Alikaa gerezani miaka 20 akisubiri kunyongwa kwa mauaji ambayo hakuhusika
Temple ni mji mdogo unaopatikana katika kitongoji cha Bell, huko Texas marekani. Unakadiriwa kuwa na wakazi wapatao 73,600. Aliyekuwa mkuu wa kituo kidogo cha polisi katika kitongoji cha Gray Bwana Randy Stubblefield alikuwa amechaguliwa kuwa mkuu wa kituo hicho mwezi wa 6, mwaka 1993. Ikiwa ni mwaka mmoja na nusu toka akaimu nafasi hiyo, ilikuwa ni tarehe 31 mwezi wa 12 mwaka 1994, yakiwa masaa machache yanahesibiwa kabla ya kuukaribisdha mwaka mpya wa 1995 Bwana Stubblefield alikuwa nyumbani kwake pamoja na familia yake wakiwa wamejumuika pamoja wakisubiria ule muda wa shangwe za mwaka mpya, mara redio yake ya upepo inasikika ikitoa sauti kutoka kwenye mhudumu wa namba ya dharura akidai kwamba amepokea simu ya dharura ya 911 na kwamba kuna mtu inasemekana kajeruhiwa kwa kupigwa risasi au kuchomwa kisu katika mji wa Campbell. Askari ajulikanaye kam Tom Waffer alikuwa njiani kuelekea huko ila pia Stubblefield kama mkuu wa Kituo alihitajika kuwa eneo hilo.
Bila kuchelewa bwana Stubblefield aliondoka nyumbani kwake kuelekea kwenye eneo la tukio ambapo alimkuta askari mwenzake amekwisha fika na kumtaarifu aligundua kijana aliyeshambuliwa alikuwa anaitwa Scooter Keiller, mwenye umri wa miaka 22 akiwa amechomwa kisu katikati ya kifua chake na akiwa ameanguka kwenye eneo la jirani mita kadhaa kutoka alipokuwa akiishi. Alikimbizwa hospitali na alifariki tu baada ya kufikishwa hospitali.
Stubblefield pamoja na Tom wanaanza upelelezi wao kwa kufuata alama ya michirizi ya damu kutoka pale alipokuwa amelala Scooter, alama iliwaongoza mpaka kwenye nyumba ambayo Scooter alikuwa akiishi na kaka yake ajulikanaye kama Randy pamoja na mama yao Bi Twila. Michirizi ya damu ilionyesha kuwa Scooter alitoka ndani ya nyumba yao akivuja damu maana ilizidi kuwaongoza mpaka kwenye mlango wa mbele ambapo makachero hao walifungua huo mlango na kuingia ndani bado sakafuni waliona mchirizi wa damu. Wakiwa ndani ya makazi ya Scooter walishuhudia mwili wa binadamu mwenye jinsia ya kike ukiwa umelala sakafuni kwenye dimbwi la damu. Walipousogelea waligundua tayari binadamu huyo alikuwa amekwisha poteza maisha, mwili wake ukiwa umelala chali uso ukiwa umeharibiwa vibaya kwa kupondwa pondwa na rungu zito la mbao lilikuwa limewekwa pembeni ya mwili huo. Damu ilikuwa imetapakaa kila mahali, matone ya damu yalikuwa yameruka mpaka kwenye kuta najuu ya meza kwenye eneo hilo. Askari walijua moja kwa moja huyu atakuwani Bi Twila.
Stubblefield alielekea kwenye chumba kilicho uani na baada ya kuingia kwenye hicho chumba, alishuhudia mwii wa Randy akiwa kalala kifudifudi kitandani kwake akiwa amejifunika shuka zitompaka chini ya mabega, huku akiwa amevaa earphone masikioni ambayo ilikuwa imechomekwa kwenye kifaa cha kusikilizia mziki (walkman) kikiwa pembeni ya kiwiliwili chake. Stubblefield laimsogelea na alipomfikia aligundua Randy alikuwa amekwishafariki. Mwili wake ulikuwa na majeraha ya kuchomwa visu matatu na jereahakubwa lilikuwa limepenya kwenye moyo wake.
Stubblefield alikuwa akiifahamu hii familia kwa ukaribu sana kwakua hakuwa akiishi mbali sana na makazi yao, na pia alikuwa akikutana nao kanisani kwenye ibada. Pia watoto wa Twila walikuwa ni watoto mashuhuri kwakuwa walikuwa wana vipaji mbalimbali vya michezo hivyo walikuwa wakishiriki sana kwenye michezo jambo liliwafanya wajulikane sana kwa watu mbalimbali.
Stubblefield alikuwa na taarifa kwamba mpenzi wa kiume wa Twila, Bwana Hank Skinner mwenye umri wa miaka 31, alikuwa kahamia hapo miezi mitatu iliyopita. Katika tukio la kuawa kwa familia nzima miili ya watu watu yote ilipatikana kasoro Bwana Skinner ndiye mpaka wakti huo alikuwa hajaonekana jambo ambalo kwa polisi huchukuliwa kwamba huyo mtu ndiye atakuwa mtuhumiwa wa mauaji au na yeye makweisha uawa na mwili wake umefukiwa sehemu nyingine.
Mbaya zaidi Skinner alikuwa kaachiliwa siku kadhaa nyuma kutoka gerezani baada ya kutumikia kifungo cha miezi 8 kwa kosala kushiriki katika uporaji na unyanganyi. Pia alikuwa amekamatwa mara 38 kwa tuhuma mbalimbali. Katika macho na mtazamo wa Stubblefield, alimchukulia Skinner kama mtu mbaya mwenye tabia na mawazo ya kihalifu.
Baada ya Skinner kutoonekana pale, askari walipewa vibari kumtafuta kila mahali kuanzia kwenye mitaa ya karibu na popte atakapoonekana akamatwe. Stubblefield muda wa saa 9 usiku, alielekea kwenye makazi ya mpenzi wa zamani wa Skinner aliyekuwa akijulikana kama Andrea Leed. Leedd alikuwa mpenzi wake Skinner siku za nyuma na mpaka muda huu walikuwa marafiki na ndiye aliyekuwa akimfadhili Skinner kwa kumpatia fedha mara kwa mara.
