Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,296
- 122,540
Vitoto vingi sana humu aisee 🤣.Hakika mimi nitakua napiga misele huu uzi utafika mbali sana maana hio 2004 kuna dogo anasoma uzi huu muda huu kipindi hicho yeye alikua ndio kwanza ana mwaka mmoja na bado hajamaliza kunyonya hapa anachoona ni maluweluwe tu memories zitaendelea kuishi
Halafu tunategemea nchi isonge mbele Kama jitu linakumbuka pop star tuHuu uzi unahusu matukio yoyote yaliyotokea mwaka 2004, basi na wewe mwanajukwaa andika hapa tukio lolote lililotokea mwaka 2004.
Mimi nitaanza na tukio la shindano la kutafuta vipaji vya waimbaji mwaka 2004 lililotambulika km East Afrika Coca Cola Pop Stars Talent Search Competition, ili ni tukio lililohusisha kusaka vipaji vya waimbaji mbalimbali, nakumbuka kipindi hicho tulikua tunafuatilia kipindi mida ya jioni jioni kwenye Luninga (Televisheni) km nitakua sijasahau ilikua ni ITV, baadae mwisho wa shindano wakaibuka washindi watatu ambao ni Witness Mwaijage 'Witness' (Bad Gear), Langa Kileo 'Langa' (RIP) & Sarah Kaisi 'Shaa'.
Baada ya ushindi huo washindi hao wa Coca Cola Pop stars Talent Search Competition wakaunda kundi lililotambuliwa km 'Wakilisha' ikiwa ni muungano wa majina yao ya kisanii yaani Witness, Langa na Shaa, meneja wa kundi hilo alikua anaitwa Daniel Kiondo na wakaachia kibao chao cha kwanza kilichoitwa 'HOI'.
Baadae wakaachia kibao kingine cha pili kikali kilichokwenda kwa jina la 'Kiswanglish'. Baada ya hapo mwaka uliofuatia kundi hilo likafika tamati rasmi na kila mmoja akaanza kufanya kazi zake peke yake.
Shaa akaelekea zake Washington DC kuendelea na masomo. Huku Langa' yeye akaanza kuachia vibao vyake vikitanguliwa na kibao cha kwanza kilichoitwa 'Matawi ya Juu' kule 'Witness' akitoa kibao chake cha kwanza kilichoitwa 'Kichekesho' na pia kupita kwenye kolabo ya kushiriki kwenye kibao cha Fid Q kilichoitwa 'Zero'.
Baadae Witness na Langa waliungana wakaunda kundi lililoitwa 'Wakili' ambalo pia halikudumu muda mrefu sana.
KamweneHalafu tunategemea nchi siongei mbele Kama kitu linakumbuka pop star
Ndinalioooooo 🥹🥹
Ukimwi wa zamani ulikuaga balaa umemmaliza wengi.Aah Washikaji zangu eeh sukari imeingia shubiri uwazi tuuweke mbele usione sooo, tuongee kuhusu subira.. washikaji msione soo.. tuongee kuhusu kinga.. washikaji msione soo
Aah usione soo sema nae...
Hii nimekumbuka sasa kipindi watu walikua wanakwenda na moto huko Iringa, watakuja kusimulia wenyewe wenye story zao za Njombe, Makete & Mafinga
Hakika Mwaka 2004 ulioongoza kwa vipindi vingi vya kutoa elimu ya uelimishaji rika juu masuala ya ngono salama, ngono zembe, athari za ngono zembe, faida za ngono salama, visababishi vya Ukimwi na virusi vya ukimwi, jinsi na namna ya kujikinga na kuwakinga wengine na virusi vya ukimwi na ukimwi.Nilikuwa mdogo lakini nachokumbuka 2004 matangazo ya kujikinga na ukimwi yalikuwa mengi sana, NGO's za ukimwi zilikuwa nyingi sana na wasanii wengi walikuwa wakishindana kutoa ngoma kali juu ya elimu ya ukimwi.
Guess what! sasa ukimwi ni kama mafua tu, hakuna mtu anauogopa na ARVs zilifanya kazi yake vyema na bado zinafanya kazi yake.
Duh sasa nimekumbuka kitu maana kuna hio siku niliingia na yule binti kigoli ghetto kwangu ila kabla hatujafanya kitu chochote mara ghafla likapigwa tangazo la kondomu kwenye redio ndio hapo binti akaniuliza 'una kinga?' ilibidi niwahi dukani kwa mangi chapu nikachukue dhana na hio ndio ikawa mara yangu ya kwanza kuvaa Salama kondomuHakika Mwaka 2004 ulioongoza kwa vipindi vingi vya kutoa elimu ya uelimishaji rika juu masuala ya ngono salama, ngono zembe, athari za ngono zembe, faida za ngono salama, visababishi vya Ukimwi na virusi vya ukimwi, jinsi na namna ya kujikinga na kuwakinga wengine na virusi vya ukimwi na ukimwi.
PSI Tanzania waliendesha kampeni kabambe katika kutekeleza hilo kwa kuja na matangazo mbalimbali ya kwenye vipindi vya redio na luninga (televisheni) vilivyotoa elimu mahususi ya ukimwi na virusi vya ukimwi ikiwa na kaulimbiu mbalimbali zikiwemo :
View attachment 3131518
‘’Kama Kweli Unampenda Utamlinda’’
View attachment 3131513
‘’Salama Chaguo la Kweli’’
View attachment 3131512
"Michepuko Sio Dili" na "Kuwa Original, Tumia Original’’.
View attachment 3131508
Haya matangazo yote yalikua yanalenga matumizi ya kondomu sana sana 'Salama' kondomu.
Bila kusahau mwaka huo huo 2004 kulikua na michezo mbalimbali ya Maigizo kupitia televisheni channel ya ITV na vikundi mbalimbali vilitoa michezo ya maigizo inayotoa elimu kuhusu ukimwi na virusi vya ukimwi, kwa mfano kundi la Nyota Academia km sijakosea walitoa mchezo wa maigizo, ambapo siku hizi nyinyi mnaita tamthiliya ila kipindi hicho sisi tulikua tunaita maigizo au igizo na televisheni ilikua inasema igizo linalofuata, mchezo huo wa maigizo pia uliokua ukitoa elimu kuhusu ukimwi na virusi vya ukimwi na km sijakosea mhusika mkuu aliigiza km muathirika kweli wa virusi vya ukimwi, kwenye igizo hilo muhusika mkuu aliigiza kua ana kikohozi fulani hivi kikavu sana na jinsi alivyokua anajiweka kiugonjwa ugonjwa km mgonjwa kweli wa ukimwi ilipelekea kila mtu alikua anaogopa kupata ngwengwe kipindi hicho.
Kipindi hicho ndio kulikua na makundi mengi ya maigizo yaliyochuana vilivyo kupitia redio na televisheni km vile Kaole Sanaa Group, Mambo Hayo, Kidedea, Kidedea Original, Nyota Academia na mengine sijayataja
Pole sana kakaNilimpoteza uncle wangu.