipaji vya waimbaji mbalimbali, nakumbuka kipindi hicho tulikua tunafuatilia kipindi mida ya jioni jioni kwenye Luninga (Televisheni) km nitakua sijasahau ilikua ni ITV, baadae mwisho wa shindano wakaibuka washindi watatu ambao ni Witness Mwaijage 'Witness' (Bad Gear), Langa Kileo 'Langa' (RIP) & Sarah Kaisi 'Shaa'.
Baada ya ushindi huo washindi hao wa Coca Cola Pop stars Talent Search Competition wakaunda kundi lililotambuliwa km 'Wakilisha' ikiwa ni muungano wa majina yao ya kisanii yaani Witness, Langa na Shaa, meneja wa kundi hilo alikua anaitwa Daniel Kiondo na wakaachia kibao chao cha kwanza kilichoitwa 'HOI'.
Baadae wakaachia kibao kingine cha pili kikali kilichokwenda kwa jina la 'Kiswanglish'. Baada ya hapo mwaka uliofuatia kundi hilo likafika tamati rasmi na kila mmoja akaanza kufanya kazi zake peke yake.
Shaa akaelekea zake Washington DC kuendelea na masomo. Huku Langa' yeye akaanza kuachia vibao vyake vikitanguliwa na kibao cha kwanza kilichoitwa 'Matawi ya Juu' kule 'Witness' akitoa kibao chake cha kwanza kilichoitwa 'Kichekesho' na pia kupita kwenye kolabo ya kushiriki kwenye kibao cha Fid Q kilichoitwa 'Zero'.
Baadae Witness na Langa waliungana wakaunda kundi lililoitwa 'Wakili' ambalo pia halikudumu muda mrefu sana.
Mimi nitaanza na tukio la shindano la kutafuta vipaji vya waimbaji mwaka 2004 lililotambulika km East Afrika Coca Cola Pop Stars Talent Search Competition, ili ni tukio lililohusisha kusaka vipaji vya waimbaji mbalimbali, nakumbuka kipindi hicho tulikua tunafuatilia kipindi mida ya jioni jioni kwenye Luninga (Televisheni) km nitakua sijasahau ilikua ni ITV, baadae mwisho wa shindano wakaibuka washindi watatu ambao ni Witness Mwaijage 'Witness' (Bad Gear), Langa Kileo 'Langa' (RIP) & Sarah Kaisi 'Shaa'.
Baada ya ushindi huo washindi hao wa Coca Cola Pop stars Talent Search Competition wakaunda kundi lililotambuliwa km 'Wakilisha' ikiwa ni muungano wa majina yao ya kisanii yaani Witness, Langa na Shaa, meneja wa kundi hilo alikua anaitwa Daniel Kiondo na wakaachia kibao chao cha kwanza kilichoitwa 'HOI'.
Baadae wakaachia kibao kingine cha pili kikali kilichokwenda kwa jina la 'Kiswanglish'. Baada ya hapo mwaka uliofuatia kundi hilo likafika tamati rasmi na kila mmoja akaanza kufanya kazi zake peke yake.
Shaa akaelekea zake Washington DC kuendelea na masomo. Huku Langa' yeye akaanza kuachia vibao vyake vikitanguliwa na kibao cha kwanza kilichoitwa 'Matawi ya Juu' kule 'Witness' akitoa kibao chake cha kwanza kilichoitwa 'Kichekesho' na pia kupita kwenye kolabo ya kushiriki kwenye kibao cha Fid Q kilichoitwa 'Zero'.
Baadae Witness na Langa waliungana wakaunda kundi lililoitwa 'Wakili' ambalo pia halikudumu muda mrefu sana.