Stubblefield baada ya kufika na kugonga mlango, Leed alikuja na kufungua mlango na baada ya kujitambulisha alimwambiakuwa anamtafuta Skinner, akamuuliza kama amebahatika kumuona. Jibu la Leedd lilikuwa ndiyo yuko ndani kwangu. Stubblefield na askri mwingine aliyekuwa naye walingia ndani walimshuhudia Skinner akiwa kasimama kwenye korido akiwa kava suruali lilitapakaa matone amdogo madogo ya damu. Pia alikuwa amejifunga bandeji kwenye mkono wake. Stubblefield alipotazama soksi alizovaa Skinner zilikuwa zimejaa damu. Stubblefield alimwambia unahitajika kwa tuhuma za kupiga na kujeruhi mama na watoto wake. Jibu alilotoa Skinner ni swali, “Ni hayo tu hakunatuhuma nyingine?” Skinner alikamatwa na akafunguliwa mashitaka yanayohusiana na makosa matatu ya mauaji ambayo adhabu yake ni kunyongwa mpaka kufa.
Mwanasheria ajulikanaye kama Harold Comer alipewa jukumu la kumtetea Skinner. Kesi yake ilianza kusikilizwa tarehe 4 mwezi wa 3 mwaka 1995. Upande wa mashitaka ukiwa unaongozwa na mwanasheria mkuuw wa wilaya Bwana John Man aliwasilisha mashitaka yake mbele ya mahakama. Ushaidi aliowasilisha John mahakamani ni ushahidi uliopatikana kwenye eneo yaliyotokea mauaji yale. Eneo la tukio kulikuwa na damu nyingi imetapakaa kila mahali na alama za vidole zenye damu za Skinner hasa kwenye mlango wa chumba cha Randy.
Uwepo wa alama za vidole za Skinner halikuwa jambo la kushangaza maana alikuwa akiishi mle, ila uwepo wa alama zake za vidole zenye damu ndiyo ilikuwa ni hoja ya kwamba alitenda kosa lile. Pia awakati anakamatwa alikuwa kava nguo zenye zilizotapakaa amtone ya damu ambayo yalipofanyiwa vipimo vya maabara iligundulika ni damu za marehemu. Huu ushahidi ndiyo bwana John alikuwa akisimamia akitaka mahakama imempe adhabu kali kwa kosa la mauaji ya watu watatu.
Skinner yeye alidai kwamba alikuwa amelewa kwa kutumia dawa za kulevya na pombe, na alikuwa kasinzia kwenye kiti hajielewi wakati tukio la mauaji linatendeka. Kwa maelezo yake wakati wa mahojiano na makachero wa polisi anasema hivi
“Ninakumbuka niliamka kutoka usingizini pale kwenye kwenye kiti, na kugundua kuna mtu kasimama mbele yangu akiwa ameshikilia kisu. Nakumbuka nilirusha mikono, na kunyanyuka kasha kukimbia na kutoka nje ya nyumba. Hayo ndiyo ninayokumbuka tu.”
Asklari aliyekuwa anamhoji anamwambia “Inaonekana kama wewe ndiyo umetenda mauaji hayo”
Skinner anajibu, “KIla mtu anajua ni kitu gani kilitokea kasoro mimi. Laity ningejua ni kitu gani kimetokea ningeliwambia. Lakini sina nilalojua zaidi ya nilichosema. Nawaapia kuwa ninalosema ni ukweli mtupu Mungu ndiye shahidi yangu ni kwamba sijui. Nitamani ningekuwa ninafahamu ni kitu gani kilitokea.”
Stubblefield anadai kwa maelezo ya Skinner anadai kwamba hizo dawa za kulevya na pombe aliyotumia, zilimfanya apoteze fahamu. Stubblefield anadai kuwa haiwezekani uzinduke baada ya kupoteza fahamu umuone mtu ana kisu uwe na uwezo wa kukimbia hapo hapo, pia haiezekan mtu aliyetoka zinduka kutoka kwenye kupoteza fahamu aweze kuzungumza vizuri, kutafakari kwa kina na kujua kwanini alikamatwa na polisi.
Mpenzi wa zamani wa Skinner Bi Andrea Leed, alikuwa ndiye shahidi wa kutegemea na namba moja kwa waendesha mashitaka. Kwa maelezo ya Bi Leed alidai kwamba Skinner alikuja nyumbani kwake, akiwa na damu na jeraha mkononi ambapo alimuomba amsaidie kushona jeraha lake la mkononi na kumwambia aape kuwa hatomwambia mtu kuhusu jambo hilo.
Pia anadai Skinner alimwambia kuwa anahisi amemmuua Twila kwa kudai kwamba amempiga mateke.
Baada ya majaji kusikiliza mashitaka, ushahidi na utetezi wa pande zote mbili, walirudi baada ya saa mbili na nusu na kusoma hukumu kuwa mahakama imemkuta Skinner na kosa la kuua watu watatu. Na pia waliongeza kwamba adhabui ya kunyongwa ndiyo adhabu anayostahili skinner kwa kosa alilotenda.
Skinner alikaa gerezani kwa zaidi ya miaka 20, akisubiria kutekelezwa kwa adhabu yake, kwa kipindi hiki kuna taarifa mpya ilijitokeza ambayo ilikuwa inaonyesha kuwa Skinner hakuwa mhusika katika mauaji hayo baada ya kupatikana mshukiwa mwingne kwenye mauaji hayo.
Akiwa gerezani kwa muda huo wote Skinner alikuwa akiendelea kushikiria msimamo wake kuwa siyo yeye aliyetenda kosa hilo la mauaji. Alizidi kudai mpenzi wake Twila na Watoto wake wanastahili kupata haki kwa polisi kumkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya dola muaji halisi ambaye huenda yuko mtaani akiwa huru anaendela na maisha yake huku yeye akiwa jera akishubiri kunyongwa kwa kosa ambalo hakulitenda.
Lakini waliokuwa majirani zake huko Pampa Texas wao walikuwa wanaamini kwamba haki ilitendeka na Skinner ndiye alikuwa mhusika wa mauaji hayo na kwa sasa alikuwa gerezani akisubiria kunyongwa. Mtu yeyeote angeenda sehemu yoyote katika mji wa Pampa akauliza watu mnawaza nini kuhusu hukumu ya Skinner, watu wangejibu kwamba inafaa awe amenyongwa kabisa wanamchelewesha.
Akiwa anasubiria kunyongwa, ilikuwa imepita miaka mitano toka hukumu yake imetoka, na mwaka 2000 kundi la wanafunzi wa kitovu cha Uandishi wa habari za kiuchunguzi katika Chuo Kikuu cha Nerthurstern walianza kupitia kesi ya Skinner kama mojawapo ya mazoezi katika masomo yao. Emily Probist Miller ambaye alikuwa mkufunzi wa masuala ya kiupelelezi kwa wanafunzi wao akishirikia na Profesa aliyejulikana kama Protass. Ikatokea nafasi kwa Emily kwenda katika Jimbo la Texas kwenye gereza linaloshikiria wafungwa waliohukumiwakunyongwa ili akamfanyie mahojiano Skinner. Yeye kama mwandishi wa habari za kiupelelezi hii ilikuwa ni nafasi ambayo asingeweza kuacha ipite.
