Matukio ya Utekaji yanaumiza na kutupa hofu Wananchi hasa tunapoona Wahusika hawapatikani, Serikali ifanye maamuzi magumu

Matukio ya Utekaji yanaumiza na kutupa hofu Wananchi hasa tunapoona Wahusika hawapatikani, Serikali ifanye maamuzi magumu

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Nimekaa nikatafakari kuhusu matukio ya utekaji yanayoendelea Nchini, sisi Wananchi tumekuwa tukiumia kadiri siku zinavyoenda, matukio ya utekaji yanaendelea, imani yetu kwa vyombo vya Ulinzi inaanza kupotea.

Mawazo hayo yamekuja baada ya kuona tukio la Mfanyabiashara Deogratius Tarimo alivyonusurika kutekwa na Watu ambao hawajulikani lakini angalau sura zao tumeanza kuziona.

Tukio hilo limeanza kutupa hofu Wananchi wengi wa kujiona hatupo salama, kama matukio yanafanyika mchana kweupe, sura za Watu zinaonekana huku Vyombo vya Usalama vikiishia kusema uchunguzi unafanyika baada ya hapo tunasahau tunasubiri tukio lingine, naona sio sawa.

Pia soma - Inasemekana tukio hili la utekaji limetokea Kiluvya, kutokana na uzito wa jamaa walishindwa kumchukua. Hakuna aliyetoka kumsaidia

Pia soma - Polisi watoa tamko tukio la jaribio la utekaji Kiluvya, wasema uchunguzi umeanza toka aliporipoti Novemba 11, 2024

GcNumyWWgAAEDgu.jpeg
Inawezekana Watu hawasemi lakini haya mambo yanayofanyika hivi, mdogomdogo yanazidi kuwaaminisha Wananchi kuwa hatupo salama. Serikali inatakiwa kufanya maamuzi magumu kuhusu hao "Watekaji" au ambao "Hawajulikani", tutaishi kwa hofu hivi hadi lini?

Miaka ya nyuma ilikuwa utekaji unafanyika kwa kificho, kama imefikia hatua mambo yanafanyika hadharani basi tunaelekea kubaya.

Hii ni mifano michache tu ya matukio ya hivi karibuni ya Mwaka 2024, achana na yale ya kina Roma na kina Mo Dewji na wengine wengi, haya machache ni ya mwaka huu, mnaweza kunikumbusha mengine pia:

Juni 2024: Edger Mwakalebela “Sativa” alitekwa akiwa Dar es Salaam akapatikana Katavi akiwa amejeruhiwa vibaya, Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
SATIVA: Nilitekwa nikapelekwa Karakana ya Polisi Oysterbay kabla ya kusafirishwa sehemu nyingine na nimepigwa risasi ya kichwa

Septemba 2024: Mwanachama wa CHADEMA, Ally Mohamed Kibao alichukuliwa na Watu wasiojulikana ndani ya basi, mwili wake ukapatikana baadaye akiwa ameuawa. Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
Kuelekea 2025 - Polisi: Tunachunguza kubaini chanzo na watu waliohusika kumchukua Ali Kibao

Novemba 2024: Mkurugenzi wa Dar24 Media, Maclean Mwaijonga alipotea kwa siku mbili akiwa hajulikani alipo, Taasisi yake ikatoa taarifa kwa umma, akapatikana Kigamboni na kueleza kuwa alikuwa na Watu anaofanyanao biashara, akanywa juisi ambayo anaamini ilimfanya akapoteza fahamu.
Mkurugenzi wa Dar 24 apatikana Kigamboni

Agosti 2024: Kijana Shadrack Chaula (24) alichukuliwa na Watu wasiojulikana Mkoani Mbeya, Wazazi wake wakajitokeza kuomba msaada wa kumtafuta kijana wao, Jeshi la Polisi likasema linachunguza na kumtafuta mhusika.
Sakata la kijana aliyechoma picha ya Rais kutoweka lawaibua polisi

Novemba 2024: Vijana wawili walipoteza maisha kwa kupigwa risasi, wengine wawili walijeruhiwa vibaya ikidaiwa walikuwa wakiwakimbia Askari Polisi, chanzo kikidaiwa ni kesi ya uchimbaji mchanga, Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
Zanzibar: Vijana wawili wauawa na wengine 2 kuumizwa vibaya. ACT yataka Jeshi na Polisi kufanyiwa mabadiliko Kimuundo na Kiutendaji

Julai 2024: Mwanachama wa CHADEMA - Tanga, Kombo Mbwana alipotea kwa siku 29, Jeshi la Polisi likatangaza kuwa lilikuwa likimshikilia, akikabiliwa na kesi ya Jinai.
Tanga: Mahakama kutoa uamuzi kuhusu Polisi kuendelea kumshikilia Kombo Mbwana

IMG_20241112_224611_737.jpg

Unadhani matukio kama haya yanatoa picha gani kuhusu hali ya usalama wetu Wananchi? Ni kweli watu kama hawa hawajuliani?
 
