Matundu 19 ya Risasi Katika Gari ya Tundu Lissu.. Hao wahalifu hawana mafunzo ya kitaalamu ya silaha!

..smg siyo rahisi kupiga risasi zikaelekea eneo moja.

..pia uharaka wa waliofanya shambulizi hilo.

..vilevile mtumia bunduki alivyokuwa amekaa. Inasemekana alikuwa ndani ya gari.

.
Usijadili kitu usichokijua, hakuna silaha rahisi kutumia kama smg
 
tuwajua tuu

try me
 
Usijadili kitu usichokijua, hakuna silaha rahisi kutumia kama smg

..siyo kweli.

..na ktk mazingira ya tukio jaribio la mauaji dhidi ya TL siyo rahisi kufanya vile ambavyo mtoa mada is suggesting.
 
Ukiona jini linavuka barabara kwenye alama ya zebra crossing,jua unatazama bongo movie.

Risasi 20+ halafu mpaka sasa mtu yupo hai,acheni masihara labda risasi zilikuwa zinarushwa kwa mkono au kwenye manati.
 
Ukiona jini linavuka barabara kwenye alama ya zebra crossing,jua unatazama bongo movie.

Risasi 20+ halafu mpaka sasa mtu yupo hai,acheni masihara labda risasi zilikuwa zinarushwa kwa mkono au kwenye manati.


Kwa Hiyo Mkuu Unataka Kutuambia Kuwa Hata Taarifa Iliyoyolewa Na Jeshi La Polisi Kuhusu Risasi Zilizopigwa Kwenye Gari Ya Mh Lisu Ni Taarifa Za Uongo????

Taarifa Iliyopo Ni Kwamba Risasi Zilizomiminwa Ni Kuanzia 28-32 Lakini Zilizofika Mwilini Mwake Ni Risasi 5 Tu.

Au Ulitaka Ama Ulielewa Kuwa Risasi 20 Ndio Zilizomfika Moja Kwa Moja???
 
1. Covert operation - Operation inayotakiwa kufanyika kwa siri na ujasiri mkubwa na ukihusisha watu wenye uwezo wa kufanya hiyo shughuli. Kwanza anatakiwa kuwa mtu mwenye shabaha 95% specific and awe sensitive and precise 95%.

2. Clandestine Operation - Inatakiwa kufanyika kwa kuhusisha a troop of a trained soldier hiyo inaweza kuonekana lakini kwa malengo maalum.

Hizo operation zikikosewa huweza kusababisha mtafaruku kwenye jamii, so I mean state of un certainty so it can create political instability.

Kumbukeni
Kombe alipigwa risasi nyingi hadharani.

Hiyo ni elimu bure na ni kwa wale waliobahatika kuipata.

Lissu upone haraka uje tuijenge Tanzania
 
Hakuna cha competency wala nini. Mungu akiamua kumlinda mtu wake anamlinda tu! Miaka ya nyuma hapo UDSM palikuwa na Prof. mmoya alivamiwa na majambazi kwenye SMG full loaded wakamtaka anyooshe mikono juu; akawajibu siwezi msujudia mwanadamu tangu niokoke huwa namnyooshea Kristo Bwana pekee! Jamaa akamwambia mwenzake kamanda washa, akawasha mtambo akamnyooshea Prof akatandika magazine yote ikaisha (aliseti kwenye rapid). Huwezi amini walipomaliza wakaamini Prof atakuwa uji. Prof akawaulizs mmemaliza? Mbio walizotimua ni Mungu tu anajua! Huyo ndio Mungu bhana....!
 
SAIDWE; Ni sawa Mungu yupo na wengi tunaamini yupo! Ila kuna swala kuwa wanaokuwa wamepewa kufanya hizo operations hawana uwezo. Operation nilizozitaja ziliwahi kufanywa na Watanzania huko Liberia wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe, ndizo zilizofanikisha ukombozi wa nchi hizo. Ni operation ambazo zikitumiwa uwezekano ni 98%.
 