Emily aliwatuma wanafunzi wake wamtafute aliyekuwa mpenzi wa Skinner Bi Leed ambaye kwa muda huu alikuwa amebadilisha kwa kupinga ushahidi alioutoa dhidi ya Skinner wakati wa kesi. Wanafunzi walimtafuta na kufanikiwa kumpata kasha walifanya mahojiano naye. Kitabia alikuwa mwanamama mtata sana ambaye alikuwa anakasirika haraka na ndani mwake alikuwa akiishi na nyoka.
Sharti alilowapa ni kwamba asirekodiwe kwa video au kupigwa picha bali alikodiwe sauti tu. Haya chini ni mahojiano yake baina yake na wanafunzi wa Emily.
Mwanafunzi: Uliwambia polisi, na kutoa ushahidi mahakamani kuwa Skinner alikuja mwenyewe hapa, na alipokuja ulienda uani kuwatazama watoto wako. Je ni kweli?
Leed: Hapana. Askari walikuwa walikuwa wananitisha, na kunifanya nijihisi kama ninajaribu kumlinda Skinner, na kama ningeendelaa kumtetea ningeweza kufungwa pia.
Mwanafunzi: Je ni kweli kwamba Skinner alithibitisha kwako kuwa alimuua Twila na watoto wake wakiume wawili?
Leed: Hapana hakuwahi.
Mwanafunzi: Hivyo una maana kwamba alikuelezea juu ya kutenda kwake jambo flani, lakini wewe hukuamini kama alikuwa anakiri juu ya kuhusika kwake kwenye mauaji?
Leed: Hapana
Wakati wa kesi, waendesha mashitaka alimchukua Andrea Leed wakampandisha ndege mpka Fort Worth na kumpangia chumba kwenye hoteli. Leed anadai kwamba alikuwa kama kawekwa kwenye kifungo cha nyumbani.
Emily anasema kwamba aliona kiapo alichokula Leed mwaka 1997, Leed anadai kwamba alikuwa akitishiwa na polisi na kujiona kama mfungwa na alianza kupata wasiwasi kuwa huenda na yeye wanaweza kumtafutia ushahidi utakaomweka pia katika eneo la tukio hivyo aliamua kukubari kufanya kile askari watakachotaka.
Emily akiwa kwenye gereza la wafungwa wanaosubiri kunyongwa, Skinner aliletwa kwa ajili ya kufanya naye mahojiano na anakumbuka kitu cha kwanza alichomwambia Emily ni kwamba hahusiki namauaji yale. Alimwambia angependa dunia ijue kuwa yeye siyo mhusika kwasababu failia ya marehemu wanaumia sana kwasababu ya kilichotkea na mtuhumiwa halisi yuko mtaani. Aliendela kusema kuwa hakukuwa na sababu yoyote ya yeye kumuua Twila na wanaye kwakuwa alikuwa anampenda sana Twila kuliko kitu chochote dunia hii. Emily anadai katika kuzngumza naye Skinner alimwambia kuna mshukiwa mwingine ambaye polisi hawakumfuatilia na anaitwa Robert Donnell.
Robert Donnell aliwahi kufungwa kwa kosa la wizi, uporaji na kudhuru watu. Alikuwa ni mjomba wake Twila na watu wengi walikuwa wakimwita kama Uncle Bob. Skinner anadai alikuwa ana tabia ya kuja nyumbani kwa Twila na kumyeshwa pombe kasha Twila akishalewa alikuwa anajaribu kumwingilia kinyume na maumbile. Jopo la wanasheria waliokuwa wakimtetea Skinner walimwambia Emily pia kuwa walimwingiza Donnel kwenye kesi kama mshukiwa ambaye anaweza kuwa alihusika kwenye mauji hayo badala ya Skinner kutokana na maelezo ya Skinner kuwa aliwahi kumkuta Donnel akiwa anajaribu kumbaka Twila ndipo yeye akaingia ndani ghafla. Hili tukio lilitokea wiki kadhaa kabla ya mauaji hayo.
Skinner anadai kwamba alimkuta Donnell akiwa kamfunga kamba Twila huku akiwa katika harakati za kumuingilia nyuma huku Twila akiwa anajaribu kujitetea, Donnell akawa anamambia akileta vurugu atamuua. Skinner anadai alimvamia Donnell akampiga kasha kumburuza na kumwingiza kwenye gari lake na kumwamuru aondoke na asirudi hapo kamwe. Anasema kuwa hawakutoa taarifa polisi kwakuwa lilikuwa tukio la aibu ukizingatia yule alikuwa ndugu wa damu kwa Twila hivyo waliamua kuwa hawatolizungumzia.
Wanafunzi wa Emily, waliafanya kazi ya kutafuta mashahidi wanaoweza kuthibitisha madai haya ya Skinner na wanafanikiwa kumpata mwanamama Vicki Treat ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Twila. Vicki anadai kuwa anamfahamu Uncle Bob kama mjomba wake Twila na anadai walikuwa wakifanya ngono mra kwa mara na Twila alipoamua kuacha kufanya ngono naye Uncle Bob mara kadhaa alijaribu kumbaka. Na alidai kwamba Twila mwenyewe aliwahi kumwambia mara kadhaa kuwa Uncle Bob amejaribu kumbaka. Pia anadai kwa upande wake anahisi ni Uncle Bob aliyeua ile familia kwakuwa alikuwa anaona wivu Skinner kuishi pale nyumbani kwa Twila.
Katika mahojiano ambayo Emily alifanya na baadhi ya watu waliomuona Skinner usiku ule wa mauaji, wote hawaamini kama Skinner alitenda mauaji yale kwa jinsi alivyokuwa kalewa na hajiwezi. Howard Mitchell ambaye alikwua ni rafiki yake Twila anadai kwamba yeye alipita kwa Twila kusalimia usiku huo na alimuona Skinner akiwa kalala kwenye kiti hajitambua anakoroma tu akiwa kasinzia na ananuka pombe.
Wakati Skinner akiwa kalala pale kwenye kiti, Twila aliondoka na gari kuelekea kwenye tafrija ya kusubiri mwaka mpya ambapo kwenye tafrija hiyo Uncle Bob alikuwepo. Mtoto wa wa kike wa Horwad Mitchell ajulikanaye kama Sarah alikuwa kwenye hiyo tafrija pamoja na Twila na Uncle Bob.
