Matukio ya viongozi wa CCM kuanza kushambuliwa na kuuawa wa kulaumiwa ni CCM na serikali yake, wameyalea kwa muda mrefu na sasa yanawageukia

Matukio ya viongozi wa CCM kuanza kushambuliwa na kuuawa wa kulaumiwa ni CCM na serikali yake, wameyalea kwa muda mrefu na sasa yanawageukia

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Nimesoma kwamba katibu wa CCM wa wilaya ya Kilolo ameshambuliwa na kuuwawa kwa risasi na watu wasiojulikana. Hivi karibuni huko Songwe kulikuwa na tukio jingine la katibu wa CCM kuvamiwa wa watu wasiojulikana na kuvunjwa miguu.

Songwe: Katibu wa CCM avamiwa na watu wasiojulikana na kuvunjwa miguu yote miwili

Sasa, watu wenye akili walijua kwamba hili lilikuwa ni suala la wakati tu kabla ya kuanza kutokea, kwamba kuna wakati haya matokio dhidi ya viongozi wa CCM yangeanza kutokea, na kuna uwezekano mkubwa yataendelea sana.

Sababu ni kwamba, kwa muda mrefu sana, watu walioonekana kuwa wako vyama vya upinzani ndio walifanyiwa utekeaji na hata kuuwawa. Kila watu walipolalamika, serikali ya CCM haikutaka kuchukua hatua. Katika hali ambayo watu waliouwawa mara zote walikuwa walioonekana kuikosoa au kuikashifu CCM na serikali yake, uongozi wa CCM ulionekana "kufaidika" na kutekwa au kuuwawa kwao, ndio maana kukawa na hisia kuwa vyombo vya dola vilihusika na matukio ya utekaji na uuaji wa hawa watu.

KIla mtu anajua kwamba uongozi wa serikali haikulishinikiza jeshi la polisi kufanya uchunguzi juu ya matukio ya uuaji na utekaji.

Sasa uonevu huu wa muda mrefu wa watu wa upinzani ni wazi ulitoa muda wa kutosha kwa upande wa waliotekwa na kuuwawa kujipanga na kuanza kufanya yale ambayo waliona kuwa wakifanyiwa, bila serikali kuchukua hatua. Matokeo ndio haya tunayaona Kilolo, Songwe, na sijui waapi kwingineko tutarajie.

CCM na serikali yake wanapaswa kulaumiwa kwa haya matukio yanayohusu utekaji uuaji nchini, iwe yanafanywa na kwa sababu za kisiasa au kijambazi, dhidi ya wapinzani au CCM. Mmelilea jambo hili, mliamua kukaa kimya badala ya kulizuia na hatimae wale waliokuwa wakionewa kwa muda mrefu ni wazi walifikia muafaka kwamba njia pekee ni kuwapa radha ya dawa mliyoitengeneza wenyewe dhidi ya wapinzani na wakosoaji wa serikali.

Ni wazi kwamba hawa wanaofanya matukio haya dhidi ya viongozi wa CCM wameandaliwa kwa muda mrefu, na wana ujuzi wa kufanya kile ambacho waliona mnawafanyia wao.

Mliona mkuki kwa nguruwe ni mzuri sana, na sasa mtaona uchungu wa mkuki kwa binadamu, kwa sababu nyie mlijiona ni binadamu na watu wa upinzani waliokuwa wakitekwa na kuuwawa ni nguruwe na hivyo hamkupaswa kufanya chochote. What goes around comes around.
 
gentleman,
acha upotoshaji wa kishirikiana 🐒
Tatizo la hapa Tanzania ni kwamba watu hawataki kuambiwa ukweli. Ukweli wasioupenda watauita porojo au uzushi

1731485723571.png
 
Watu wanapotekwa na kuuwawa na unapata comment kama hizi toka kwa waandamizi wa CCM, unatarajia nini kitafuata?

1731485917789.png
1731489880167.png
 
Kuna mtu anatafutwa hapa. Na lazima apatikane. Hata akihamia Cuba.
 
Tatizo la hapa Tanzania ni kwamba watu hawataki kuambiwa ukweli. Ukweli wasioupenda watauita porojo au uzushi

View attachment 3151197
Ni muhimu sana kutenganisha watu kutolewa kafara na vijana kuchukuliwa misukule kichawi na watu wa chama chao, kwasabb tu ya uongozi ndani ya chama, na mtu kupigwa risasi wazi wazi kabisa suala ambalo ni specific 🐒
 
ni muhimu sana kutenganisha watu kutolewa kafara na vijana kuchukuliwa misukule kichawi na watu wa chama chao, kwasabb tu ya uongozi ndani ya chama, na mtu kupigwa risasi wazi wazi kabisa suala ambalo ni specific 🐒
Hiyo ni psychology tunaita "looking for a flimsy excuse". Yaani hutaki kuchukua hatua kwa sababu unajipa flimsy excuse kuhalalisha wewe kutochukua hatua. Ni ugonjwa wa akili
 
Kama mnavojua ndugu Wananchi. Kwasasa CCM inapitia changamoto mbalimbali za kiuongozi na maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa na ule wa serikali kuu mwakani.
Kutokana na Wananchi wengi kuonekana kukichoka chama hiki kikongwe wameamua kuja na hii sinema ya kumpigia Risasi Katibu wa CCM wilaya ya Kilolo ili ionekae kuwa na viongozi wa CCM wanauwawa hivyo Wananchi wabalance masuala. Ngoja tuone
 
Hata tukio la kushambuliwa Tundu lisu,huenda ni mbinu za chadema kutafuta huruma Kwa wananchi Archana na habari za Chacha Wangwe kuwa na beef na Waandamizi
 
Walisema ni drama.Sasa bila shaka ile drama inaendelea kwenye viunga vya Lumumba.Wajiandae kisaikolojia 'kushiriki' hii drama maana 'script' zimeshaanza kugawiwa.
 
Kila kitu kwako ni ushirikina inaonesha ndio kazi yako hiyo kama huyu
sasa mpotoshaji anatofauti gani na mshirikina gentleman?

mihemko, ghadhab, porojo na story za pata potea bila point ya maana ni ushirikina pia gentleman 🐒
 
Back
Top Bottom