mcTobby
JF-Expert Member
- Feb 16, 2018
- 4,072
- 12,119
Wadau , wakubwa kwa wadogo natangauliza salamu zangu kwenu, natumai mu buheri wa afya .
Nadhani wengi wenu mliopita shuleni hususani advanced level mnamkumbuka mwamba mmoja aliyejulikana kama Josip brozi Tito, rais wa yugoslavia. Ingawaje historia inamsema vizuri kutokana na ujasiri wake wa kukataa kuwa chawa wa kiongozi wa umoja wa kisoviet wakati huo bwana stalin , lakini chini ya kapeti utawala wake uligubikwa na unyanyasaji wa makundi kadhaa yaliyokuwepo ndani ya yugoslavia,mauaji ya koholela pamoja na utekaji na vifungo kwa wapinzani wake wa kisiasa.
Tito kwenye historia huonyeshwa kama kielelezo na mfano wa kuigwa kama kiongozi aliyeiunganisha yugoslavia iliyosaidia kudhibiti vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini mwake.
Lakini kwa wengi wa raia , wengi waliona nchi yao kama gereza kubwa
Kivipi? Twende kazi. Baada ya vita kuu ya pili ya dunia kuisha mwaka 1945, makundi kadhaa ndani ya yugoslavia ambao walikuwa wakiupinga utawala wa wa Brozi Tito walijisalimisha kwa jeshi la ukombozi la uingereza ( British expeditiary Force), lakini waingereza wakawakabidhi hawa walio salimu amri kwa utawala wa brozi Tito. Makundi haya yaliyopigana na utwala wa Tito ilikuwa ni jamii za watu wa Croatia, waserbia na wa Slovenia ndani ya yugoslavia.
Kilichofuata baada ya hapo ni jambo lililoisikitisha dunia japo jambo hili lilifichwafichwa.
Inakadiriwa raia wapatao 50,000 waliuliwa pasipo kufunguliwa mashtaka ( summary execution).
Raia ,hususani wanawake na watoto ndio waliokuwa waathirika wakubwa.
Ndani ya yugoslavia kulianzishwa death marches , ambapo raia waliokuwa wanampinga josep brozi tito walilazimishwa kujipanga kwenye mistari na kisha kutembea hadi sehemu maalumu ambapo wangeuliwa. Hii ilijulikana kama " way of the cross " au njia ya msalaba. Ndugu zangu wakatoliki wanaelewa hapa vizuri.
Ujumbe wa rais huyu wa Yugoslavia ulikuwa clear " No mercy to those who oppose him.
Pia jeshi la josep brozi tito liliwalenga makundi ya waitaliano waliokuwa kwenye miji midogo ya istria na dalmatia,(kwa sasa miji hii ni sehemu ya nchi za Slovenia na croatia). Lengo la kuwakamata waitaliano pamoja na kuzichukua Mali zao ni kisasi dhidi ya utawala wa Mussolini Dikteta wa Italia aliyekuwa amekalia kimabavu maeneo ya yugoslavia.
Inakadiriwa zaidi ya waitaliano 10,000+ waliluliwa kwa kutumbukizwa kwenye shimo moja lililojulikana kama FOIBE. Wengine wakanyang'anywa Mali zao na kufukuzwa .
Kwa kifupi tito alikuwa anafanya kitu kinachojulikana kama ethnic cleansing .
Kwa sasa nchi ya italia huadhimisha siku ya mauaji haya kama " Foibe remembrance day" kila ifikapo tarehe 10 February. Kwa ajili ya kuwakumbuka wale wote waliouliwa kwa kutumbukizwa ndani ya shimo la foibe na utawala wa tito
Na pia kabla hata ya vita ya pili ya dunia zaidi ya raia laki tano jamii za wajerumani ambao ni swabian Danube ,walikuwa wakiishi ndani ya yugoslavia lakini tito alitaka kuwafuta wote kabisa. Wengi waliuliwa ikikadiriwa idadi ni wajerumani laki moja. Wengine walifungwa kwenye kambi za mateso ili wafie huko na njaa huku wengine zaidi ya wajerumani laki mbili na nusu wakifukuzwa kwenda kwao Ujerumani. Vijiji vyote walimokuwa wanakaa jamii hizi vikafutwa kwenye ramani.