Haya ni mahojiano aliyofanyiwa na wanafunzi wake Emily
Mwanafunzi: Je uliona jambo lolote la ajabu baina ya Uncle Bob na Twila usiku huo?
Saraha: Ndiyo, Uncle Bob alikuwa akimfuata fuata Twila kila mahali akimghasighasi, pia alikuwa hatakiazungumze na wanaume na alikuwa akifanya vitu vya ajabu ambavyo hakupashwa kufanya. Pia alikuwa akijaridbu kuanzisha mazungumzo ya kingono na Twila.
Twila na Uncle Bob walikuwa sehehmu moja muda mfupi kabla ya mauaji hayo kutokea, na shuhuda andai alikuwa akimghasighsi na kumsumbua. Jambo hili lilihitaji kufanyia upelelezi na polisi lakini hawakufanya hivyo.
Wakiwa sasa wamepata sababu za kufikiria kuwa huenda Uncle Bob ndiye mhusika wa mauaji hayo, Emily na wanafunzi wake sasa wanakaribia kugundua kuwa kulikuwa an ushahidi unaonyesha uwepo wa Uncle Bob katika eneo mauaji yalipotokea.
Emily akiwa na wanafunzi wake anapewa picha zilizopigwa eneno la tukio wakati wa kukusanya ushahidi. Katika picha hizo wanaona koti la kuzuia baridi lililokuwa pembeni ya mwili wa Twila. Koti hilo lilikuwa ni kubwa likiwa na size kati ya 44-46, hii ilikuwa nisize kubwa kwa Skinner kwakuwa hakuwa na umbo kubwa la kuvaa koti kubwa kiasi hicho. Mtaalamu wa masuala ya kukusanya ushaidi eneo la tukio aliyekusanya ushahidi siku ya mauaji alisema bila shaka mhusika alikuwa kava koti hilo wakati akitenda mauaji hayo kutokana na sababu kwamba, sehemu ya mikono ya koti hiyo ilikuwa imelowa damu na pia koti zima lilikuwa lina madoa ya damu.
Kwa kuhisi huenda lile koti lilikuwa limevamiliwa na Uncle Bob, wanafunzi walifanya mahojiano na Beborah Ellis jirani yake Uncle Bob. Deborah ndiye aliyekuwa akimwangalia mkeweUncle Bob ambaye alikuwa mgonjwa asiyejiweza. Yafuatayo ni mahojiano baina ya wanafunzi na Deborah.
Mwanafunzi akimpa picha ya koti hilo Deborah: Hii ni picha ya koti lililokutwa eneo la tukio.
Deborah: Sijui lilifikaje eneo hilo ila hili ni koti la Robert donnell, nina hakika juu ya hilo. Na sikuwahi tena kumuona Robert akiwa kava koti hili baada ya kutokea mauaji hayo. Sikuwahi hata siku moja.
Pia Deborah anakumbuka kumuona Uncle Bob akilifanyia usafi gari lake asubuhi sana baada ya usiku wa mauaji. Anadai kuwa Bob alitoa kila kitu kwenye gari ikiwemo viti na makapeti na alifanya usafi ambao hakuwahi kumuona akiufanya kwenye gari hilo. Na Deboraha anadai mke wake Donnell alikuwa anahisi kuwa mumewe kahusika kwenye mauaji hayo na alikuwa kaimuuliza mara kwa mara ni nini kilitokea kwa kwa Twila na watoto wake na kama alikuwa kahusika.
Deborah anadai mke wake Bob alimwambia kuwa Bob alimwambia kama hatofunga mdomo wake na kuacha kumuuliza kuhusu masuala hayo atapata kilichowapata na atamfanya kama vile alivyowfanya watu hao anaowaulizia. Hii kauli ina maana alikuwa anamwambia kuwa atamuua kama alivyowaua akina Twila.
Miaka mitatu baada ya mauaji hayo, Robert Donnell alikuwa akiendesha gari huku akiwa amelewa sana alipovamia trela la trekta na kuligonga, alifia pale pale kwenye ajali. Hivyo muda huu hakuwepo kuhojiwa wala kujitetea jambo ambalo aliyekuwa Mkuu wa kituo na aliyechunguzqa kesi hiyo na kumkamata Skinner Kachero Stubblefield anadai kwamba Donnell hakuwahi kuwa mshukiwa, hivyo kwakuwa alikuwa tayari amekwishafariki Skinner aliamua kumtuhumu mtu ambaye alijua wazi hawezi kujitetea maana ni marehemu tayari.
Kutokana na ugunduzi huu, mwanasheria ajulikanaye kama Robert Owen anaamua kuungana na wanasheria wake kukata rufaa dhidhi ya hukumu aliyopewa. Hallen pia ambaye alikuwa ni mkufunzi katika chuo Kikuu cha Texas, alishangaa kugundua kuwa lile koti halikuwahi kupelekwa maabara kwa ajili ya kupima DNA la aliyekuwa kalivaa. Anadai kuwa lile koti lilikuwa na nywele, jasho pia damu kitu ambacho ilikuwa ni rahisi kupata DNA kutoka kwenye koti lile. Lakini polisi hawakuwahi kufanya hivyo.
Owen aliamini alikuwa na sababu tosha zitakazomwezesha kukata rufaa kwakuwa waendesha mashitaka walishindwa kufanyia vipimo vya DNA lile koti na kuna ushahidi mwingine ambao hawakuuzingatia. Hapo sebuleni polisi walikuwa kuna mfuko wa plastiki mweusi wa takataka ambapo ndani yake kulikuwa na kisu na taulo kwa ajili ya kukaushia mikono baada ya kunawa. Pia vitu hivi polisi hawakuvifanyia vipimo. Pia kulikuwa na kisu kingine kilichopatikana kwenye mlango wa mbele wa kuingia kwenye nyumba ya Twila ambacho ndicho kinahisiwa kuwa ndicho kilitumika kuwaua Randy na Scooter, pia polisi hawakufanya vipimo pia.
Mwaka 2001 wanasheria wa Skinner waliomba mahakama itoe kibari cha kufanyia vipimo vya DNA, ushahidi uliokusanywa kutoka eneo la mauaji. Mwanasheria mkuu wa Wilaya John Man alikataa kwa kupinga ombi hilo kwamba kwenye kesi hilo hawakuhitaji kupima DNA kwakuwa walikuwa na ushahidi wa kutosha unaoonyesha kwamba Skinner ndiye alihusika na mauaji hayo. Hivyo walikuwa na sababu zote za kuamini kuwa watashinda pasipo kuhitaji kufanya kipimo cha DNA.
