Mauaji ya Polisi wetu ni Ujambazi, Ugaidi au Retaliation? Nini kifanyike kukomesha hali hii?

Mauaji ya Polisi wetu ni Ujambazi, Ugaidi au Retaliation? Nini kifanyike kukomesha hali hii?

Kisifanyike chochote juzi kuna Wabunge wameomba hilo swala lijadiliwe bungeni kuna wanawake jenista mhagama na mwenzie bila hata aibu wanasema ni uchochezi!
Yakasikika makofi ya Wabunge wa ccm waaaa...waaaa....waaaa....
Acha tuendelee hivi hivi
Ngushi unaongea nini mkuu.

Acha siasa njoo kwenye ubinadamu mkuu
 
Tukiwa vijana wadogo wakati huo kijijini,kuna Mzee alikuwa mtemi sana,anapiga mpaka wazee wenzake mbele za watoto na wake zao.Ilikuwa nj zile enzi za "wababe" ndio wanaheshimika,kuna siku aliwahi kumpiga kerebu mzee mwenzake mbele ya mwanae wa kiume.

Kile kitendo kilimuuma sana yule dogo,akakaa na kinyongo moyoni bila kusema,siku ya siku Mzee mbabe tukasikia ameokotwa korongoni kijiji cha Muhunze akiwa hana kaptula ya ndani wala shati,na jana usiku alionekana kilabuni akinywa pombe,miaka kumi baadae ikaja kugundulika alitandikwa na yule dogo ambaye alishuhudia baba yake akitandikwa kerebi kama miaka mitano iliyopita.

Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana,saikolojia ya binadamu ni ngumu kuielewa.Unapofika na kusikia kuwa Masheikh ambao ni mababa wa familia na viongozi wa dini wamelawitiwa na kuminywa korodani mpaka kupoteza uwezo wa kusimamisha,unategemea hii chuki inakaa wapi?

Unapombambikia mtu kesi ya uwizi,anasota rumande kwa mateso na karaha,tambua huyu ana ndugu na watu wanaompenda walio tayari kulipa kisasi ili kuridhisha nafsi zao.

Wapo watu wanaofungwa bila makosa,wapo wanaobambikiwa kesi kwa sbb za kisiasa,haya yote yanajenga chuki kati ya raia na askari polisi.

Polisi unafika kwenye kijiwe cha bodaboda unasomba pikipiki 20 kisa wamezidi muda wa "serikali" wa saa sita usiku,na ili wazitoe pikipiki zao,basi kila mtu anatakiwa kutoa elfu50....hii chuki inamea kama mmea kando ya kijito

Umeongea kwa hisia sana mkuu,,ila kweli ifikie wakati Jeshi la police wafanye kazi kisayansi na kujenga ukaribu na raia,, ila haya matukio inavyonyesha kama Kuna ulipizaji visasi fulani,,,,hapa ndio idara ya usalama wa Taifa inatakiwa wapandikize watu katika ivyo vijiji mkoa wa pwani ili kupata kiini aswa cha haya matukio yote
 
Mkuu;
Hii haipo kokote kati ya hayo ulioyataja. Wala watu wasidhan ati majambazi wamefikia mahali pa kuweza okota/kusanya bunduki nyingi hivyo. Za kazi gani?? Una maana hawana akili ya kujua kuwa wanawatibua jeshi?? Naomba Serekali, iache papara za hasira za kuwatafuta msituni. Sidhani kama wapo huko. Intelijensia yetu itulize vichwa na kulisoma hili somo.
Naamini watatoka na kitu cha kuweza kumaliza kabisa jambo hili na liwe somo kwa wahusika hao waovu. Bado tuna serekali makini Tz.
Nasema, hawa sio magaidi, sio majambazi bali ni watu wenye nia ya kututoa kwenye njia sahihi. Naunga mkono kuwa, kwa sasa nchi sio tulivu.
 
Ndio maana nakwambia hili.la.pwani ni chezo. Maana haiwezekani kama mamlaka zinajua halafu ziko kimya...huo ni usalama wa aina gani??? Nini kinaandaliwa hapa ambacho hatukijui...Je wanatengenezwa ******** ndio maana hakuna hatua....Mbona wale wasomali kipindi kile walivyoua polisi waliisoma namba dakika tu kutoka kwa jwtz?? Imekuwaje hapo pwani katikati ya nchi watu wanafanya mauji tangu mwaka jana wanaua viongozi but watu wako kimyaaaaa as if kuna sio roho za watu zile.
Ni kweli kabisa kuna mambo mengi nyuma ya pazia.ila ukweli utafahamika very soon
 