Kiukweli matukio haya yanaleta hofu kwa raia, uwajibikaji unahitajika ili kuondoa hii sintofahamu
 
Nimekaa nikatafakari kuhusu matukio ya utekaji yanayoendelea Nchini, sisi Wananchi tumekuwa tukiumia kadiri siku zinavyoenda, matukio ya utekaji yanaendelea, imani yetu kwa vyombo vya Ulinzi inaanza kupotea.

Mawazo hayo yamekuja baada ya kuona tukio la Mfanyabiashara Deogratius Tarimo alivyonusurika kutekwa na Watu ambao hawajulikani lakini angalau sura zao tumeanza kuziona.

Tukio hilo limeanza kutupa hofu Wananchi wengi wa kujiona hatupo salama, kama matukio yanafanyika mchana kweupe, sura za Watu zinaonekana huku Vyombo vya Usalama vikiishia kusema uchunguzi unafanyika baada ya hapo tunasahau tunasubiri tukio lingine, naona sio sawa.

Pia soma - Inasemekana tukio hili la utekaji limetokea Kiluvya, kutokana na uzito wa jamaa walishindwa kumchukua. Hakuna aliyetoka kumsaidia

Pia soma - Polisi watoa tamko tukio la jaribio la utekaji Kiluvya, wasema uchunguzi umeanza toka aliporipoti Novemba 11, 2024

Inawezekana Watu hawasemi lakini haya mambo yanayofanyika hivi, mdogomdogo yanazidi kuwaaminisha Wananchi kuwa hatupo salama. Serikali inatakiwa kufanya maamuzi magumu kuhusu hao "Watekaji" au ambao "Hawajulikani", tutaishi kwa hofu hivi hadi lini?

Miaka ya nyuma ilikuwa utekaji unafanyika kwa kificho, kama imefikia hatua mambo yanafanyika hadharani basi tunaelekea kubaya.

Hii ni mifano michache tu ya matukio ya hivi karibuni ya Mwaka 2024, achana na yale ya kina Roma na kina Mo Dewji na wengine wengi, haya machache ni ya mwaka huu, mnaweza kunikumbusha mengine pia:

Juni 2024: Edger Mwakalebela “Sativa” alitekwa akiwa Dar es Salaam akapatikana Katavi akiwa amejeruhiwa vibaya, Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
SATIVA: Nilitekwa nikapelekwa Karakana ya Polisi Oysterbay kabla ya kusafirishwa sehemu nyingine na nimepigwa risasi ya kichwa

Septemba 2024: Mwanachama wa CHADEMA, Ally Mohamed Kibao alichukuliwa na Watu wasiojulikana ndani ya basi, mwili wake ukapatikana baadaye akiwa ameuawa. Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
Kuelekea 2025 - Polisi: Tunachunguza kubaini chanzo na watu waliohusika kumchukua Ali Kibao

Novemba 2024: Mkurugenzi wa Dar24 Media, Maclean Mwaijonga alipotea kwa siku mbili akiwa hajulikani alipo, Taasisi yake ikatoa taarifa kwa umma, akapatikana Kigamboni na kueleza kuwa alikuwa na Watu anaofanyanao biashara, akanywa juisi ambayo anaamini ilimfanya akapoteza fahamu.
Mkurugenzi wa Dar 24 apatikana Kigamboni

Agosti 2024: Kijana Shadrack Chaula (24) alichukuliwa na Watu wasiojulikana Mkoani Mbeya, Wazazi wake wakajitokeza kuomba msaada wa kumtafuta kijana wao, Jeshi la Polisi likasema linachunguza na kumtafuta mhusika.
Sakata la kijana aliyechoma picha ya Rais kutoweka lawaibua polisi

Novemba 2024: Vijana wawili walipoteza maisha kwa kupigwa risasi, wengine wawili walijeruhiwa vibaya ikidaiwa walikuwa wakiwakimbia Askari Polisi, chanzo kikidaiwa ni kesi ya uchimbaji mchanga, Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
Zanzibar: Vijana wawili wauawa na wengine 2 kuumizwa vibaya. ACT yataka Jeshi na Polisi kufanyiwa mabadiliko Kimuundo na Kiutendaji

Julai 2024: Mwanachama wa CHADEMA - Tanga, Kombo Mbwana alipotea kwa siku 29, Jeshi la Polisi likatangaza kuwa lilikuwa likimshikilia, akikabiliwa na kesi ya Jinai.
Tanga: Mahakama kutoa uamuzi kuhusu Polisi kuendelea kumshikilia Kombo Mbwana


Unadhani matukio kama haya yanatoa picha gani kuhusu hali ya usalama wetu Wananchi? Ni kweli watu kama hawa hawajuliani?
Ifike sehemu hawa watekaji tukiwashtuki tuwakamate na tuwauwe ndio itakua mwarobaini wa hili tatizo na kama tutakua kila siku tunalalamika watajiona wapo juu alafu tunawapa promo ili wapande vyeo.
 
