Mau fundi ni mchekeshaji Bora kuliko wote tz

yule kiziwi huwa dishi limecheza, unamwambia hiki ye anakujibu hiki alafu kwa kujiamini.

anahamisha(ga) mada boya yule
We nae mi si nimekwambia Max ndio founder wa Jf...eeeh kwani umesemaje sijakusikia
 
Kuigiza matukio sio shida cha muhimu uwe na kipaji mbona akina Masanja na Ze comedy baadae orijino comedy walikuwa wanaigiza baadhi ya matukio na bado walikuwa wanabamba
Wako Realistic hao jamaa wote, mi sipendi comedians wa kuigiza matukio kama Idris Sultan ama kufanya utoto eti ndio comedy! Nataka mtu awe realistic na still niweze kufurahia! Joti anakidhi kwa 90%
 
Huyo sumaku yupo insta?
Hahahah kama Joti anakuchekesha hata Sumaku atakuchekesha,sema Sumaku hayupo exposed sana kama hawa wengine. Mi napenda comedians ambao hawaigizi matukio wala kufanya upumbavu, wawe realistic ila nikiwaskiliza tu nicheke!
 
Mleta mada upo sahihi kabisa huyu jamaa kweli ni fundi kweli hakuna wakumfikia joti nae alikuwa vizuri ila sasa anachekesha kibosi zaidi
 
Sijaona cha kuchekesha hapo, binafsi mtu pekee anaeweza kuweka tabasamu langu usoni kwa sasa ni:
1. Joti
2. Sumaku
3. Brother K

Wengine wote waliobaki michosho tu, waende shule za msingi ndio kuna wa kuchekea wanayoyafanya!
Huyu sumaku halafu yuko serious, sasa ukicheki maneno anayayotoa.
 
Huyu sumaku halafu yuko serious, sasa ukicheki maneno anayayotoa.
Ndio mchekeshaji mahiri anavyotakiwa awe vile, yuko na sura ya kazi ila ukimuangalia na kumsikiliza tu unavunjika mbavu! Hao ndio watu wanaoweza kunichekesha mimi ila sio wale wa matumbo tumbo, kujitia ulemavu wa ulimi na maskio ama wanaotumia kejeli kuchekesha watu kama Idris sultan
 
tz wachekeshaji ni lile kundi la original comedy pekee ndio lilikua na uwezo wa kuchekesha kila mtanzania bila kujali elimu yako, dini yako. ILIKUA NI NGUMU SANA KUWAANGALIA USICHEKE
 
Mau Fundi
Ringo na Tiny white hawa ukiwaweka pamoja unapata burudani mpaka unahisi kuwa unawadhulumu hawa wasanii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…