Siwezi kumlaumu mtoa mada, nyinyi nyote mnaomkebehi hata kesho zenu hamzijui. Hujui utaangukia kwa nani, msiongee kama maisha mmeyamaliza wakati bado mnavuta pumzi.
Niliwahi kuongea hivyohivyo, nikaambiwa hujapenda ndiyo maana nikipenda nitakaa kimya mwenyewe. Mungu si Athumani, nikaja kupenda kufa kuoza. Nilipokuja kupigwa chini nilikaribia kupagawa, nili move on kwa kuhakikisha ninamsahau tu.
Hivyo Mtoa Mada kama unataka umsahau ili upige hatua mbele, inabidi uondoe kila kitu ambacho kinakufanya umkumbuke. Hivyo vitu vyake kuwa na msimamo wa kueleweka, mwambie aje kuchukua la si hivyo unaviharibu, kuvitupa au kuvigawa. Muwekee deadline kabisa kuwa serious unapomwambia, ikifika siku hiyo hajaja viondoe. Maana ndiyo vinakukumbusha kuhusu yeye, huwezi kumsahau kama vipo.
HAPA KAMA KWELI ANAMAANISHA MWACHANE ATARUDI NA KUVICHUKUA, KAMA ANAKUPIMA IMANI ATAREJEA PIA ILA ATAFANYA KILA HILA ASIVICHUKUE ANAJUA KAACHA KUMBUKUMBU.
KAMA KESHACHUKUA VITU ENDELEA SASA;
Picha zote mlizokuwa pamoja ziondoe, ubaki kama ulikuwa humjui. Pia kama una simu ndogo ya kawaida tumia hiyo, smartphone fungia kwa wiki tatu au mwezi hivi kama hiyo whatsapp usioone kama haina tija kwako zaidi ya kuchat. Ukisema ubaki nayo utajikuta umeingia huko na kusoma hivyo vijembe tu, dawa ni kukaa mbali na simu.
Muda ambao mliokuwa mkiutumia kuwa pamoja, jaribu kutafuta kitu kingine cha kufanya. Mazoezi ya viungo ndiyo yanafaa zaidi, nyakati nyingine kuwa active kwenye kazi kuliko kitu kingine. Ukiwa kwako utahitaji kupumzika kuliko kitu chochote, hutoweza kumkumbuka tena maana huo muda wa free kwako utahitaji kupumzika tu na si kufikirisha akili.
Kipindi unajaribu kumsahau, tafadhali sana usijihusishe kimahusiano na mwingine. Hata kama utamsahau usikimbilie kuanza mapenzi mapya, pumzisha moyo na akili kiupande wa mapenzi.
HUWEZI JUA MUNGU KAKUEPUSHIA NINI ALIPOKUACHA, PIGA KAZI UJIONGEZEE KIPATO