Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)

Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,030
Reaction score
20,391
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!
.
Sehemu ya kwanza.
.
Mwaka 2016 ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia chuoni, ilikua katika chuo cha kimataifa cha Kampala.
Naikumbuka siku yangu ya kwanza nilikua naonekana mnyonge sana, hasa kutokana na ugeni wangu na kila mmoja ndani ya darasa alikua ameonekana kutokumzoea mwenzake.
.
Pindi lecture inaendelea, nilikua niko makini sana kusikiliza kile ambacho lecturer alikua akifundisha darasani, nikatupa macho yangu pembeni kuwatazama classmates wangu, kila mmoja alionekana yuko busy akimsikiliza.
Lakini pembeni yangu nilishangaa kumuona kijana mmoja akiwa ameduwaa, na wala hakuonyesha kufatilia kinachofundishwa. Nikapata shauku ya kutaka kujua kinachoendelea, anatazama nini hicho kiasi cha kumfanya aduwae kiasi kile, nikatupa macho kwa mbele zaidi kuelekea uelekeo wa macho yake.
.
Nilipigwa na bumbuwazi, nami niliduwaa zaidi ya yule kijana, macho yalinitoka huku nikiongeza umakini zaidi wa kutazama kile nilichokiona.
Macho hayana panzia, yalitua kwa msichana mmoja mrembo aliyefanya mimi na yule kijana tuduwae. Wala hakujua kama tunamtazama, alikua busy akifatilia lecture.
Nilitengeneza movie nyingi za mahaba kichwani mwangu juu ya yule msichana.
.
Ghafla nilishtushwa mawazoni mara baada ya lecturer kuuliza swali, na kuniomba mimi niliyeonekana sifatilii somo nilijibu swali hilo.
.
Lecturer: Differentiate between a manager and an entrepreneur???
.
Kwa mbwembwe zote, tena huku nikimtazama mtoto mkali, nikanyanyuka, nikamtazama lecturer na kujibu swali.
.
Siku ya kwanza ikapita kama hivyo, na ndiyo siku niliyoanza kumpenda.
.
Siku kadhaa zilipita, nikiwa tayari nimeshayazoea mazingira chuoni hapo, nikijulikana kama kijana mstaarabu na mcheshi ndani na nje ya darasa.
.
Siku moja nilipokuwa darasani nikifanya assignment kwenye laptop.
Ghafla ilisikika sauti nyororo yenye kumtoa nyoka pangoni, moyo ulinipiga Paaah, damu ikaanza kunichemka, nikapata shauku ya kutaka kujua ni nani huyu ananiongelesha.
.
Nikanyanyua uso ili nimtazame uso, macho yangu yalikutana na mavazi safi yenye kung'ara, zaidi ilikua ni harufu yake ya pafyumu iliyozidi kunivutia, nikapanda mpaka juu na kukutana uso kwa uso na msichana mrembo aliyekuwa akilini mwangu siku zote tangu nianze chuo.
.
Nilibaki nashangaa kwa sekunde kadhaa, ikabidi arudie salam yake.
Yeye: Hi.
Mimi: Hi, how umh how you doing?
Yeye: Doing great, sorry for disturbance, can you do me a favor?
.
Nikasikiliza jinsi anavyoteleza kwenye lugha ya kigeni, nikaona hapana, huku tunako endelea atanipoteza mwisho nipate aibu, mimi st.kayumba, English ilipanda ndege.
.
Nikamjibu: Bila samahani, wala hujanisumbua. Yes unaweza sema tu maybe naweza saidia.
Yeye: Onh asante kwa ukarimu wako, naomba unielekeze jinsi ya kuset hotspot kwenye iPhone, nataka niconnect na laptop yangu ".
.
Alizidi kunivutia kwa maneno yake matamu, nikajisemea kimoyo moyo "Haya ni maneno ambayo kina Mwajuma Ndalandefu uswazi hawawezi kuyasema, na leo ndo chance nzuri ya kujuana nae vizuri ".
Sikutaka kuchelewa nikachukua kiti, nikamsogeza karibu na kuanza kumpa maelekezo.
.
Nilipomaliza alishukuru sana, lakini alipotaka kuondoka tu akatupa jicho kwenye laptop na kugundua nilikua nafanya assignment.
Akasema na yeye alikua bado hajafanya, nikamuomba tujumuike ili tufanye wote.
.
Shida yangu haikuwa tufanye wote assignment, shida yangu ilikua tuzidi kuzoeana ili hata kesho yake nisipate tabu tena kuanza kujitambulisha.
Nilizidi kumnogesha kwa story ambazo zilimfanya azidi kucheka huku tukifanya assignment.
.
Tulipomaliza wala hakunyanyuka kama mwanzo, aliendelea kukaa na tukazidi kupiga story.
Nikaona nisichelewe kutaka kumjua.
.
Mimi: Hahah yale makoti hayafai kwa Dar es salaam hii, labda utembee huku na feni pembeni.
.
Akacheka, kisha akatazama saa yake, nikastuka nikajua huu utakua muda wa lunch au kuondoka tayari.
Nikamuwahi "Btw nimefurahia sana uwepo wako, na umefanya niione assignment nyepesi pia.".
.
Akanijibu "Asante sana, tangu nianze chuo leo ndo nimefurahi sana, ndomana nimetazama saa hapa nikashangaa leo nimebaki hadi saa 7".
.
Mimi: Onh nimefurahi kusikia hivyo, kwani haujapata marafiki bado?!
.
Yeye: You know what, mahali kama hapa pana watu tofauti, waliotokea kwenye malezi tofauti. Na usipokua makini kwenye uchaguzi wa marafiki, ukawa unaparamia tu, basi unaweza jikuta unapata marafiki wa hovyo hovyo.
Najiheshimu sana, na napenda niwe na marafiki wanao jiheshimu pia, hata wewe nimekufata mpaka kukuomba unisaidie, sababu nilijua wewe mstaarabu na ni tofauti na vijana wengine darasani."
.
Nikashusha pumzi nzito sana, maneno yaliniingia sana akilini. Mwanzo nilikua na wazo la kumuomba namba leo leo, lakin nikaona hapana huyu nikienda nae haraka nitampoteza, anajithamini na kujiheshimu sana tofauti na nilivyofikiria.
.
Nikamjibu: Uko sahihi kabisa, hata mimi ndio maana unaona nakaa peke yangu sana sababu hiyo hiyo, naogopa kujiingiza kwenye makundi ya watu wasio na maadili.
Hata hivyo, nimefurahi kujua kama uko tofauti na wasichana wengine, naitwa Chris. "
.
Yeye: Nice to meet you Chris, naitwa Careen".
.
Mimi: "Damn, nice name''
.
Akafurahi sana, tukaagana na kuondoka. Nakumbuka nilijilaumu sana kwanini sikumuomba namba yake ya simu, lakini nilijipa moyo kuwa huo ni mwanzo mzuri sana kwangu, na pia ni jambo zuri kutokumuomba namba mapema kiasi hicho kutamfanya asihisi chochote kuhusu hisia zangu kwake.
.
Siku iliyofata mambo yalizidi kuwa moto darasani, nakumbuka alibadili sehemu yake ya kukaa na kuja kukaa karibu nami, alikua akipenda kuniita kaka Chris, japo sikupenda kuitwa "Kaka" lakini nililivumilia tu sababu sikupenda ahisi kuwa nina hisia juu yake.
.
Watu walikua wakitutazama sana, na wengine kuulizana hawa Wamezoeana saa ngapi, sababu hakua na mazoea na mtu yeyote yule zaidi yangu, na wengine aliishia kuwapa salamu na story mbili tatu pale inapobidi.