Nimekaa nikatafakari kuhusu matukio ya utekaji yanayoendelea Nchini, sisi Wananchi tumekuwa tukiumia kadiri siku zinavyoenda, matukio ya utekaji yanaendelea, imani yetu kwa vyombo vya Ulinzi inaanza kupotea.

Mawazo hayo yamekuja baada ya kuona tukio la Mfanyabiashara Deogratius Tarimo alivyonusurika kutekwa na Watu ambao hawajulikani lakini angalau sura zao tumeanza kuziona.

Tukio hilo limeanza kutupa hofu Wananchi wengi wa kujiona hatupo salama, kama matukio yanafanyika mchana kweupe, sura za Watu zinaonekana huku Vyombo vya Usalama vikiishia kusema uchunguzi unafanyika baada ya hapo tunasahau tunasubiri tukio lingine, naona sio sawa.

Pia soma - Inasemekana tukio hili la utekaji limetokea Kiluvya, kutokana na uzito wa jamaa walishindwa kumchukua. Hakuna aliyetoka kumsaidia

Pia soma - Polisi watoa tamko tukio la jaribio la utekaji Kiluvya, wasema uchunguzi umeanza toka aliporipoti Novemba 11, 2024

Inawezekana Watu hawasemi lakini haya mambo yanayofanyika hivi, mdogomdogo yanazidi kuwaaminisha Wananchi kuwa hatupo salama. Serikali inatakiwa kufanya maamuzi magumu kuhusu hao "Watekaji" au ambao "Hawajulikani", tutaishi kwa hofu hivi hadi lini?

Miaka ya nyuma ilikuwa utekaji unafanyika kwa kificho, kama imefikia hatua mambo yanafanyika hadharani basi tunaelekea kubaya.

Hii ni mifano michache tu ya matukio ya hivi karibuni ya Mwaka 2024, achana na yale ya kina Roma na kina Mo Dewji na wengine wengi, haya machache ni ya mwaka huu, mnaweza kunikumbusha mengine pia:

Juni 2024: Edger Mwakalebela “Sativa” alitekwa akiwa Dar es Salaam akapatikana Katavi akiwa amejeruhiwa vibaya, Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
SATIVA: Nilitekwa nikapelekwa Karakana ya Polisi Oysterbay kabla ya kusafirishwa sehemu nyingine na nimepigwa risasi ya kichwa

Septemba 2024: Mwanachama wa CHADEMA, Ally Mohamed Kibao alichukuliwa na Watu wasiojulikana ndani ya basi, mwili wake ukapatikana baadaye akiwa ameuawa. Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
Kuelekea 2025 - Polisi: Tunachunguza kubaini chanzo na watu waliohusika kumchukua Ali Kibao

Novemba 2024: Mkurugenzi wa Dar24 Media, Maclean Mwaijonga alipotea kwa siku mbili akiwa hajulikani alipo, Taasisi yake ikatoa taarifa kwa umma, akapatikana Kigamboni na kueleza kuwa alikuwa na Watu anaofanyanao biashara, akanywa juisi ambayo anaamini ilimfanya akapoteza fahamu.
Mkurugenzi wa Dar 24 apatikana Kigamboni

Agosti 2024: Kijana Shadrack Chaula (24) alichukuliwa na Watu wasiojulikana Mkoani Mbeya, Wazazi wake wakajitokeza kuomba msaada wa kumtafuta kijana wao, Jeshi la Polisi likasema linachunguza na kumtafuta mhusika.
Sakata la kijana aliyechoma picha ya Rais kutoweka lawaibua polisi

Novemba 2024: Vijana wawili walipoteza maisha kwa kupigwa risasi, wengine wawili walijeruhiwa vibaya ikidaiwa walikuwa wakiwakimbia Askari Polisi, chanzo kikidaiwa ni kesi ya uchimbaji mchanga, Jeshi la Polisi likasema linafanya uchunguzi.
Zanzibar: Vijana wawili wauawa na wengine 2 kuumizwa vibaya. ACT yataka Jeshi na Polisi kufanyiwa mabadiliko Kimuundo na Kiutendaji

Julai 2024: Mwanachama wa CHADEMA - Tanga, Kombo Mbwana alipotea kwa siku 29, Jeshi la Polisi likatangaza kuwa lilikuwa likimshikilia, akikabiliwa na kesi ya Jinai.
Tanga: Mahakama kutoa uamuzi kuhusu Polisi kuendelea kumshikilia Kombo Mbwana


Unadhani matukio kama haya yanatoa picha gani kuhusu hali ya usalama wetu Wananchi? Ni kweli watu kama hawa hawajuliani?
Inasikitisha kuona wananchi wakitizama mwananchi mwenzao akilalamika kwenda kuuawa lakini bado wanaangalia. Tanzania bado ina hofu sana, bado watu hawawezi kusimama kujaribu kutetea uma.

Kuna wakati mwingine watu wanaweza kutumia mgongo wa serikali kumbe hata sio serikali ni watu wanadaiana au wana visa vyao binafsi, mwisho wa siku tukapoteza Mtanzania mwenzetu kwa hofu za kizembe kabisa.
 
Back
Top Bottom