Mkuu;
Hii haipo kokote kati ya hayo ulioyataja. Wala watu wasidhan ati majambazi wamefikia mahali pa kuweza okota/kusanya bunduki nyingi hivyo. Za kazi gani?? Una maana hawana akili ya kujua kuwa wanawatibua jeshi?? Naomba Serekali, iache papara za hasira za kuwatafuta msituni. Sidhani kama wapo huko. Intelijensia yetu itulize vichwa na kulisoma hili somo.
Naamini watatoka na kitu cha kuweza kumaliza kabisa jambo hili na liwe somo kwa wahusika hao waovu. Bado tuna serekali makini Tz.
Nasema, hawa sio magaidi, sio majambazi bali ni watu wenye nia ya kututoa kwenye njia sahihi. Naunga mkono kuwa, kwa sasa nchi sio tulivu.
Kafara za Bashite hizo na njia anazosaka ni kuwasahaulisha watanzania juu ya vyeti vyake pia ameingia gharama kubwa kuwaleta waganga wa kienyeji toka pande nyingi Duniani anahofia akitumbuliwa jipu ni nani atampa pesa za kuwagharamia ikiwemo kuwarejesha kwao.
 
Kafara za Bashite hizo na njia anazosaka ni kuwasahaulisha watanzania juu ya vyeti vyake pia ameingia gharama kubwa kuwaleta waganga wa kienyeji toka pande nyingi Duniani anahofia akitumbuliwa jipu ni nani atampa pesa za kuwagharamia ikiwemo kuwarejesha kwao.

Mkuu;
Naogopa kabisa kuchangia neno hapo kwa sababu unayemtaja aweza hata tokea hapa kwenye hii pc yangu. Nitamjibu nini??
 
Matukio yanayotokea huko Pwani ni asilimia 100 ugaidi. Kitu cha kushangazaa ni hawa magaidi kuua na kuchukua silaha je wanamipango gani na hiyo silaha. Serikali isichukulie suala hili mzaha ama ujambazi wa kawaida kwani tunatakiwa tujifunze kutoka Nigeria jinsi Boko Haram ilivyoanzishwa. Mkoa wa pwani unapakana na bahari ya hindi na mnavyoelewa kuna tatizo la magaidi Kenya na Somalia je serikali inatathimini vipi watanzania wangapi wamejaribu ama wamejiunga na vikundi hivyo vya kigaidi na kurudi hapa nchini. Leo hii tunaona nchi za ulaya kuna vijana waliokuwa wamejiunga na Islamic State huko Syria wamerudi ulaya na kuanza kufanya ugaidi. Tuangalie suala la uchumi pia sasa hivi sisi na majirani zetu tuko kwenye vita vya kiuchumi katika ujenzi wa bomba la mafuta, reli na utalii majirani zetu wameonekana sio salama na Tanzania imeonekana ni nchi salama kunauwezekano wa hawa majirani zetu wakatumia watu wabaya ili Tanzania isionekane nchi salama,
Serikali ilichukulie hili suala very very serious kabla halijawa out of control.
Umeongea Pumba tu, na uchochezi wa hali ya juu.
Inaeesekana pia weewe ni mmoja wa wahusika wa hili tukio, ndio unawahi kujikosha mapema kusingizia ugaidi.
Wewe unaujua ugaidi au unausikia redioni tu.
Kama hujui chochote nyamaza kimya, utakapochkuliwa utoe ushahidi wa kusema kuwa una asilimia 100 utasemaje saasa kama na wewe sio muhusika wa tokeo.
Acha upumbavu na ujinga wako huo wa Chuki binafsi, tafuta vitabu usome maana shule haikukusaidia kitu.
 
Askari kama Mtanzania yeyote ana haki ya kujilinda na kama kujilinda huko kunaitaji kuua ili asiuwawe yeye basi anaruhusiwa kuua. Haki ya kujilinda ipo kwenye Katiba ya JMT.
 
Mkuu Panzi Mchanga, kwanza asante kuchangia uzi huu. Pili asante kunifuatilia tangu enzi za Kiti Moto.

Huu uzi ni uzi wa swali, hivyo solutions inatokana na michango ya wachangiaji.

Hiyo link umeifungua na kuisoma uone nilisema nini lini na leo kimetokea nini? .

Hii thread ni ya kichonganishi kumchonganisha nani na nani? .

Paskali

Paskali;

Shukrani kwa kufuatilia.