Nilifurahishwa sana na mwenendo wake, hasa ukizingatia hakuna mwanaume anayependa kuwa na mwanamke ambaye Mcharuko, au anajifanya ana mazoea na kila mtu.
.
Nakumbuka siku ya tatu ya urafiki wetu, majira ya saa 6, nilimuomba twende tukapate lunch wote, hasa ukizingatia nilitaka niwe rafiki yake wa karibu zaidi ambaye ataweza kula nae, kuongea nae, kuniambia jambo lolote hata lile lisilo ambikika kiurahisi, ambaye atamkumbuka wakati wa huzuni na furaha.
Kwakifupi, nilitaka niwe kila kitu kwake, ili hata pale nitakapo muhitaji tuwe wapenzi basi asiweze kukataa, yani niwe nimemtengeneza kihisia zaidi.
.
Tulielekea wote mpaka maeneo pakulia, maarufu kwa jina la PEPSI, sote tulichukua chakula na kuelekea mezani, story zilikuwa nyingi na chakula kilinoga.
Alikua akiniambia jinsi anavyojisikiaga aibu kula mbele za watu hasa wanaume, ila anashangaa leo hii ameweza kukubali kukaa meza moja na mimi.
Nilimshika mkono, nikamtazama usoni, nikamwambia ''Mimi ni rafiki yako, usiniogope, usinioneee aibu, jisikie huru kufanya lolote unapokua nami, ili tuwe marafiki bora basi inabidi tusioneane aibu."
.
Alitabasamu na chakula kiliendelea kuliwa, tulipomaliza tukaelekea mahali pakulipia, kwavile mimi ndiye niliyemualika, na ndiyo mwanaume, basi nikataka kuvimba ili nilipe bill.
.
Nikaingiza mkono mfukoni ili kuchukua wallet, nikastuka, nikaanza kupagawa baada ya kuikosa wallet kwenye mfuko wa nyuma wa suruali ninako wekaga.
.
Nikasearch na mifuko mingine sikukuta kitu.
Mwanadada ambaye ndiye mpokea malipo akaniongelesha tena "Nakusubiria wewe kaka".
.
Careen aliyekuwa kwa pembeni akageuka na kunitazama usoni, ikabidi nivunge nisionyeshe wasiwasi wangu.
Nikarudisha mikono mfukoni kuhakikisha kwa mara ya pili, mapigo ya moyo yalizidi kunidunda baada ya kugundua kuwa mfukoni ni kweupe, na dada mpokea malipo alikua akinitupia jicho.
.
Mawazo yakawa huyu binti, atanionaje??? Je atanisaidia kulipa??? Au nae hana hela?? Sindo mwanzo wa kuaibika huu??!
.
_______________________________
Usikose sehemu ya pili
Itaendelea....

Soma Sehemu ya pili hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN).

Sehemu ya pili....

#Ilipoishia: Nilimuomba Careen tukapate wote chakula cha mchana, tulikula pamoja na kukifurahia, lakini tatizo lilikuja baada ya kufika wakati wa kulipa bill za chakula tulichokula.

Kama mwanaume nilijitutumua na kuingiza mkono mfukoni ili kulipa bill, bahati mbaya wallet haikuwepo mfukoni.
Nikachanganyikiwa sana, nikarudia mara mbili mbili kutafuta wallet mifukoni kote lakini sikuiona.
*****************
#Inaendelea:
Uso ulilowa jasho la ghafla, nilikuwa kama niliye changanyikiwa, sikujua la kufanya na zaidi kilichoniumiza ni kuwa leo hii na kwenda kuaibika mbele za msichana ninaye mpenda.

Nikapukuta mifuko yangu yote, bado kweupe, ikabidi nirudi mpaka kwenye viti tulivyokalia wakati wa kula ili kutazama endapo kama ipo wallet yangu.
Wala sikuikuta, nikawa narudi na mawazo mengi kichwani je atanielewa??? Nitaaibika kiasi gani???

Nilianzwa kulengwa na machozi, huku mwili ukiwa umetapakawa na jasho.
Nikapiga moyo konde na kusema liwalo na liwe.
Careen alinitazama kwa huruma pindi nilipokuwa narejea, sikumwambia nilichokua natafuta ila kwa zile purukushani basi nahisi alijua.

Nikamuona anaingiza mkono kwenye pochi yake, na kutoa noti ya wekundu wa msimbazi, kisha akarudishiwa chenji, akaipokea na kubaki akinisubiri ili tuondoke.