SMG magazine huwa inachukua risasi 30 tu. Je inamaana wauwaji walikuwa na magazine mbili au SMG mbili. Nahisi hiyo report ni ya uongo siokweli yaani risasi 28-32 at per.
 
Ndugu hawa jamaa ni wajuzi sana......tumia akili ndogo tu ya kwanini wewe umewaza hivi? Bila shaka ni western movie zimekueleka

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Imagine risasi ishirini hujagusa kichwa? Pole kwa Lisu
 
5/30 x 100% = 16.67%
Au waweza kusema kua katika kila risasi 6 zilizotoka kwenye mtutu wa wale jamaa, only moja tu ndio ilimpata TL
 
Hili swala la TLS Ni zito, na kuna watu wanakuja na hoja dhaifu eti walishambulia sio professional killers au walikua wazembe, mimi nasema la hasha....hawa watu Ni wauaji maalumu na Hawakua wazembe hata kidogo, kwanini?

Kwasababu ukiangalia vizuri matobo ya zile risasi yalilenga sehemu zote muhimu....KICHWANI, MIGUUNI, KIFUANI, UBAVUNI NA TUMBONI ...Risasi nyingine zilipigwa mlango wa nyuma means yake Ni kwamba hata angelaza seat bado angekutana nazo!!! Oh my God this was not just an attack,, it was a serious killing incident.

Sasa swali la kujiuliza aliponaje?????? Hapa sijui wengine mna majibu gani ila mimi nasema Mungu yupo (God Exists) kama unabisha jiulize zile risasi za chini, juu, pembeni katikakati ziliishia wapi na sio mwilini mwa Lisu?????

Kama Mungu amemuokoa Lisu katika hili Basi wauaji kuweni makini Jicho lake linawatazama... japo maneno kama haya wengi huyapuuza wakidhani yanatolewa na wafia dini watu wasiofikiri sana.

Kwa hili lazima serikali ihusishwe na msijifiche kwenye mgongo wa kusema hatuwezi kumdhuru Lisu waziwazi wakati kila mtu anajua migogoro iliyopo!!! La hasha....kina Mwangosi waliuawa hadharani na kikao mtu alikua anajua migogoro iliyokuwepo,,kina Alphonce Mawazo, kina Ulimboka waking'olewa meno bila ganzi wakaponea chupuchupu na kila mmoja alikua anajua migogoro yao na Serikali ovu ya CCM.

Ben Saanane alihoji vyeti akapotea hadharani na kila mtu anajua,,Roma alitekwa kila mtu anajua,,, Sasa la Lisu linadhindikana??????

Serikali na viongozi wa Afrika wakishaapishwa nadhani wanakatwa mishipa yote ya aibu...wakiamua kufanya Jambo lolote hulifanya bila aibu na bila uoga wala kujali nani atawaza au kusema nini...Kwa kusema hayo siituhumu serikali moja Kwa moja ila nasema haiwezi kujisafisha kutokana na mlolongo wa matukio ya huko nyuma.

Kikubwa hapa sio Siasa na propaganda za kina Sirro na mkuu kufunifunika mambo, Ni kuja na majibu kamili ya maswali yafuatayo.

1. Nani alivamia Clouds FM na kwanini na hatua gani zilichukuliwa,

2. Nani amemteka Ben Saanane, amempeleka wapi na hatma yake Ni Nini,

3. Nani alimteka Roma na kwanini na hatua zilizochukuliwa dhidi yake,

4. Nani alimtolea nape Bastola na hatua zilizochukuliwa dhidi yake,

5. Kina nani wamemmiminia Lisu risasi kama mvua ya mawe na nani kawatuma na kwanini.

Serikali ikiyajibu haya maswali, narudia tena bila siasa wala propaganda za kina Sirro na Mwenyekiti wa chama...Basi hapo itaweza kutuambia kwamba kweli haihusiki na haya matukio.

Toa maoni yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…