Vilevile jamii za waserbi wa chetniks waliokuwa wakiendesha vuguvugu wakipinga unazi na ukomunisti waliitwa maadui wa taifa la yugoslavia. Na kweli , kati ya mwaka 1945 hadi 1946 wengi wao waliuliwa huku familia zao zikifungwa jela au kupelekwa uhamishoni. Na pia makanisa ya wa Serbia ya orthodox yalivunjwa na kuharibiwa.
Kwa kifupi baada ya josep brozi tito kutwaa madaraka alihakikisha hakuna upinzani dhidi yake ndani ya yugoslavia.
Na kweli wengi wafungwa wa kisiasa waliishia kwenye kambi za mateso na wengine walifungwa kwenye gereza la Goli Otok ,moja ya gereza baya zaidi huko yugoslavia wakati huo.
Gereza hili ambalo lilikuwa kisiwani ndilo lililokuwa likiwafunga wakisindikizwa na mateso makali kwa wale wote walio mpinga tito.
gereza la Goli Otok
Josep brozi tito hakuishia hapo. Wale wote waliokuwa wanampinga wakiwa nje ya Yugoslavia hususani marekani, Argentina na hata Ujerumani aliwatumia " kikosi kazi" na kuuliwa na Wasiojulikana . Hii ina maana yugoslavia ilikuwa ni police state .
Sera ya huyu bwana tito ya "brotherhood and unity" yaani undugu na umoja ilikuwa ni sera ya kulazimisha makundi au jamii tofauti tofauti( waserbia ,wa Slovakia,wa Slovenia na jamii zingine) ziishi kwa pamoja ndani ya serikali kuu "central government " lakini minyukano iliendelea chini kwa chini. Kwa sera yake hii ilisaidia kudhibiti vita vya wenyewe kwa wenyewe visitokee mpaka ilipofika miaka ile ya 1990 moto wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vilipolipuka.
Huyu mwamba alipokufa mwaka 1980 nchi ya yugoslavia ikatumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyopelekea umwagaji mkubwa wa damu. Kitu ambacho hakutaka kitokee ndani ya nchi yake ya yugoslavia .
Yote kwa yote wanahistoria wanafunika uovu wake kutokana na ukweli ya kwamba alimpinga stalin waziwazi hadharani. Ila Ukweli ni alikuwa mhusika mkuu wa mauaji ya kimbari ndani ya yugoslavia.
Nadhani wengi wenu mliopita shuleni hususani advanced level mnamkumbuka mwamba mmoja aliyejulikana kama Josip brozi Tito, rais wa yugoslavia. Ingawaje historia inamsema vizuri kutokana na ujasiri wake wa kukataa kuwa chawa wa kiongozi wa umoja wa kisoviet wakati huo bwana stalin , lakini chini ya kapeti utawala wake uligubikwa na unyanyasaji wa makundi kadhaa yaliyokuwepo ndani ya yugoslavia,mauaji ya koholela pamoja na utekaji na vifungo kwa wapinzani wake wa kisiasa.
Tito kwenye historia huonyeshwa kama kielelezo na mfano wa kuigwa kama kiongozi aliyeiunganisha yugoslavia iliyosaidia kudhibiti vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini mwake.
Lakini kwa wengi wa raia , wengi waliona nchi yao kama gereza kubwa
Kivipi? Twende kazi. Baada ya vita kuu ya pili ya dunia kuisha mwaka 1945, makundi kadhaa ndani ya yugoslavia ambao walikuwa wakiupinga utawala wa wa Brozi Tito walijisalimisha kwa jeshi la ukombozi la uingereza ( British expeditiary Force), lakini waingereza wakawakabidhi hawa walio salimu amri kwa utawala wa brozi Tito. Makundi haya yaliyopigana na utwala wa Tito ilikuwa ni jamii za watu wa Croatia, waserbia na wa Slovenia ndani ya yugoslavia.
Kilichofuata baada ya hapo ni jambo lililoisikitisha dunia japo jambo hili lilifichwafichwa.
Inakadiriwa raia wapatao 50,000 waliuliwa pasipo kufunguliwa mashtaka ( summary execution).
Raia ,hususani wanawake na watoto ndio waliokuwa waathirika wakubwa.
Ndani ya yugoslavia kulianzishwa death marches , ambapo raia waliokuwa wanampinga josep brozi tito walilazimishwa kujipanga kwenye mistari na kisha kutembea hadi sehemu maalumu ambapo wangeuliwa. Hii ilijulikana kama " way of the cross " au njia ya msalaba. Ndugu zangu wakatoliki wanaelewa hapa vizuri.