Nilikumbwa na aibu kubwa sana mbele ya msichana ninaye mpenda, lakini hata hivyo nilitamani nishangilie sababu niliona afadhali alivyolipa amenipunguzia kupata aibu kubwa zaidi.

Nikamsogerea, akanitazama na kuniambia "Umedondosha wallet??? "

Nilitamani kumjibu "Kwani ulikua huoni nilichokua natafuta au?", lakini nikawa mpole zaidi, nikainamisha kichwa changu chini kwa aibu, nikamjibu "Yeah, na sijui imedondokea wapi. I'm really sorry for what happened ".

Careen: Usijali, pole zaidi, kama hapa umeikosa basi ujue itakua umeidondosha darasani au umeisahau kwenye bag."

Mimi: Nadhani itakua hivyo.(nikazungumza huku tukiondoka, kidogo nilipata nguvu ya kujifuta jasho, lakini nilikosa kabisa nguvu ya hata kunyanyua uso wangu kumtazama usoni.)
.
Njiani nilitamani nitembee haraka niwahi darasani nilikoacha bag, nikatazame kama wallet ipo ili nimlipe pesa yake ... ila pia nafsi ikaniambia tembea nae taratibu tu, usijionyeshe dhaifu sana.)
.
Tulitembea kama mabubu, kuna muda alijaribu kuniongelesha lakini nilikua muitikiaji tu, nahisi hata angesema "Wewe mjinga" mimi ningeitikia tu "Ndio" bila kujijua.
Akanishika mkono, akaniambia "Sasa kaka Chris, tutaonana tomorrow, nahitaji kuwahi kwenda kwenye semina kanisani jioni "
.
Nilistuka, nikamjibu "Sawa, ila tungeenda hivi ili kama nitaikuta wallet basi nikurudishie hela yako".
.
Akanitazama, akatikisa kichwa akiashiria kukataa, akanijibu "Hapana usijali, wewe rafiki yangu, so sio mbaya leo nikalipa mimi, kesho utalipa wewe, tutakua tukishare kidogo tulichonacho.".
.
Maneno yaliniingia moyoni, nikahisi niko na mwanamke tofauti sana.
Najua hapa mwingine angenichamba au pale pale angeniacha niaibishwe mbele za watu.
.
Kwa aibu nikajibu "Dah, asante sana maana nilivurugwa ghafla, ubarikiwe sana ".
Akanijibu "Asante, what if ukikosa wallet huko? Chukua hii chenji itakusaidia hata kwa nauli ya kurudia nyumbani ".
.
Nikamtazama, nikamjibu "Anh no, no, asante sana, mi sikai mbali, nimepanga hostel ya hapo nje tu. Na nimeacha kiasi cha kutosha mwezi mzima hostel". (Nikazungumza kwa kujiaminisha ili nisionekane dhaifu).
.
Akaniamini, tukaagana na akaniachia mkono na kuondoka.
Sikutaka kumsindikiza kwa macho wala nini, nilitoka nduki mpaka kwa jamaa niliyemuachia bag langu, nikatafuta wallet na kuikuta imetulia bila wasiwasi kwenye kimfuko kidogo cha bag.

Nikasonya, nikaitia makofi matatu, "Shenzi kabisa, yani kuniaibisha kote kule kumbe umetulia tuli kwenye bag"- nilizungumza kwa hasira.

Hasheem: "Chris vipi? Mbona unaongea peke yako bro? "
Chris: "Dah acha tu bro, nimeitafuta wallet sana, kumbe iko kwenye bag ".
Hasheem: "Hahah hiyo kawaida sana, nilishawahi weka simu kwenye mfuko wa shati, halafu nikasahau, nilitafuta siku nzima, nikarudia sehemu zote nilizopitia siku hiyo. Baadae sana ndio nikaja kuiona mfukoni".

Chris: Hahaha (Nilicheka kinafki tu maana sikuwa hata kwenye mood ya kucheka kwa siku hiyo, nikaaga na kwenda hostel, mawazo yalikuwa mengi sana juu ya Careen na niliwaza sana je atanifikiriaje kwa huko alipo?? Si itakua nimejishusha vyeo vyangu, na thamani yangu imepungua zaidi, lakini jambo lililozidi kunivutia juu ya Careen ni jinsi alivyoweza kulimaliza swala kimya kimya, naamini angekuwa mwengine basi ningeaibika.).
.
Na hivyo ndivyo siku yangu ya tatu ilivyokua tangu niwe karibu nae.