Skinner alisema tatizo ni kwamba Mwanasheria wa Wilaya alikuwa amekwishafanya maamuzi yake moja kwa moja usiku huo alipfika kwenye eneo mauaji hayo yaliyotokea. Alikuwa amekwisha hitimisha kwamba Skinner ndiye aliyetenda kosa hilo hivyo hawakutazama uwezekano wa kuwepo kwa mtu mwingine ila walikuwa wanafanya upelelezi wao wakilenga matokeo yahitimishe majibu kwamba Skinner ndiye muaji. Aliendela kusema kuwa kuna ushahidi kuwa mwanasheria alizungumza mara kadhaa na vyombo vya habari akimtuhumu kuwa Skinner ndiye muaji hata kabla ya Mahakam kumkuta na hatia hiyo. Mfano kuna chombo cha habari kilimnukuu John akisema kuwa ataiomba mahakama imhukumu kunyongwa Skinner kwa kosa alilotenda.
Skinner alizidi kudai kwamba, ni vigumu kwao kukiri kuwa walifanya makosa na kukubari upelelezi na ushahidi ufanyike upya. Alidai jambo ambalo wanqataka kwa muda huo ni yeye kunyongwa na habari ili habari yake iishe bila makosa yao kuonekana na anahisi watafanikiwa katika mpango huo.
John anadai kwamba mwanasheria wa mwanzo aliyemsimamia Skinner alikuwa anajua kuhusu ushahidi wa koti na visu na kwamba polisi hawakuufanyia vipimo, ila nay eye aliamua kutoomba ufanyiwe vipimo.
Emily baada ya kuona ,wamasehria wa wilaya kagoma kuruhusu vipimo vya DNA kufanyika hivyo ni vigumu rufaa ya Skinner kusikilizwa, aliamua kugeukia vyombo vya habari kwa kulipeleka hili swala katika vyombo vya habari ili lipate umaarufu na kuifanya msukumo wa kutaka ukweli ujulikane utoke kwa jamii ili kuilazimu serikali kuangalia upya hii kesi. Kila chombo cha habari kilichopata kusikia kisa hiki kutoka kwa Emily kilirusha habari hiyo.
Mwendesha kipindi wa Tv moja ajulikanaye kama nancy Grace aliwaalika Emily na mkufunzi mwenzake Profesa Protas pamoja na Mwanasheria wa wilaya Bwana John aktika kipindi chake ili apate kuwahoji na washindane kwa hoja. Hii ni baadhi ya shemu ya mahojiano:
Grace: Inawezekanaje Skinner akawa an damu kwenye nguo zake kama siyo muuaji na hakuwepo eneo la tukio.
Prof Protas: Skinner hakatai uwepo wake wakati mauaji yanatokea, bali anadai kwamba alikuwa hajitambui na alikuwa kalal kwenye kiti na ripoti ya vipimo vya ulevi inaonyesha kweli alikuwa kalewa. Pia wanafunzi wangu walihoji watu mbalimbali ambao wanaunga mkono kuwa Mjomba wake Twila ndiye anaweza kuwa muuaji halisi katika kesi hii.
John: Tulipata anfasi na tulikuwa na taarifa zote hizo unazosema, Donnell alifuatiliwa na akaonekana hakuwa na uhusika wowote. Unaongea tu habari ulizosikia kutoka huko mtaani ila nakwambia Skinner ndiye mhusika na kapata haki yake ambayo ni kunyongwa.
Prof Protas: Bwana John samahani, kuna alama za vidole zenye damu zilikutwa kwenye mlango na pia kwenye kisu. Je unaweza kuungana na mimi kwa kukubari kufanyika vipimo vya ushahidi uliokusanywa kutoka eneo la mauaji kabla ya mtu huyu asiye na hatia hajanyongwa?
Baada ya mwezi mmoja toka hicho kipindi cha mahojiano kirushwe, John alibadiri msimamo wake na kukubari kufanyika kwa vipimo vya DNA kimya kimya bila kuhusisha jopo la wanasheria wanaomtetea Skinner. Alichukua baadhi ya vitu na kuvituma kwenye maabara na kuwapa maelekezo nini wapime kutoka kwenye vitu hivyo.
Kati ya vitu alivyotuma kwa ajili ya kufanyia vipimo zilikuwemo neywe ambazo zilikutwa katika kiganja cha Twila. Kutokana na DNA majibu yalirudi kua nywele zile siyo za Skinner ila ni nywele ambazo mwenye nazo atakuwa na undugu naTwila upande wa mama. Nywele zile zilionekana toka mwanzo kuwa siyo za Twila wala watoto wake kutokana na kwamba zilikuwa nywele tatu zenye rangi tofauti japo kwa mbali ungehisi zina rangi moja. Hivyo wakina Emily walitegema aktika hali ya kawaida Mahakams ianze kufikiria kuwa mwenye hizo nywele huenda akawa Donnell. Lakini kwakuwa haikuweza kuthibitika moja kwa moja kuwa zile nywele zilikuwa za Donnell, mwanasheria wa wilaya alifunga kabisa uwezekanao wa kufanya DNA kwa vitu vingine kwakuwa yeye na wenzake walidai huenda zile nywele zilikuwa za watoto wake.
Stubblefield yeye alikuwa anahisi Skinner anajua kabisa kuwa alitenda kosa hilo ila tu anajaribu kukata rufaa moja baada ya nyingine akiwa anaamini kuwa kukata kwake rufaa kutamsaidia mahakama ya Texas kumwondolea hukumu ya kifo apewe hukumu ya maisha.
Skinner yeye anadai swala la kuthibtisha nani aliua siyo kazi yake hiyo ni kazi ya polisi, yeye kazi yake ni kuthibitsha kuwa hakuua na kupitia huo ushahidi ambao hawataki ufanyiwe vipimo vya DNA.
Picha ya pamoja kati ya Sadrina na Skinner
Mwaka 1996, mwanaharakati wa ufaransa mpinga adhabu ya kifo, mwanamama Sandrina O’jeoj alianza kuwa anaawaandikia barua baadhi ya wafungwa wanaosubiri kunyongwa kwenye gereza la Texas, mmoja kati ya wafungwa aliokuwa akiwandikia barua alikuwa Skinner. Andai kwamba Skinner ni mtu anayependa kujichanganya, ana huruma japo mara nyingine ni mkali. Anasema walianza kuwa wanaandikiana barua na Skinner alimuadikia kuhusu kisa chake na moja kwa moja alianza kuona kuwa kuna mashaka juu ya uhusika wake kwenye mauaji yale.
