Mauaji ya Polisi wetu ni Ujambazi, Ugaidi au Retaliation? Nini kifanyike kukomesha hali hii?

Pasco licence to kill inaweza kutumika kwenye nchi zenye Polisi watenda haki, hivi hiyo licence to kill wangepewa leo Nape angekuwa hai?

Kutazuka mauwaji ya kubambikiana ujambazi fake kisa kugombea demu.

Kwa upeo wangu mdogo jeshi la polisi linaujuwa vizuri mtandao wa ujambazi.

Inasikitisha sana jeshi letu kutumia resource nyingi pesa za umma kukimbizana na kina Tundu Lisu wanaotimiza wajibu wao wa kikatiba na kuwaacha hasa maadui halisi wa usalama wao na wa raia.

Jeshi la Polisi lijitenge na siasa na litapata sapoti ya umma.

Hakuna nchi yenye majambazi waliopinda hapa Africa zaidi ya South Africa lakini kamwe hawawezi hata kufikiria hata siku moja kuwavamia polisi au kupambana nao.

IGP atoke huko mafichoni aongee na IGP mwenzake wa South Africa tuwapeleke vijana wetu training kule, na wale vijana wenye maumbo six park na ya kimazoezi sasa waondolewe FFU na waletwe kwenye vikosi vya anti robbery.

Huwa sielewi eti wale vijana wenye maumbo shupavu ati wanapelekwa FFU kula kulala kusubiri kuwapiga mitana na virungu raia wema wanaondamana kudai haki zao.

Mwigulu Nchemba soma ushauri huu, nenda pale FFU piga king'ora cha parade uone mijibaba ilijoza kimazoezi itakayofika pale halafu fananisha na kikosi chako cha Anti robbery utagunduwa wazi sisi tuna matatizo kichwani.

Mimi si mtaalam wa mambo ya ulinzi lakini ni muda muhafaka sasa wa kuwa na kikosi maalum na siyo kikosi kazi, kikosi hiki kiundwe na FFU pamoja na JWTZ na kiitwe Cobra, hakuna jambazi tena atakayetamani kukutana na Cobra.
 
uwe unarelate lugha iliyotumika kuleta mada na lugha unayotumia kucoment we mzee...
 
Mkuu Pascal Mayalla heshima kwako.

Ni kweli hili jambo linahuzunisha saaaana. Pole kwa walioguswa na msiba huu.

Lakini jambo la kutisha zaidi ni mwitikio wa jamii. Watu hawana feelings kabisa na matukio ya askari polisi kuuwawa!!! Wenye feelings ni kama akina Magufuli na akina sisi wachache. Inahuzunisha.

Hao waliovamiwa wangekuwa ni jeshi lingine nje ya polisi, au wangekuwa ni raia wa kawaida, au wanafunzi, mwitikio ungekuwa tofauti kabisa.

Kuna shida sehemu fulani ya mahusiano ya polisi na jamii. Si siri Polisi wanachukiwa na kuogopwa na jamii. Labda polisi hawapewi taarifa za kiintelijensia na wananchi.

Ukitaka kuua kila mtu mwenye silaha tutaalika vifo vingi vya kupangwa. Hatutapunguza, bali tutaongeza chuki zaidi.

Kuna kitu hakiko sawa sehemu fulani. Tujitafakari bila unafiki.
 
Polis nao waache kutafuta kiki...mbona Tanzania yetu iko salama tu..wamepewa hela hao wajifanye wameuliwa....wazir kasema hakuna mauaji wala utekaj unaoendelea Tanzania
 
Kwa pale pwani kuna kitu ambacho kinaendelea,na wazawa wanakijua,sababu viongozi wamekua wakiuliwa toka may mwaka jana,na leo hii polisi na hakuna aliyekamatwa....kwanin viongozi,kwanini pwani??kuna kitu kilichotendwa na wale viongozi,mtu hawezi amua kuua makatibu kata,wajumbe,madiwani,arisk maisha yake na silaha usiku bila sababu,polisi waohoji hata ndugu za marehemu kujua....lasivyo tutaona mengi mabaya
 
So sad..kwa matukio yanayoendelea kule kuna kama kisasi hivi..nadhani muda utazungumza..
 
Nashauri vyombo vyadora visome comment za watu hum ndani nahisi kuna chembechembe za watu km wanajuajua jambo hili, aliyemtaja bashite naomba ahojiwe, aliemtaja mhagama nae ahojiwe, jambo hiri sihatari kwa police tu km mnavyodhani, wala sio kwa watu walindi tu bari nihatari kwa usarama wetu wote . ila police msikate tamaa najua mlikuwa ktk majukum yenu mema ya kurinda taifa poleni sana.
 
Inasikitisha na kushangaza sana. Saanane katekwa mwezi wa sita Serikali kimyaaa, Roma na wenzie wametekwa na kuteswa Serikali kimyaaa, uvamizi wa Clouds Serikali kimyaaa, vitisho dhidi ya Wabunge kutishiwa maisha yao Serikali kimyaaaa! Sasa kama Serikali inafumbia macho haya ni jukumu la nani kuhakikisha usalama wa raia na mali zao? Je, Serikali itaendelea na ukimya wake kufuatia haya mauaji ya kutisha dhidi ya polisi?

Kisifanyike chochote juzi kuna Wabunge wameomba hilo swala lijadiliwe bungeni kuna wanawake jenista mhagama na mwenzie bila hata aibu wanasema ni uchochezi!
Yakasikika makofi ya Wabunge wa ccm waaaa...waaaa....waaaa....
Acha tuendelee hivi hivi
 
Hakuna mifumo imara ya ulinzi na usalama nchi hii. Wanachojua askari wetu ni kufuatana na maafisa wa TRA na kuanza kupora pesa kwa wafanyabiashara kwa kisingizio cha kutoza kodi.
 
Sio sehemu ya vipaumbele vyetu. Nchi ni salama sana mengine ni matukio ya kawaida tu.
 
Inawezekana sawa adhabu ikawa kifo lakini ujue wazi sheria hiyo ikipita watakaonyongwa si majambazi tena bali tutakufa tusio majambazi kwa sababu ya chuki tu zisizo na maana.
Kwa ufupi serikali yetu ni legelege vitu vya msingi haisimamii ila vya ovyoovyo. Kuna uzembe mkubwa sana ktk ulinzi.
 
We we ulitakaje ? Waachiwe na silaha
Ukiona jambazi use your common sense haya ni maisha utaacha watoto wako wanahainga bure huku mke wako akiliwa na marafiki zako
 
Mkiona jambazi ana bunduki umuwahi uchukue bunduki hiyo kauli inawaponza sana sasa jambazi gani atakubali mtaji wake uondoke kirahisi rahisi
Hii kauli ili pokelelewa tofauti hivi jambazi unamnyang'anya vipi silaha yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…