Siku iliyofata kipindi kilikua saa sita, niliwahi mapema tu majira ya saa 4.
Macho yangu yalikuwa yakiangaza huku na huko ili kama naweza kumuona mtoto mzuri Careen.
Hamu yangu kubwa ilikua lazima nipate namba yake leo, na lazima nimchimbe kiundani mpaka nijue kama ana boyfriend au laanh.
.
Nilimuona kwa mbali akiwa ameketi peke yake maeneo ya garden, nikamuita muuza Ice cream, nikanunua mbili za kopo na kumfata mahali alipo.
Pindi naelekea nikapishana na waNigeria wawili wakinong'onezana kuhus uzuri wa Careen.
Nikaona hapa nikichelewa kumtongoza huyu msichana basi wengine wataniwahi.
.
Nikamfikia alipo na kutoa salamu.
Mimi: Hi, (Nilitoa salamu huku namkabidhi ice cream).
Careen: Hi, wow thank you. How are you???
.
Mimi: I'm good, yani niko poa mpaka najionea wivu...!!! Sijui wewe??.
Careen: Hahah una maneno wewe, niko poa sana na ashukuriwe Mungu kwahilo. Uumh asante sana kwa ice cream, hata hivyo nilikumiss sana.
.
Alinigusa sana, maana ni mara chache sana nimepokea neno "Asante", ex wangu alikua hana tabia hiyo... hata ukimpa laki moja ya kwenda kununua nguo basi lazima aulize "Na hela ya nauli je?".
.
Kwa Careen hili nililiona jambo la kipekee sana, nikatabasamu na kumjibu "Hata mimi nilikumiss sana mpaka nikapatwa na homa mpaka nikajihisi nitaambiwa R.I.P sasa hivi".
.
Akacheka sana, akajibu "Halafu nisingekuja kwenye msiba wako "
.
Mimi: "hahaha ningekununia".
.
Careen alicheka sana.
Nikaona huu ndo wakati wa kuomba namba.
.
Mimi: Halafu nimekumbuka, jana nilitumiwa soft copy ya notes, nikutumie kama unaitaka???
.
Careen: Ndo nilikua nataka nikamfate Cr anitumie, nitumie kwenye email basi.
.
Mimi: Anh email mzunguko wote huo, nitajie namba tu nikutumie WhatsApp chap tu. (Nikazungumza kwa msisitizo ili akubali, shida yangu ilikua namba tu, na nikajua hapa kivyovyote hawezi kuchomoka kwenye huu mtego).
.
Careen akanitazama usoni ikiwa kama mtu anayejaribu kusoma kitu kwenye uso wangu.
Kisha kwa utaratibu akanijibu ''Nitumie tu kwenye email sababu nitataka niifungue baadae kwenye laptop."
.
Nikashusha pumzi nzito baada ya kuona mtego wangu umefeli.
Nikajisemea kimoyoni "Dah huyu smart sana kichwani, hakamatiki kiurahisi, sasa hiyo email yake ina faida gani kwangu".
Nikachukua email yake kishingo upande na kumtumia notes.
.
Nikaona sio mbaya, anaonekana mwenye misimamo, ngoja nianze kumchimba nijue kama ana boyfriend ili nijue kama niko vitani, au ndio basi tena, au yuko single ili nislide moja kwa moja kabla wajanja hawajaniwahi.
.
Mimi: Leo nilikaa asubuhi nikawaza sana, hivi inakuaje mtu unampenda na yeye anaonyesha anakupenda pia, lakini mwisho anakusaliti?! Au anakuacha kabisa.
.
Akanitazama sana, akionekana mwenye kutafakari.
Akanijibu "Kaka Chris, moyo wa mtu kichaka na kamwe huwezi kujua lile alilolificha moyoni mwake juu yako."
.
Akanyamaza kidogo, akaendelea "Mwingine anakua anajifanya anakupenda sababu kuna kitu anakitaka, akishakipata tu basi anaanza kuonyesha makucha yake."
.
Akanyamaza tena, nilielewa sana points zake, ila shida yangu haikuwa kusikia maneno yake ya busara, shida yangu nikujua kama ana boyfriend au hana.
.
Nikaingiza neno "Kweli kabisa usemayo, moyo wa mtu kichaka. Ila rafiki yangu wewe unajitambua sana, natumaini boyfriend wako hana tabia mbovu mbovu, tena ulivyo mzuri hivyo, kwako kafika."
.
Careen akatabasamu sana, kisha akatoa jibu lililoniacha mdomo wazi, akajibu "Hata kama mimi mzuri, binadamu hawatabiriki, siwezi jiaminisha kwa asilimia zote kwa yeyote yule.".
.
Jibu lilikua zito sana kwangu, yani leo namba nikose, na ukweli kuwa ana boyfriend au hana nao nikose.
Nikamuona Careen ni mwanamke mwerevu sana, ana matumizi mazuri ya ubongo na kinywa chake.
.
Uvumilivu ukanishinda, ikabidi nitupe swali kavu kavu, nikauliza "Kwani una boyfriend au huna??! ".
.
Alinigeukia na kunitazama, nikapata shauku ya kutaka kusikia atakachojibu.
Akatabasamu, akanishika mkono na kuniambia "Usijali, bado mapema sana,kuwa na subira utanijua tu".
.
Nikachoka kabisa kwa jibu lake, nikajiuliza huyu ni mwanamke wa aina gani huyu?? Mbona ananishangaza kwenye kila jambo.
Ila nilibaki na kujilaumu kwanini nimeharakisha mambo mapema hivyo.
.
Nilihisi ameanza kunistukia kuwa nina hisia juu yake, nikajisikia vibaya sana. Ikanibidi niombe kwenda toilet mara moja, nikanyanyuka na kuelekea toilet, nikakaa kwa muda wa dakika 5, pindi narejea kutoka toilet ndipo nilipoona kwa mbali jambo lililonistua sana.
.
Nilimuona kijana mmojawapo kati ya wale waNigeria wawili niliopishana nao mwanzo.
Alikuwa ameketi pale pale nilipokuwa nimeketi, na alikuwa akionekana Akizungumza na Careen kwa hisia zaidi.
.
Nilisimama kwa mshangao, mapigo ya moyo yalizidi kunienda mbio, nikawaza je ndo ananiwahi mapema kiasi hiki?? Ndo naibiwa??
Roho iliniuma zaidi baada ya kuona mNigeria anachukua simu yake na kumnyooshea Careen achukue aandike namba.
.
Nilishika kichwa nikijua kuwa tayari mbuzi kashafia kwa muuza supu.
Nilizidi kushangaa zaidi baada ya kuona jambo ambalo Careen alilifanya
.

Je Careen alifanya jambo gani???!!
.
Usikose sehemu ya tatu*

Itaendelea....

Sehemu ya tatu bonyeza hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!!

Sehemu ya tatu...

#Ilipoishia: Baada ya kutoka na kwenda toilet kwa muda wa dakika 5, pindi narejea ndipo nilipomuona mmojawapo kati ya wale waNigeria wawili akiwa ameketi karibu na Careen, alionekana akizungumza kwa hisia sana, kisha akachukua simu yake na kumpa Careen aandike namba.

Moyo ulizidi kuniuma sana baada ya kumuona Careen akiipokea ile simu na kuandika kitu kama namba hivi.
************
#Inaendelea
Nafsi yangu ilijutia sana kwanini nilitoka na kwenda toilet, kwanini nisingebaki pale pale angalau mNigeria angeogopa kuja.

Nilibaki nimesimama kwa muda mrefu sana, nikiwa na mawazo mengi sana, nilijua ndo tayari tena Careen kasharubuniwa na mwanaume mwingine, nilijutia sana kuchelewa chelewa kwangu, nilijutia sana kupenda kutumia kwangu mzunguko mrefu hadi kwenye uombaji wa namba.