Nimesoma hiyo link; na kimsingi nisingeandika niliyoandika hapa kama sikuisoma hiyo link. In fact ningekuwa reader tu. Ni kweli umeuliza swali na watu wachangie. Bahati mbaya swali lako ni la kimkakati (a strategic question). Ingawa ni swali, platform ulipoliweka hilo swali hasa kwa kulink na thread ya nyuma; tayari ulitaka watu wafahamu hii ni ngoma ya aina gani na tunaenda na mavazi gani kuicheza. Na kimsingi ndicho kilichojitokeza kwa coments za watu humu.

Nimesema thread imekosa uzalendo, kwa maana structure ya swali imeibua mijadala amabyo haiwatendei haki wenyeviti karibu kumi waliouliwa na hawa wahalifu. Imekosa uzalendo pia kwa kutengeneza structure ya swali ambapo mijadala inayoibuka inakatisha tamaa kwa askari walioenda kulinda wananchi na wenyeviti wa vitongoji wasiuliwe na zaidi ya mia.

Ukichanganya thread ya leo na attachement yako, ni dharihi ulitaka wachangiaji wajenge uhasama kati ya serikali (jeshi la polisi) na wananchi.

Najua una uwezo mzuri tu. Kipindi kile ulikuwa unatangaza hoteli za Tanzania na nafikiri hii product ulitengeneza mwenyewe, na pia jinsi ulivyokuwa unaleta coverage za saba saba; basi ina imani ukijichimbia kule kibiti unaweza kuibuka hali halisi.

Shukran
 
Mkuu Pascal heshima kwako. Kwanza nitoe pole kwa jeshi la polisi na kwa familia na ndugu wote waliopatwa na misiba hii. Mimi nitachangia upande wa recruiting and training za polisi wetu. Mkuu, utaratibu wa kuajiri na mafunzo kwa vijana wetu nadhani haupo sawa, huwezi kuajiri watu kwa kujuana, watu wenye elimu zao halafu, wasio na wito, utayari, kujitoa halafu unawapeleka kwenye mafunzo ambayo kimsingi hayaendani na wakati tulionao. Unamchukuaje mtu ambaye amemaliza chuo, hajaoa, hajamaliza hata mkopo wake wa bodi, ambaye kwao waliuza rasilimali zilizokuwepo akasomea halafu unampeleka kwenda kupambana na jambazi. Automatically ndo maana linapotokea tukio la uhalifu polisi hufika baada ya nusu saa au saa moja na wakikaribia hupiga risasi hewani ili kukwepa kukabiliana na majambazi live. Inawezekana mbinu za mafunzo , aina ya askari wetu (watoto wa wakubwa) hawawez kuifanya hii kazi kwa ufanisi au wanaogopa kutokana na kwenda huko kama sehemu ya kukulia au kutafta kipato na si vinginevyo. Naamini utaratibu wa zaman uliokuwa unatumika kuajiri wana usalama ilikuwa nzuri, huko mitaani kuna watu ukiwapeleka huko kufanya kazi kama hiyo wataifanya vyema. Mkoa wa Mara kwa mfano kuna watu wakiskia risasi ya jambazi wanaanza kukimbia kwenda inapotokea, huku Pwani hawa waswahili ni kinyume. Sikatai jeshi kuwa la wasomi, ila wasomi wawepo wachache wenye kupanga mipango ila wale rapid responders si lazima wawe wasomi amabao huenda huko huku akikumbuka amesoma miaka mingi hajatimiza malengo yake n.k. Tuachane na huu utaratibu wa sasa wa kuajiri kwa kujuana huku tukijaza watoto wa vigogo kwenye majeshi yetu ambao wakifika huko akili zao ni kuzichanga na si vinginevyo, hivi mmewahi kujiuliza Kwanini polisi wakitumwa kwenda kumkamata mwanasiasa wanaenda kwa mbwembwe ilihali shughuli kama hii ya kupambana na wahalifu /majambazi kabla ya kufika eneo la tukio huanza kufyatua risasi hewani ili kuwa alert majambazi kukwepa kupambana nao? Mtaala wa mafunzo ndani ya jeshi letu ubadilishwe ili kuendana na wakati na ufocus miaka mingi ijayo. Jeshi letu inawezekana ni worse kulikon tunavyofikiria, wamejaa wapiga dili, watoto wa vigogo, wavivu na watu wasiokuwa na mori, uzalendo. Tutengeneze kikosi imara, wenye ari. Kuna vijana huko vijijin ukiwachukua na kuunda kikosi maalum ndani ya jeshi letu let's say "First Responders" na mbinu mpya tutasonga mbele. Asante.

