Matumizi ya connect za Upwork

Matumizi ya connect za Upwork

kuna kazi nimepata hapo ni ngumu kuliko nilivotegemea
client anataka link za video za kibena zaidi ya masaa 500( Yaani total length ya video zote ziwe masaa 500) hapo hawahitaji nyimbo za asili wala ngoma!!
Hahaa mkuu unamoyo mimi nilipata gig kama 3 za kufanana nikazikataa baada ya clients kugoma kupandisha malipo atleast 1$ per link regardless of length
 
Mnafanyaje KU-Verify account zenu Upwork? Vitambulisho gani mnatumia.
Kweli mbongo ni mbongo

Mbongo kumwelekeza mbongo mwenzie hususani linapokuja swala la umate mate na chapaa anakua mzito saaaana ni wachache saaana wenye mioyo ya kukunjua roho na kuachia pumzi yao iseme ila wengi wao wanapenda kukunja roho wanachohitaji ujipambanie wewe kivyako usipende mseleleko, ukumbane na changamoto na ujifunze mwenyewe usijifunze kupitia wao ili hata km yakikukuta makuu usipate mtu wa kumlaumu kwamba huyu ndie alienisababishia haya yote

Ingia Google andika upwork zitakuja link zaidi ya million za wazungu waliokunjua roho wanaelezea mchongo unavyokua

Ingia YouTube andika upwork utakutana na video zaidi ya million za wazungu wenye roho safi wameelezea step by step

Ukikwama rudi tena Google rudia tena YouTube

Ukikwama rudi Google rudia tena ingia YouTube soma jifunze kwa watu tofauti sio mtu mmoja jifunze kwa hatua kila unapokwama jifunze tena chukua makala km kuna vitabu chukua soma, pdf chukua soma

Kuna wabongo km wawili nilikua nawafuatilia YouTube nilifuatiliaga video zao nikafungua hadi account upwork ila kuna step baadhi nilikwama nikakosa wa kumuuliza nikaachana nayo mpaka leo

Sababu kuna vitu hua hawakuambii wabongo wanapenda sana kuficha 'source code' inabidi ufukue mwenyewe ujue nini na nini ni sahihi na nini na nini sio sahihi

Yaan hapo mpaka umejua ni nini ushapata hasara angalau ushaingia gharama ya muda na pesa pia, wakati mzoefu wa muda mrefu angekwambia tu hapa fanya hivi pale fanya vile kile weka pale hiki usiweke kule kile ondoa pale na pale usiguse kile usikifanye vile na kile mpe yule hiki fanya hivi boom dollars hizi hapa
 
Back
Top Bottom