Kwambali nilimuona mNigeria akiaga na kuondoka, ndipo nami nikaanza kuchukua hatua kuelekea alipo Careen.
Kwavile nilikua kwenye huzuni kubwa, na wala sikutaka anigundue kuwa nimekasirika, basi ikabidi nifike tu na kumuomba niondoke nielekee darasani kwa kisingizio kuwa nataka nisome kwanza kabla kipindi hakijaanza.

Careen: Ndo unataka kuniacha nibaki peke yangu?! Nisubiri twende wote.(Aliongea kwa msisitizo huku akinyanyuka)

Mimi: Anh no, wee baki tu ule upepo.(Niliongea huku nikianza kukanyaga hatua kuelekea mbele).

Careen: Chris nisubiri bwana.(Akanyanyua vitu vyake na kuanza kunifata nyuma).

Ikanibidi niongozane nae tu hivyo hivyo kishingo upande.
Kiukweli sikupenda kutembea nae, wala kuwa nae karibu kwa siku hiyo.
Nilikua nimetingwa na mawazo mengi kichwani hasa nikiwaza je itakua ametoa namba kweli, au amempa namba ya uongo, na kilichoniumiza zaidi, kwanini ampe namba yule mNigeria ambaye hata hawajuani lakini mimi ninaye juana nae ameninyima.

Nikakumbuka maneno ya dada yangu Rachel, aliwahi niambia mwanamke anaweza kupa namba hata ya uongo ilimradi usiendelee kumsumbua.
Nikajipa moyo, nikatabasamu na kuendelea na safari mpaka darasani ambapo nilikaa nae karibu, nilionekana nasoma notes kwenye laptop, lakini kiukweli sikuwa nasoma chochote, nilikua mbali kimawazo.

Saa sita ilipofika tukaingia kwenye kipindi, kilipoisha nilinyanyua bag langu na kutoka nje, siku hiyo sikutaka kabisa kuzungumza mengi, nilisahau hadi kuagana na Careen.

Mara nikasikia Careen ananiita, "Chris, chris".
Nikaitikia "Yes, " na ikabidi nizuge ili asigundue kuwa nilikuwa naondoka bila kuaga.
Akaanza kuniwahi, mpaka aliponifikia.
.
Careen: Utakua free kwa kesho???
Mimi: Hapana, nitatoka asubuhi halafu nirudi jioni kwaajili ya kuparty, siunajua kesho kutakua na bhash.(nilimdanganya nitakua busy ili nipate nafasi ya kua nae mbali kwa kesho).
.
Careen: Onh basi, nilitaka twende wote sehemu kesho mchana.
.
Niliposikia neno "Twende wote sehemu " nilistuka sana, ikabidi nibadilishe mada "Anh usijali tunaweza kwenda tu, mahali kwenyewe nilipotaka kwenda sio muhimu sana ".
.
Careen: Afadhali, nilikua nawaza ningeenda kuwa mnyonge.
.
Mimi: Okay usijali nipo kwaajili yako, niambie sehemu gani sasa mamie?!

Careen: Kuna mNigeria nilikua naongea nae leo mchana, kanialika kwenye party yake ya birthday.

Sasa akili ikaanza kunijia vizuri kichwani, nikapata picha kuumbe Careen hakutoa namba kwa gia ya kutongozwa, kumbe alitumia gia ya party.
Nikapata amani ya moyo, nikaanza kujiona mjinga kwa kukasirika vitu vidogo sana, japo nilijua wazi kuwa mNigeria alikua na nia yake tofauti na party.
"Lakini na misimamo yake yote hii, anaweza kukubali party kwa mtu asiyemjua?" Nilijiuliza swali kimoyo moyo.

Mimi: Kwani unamjua yule mNigeria??
Careen: Yeah namjua japo sio sana, anaitwa Peter, nilikutana nae siku niliyokuja kufanya usajili, ndiye aliyekuwa akinipa maelekezo.
.
Mimi: Anhaa kumbe, maana nikashangaa unawezaje kukubali kwenda sehemu kwa mtu usiyemjua.
.
Careen: Hata hivyo nilitaka kukataa, ila kwavile alinionyesha ukarimu kwenye siku yangu ya kwanza, ndio maana imenibidi nikubali, hata hivyo ndomana nataka niende na wewe.
.
Mimi: Okay nimekubali, ila sasa tutawasiliana vipi?? Na maeneo gani? Muda gani?

Akanitazama na kuniomba simu, nikampa na akaandika namba yake.
Moyoni nilikua najisemea 'Leo umeshaingia kwenye 18 zangu".
Akanirudishia simu na kuniambia party itafanyika nyumbani kwa kina Peter, maeneo ya Kunduchi Beach, majira ya saa 8 mchana.

Tukaagana na niliondoka na furaha sana baada ya kuwa nimepata namba ya Careen, na siku yangu ya 4 tangu tujuane ikawa imeisha hivyo.
.
Siku iliyofata kama kawaida, nilivunja kabati, nikatupia kuliko siku zote, nikahakikisha nanukia safi.
Safari ikaanza kutoka Gongo La Mboto mpaka Simu 2000, ambapo ndipo tulipopanga kukutana na Careen.
Tulifurahi sana kukutana tena, alikua anang'ara sana, kapendeza, nikamsifia mpaka nikahisi sasa nitasifia mwisho nitukane.

Tukachukua tax mpaka nyumbani kwa kina Peter.
Tulikaribishwa vizuri sana, utambulisho ndio ulifata.
Careen alinitambulisha kwa Peter, na rafiki yake Peter ambaye anaitwa Abdulrahman Okechi.
Naye Peter alitutambulisha mimi na Careen kwa rafiki yake.