Nakubaliana na wewe ndugu. Polisi wetu hawajakaa kiutayari. Hata jinsi wanavyolinda mabenki. Amekaa na bunduki kaweka pajani. Kule kibiti ukipishana nao kwenye gari, wamejikusanya wote wanaangalia mbele. Pia aina ya magari wanaotumia yana chuma kwa juu. Sii rahisi kureact haraka . Kile chuma ni kizuizi. Hata pale kwenye kizuizi, mmoja anazuia na wengine wamejirundika hapo chini ya mti.

Jeshi letu la polisi linapaswa kufanya mapitio ya mkakati wao wa ulizi.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Umeongea Pumba tu, na uchochezi wa hali ya juu.
Inaeesekana pia weewe ni mmoja wa wahusika wa hili tukio, ndio unawahi kujikosha mapema kusingizia ugaidi.
Wewe unaujua ugaidi au unausikia redioni tu.
Kama hujui chochote nyamaza kimya, utakapochkuliwa utoe ushahidi wa kusema kuwa una asilimia 100 utasemaje saasa kama na wewe sio muhusika wa tokeo.
Acha upumbavu na ujinga wako huo wa Chuki binafsi, tafuta vitabu usome maana shule haikukusaidia kitu.
Kuna watu huwa wanafuatilia masuala haya ya ugaidi kwenye vyombo vya habari sasa wewe bwege baki kutoa comments za kijnga wakati weledi wako ni kuwaza chai maharage.
kuna msemo usemao never argue with a fool.
 
Vikosi vya ulinzi kipolisi mkoa Wa pwani vibadilishwe haraka sana vimeshindwa kazi au kamanda siro ahamie pwani akakomeshe jambazi huo haiwezekani kila Siku habari watu kuuawa tu
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Wanabodi,
Taifa bado liko kwenye shock ya nini haswa kilichotokea kwa askari wetu?.

Mauaji haya ya Polisi Wetu ni Ujambazi tuu, ni Ugaidi au Retaliation?. Wakati vyombo vya uchunguzi vikiendelea na kazi yake, Sisi Watanzania kama taifa lazima tujiulize, Nini Kifanyike Kukomesha Hali Hii?,

Kwanza nikiri nimesikitishwa na vifo hivi vya vijana wetu askari polisi kushambuliwa na kuuwawa na majambazi wenye silaha.

Swali ni jee huu ni ujambazi tuu wa kawaida, uvamizi kwa lengo la kuiba silaha, ni ugaidi, ambush au nini haswa?.

Hili kuwaweka polisi wetu kwenye risk na kuwa an easy target, kwa majambazi wanaotumia silaha, niliwahi kulizungumza hapa kwa kirefu Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?
Kwa tukio kama la jana,jee mnadhani huu sasa ni wakati muafaka wa kuzibadili sheria zetu za jeshi la polisi ili kuwalinda polisi wetu wawe licenced to kill officially na serikali itangaze rasmi kuwa ujambazi wa kutumia silaha adhabu yake ni kifo cha papo kwa papo, no prosecution no kesi, bali ni hukumu ya kifo there and then ili kuwaogofya kabisa majambazi wote wanaotumia silaha wasithubutu?!.

Kama ni ugaidi au retaliation, tufanye nini?.

Natoa pole kwa rais wetu wa JMT, waziri wa Mambo ya Ndani, IGP na familia za askari hao!

RIP Askari Wetu.
Nini Kifanyike? .
Ijumaa Kuu Chungu!.
Paskali
Update 1.

Thanks very objective.

Paskali
Update 2 ya michango very objective

Thanks kwa mchango huu, very objective
Paskali
Update 3.
Huu ni mchango very objective

Thanks for this.
Paskali

Pascal, kuhusiana na <<<Kwa tukio kama la jana,jee mnadhani huu sasa ni wakati muafaka wa kuzibadili sheria zetu za jeshi la polisi ili kuwalinda polisi wetu wawe licenced to kill officially na serikali itangaze rasmi kuwa ujambazi wa kutumia silaha adhabu yake ni kifo cha papo kwa papo, no prosecution no kesi, bali ni hukumu ya kifo there and then ili kuwaogofya kabisa majambazi wote wanaotumia silaha wasithubutu?>>>, bila shaka umesahau kwamba hii iliwahi kujaribiwa hapa nchini na matokeo yake yakawa maafa makubwa.

Utakumbuka Kikwete alipoingia madarakani 2005 alikuja na agenda ya kutokomeza ujambazi; akaanzisha wizara mpya mbali na ile ya mambo ya ndani iliyoitwa Usalama wa Raia na kumteua Harith Bakari Mwapachu kuwa waziri wake.

