Nilitaka uniulize hilo ni somo linalohusu nini haswa? Nadhani siku hizi hata sijui kama lipo, uko vizuri sana kichwani mkuu. Miaka miwili tu umejifunza mengi sana.Sawa sawa... Asante kwa kuwepo kwenye jamii hii ya mtandao wa dunia yetu! Kuwepo kwenye majukwaa ni sehemu muhimu ya uraia.
Ulijifunza kiswahili huko Marekani? Kumbe lugha yetu imesambaa vilivyo nayo, basi mi sitasumbuka na lugha zingine, hiihii tu itanitosha.Samahani kwa kushindwa kueleza kwa kiswahili kizuri. Nilivyosema, kiingereza ni lugha yangu ya kwanza. Shuleni nilijifunza kidogo cha kispanya, kiswahili ndicho cha tatu.
Nilitaka uniulize hilo ni somo linalohusu nini haswa? Nadhani siku hizi hata sijui kama lipo, uko vizuri sana kichwani mkuu. Miaka miwili tu umejifunza mengi sana.
Nashukuru mwalimu. Ilikuwa raha yangu kujifunza yote yaliyowezekana wakati wa ile miaka mifupi miwili. Lugha, utamaduni, jinsi ya maisha. Siku moja nitarudi!Ulijifunza kiswahili huko Marekani? Kumbe lugha yetu imesambaa vilivyo nayo, basi mi sitasumbuka na lugha zingine, hiihii tu itanitosha.
East and baadhi ya central AfricaNashukuru mwalimu. Ilikuwa raha yangu kujifunza yote yaliyowezekana wakati wa ile miaka mifupi miwili. Lugha, utamaduni, jinsi ya maisha. Siku moja nitarudi!
Nilisoma kidogo huku Marekani kabla ya kuenda TZ, lakini nilijifunza mengi kule. Kiswahili ni lugha kubwa! Si milioni nyingi nyingi wanakiongea?
kwa kweli hongera sana umefanikiwa kujua kiswahili kwa kiwango cha juu sana.Hata kwetu mjini Missouri wapo wahamiaji kutoka sehemu zile. Nimewatafuta ili niendelee kuongea kiswahili nisikisahau.
Pia si sahihi kusema "Ni tatizo kwa jinsi fulani". Sema ni "tatizo kwa kiasi fulani" ama "kwa kiwango fulani." Nitaje hilo moja tu niache mengine. Mambo ya lugha kila mtu na ya kwake. Sahihisha wa-Tanzania Kiingereza nao watakusahihisha Kiswahili. Kiingereza si chetu na Kiswahili sio chako. Hatusemi pia "nimejiunganisha", tunasema "nimejiunga," ama "nimeungana na...." Niendeleee? Acha bwana!Habari gani jamani. Mimi ni mmarekani aliyeishi Tanzania miaka miwili kuanzia 2014 mpaka 2016. Nimejiunganisha na jamii forums hivi karibuni tu lakini... Samahani nimechelewa. Basi...
Wakati nilikuwa kule, nilisikia sana kosa dogo moja la kiingereza. Niliona kwamba, kati ya kiingereza cha Marekani na kile cha Tanzania, matumizi ya "somehow" na "somewhat" kumbe yamegeuka. Kabla sijatoa mifano, nitafsiri hayo maneno kwa maana zao sahihi:
SOMEHOW: kwa jinsi fulani (tukumbuke kwamba "how" ndiyo "vipi" kwa kiswahili)
SOMEWHAT: kiasi fulani, kidogo
KIINGEREZA CHA TANZANIA (ambacho napendekeza si sahihi):
"It is somehow cold today" (Ni baridi kwa jinsi fulani leo) - lugha mbovu, hatueleweani
"It is somehow a problem" (Ni tatizo kwa jinsi fulani) - lugha mbaya sana, ina maana gani hiyo?
KILICHO SAHIHI ZAIDI (tutumie "somewhat" badala ya "somehow")
"It is somewhat cold today" (Ni baridi kiasi fulani leo) - lugha nzuri
"It is somewhat of a problem" (Ni tatizo dogo) - nzuri tu, tunaeleweana
"Somehow, I was able to get to work on time" (Kwa jinsi fulani, niliweza kufika kazini mapema) - matumizi mazuri ya "somehow"
Je, tumeelewa? Kama kuna maswali nitayajibu.
Missouri ni mji ama Jimbo? Ndiyo makosa yenyewe hayo. Ungesema jimboni Missouri basi. Miji ni kama Springfield.Hata kwetu mjini Missouri wapo wahamiaji kutoka sehemu zile. Nimewatafuta ili niendelee kuongea kiswahili nisikisahau.