Tulipewa vinywaji, na party ikawa ikiendelea.
Lakini kuna nyakati nilihisi kuna kitu hakiko sawa, hawakuonyesha kuwa karibu nami, ilikuwa kama nimetengwa hivi.
Rafiki yake na Peter alikuwa karibu sana na Careen, kiasi cha kuanza kunitia wasiwasi.
Niliona aibu sana, party ilikua na watu wengi, lakini kila mmoja alikua karibu na anayefahamiana nae, ni mimi tu ndiye niliyekua mkiwa.
.
Nilitamani party iishe ili tuondoke tu maana nilihisi moyo kupasuka.
Party ilivyoisha tukajiandaa kuondoka, lakini Careen aliniambia subiri tutarudishwa na magari yao.
Nikashangaa sana.
.
Lakini lililo nishangaza zaidi ni pale Peter na Abdulrahman walipokuja na kuniambia mimi ninae enda Gongo La Mboto nipande gari la Abdulrahman.
Na Careen atapanda gari la Peter.
.
Nilistuka, nikaona mbona picha ninayochezewa ni ya kihindi...
Nikauliza "Kwani Careen nae si tunaelekea njia moja, si anakaa Tabata??"
.
Careen akajibu "Yeah ila siendi nyumbani sasa hivi, kuna mahali naelekea na Peter kakubali kunipa lift".
.
Niliumia sana, nilijua hapa nadanganywa, nikajiuliza au ndo vile vinywaji tulivyokunywa kwenye party ndo Careen anaenda kuvilipa.
Nilijilaumu sana kwanini najiita mwanaume wakati sina hata uwezo wa kununua baiskeli, niliamini ningekuwa na gari langu, haya yote yasingetokea.
.
Nikapanda gari la Abdulrahman japo sikupenda, na Careen aliondoka na Peter, nasi safari ikaanza.
.
Baada ya kimya cha muda mrefu, tulipokuwa tunakaribia maeneo ya Mwenge, Abdulrahman akaanza story.
.
Abdul: Is she your bestfriend?!(Yule ni rafiki yako mkubwa??)
.
Mimi: Yes (Nikamjibu kwa kifupi ili tusisumbuane).
.
Akaendelea, "She is so damn beautiful (Ni mrembo sana)".
Nikamjibu kwa kiswahili "Sifa na utukufu kwake muumbaji ".
.
Nilidhani hatonielewa, kumbe alielewa na akanijibu kwa kingereza maneno yaliyo maanisha "Ni mzuri sana, Peter anampenda sana Careen, na kwajinsi navyomjua Peter, najua hawezi muacha kizembe leo ".
.
Mimi: What?? (Nilistushwa sana na kauli hiyo) nikamtazama Abdulrahman kwa mshangao.
Nikauliza, "Kwani wameenda wapi?? "
.
Abdul: Bahari Beach.

Mawazo ya ghafla yakanijia kichwani, itakuwaje mzigo ukiliwa leo?? Sindo mwanzo mimi nitaonekana boya tu??, noo, nishuke niwahi Bahari Beach?? Au nivumilie tu??.

Ghafla nikasikia Abdul amezungumza tena kauli tata kwa kingereza, iliyokuwa ikimaanisha "Na jamaa yuko vizuri sana kwenye kushawishi wanawake, huwa hawamkatai".

Hapo ndipo nilipopatwa na hasira za ghafla, jasho lilianza kunitiririka, na kumwambia Abdul "Naomba unishushe hapo Mwenge".

Abdul: Why??(Kwanini)
Mimi: Just drop me there(We nishushe tu hapo) kuna mtu nataka kuonana nae.
.
Akanishangaa sana, ila akasimamisha gari na kuniacha kisha akakanyaga mafuta na kuondoka.

Sikujali Abdul atanionaje, nilikua na wazo moja tu kichwani.
Kupanda gari na kuelekea Bahari Beach.


Je Chris ataelekea Bahari Beach??? Au ataghairi?? Na kitatokea nini huko mbele ya Peter na Careen???

******-Usikose sehemu ya 4*****
#Itaendelea...

Sehemu ya nne soma hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!!

Sehemu ya nne...

#Ilipoishia: Baada ya Abdulrahman kuniambia kuwa Careen na Peter wameelekea Bahari Beach, nilipatwa na hofu ya ghafla, hasa kwa kuzingatia nipo kwenye vita na Peter, ya kugombania kumpata Careen.

Nikamuomba anishushe, akakubali na kunishusha haraka.
Nilivyoshushwa, wala sikuwa na wazo lingine tena zaidi ya wazo la kupanda gari na kuelekea Bahari Beach.
Niliwahi haraka na kupanda daladala, lakini akili ikanijia kuwa daladala zinasimama simama sana hivyo zitanichelewesha, nikashuka haraka kabla halijaondoka, ikanibidi nitafute tax haraka sana.

#Inaendelea:
Mimi: Kanyaga mafuta, tembea fasta bro.

Dereva: Unakwenda wapi??
Mimi: Huko huko mbele bwana aanh.
Dereva: Mbele kwenye zipu au??
Mimi: Acha utani, niwahishe Bahari Beach.

Akakanyaga mafuta kwa speed kali, lakin nilihisi kama anatembea taratibu.
Ghafla simu iliingia message, niliiwahi sana nilidhani ni Careen, kuitazama nikakuta missed call mbili na message moja, zote zimetoka kwa classmate wangu, Hasheem.
Alikua akiulizia niko wapi na party inakaribia kuanza chuo, nikaona ananipotezea muda, nikachukua simu nakuitia mfukoni.

Kichwa changu kilikuwa kizito sana, kilijawa na mawazo mengi sana juu ya Careen, kuna muda nilijiona mjinga sana, kwanini nafanya yote haya?? Hata huko nakoenda nitafaidika nini hasa?

Pindi gari lilinakaribia maeneo ya Mbezi Beach Tangi bovu, nilikatishwa kwenye mawazo baada ya simu yangu kuita.
Niliidharau sikuipokea, "Hasheem huyu anapiga piga kila mara hadi kero sasa ''- Nilijisemea kwa nguvu bila kuitazama simu kujua anapiga nani.

Simu iliita mpaka ikakata, lakini ikapigwa tena kwa mara ya pili, nikaona sasa Hasheem kazidisha fujo, nikaitoa simu mfukoni ili nifunge mtandao kwa kuweka "Airplane Mode".

Nilipoichukua na kuitazama, nilishangaa kukuta ni Careen ndiye ananipigia.
Sikuamini, nikaitazama simu mara mbili mbili mwisho nikaipokea.