Ujumbe wa rais huyu wa Yugoslavia ulikuwa clear " No mercy to those who oppose him.
Pia jeshi la josep brozi tito liliwalenga makundi ya waitaliano waliokuwa kwenye miji midogo ya istria na dalmatia,(kwa sasa miji hii ni sehemu ya nchi za Slovenia na croatia). Lengo la kuwakamata waitaliano pamoja na kuzichukua Mali zao ni kisasi dhidi ya utawala wa Mussolini Dikteta wa Italia aliyekuwa amekalia kimabavu maeneo ya yugoslavia.
Inakadiriwa zaidi ya waitaliano 10,000+ waliluliwa kwa kutumbukizwa kwenye shimo moja lililojulikana kama FOIBE. Wengine wakanyang'anywa Mali zao na kufukuzwa .
Kwa kifupi tito alikuwa anafanya kitu kinachojulikana kama ethnic cleansing .
Kwa sasa nchi ya italia huadhimisha siku ya mauaji haya kama " Foibe remembrance day" kila ifikapo tarehe 10 February. Kwa ajili ya kuwakumbuka wale wote waliouliwa kwa kutumbukizwa ndani ya shimo la foibe na utawala wa tito
Na pia kabla hata ya vita ya pili ya dunia zaidi ya raia laki tano jamii za wajerumani ambao ni swabian Danube ,walikuwa wakiishi ndani ya yugoslavia lakini tito alitaka kuwafuta wote kabisa. Wengi waliuliwa ikikadiriwa idadi ni wajerumani laki moja. Wengine walifungwa kwenye kambi za mateso ili wafie huko na njaa huku wengine zaidi ya wajerumani laki mbili na nusu wakifukuzwa kwenda kwao Ujerumani. Vijiji vyote walimokuwa wanakaa jamii hizi vikafutwa kwenye ramani.
Vilevile jamii za waserbi wa chetniks waliokuwa wakiendesha vuguvugu wakipinga unazi na ukomunisti waliitwa maadui wa taifa la yugoslavia. Na kweli , kati ya mwaka 1945 hadi 1946 wengi wao waliuliwa huku familia zao zikifungwa jela au kupelekwa uhamishoni. Na pia makanisa ya wa Serbia ya orthodox yalivunjwa na kuharibiwa.
Kwa kifupi baada ya josep brozi tito kutwaa madaraka alihakikisha hakuna upinzani dhidi yake ndani ya yugoslavia.
Na kweli wengi wafungwa wa kisiasa waliishia kwenye kambi za mateso na wengine walifungwa kwenye gereza la Goli Otok ,moja ya gereza baya zaidi huko yugoslavia wakati huo.
Gereza hili ambalo lilikuwa kisiwani ndilo lililokuwa likiwafunga wakisindikizwa na mateso makali kwa wale wote walio mpinga tito.
gereza la Goli Otok
Josep brozi tito hakuishia hapo. Wale wote waliokuwa wanampinga wakiwa nje ya Yugoslavia hususani marekani, Argentina na hata Ujerumani aliwatumia " kikosi kazi" na kuuliwa na Wasiojulikana . Hii ina maana yugoslavia ilikuwa ni police state .
Sera ya huyu bwana tito ya "brotherhood and unity" yaani undugu na umoja ilikuwa ni sera ya kulazimisha makundi au jamii tofauti tofauti( waserbia ,wa Slovakia,wa Slovenia na jamii zingine) ziishi kwa pamoja ndani ya serikali kuu "central government " lakini minyukano iliendelea chini kwa chini. Kwa sera yake hii ilisaidia kudhibiti vita vya wenyewe kwa wenyewe visitokee mpaka ilipofika miaka ile ya 1990 moto wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vilipolipuka.
Huyu mwamba alipokufa mwaka 1980 nchi ya yugoslavia ikatumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyopelekea umwagaji mkubwa wa damu. Kitu ambacho hakutaka kitokee ndani ya nchi yake ya yugoslavia .
Yote kwa yote wanahistoria wanafunika uovu wake kutokana na ukweli ya kwamba alimpinga stalin waziwazi hadharani. Ila Ukweli ni alikuwa mhusika mkuu wa mauaji ya kimbari ndani ya yugoslavia.