Akifanyiwa mahojiano na kituo cha TV cha CNN Sandrina aliuliza na mwendesha kipindi kwanini anaamini kuwa Skinner hakuhusika wakati hakuwepo eneo la tukio. Sandrina alijibu kwamba hii ni kutokana na sababu kwamba ushahidi uliokuwa eneo la tukio koti na kisu kilichotumika kuwaua watoto mpaka leo havijawahi kufanyiwa kipimo cha DNA.
Akiwa na shauku ya kutaka kujua ni kwanini John hakuwa amepeleka huo ushahidi kufanyiwa vipimo, Sandrina anaamua kusafiri kwenda Pampa kwa ajili ya kukutanana John. Alama za vidole vyenye damu zilizokuwa kwenye mlango na kwenye kisu hazikuwa za Skinner, je zilikuwa za nani na kwanini mwendesha mashitaka hafanyi juhudi kupima ili ijulikane ni alama za nani.
John alidai kwamba kukataa kwake kufanyaia DNA kwakila kitu ilitokana na sababu kwamba huwezi kumpakazia marehemu kuwa amehusika kwenye mauaji kwa kusingizia kwamba kuna vitu ambavyo havikupimwa DNA. Aliendelea kudai kuwa wanasheria wa Skinner hawakutaka kusisitiza vipimwe DNA kipindi cha kesi kwakuwa walijua kuwa isingemsaidia ila yeye baaada ya kusikia kuwa Donnell kafariki ndipo alianza kudai DNA kwa kuwa aliona ni njia itakayomsaidia kupata rufaa na kuanza kukata rufaa ikishindikana anakata nyingine na hiyo kweli ilimsaidia maana angekuwa amekwisha nyongwa kufikia wakati huo.
Owen yeye anadai kwamba , huo utetezi ni wa ajabu ukichukulia kwamba kuna mtu ambaye anasubiri kunyongwa nab ado anadai kutohusika kwake kwenye mauaji hayo, kwanini ili kuondoa mashaka wasipime kila kitu.
Mwaka 2005, Owen alikata rufaa akidai kwamba John alikosea kwa kutofanya vipimo vya DNA kwenye ushahidi uliokusanywa eneo la tukio, jambo amabalo lilifanya ushahidi kutokamilika. Pia John aligundua kwamba mwanasheriahuyo hakupeleka majibu ya vipimo vya pombe aliyofanyiwa Skinner mahakamani. Mtaalamu aliyepima kiwango cha pombe kwenye damu ya skinner aliandika kwenye ripoti yake kwake kiwango cha pombe kwenye damu ya Skinner kilikuwa 44 ambacho kinatosha kumfanya azimie na kutojitambua. Lakini John anapinga kwa kusema kwamba Skinner alikuwa kavunjika mbavu miezi miwili nyuma na alikuwa akitumia dawa za kutuliza maumivu ambazo zinaweza kuonekana kama pombe kwenye kipimo ndiyo maana hakuona umuhimu wa kupeleka majibu hayo mahakamani.
Kuthibitisha haya Mahakam ilimuita Daktari Michael Chimales ambaye alikuwa amemtibu Skinner majeraha ya kuvunjika mbavu nne miezi miwili kabla ya mauaji. Dakatari anadai kwamba Skinner alimwambia kuwa dawa za maumivu alizokuwa akimpatia hazimsaidii bado anahisi maumivu, aliamua kumuanzishia dawa zenye nguvu sawa na dawa za kulevya zijulikanazo kama Nacotics. Akiwa hapo hospitali anakumbuka kutokana na nguvu za dawa hiyo aliwamwambia nesi kuwa anataka akae amefungua mlango wa wodi alipokuwa kalazwa Skinner na awe anamtazama mara kwa mara, na nesi alikuja kumwambia dakatari kuwa alimuona Skinner akichomoa sindano ya drip kutoka mwilini mwakae na kuiweka kwenye mfuko wa suruali lake. Daktari anadai kuwa Skinner alikuwa mjanja sana hakutaka kununua madawa mtaani.
Owen anadai kwamba kutokana na maelezo ya daktari ni kwamba Skimmer alikuwa hapendi kununua dawa za kulevya mtaani na ndiyo maana hata dawa za maumivu ziliposhindwa kumsaidia alimfuata daktari ampe dawa mwenyewe, hii inaashiria kwamba ahkuwa mtumiaji wa mara kwa mara wa dawa za kulevya. Anaendelea kudai kwamba pombe na Nacotics alizokuwa akimeza lazima zilimfanya apoteze fahamu siku ile ya mauaji kwa kipimo cha 44, njia pekee ambayo ingeweza kumfanya asipoteze fahamu ni kama angekuwa mtumiaji wa dawa za kulevya mara kwa mara.
Skinner mwenyewe anasema walikuwa na tafrijajioni ile, alitumia dawa zakea na akanywa pombe baada ya hapo alianza hisi kizunguzungu, hakuweza kutembea vizuri hakuweza kuongea hivyo alijivuta mpaka sebuleni kajitupa kwenye kiti ambapo hakumbuki chochote mpaka alipokuja kushituka akakuta Twila amelala sakafuni na kuna mtu kasimama mbele yake na kisu.
Mahakama inakubariana na Owen kwamba, John alipashwa kuleta ripoti ya vipimo vya pombe mahakamani wakati wa kesi lakini waliongeza kuwa ripoti hii isngebadilisha maamuzi ya mahakama. Pia wanakubariana na John kwamba maamuzi yake ya kutopima DNA baadhi ya vitu ilikuwa ni njia sahihi nay a kisheria wakati wa kujaribu kumtia hatiani mtuhumiwa.
Owen anadai kila ushahidi waliokuwa wakiiuleta mahaka ilikuwa inadai usingeweza kubadilisha maamuzi ya mahakama kwakuwa haukuwa na nguvu. Owen anadai haukuwa na nguvu kwakuwamahakama ilikuwa ikitazama ushahidi kama kitu kimoja kimoja lakini ingeutazama kwa vitu vikiwa pamoja, kuna sababu ya kuwa na mashaka juu ya hukumu aliyopewa Skinner.
Kabla hata ya DNA kupimwa, mahakama inapanga tarehe ya Skinner kunyongwa ambayo ni tarehe 24, mwezi wa 2 mwaka 2010.
Mwaka 2010 Skinner alikuwa amekaa gerezan kwa miaka 15, akiwa amejaribu kukata rufaa mara kadhaa na kukataliwa. Tarehe 24, mwezi wa 2 mwaka 2010, Skinner alihamishiwa kwenye kitengo cha unyongaji kilijulikanacho kama HuntsVille Unit kilichopo katika jimbo la Texas. Hapa ndipo watuhumiwa wengi wa mauaji USA huletwa kwa ajili ya kunyongwa. Muda wake wa kunyongwa ulipangwa kuwa ni saa 6 kamili mchana.