Careen: Hallow.
Mimi: Hello, uko okay?

Careen: Niko poa ila umeniudhi, simu uliweka kwenye kibubu nini?? (Aliuliza huku akijichekesha).

Sikucheka wala nini, nikamjibu "Hapana, niliiweka mfukoni halafu ilikua na sauti ndogo. Bado uko na Peter?? " - (Ilibidi niulize kabisa adui yangu yupo au laanh.)

Careen: Hapana aliniacha tu mahali na kila mtu akaendelea na safari yake.

nikastuka kidogo, nilitamani kuuliza "Mbona Abdulrahman alisema mpo wote Bahari Beach ", ila ikabidi ninyamaze ili nipewe uhakika zaidi.
Nikauliza "Kwani uko wapi sasa hivi??".

Careen: Nipo Kinondoni sasa hivi, nitalala huku huku kwa dada yangu.
Hata hivyo nimekupigia nijue umefikia wapi??

"Kheee " nilitoa mshangao, nikajisemea kimoyoni "Sasa kwanini niliambiwa yuko Bahari Beach?"

Sikujibu swali la Careen, nikakata simu kwanza, na kumwambia dereva tax asimamishe gari "Oya broo, hebu simamisha mbele hapo kwenye zipu, tangi bovu " (Nikatumia utani wake).
Akaniuliza "Vipi mbona umekatisha safari? "

Nikamwambia "Anh nayemfata hayupo huko "
Akajibu "Basi niongeze mkwanja nikurudishe mpaka Simu 2000".
Nikamcheck, nikamjibu "Acha ujinga wewe, daladala nauli bei chee tu."

Akasimamisha gari, nikashuka na kumlipa hela yake.
Nikaelekea moja kwa moja mpaka kwenye kituo cha kusubiria daladala.

Nilijicheka sana, nikajiona boya, lakini nilijiuliza sana kwanini Abdulrahman alinidanganya, nikapata jibu kuwa huenda wanahisi kitu kati yangu na Careen, hivyo wanajaribu kunipima hisia, au kuniharibu kisaikolojia.

Kutokana na tabu ya usafiri, nilifika Gongo La Mboto majira ya saa 4 usiku, kwavile nilichoka sana, nilienda hostel tu kulala na wala sikuwa na hamu ya kwenda kwenye bhash chuoni.

Weekend niliitumia vizuri sana kuchat na Careen, na ilizidi kunoga zaidi na zaidi, huku nikionyesha umahiri wangu kwenye kujali, kuheshimu , kumthaminisha na kumchekesha pia.
Alifurahia sana kuchat na mimi, na kuna nyakati alinipigia tukazungumza sana kwa muda mrefu mazungumzo ya maisha na mambo mbalimbali.

Lakini mwisho tulijikuta tumedondokea kwenye mazungumzo ya mahusiano.
Careen: Unajua kaka Chris tangu nikujue, unanifurahisha jambo moja.

Mimi: Jambo gani hilo mamie??

Careen: Unanijali sana, unanipa sana kipaumbele, na hata kunithamini pia. Kiukweli najisikia furaha sana kuwa na rafiki kama wewe.

Mimi: Asante sana, ni jukumu langu kuhakikisha rafiki yangu anajisikia yupo na rafiki anayejali uwepo wake.

Careen: Nashukuru sana kwa hilo, Mungu akuweke miaka mingi. Huwa unanikumbusha mbali sana.

Mimi: Mbali wapi tena mamie?

Careen akakaa kimya kidogo, kisha akaendelea maongezi "Leo ngoja nikupe siri moja maana umeshakua rafiki yangu, na ni zaidi ya rafiki, umekuwa kama ndugu kwangu.
Kaka Chris unanikumbushaga mwanaume ambaye sikuwahi kumpenda hapo zamani, alikua anaitwa Khalfan."

Akanyamaza kidogo, nikazidi kupata shauku ya kutaka kujua zaidi, maana nilijua nikijua madhaifu ya Careen basi lazima nitafanikiwa kumpata kiurahisi.

Akaendelea "Huyo kaka tulianza uchumba kipindi hicho niko form two, alinipenda sana ila tatizo mimi sikumpenda, nilimkubali tu sababu enzi hizo kundi langu wote walikua na maboyfriend kasoro mimi, halafu Khalfan alikua na vijisent kidogo "

Nikaguna "mmmh ", akaendelea "Sasa kipindi hicho nilikua sijui mapenzi nini, kwahiyo zile kuonyesha kunijali, mara message, mara anipigie simu, halafu alikua na wivu.
Basi nikawa naona kero sana, mpaka kuna muda nilikua namkatia simu, au naizima tu kwa makusudi "- (akazungumza huku anajichekesha).
.
Nikamuuliza "Kwahiyo bado mpo pamoja??? "

Akajibu "Hapana, tuliachana form 4. Aliniheshimu sana, na wala hatukuwahi kusex."

Nikamjibu "Duh kweli huyo alikupenda "
Akaniambia "Kweli kabisa, na najutia kumpoteza.
Sababu akili ilikuja kunijia pindi nilipokuwa form six, ndipo nilimpata huyu boyfriend wangu wa sasa "
Nikastuka sana kusikia neno "boyfriend wake wa sasa "

Akaendelea "Nilikuja kugundua mapenzi ni nini baada ya kumpenda huyu boyfriend wangu wa sasa, yani wala hanijali wala kunithamini, yani yeye kila kitu ni ubabe na kuniforce tu, najitajidi sana kujitunza kwaajili yake lakini yeye hajali, na ananisaliti mara kwa mara.
Nayatamani sana maisha yangu ya zamani, natamani ningekua na Khalfan"- (Alizungumza kwa hisia sana na kuonyesha akimaanisha kile anachosema)

Niliyapokea maneno hayo kwa masikitiko makubwa sana, nikamtia moyo, pia nikajaribu kumpa ushauri wa kinafki ili aone kama namsapoti.
Akanishukuru sana kwa ushauri wangu, na kumtia moyo, na mwisho akanitakia usiku mwema.