Pia si sahihi kusema "Ni tatizo kwa jinsi fulani". Sema ni "tatizo kwa kiasi fulani" ama "kwa kiwango fulani." Nitaje hilo moja tu niache mengine. Mambo ya lugha kila mtu na ya kwake. Sahihisha wa-Tanzania Kiingereza nao watakusahihisha Kiswahili. Kiingereza si chetu na Kiswahili sio chako. Hatusemi pia "nimejiunganisha", tunasema "nimejiunga," ama "nimeungana na...." Niendeleee? Acha bwana!
Missouri ni mji ama Jimbo? Ndiyo makosa yenyewe hayo. Ungesema jimboni Missouri basi. Miji ni kama Springfield.
Endelea tu. Si kweli kwamba makosa na masahihisho ni fursa ya kujifunza? Wote walimu, wote wanafunzi hapa.
Ni kweli, ni jimbo.
Nilitaka uniulize hilo ni somo linalohusu nini haswa? Nadhani siku hizi hata sijui kama lipo, uko vizuri sana kichwani mkuu. Miaka miwili tu umejifunza mengi sana.
Made in China SomehowNdiyo sahihi! Umesema kwamba uzi huu unasaidia kiasi!
Kwa mtu aliyekulia anaongea Kiswahili, na hana kipaji na ufuatiliaji kuhusu lugha, kujifunza Kiingereza fasaha baadaye kunaweza kuwa kugumu, kwa sababu ni kama kujifunza lugha yenye makosamakosa mengi.
Kiswahili kimenyooka sana, kina sheria za sarufi na matamshi ambazo zinapinda sehemu chache sana.
Kiingereza sheria zake za sarufi na matamshi ni kama nusu ya lugha inafuata sheria, na nusu nyingine imepinda.
Kwa hiyo, kwetu tuliozoea lugha iliyonyooka, kujifunza lugha iliyopindapinda ukubwani inakuwa vigumu sana.
Mwlsamwel
Umeandika kutumia "It is somehow cold today." na "It is somehow a problem." ni makosa.
"It is somehow cold today" na "It is somehow a problem" ni sentensi ambazo hazina makosa kama zilivyo, labda kama zimetumika pasipotakiwa, au kwa muktadha usiofaa.
Nitatoa mfano.
Umeenda sehemu uliyotegemea iwe na joto kwa kufuatilia ratiba za hali ya hewa, ukakuta sehemu haina joto, na inaanza kuwa na baridi ambalo hujalielewa.
Hapo unaweza kusema "It is somehow cold today". Yani kuna jinsi fulani imetokea ikafanya sehemu hii ambayo ilitegemewa kuwa na joto iwe na baridi, sijui ni pepo za kusi, sijui ni maumbile ya kijiografia, lakini kuna namna fulani imefanya pawe baridi,ingawa sijui ni nini kimefanya pawe na baridi.
It is somehow cold today.
"It is somehow a problem".
I like this girl, I respect her. I greet her with all the verve and fanfare of an adoring fan.
Yet to her, it is somehow a problem.
Kwake hata kumsalimia kwa bashasha zote, ni tatizo.
Sijui ana kisirani, sijui hapendi kuongeleshwa, sijui anachukia sura yangu, lakini najua nikimsalimia ananikasirikia.
It is somehow a problem.
Somehow inatumika unapoongelea how.
Somewhat inatumika unapoongelea what
Somewhat inatumika kuongelea extent.
Leo ni baridi, lakini si baridi sana. It is not too hot, actually it is somewhat cold today.
Hapa kazini kuna kitatizo, lakini sitatizo sana.
I couldn't get in, my pass badge is not working, it is somewhat of a problem, but I will call my boss and he will get me in.
Mimi mmarekani??? Labda nije na akaunti mpya kama huyu mwlimu"Acaunt" lugha mbaya
"Account" lugha nzuri
Wewe si mmarekani, eeh?
Kwakweli, mi mwenyewe nimemkubali. Nimemtega vya kutosha hajanasa hata mara moja.Wewe ni moja ya watu wastaarabu humu. Majibu yako ni ya kiungwana. Umenipa moyo kuendelea.
Hata hivyo Mimi ni mzaliwa wa Pwani! Ndo lahaja iliyonilea na kunikuza. Nashukuru kwa Masahihisho.Mkuu usimpoteze mwenzio! Tumia "hasa" badala ya "haswa". Nadhani ulikazia kipwani kwa kusudi jema.