Owen na wenzake walitoa pingamizi la kujaribu kuzuia zoezi la kunyongwa kwa Skinner lakini hawakufanikiwa. Muda ulikuwa unakimbia. Owen alimwambia Skinner kuwa, “Sikia Skinner ninataka niwe mkweli juu ya hili, ni kwamba naona huu ndiyo mwisho wake hivyo jiandae maana tumejaribu njia zote imeshindika hivyo jiandae kwa kunyongwa”.
Emily ambaye mwaka 2010 alikuwa ni mtayarishaji wa vipindi vya CNN (nadhani mnamkumbuka huyu ndiye alikuwa mkufunzi awali), alikuwa akifuatilai hiyo kesi kutoka kwenye chumba cha habari huko Atlanta. Akiwa ana ujauzito wa miezi mitano wakati huo, alisimama na kupiga kelele kuwa kuna mtu amepangiwa kunyongwa huko Texas siku hiyo, na amekuwa akiomba ushaidi ufanyiwe vipimo vya DNA, tafadhali waandishi wa habari nawaomba hili tukio lisipite hivi hivi bila kuangaziwa macho.
Kwa upande wa Sandrina ambaye alikuwa akifuatilia kesi hii kwa zaidi ya miaka 10, hii kesi kwa sasa alikuwa anaichukulia kama yake. Sandrina aliwambia rafiki zake na wafanyakazi wenzake kuwa kunajambo hamjui kuhusu maisha yangu. Aliwambia kuwa kaolewa na mumewe atanyongwa siku hiyo huko Texas. Sandrina na Skinner walikwua wakiandikaina barua kwa miaka 12, na mara kadhaa alikuwa akimtembelea gerezani, walijikuta wakianzisha mahusiano ya kimapenzi na wakaoana mwaka 2008.
Sandrina na familia ya Skinner waliruhusiwa kumuona kwa mara ya mwisho. Mtoto wa Skinner aliyemuacha akiwa na umri wa miaka mine alikuwa hamkumbuki baba yake wakati mtoto wake mwingine aliyemuacha akiwa mdogo kabisa alikuwa hamjui kabisa baba yake. Siku hiyo ndiyo walikuwa wanamuona baba yao na kufanyika utambulisho upya ambao huenda ulikuwa ni utambulisho na mara ya mwisho ya kumuona baba yao.
Akiwa gerezani anaambiwa kuwa familia yake inakuja kumuona anaambiwa kuwa ajaribu kuwa jasiri, naye anajibu kuwa atakuwa ajsiri kwa ajili ya wanaye na mkewe na wanafamilia wengine kwa kutoonyesha masikitiko. Na kweli anapozungumza na familia yake anawashauri kwamba wakitoka hapo wapande ndege warudi makwao kama hakuna kilichotokea ila tu wamkumbuke kwa mazuri aliyofanya akiwa pamoja nao. Akiwa anazungumza nao askari anakuja anamtaarifu muda wa kuzungumza umekwisha anamuondoa kwenye simu bila hata kumpa nafasi ya kuwambia kwaheri.
Kachero Stubblefield aliendesha gari mwendo wa maili 500, kushuhudia Skinner akinyongwa, ambapo yeye andai kuwa alimuahidi mama yake Twila kuwa ataenda kushuhudia muaji wa manaye na wajukuu zake akinyongwa hivyo alitaka kutimiza hiyo ahadi. Pia anadai yeye ni kati ya watu wanaounga mkono adhabu ya kifo kwa watu amabo hasa wametenda mauaji. Anaongeza kuwa asamehewe kwa mtazamo wake kama utakuwa unamkera mtu lakini Biblia inasema Jicho kwa jicho na yeye ndicho anachounga mkono.
Saa nne kamili, Skinner alipewa mlo wake wa mwisho na kuombewa mara ya mwisho kutoka kwa mchungaji. Baada ya hapo alianza kuandaliwa kwa ajili ya kupelekwa kwenye chumba cha kunyongea ambacho kimezungushiwa nondo huku upande wa pili ni sehemu kwa ajili ya watazamaji ambapo familia ya anayenyongwa na askari pamoja na viongozi wa serikali ndiyo wanaoruhusiwa kushuhudia.
Stubblefield na baadhi ya wanafamiila wa Skinner ndiyo walikuwa eneo la kushuhudia. Akiwa analetwa kutoka kwenye vyumba vya ndani kuelekea kwenye chumba cha kunyongea kwa ajili ya kufungwa kwenye kitanda cha kunyongea, mara simu inaita na habari inayoletwa ni kwamba Mahakama ya Juu kabisa (supreme court) imesitisha zoezi la kunyongwa kwako. Skinner anakosa la kusema, anshindwa zungumza, anashindwa kuhema vizuri, mate yanamkauka anahisi furaha na majonzi kwa pamoja.
Familia wanapopata hii habari wanalipuka kwa furaha na vilio pia maana ulikuwa kama muujiza. Simu ile ilikuwa imepigwa na Owen ambaye kumbe muda wote alikuwa bado hajakata tama alikuwa akihangaika kuangalia namna ambavyo anaweza kuzuia zoezi hilo.
Stubblefield na wanafamilia wanatoka kwenye kile chumba cha kushuhudia na wanakutana na watu wakiwa na mabango wakiwa wanaandamana kupinga kunyongwa kwa Skinner na mabango yakiwa yanataka vipimo vya DNA vifanyike. Stubblefield anaingia kwenye gari lake na kuondoka huku hajaridhishwa na maamuzi hayo.
Owen anadai hii ilikuwa ni kesi ya aina yake ambayo ilikuwa ni rahisi kukukatisha tamaa. Anadai kwamba japo mahakama ya juu ilisitisha kunyongwa kwake kwa muda huo, ilikuwa inaabidi warudishe shauri lao mahakama ya wilaya na kuanza upya.
Mwaka mmoja baada ya maamuzi ya mahakama ya juu, kusitisha kwa muda kunyongwa kwa Skinner, jimbo la Texas linabadiri sheria zinazohusiana na kupima DNA, na hii ilimpa nafasi Owen kuweza kupima ushahidi wote uliopatikana kwenye eneo la tukio.