Moja kati ya mikakati wa Waziri Mwapachu ya kupambana na ujambazi ilikuwa ni kuwapa polisi mamlaka ya kupiga majambazi risasi (shoot and kill) papo kwa papo.

Matokeo ya mkakati huo yalikuwa ni majanga makubwa. Majambazi hayakuguzwa ila makumi ya raia wasio na hatia ndio waliokubwa na sekeseke la "shoot and kill" wakiomo wafanyabiashara wa madini wa Morogoro na taxi driver waliouawa kinyama na polisi katika maeneo ya Ukuta wa Posta, Sinza.

Yaliyoendelea baada ya hapo ikiwa ni pamoja na kuundwa tume ya uchunguzi ya Jaji Kipenka kuchunguza hayo mauaji ni historia. Itoshe tu kukushauri uondoe hilo pendekezo katika bandiko lako.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Wanabodi,
Taifa bado liko kwenye shock ya nini haswa kilichotokea kwa askari wetu?.

Mauaji haya ya Polisi Wetu ni Ujambazi tuu, ni Ugaidi au Retaliation?. Wakati vyombo vya uchunguzi vikiendelea na kazi yake, Sisi Watanzania kama taifa lazima tujiulize, Nini Kifanyike Kukomesha Hali Hii?,

Kwanza nikiri nimesikitishwa na vifo hivi vya vijana wetu askari polisi kushambuliwa na kuuwawa na majambazi wenye silaha.

Swali ni jee huu ni ujambazi tuu wa kawaida, uvamizi kwa lengo la kuiba silaha, ni ugaidi, ambush au nini haswa?.

Hili kuwaweka polisi wetu kwenye risk na kuwa an easy target, kwa majambazi wanaotumia silaha, niliwahi kulizungumza hapa kwa kirefu Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?
Kwa tukio kama la jana,jee mnadhani huu sasa ni wakati muafaka wa kuzibadili sheria zetu za jeshi la polisi ili kuwalinda polisi wetu wawe licenced to kill officially na serikali itangaze rasmi kuwa ujambazi wa kutumia silaha adhabu yake ni kifo cha papo kwa papo, no prosecution no kesi, bali ni hukumu ya kifo there and then ili kuwaogofya kabisa majambazi wote wanaotumia silaha wasithubutu?!.

Kama ni ugaidi au retaliation, tufanye nini?.

Natoa pole kwa rais wetu wa JMT, waziri wa Mambo ya Ndani, IGP na familia za askari hao!

RIP Askari Wetu.
Nini Kifanyike? .
Ijumaa Kuu Chungu!.
Paskali
Update 1.

Thanks very objective.

Paskali
Update 2 ya michango very objective

Thanks kwa mchango huu, very objective
Paskali
Update 3.
Huu ni mchango very objective

Thanks for this.
Paskali
Before granting license to kill to the police we need to assess the degree of honesty, integrity and sense of malice towards our security personnel. Otherwise let them arrest and take the jambazi into the court of law.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Ngushi unaongea nini mkuu.

Acha siasa njoo kwenye ubinadamu mkuu
Ni kweli mkuu,ulisikia kauli ya jenista mhagama na Angela kairuki bungeni juzi?
Yaani kujadili kuhusu haya mauaji na utekaji ni uchochezi_?
Unahisi walikuwa sahihi?
Na wakapigiwa makofi kabisa kuungwa mkono.......unafiki wa aina gani huu!
Tukitaka kuteketeza haya maswahibu lazima viongozi waache unafiki....blue iitwe blue sio kuleta unafiki kama walivyofanya juzi!
Kuna yule ally kesi wanasema Roma angeuawa kabisa na anapigiwa makofi!
Halafu kwenye mambo kama haya eti tuwe pamoja......
 
Ni majambazi, neno gaidi tafsiri yake nini?
Gaidi ni mtu anaefanya vitendo vya kuvunja sheria ili kufikia malengo ya kisiasa. Hii inaweza kusababishwa na Imani za kisiasa ama kidini. Jambazi ni mtu anaeiba kwa kutumia nguvu. Kwa nini nasema hao sio majambazi, majambazi mara nyingi hununua silaha duniani kote, hawana ujasiri wa kuvamia kituo cha polisi kikubwa kama Sitaki Shari na kuua askari na kupora silaha. Psychological tu majambazi wanaogopa polisi na magereza. Hata ukiwauliza askari waliosomea hiyo kazi watakuambia hakuna jambazi ana ujasiri huo. Labda gaidi kwa sababu amejitoa kufa kwasbb ya imani flani
 
Back
Top Bottom