Koti lile lilikutwa pembeni ya mwili wa Twila ndio ushahidi wa msingi ambao owen alitegemea, kutokana na sheria mpya ofisi ya mwendesha mashitaka ilimtaarifu Owen kuwa wamekubari kufanya vipimo lakini kuna tatizo moja, hawana lile koti eti limepotea. Skinner alipopata hii taarifa alishangaa kwamba wamepanda kwa muda mrefu wakijaribu kuiomba ofisi ya mwanasehria ikubari kupima DNA lile koti na sasa wanapokubari wanadai limepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Ofisi ya mwanasheria inadai kwamba uwa inatokea kwa bahati mbaya mara nyingine ushahidi unachanganywa au unapotea wakati wa kusafirishwa kutoka chumba cha kuhifadhia ushahidi kupelekwa mahakamani lakini anadai kwamba ni makosa ya kibinadamu na hainabudi kukubari kwamba makosa hufanyika na kutarajia makosa mara nyingine.
Owen yeye anadai hakuna sababu inayoweza kueleza na kueleweka ushahidi mkubwa kama lile koti lilivyokuwa kubwa, inawezekanaje ukapotea hivi hivi tu, anaendela kudai kwamba inashangaza zaidi hasa kwenye kesi hiyo ambapo wameweza kuhifadhi hata ushahidi wa vitu vidogo kama kucha zilizookotwa eneo la tukio na nywele lakini koti lipotee. Owen anadai kwamba mwaka 2005 wakati wakipagania rufaa ya Skinner, aliwapata anfasi ya kumuuliza John aliposimama mahakamani kama shahidi na alimuuliza anafikiri kwamba kitengo cha polisi cha Pampa kilikuwa na uwezo wa kuchunguza na kukusanya ushahidi kwenye eneo la uharifu kama huo ambao uko kwenye kesi hiyo. Jibu la John lilikuwa Hapana kabisa. Sidhani kama hiki kitengo cha polisi kina uwezo unaohitajika kufanya hivyo.
Kutokana na kutokuwepo kwa koti hilo basi lisingeweza kutumika kama ushahidi hivyo walifanya vipimo vya vitu vingine, ofisi ya mwanasheria mkuu ilidai kwamba matokeo ya vipimo hivyo yalishindilia msumari juu ya uhusika wa Skinner kwenye mauaji hayo. Msaidizi wa mwanasheria mkuu anadai kwamba vipimo vilionyesha kwamba damu aliyokuwa nayo Skinner ilikuwa imesambaa kila mahali, kuanzia suruali alilokuwa amevaa maeneo ya miguu, sehemu za kola la shati lake, mikononi, ndani ya meneo ya miguu ya suruali lake, sehemu ya nyuma na oembeni ya nguo zake na hii hali wanadai isingeweza kutokea isipokuwa kama alikuwa anatembea tembea wakati damu ikiwa inaruka.
Owen yeye anadai kwamba inajulikana kwamba Skinner alikuwa na jeraha mkononi alilopata baada ya kuchanwa na kisu alichokuwa nacho huyo mtu anayedai alipozinduka alikuta kasimama mbele yake, na huenda ndio chanzo cha damu ile kuruka nyuma ya nguo zake.
Pia vipimo vilionyesha kwamba alama za kiganja chenye damu iliyoachwa kwenye Mlango wa chumba cha Gray ilikuwa sawa na kiganja cha Skinner. Kile kisu kilichoachwa mlango hakikuwa na damu ya Skinner jambo ambalo Owen anadai kwamba kama kweli Skinner ndiye muaji kile kisu ilibidi kiwe na damu yake pia maana atakuwa alikuwa kakishikiria wakati ana jeraha kwenye kidole basi kungekuwa na mchanganyiko wad emu za marehemu na damu yake lakini vipimo vilionyesha hakikuwa na damu ya Skinner.
Taulo iliyokutwa kwenye mfuko ule mweusi pamoja na kisu, ilikutwa ina DNA ya mtu asiyefahamika. Hiyo taulo ilikutwa na damu ya Twila na DNA ya mtu mwingine asiye Skinner wala watoto wa Twila. Pia kluna DNA ilikutwa upande wa pili wa taulo hiyo ambayo inafahamika ni ya nani, hiyo DNA ni ya mtaalamu wa masual ya DNA ambaye pia alikuwa shahidi upande wa serikali. Dna yake ilikutwa kwenye vitu viwili kisu pamoja na taulo.
Hii inadhihirisha kuwa hawa atu hawakuwa makini na kuhifadhi ushahidi kama waliweza kuhifadhi na kuushika ovyo ovyo mpaka huyo anayeitwa matalaamu anaacha DNA yake kwenye ushahidi ni jambo la ajabu sana.
Jaji alifikia hitimisho kuwa ushahidi mpya ulikuwa haujitoshelezi kubadiri uamuzi wa majaji waliotoa hukumu ya kwanza. Aliendelea kusema kuwa hata huu ushahidi ungekuwepo toka mwenzo huenda majaji wa mwanzo wangempa adhabu ile ile.
Baada ya zaidi ya miaka 20, ya mapigano ya kujaribu kumuokoa Skinner na mamiliona ya dola kutumika katika kulipia msaada wa kisheria, Skinner bado anasubiri kutekelezwa adhabu yake ya kunyongwa huku bado akishikiria msimamo wake kuwa hakuhusika. Leo skinner tumaini lake limebakia kwenye kurudia tena upimaji wa DNA, na kama hakuna jambo jipya litakalopatikana kwenye zoezi hilo tarehe yake mpya ya kunyongwa itapangwa.
John yeye anadai kwamba anaona pesa nyingi na muda uliotumiaka na wanaomtetea Skinner umetosha, hakuna njia nyingine zaidi yahiyo adhabu kutekelezwa. Msaidizi wake John yeye anasema haingii akilini kuwa ulikuwa umelala unashituka unakuta mpenzi wako na watoto wameuawa na mbele yako kuna mtu mwenye kisu unatoka ndani umekimbia, unaelekea kwa mpenzi wako wa zamani akushine jeraha lako hata hujishughulishi kutoa taarifa polisi halafu baadae unakuja kudai kuwa hukuhusika.
John anadai yeye hana shaka kuwa Skinner alihusika na siku ya kunyongwa ikapangwa ataenda kushuhudia akinyongwa bila shaka.
Hitimisho: kuna mambo mengi sikoyaandika kwenye kisa hiki ila nina amini Skinner alihusika kwenye mauaji hayo. Kwa mfano akiwa gerezani aliweza kuipenyezewa simu mabyo aliitumia kumtishia mwendesha mashitaka wa Texas, polisi vamia anapolala kujaribu kutafuta hiyo simu hawakuipata ila walikuta line za simu mbili kwenye Biblia aliyokuwa nayo. Baadaye walimpiga X-ray iliyoonyesha kuwa alikuwa na simu kwenye utumbo wake.
Hii inadhihirisha kuwa Skinner alikuwa ni muarifu mzuri tu.
Mpaka leo Skimmer bado anasubiri kunyongwa.
**********************mwisho****************************