Jumatatu iliyofata niliamka nikiwa mwenye furaha sana, huku nikiwa na matumaini mapya ya kumpata Careen hasa ukizingatia nimeshajua madhaifu yake yako wapi, nini anakosa kwa boyfriend wake.

Nilimtumia message, akaniambia yuko anapata kifungua kinywa kwenye mgahawa wa kifahari wa Legacy, uliopo ndani ya chuo.
Nikawahi mpaka mahali hapo, lakini sikufurahishwa na nilichokiona, nilimkuta Careen akiwa anapata breakfast pamoja na Peter na Abdulrahman.

Nikasonya kwa mbali.
Nikawasogerea, nikatoa salamu, kisha nikaagiza chakula na kujumuika nao.
Story zilinoga, tukamaliza kula, tukanyanyuka na sote tukaelekea mahali pakulipia bills.
Kimbembe kilianza wakati wakulipa bill.

Muhudumu: Jumla Tsh.9500.
Nikamtazama muhudumu, nikajisemea kimoyo moyo "Leo lazima niwavimbie hawa watu ".
nikaingiza mkono mfukoni na kutoa noti ya Tsh elfu 10 na kumpa muhudumu, nikamwambia "kata yote".
Peter kwa kutaka sifa nae, akasema "Bro, don't worry, i'll pay(Kaka usijali, nitalipa mimi)".

Nikamtazama Peter, nikamsisitizia muhudumu "Kata yote humo humo tu "
Abdulrahman akanitazama, aliniona pindi naichungulia pesa mfukoni, alijua wazi sina hela nyingine zaidi ya hiyo elfu 10 niliyotoa.

Akamtazama muhudumu, na kumwambia kwa kingereza maneno yaliyo maanisha "Utaniletea juice ya elfu 3 ya Azam Mango kwaajili ya Careen, na maji ya kilimanjaro lita moja kwaajili yangu, atalipa Chris."

Nikashangaa sana kauli alizotamka Abdulrahman, nilihisi huyu jamaa ana nia ya kuniua kwa presha.
Nilianza kuvurugwa akili, nikajihisi kama mwenye bahati mbaya siku zote, kila siku niaibike mimi tu.

Careen aliustukia mchezo na kutamka maneno yaliyonipa nguvu, akasema "No, sihitaji juice, nitachukua maji tu, na Peter utalipia bill yote."
Akageuka na kuelekea kwenye fridge la kuchukulia maji.

Peter akatoa hela na kulipa, kipindi Abdulrahman akinisogerea karibu, akanong'ona "Hey young man, did you really follow her that day?? (Hey kijana, ulimfata kweli siku ile???).

Nikajua sasa bifu la mafahari wawili, ndipo linapoanzia.
Nikamjibu, "Its none of your damn business bro"(Haikuhusu kaka).

Akacheka kinafki, akaongeza sauti na kusema kwa kingereza maneno yaliyo maanisha "Hahah kumbe unampenda sana eenh??!! Hujaona wasichana wengine? Wewe sio wa aina yake, anahitaji mwanaume, sio mvulana kama wewe."

Nilipandwa na hasira, nikasahau niko maeneo gani, sikutazama nyuma yangu kuna nani, nikaropoka " Kwa uzuri gani hasa aliokua nao, nimpende yeye nani?? Wewe kula kulala ndio unajiita "Mwanaume ", unachekesha sana, sina shida na huyo kinyago wenu, Careen Careen, kwanza sio type yangu. Kimwanamke kimechongoka kama spoku, mxieeeeew.
Nikasonya ".

Wote wakabaki wananitazama, sikuelewa kwanini hawakujibu walibaki wameduwaa, niligeuza macho pembeni nikaona jinsi wengine pia wanaokula kwenye meza wakinitazama.
Nilijistukia, lakini nilishangaa zaidi kuona Peter na Abdulrahman wakiwa wameduwaa kuelekea upande mmoja, ikanibidi nigeuze macho yangu kutazama wanachotazama.

Uso kwa uso, macho yangu yalikutana na ya Careen aliyekuwa amebaki ananishangaa huku akilengwa na machozi
.

Je nini kitafuata??! Careen atamchukuliaje Chris???.

******Usikose sehemu ya 5*****
#Itaendelea...

Sehemu ya 5 soma hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)..!!!

Sehemu ya tano...

#Ilipoishia : Kutokana na hasira ilivyonipanda nilijikuta namtolea maneno makali Abdulrahman juu ya Careen.
Wote walibaki wakinitazama kwa mshangao mkubwa, hata watu waliopembeni pia.
Lakini Abdulrahman na Peter wao walionekana kuangalia kuelekea upande mmoja, nyuma yangu, ndipo nilipopata wazo la kugeuka kutazama wanachoshangaa.

Macho yangu yalikutana uso kwa uso na Careen aliyekuwa ananishangaa, huku akilengwa na machozi.

#Inaendelea:
Moyo ulistuka sana, nilihisi mwili kama umemwagiwa maji ya baridi, nikajiuliza kimoyomoyo "Nimefanya nini mimi leo ".

Careen alikuwa ameganda kama sanamu akinitazama, macho yake yalikuwa yakimlenga lenga machozi, alionekana kuguswa na kuumizwa juu ya yale maneno machafu niliyo yatoa hasa ukizingatia mbele za watu.

Akashindwa kuvumilia, akaanza kulia huku akianza kutembea kwa haraka sana kuelekea nje ya mgahawa.

Akili ya fasta ikanituma nimkimbilie nimuombe msamaha hapo hapo, nikamuwahi kwa mbele, alikua na hasira sana, akanisukumiza pembeni na kuongeza mwendo kama anakimbia vile.

Nikanyanyuka na kumkimbilia tena.
"Careen, Careen, pls nisamehe, nimeropoka hasira tu"- Nilizungumza huku nimemkamatia mkono wake wa kushoto, akautikisa kwa nguvu na kuongea kwa hasira "Niache, niache kabisa, "- Alizungumza kwa hasira huku analia.

Lakini sikumuachia mkono wake, ikabidi atumie nguvu kuniachisha mkono, bado nikawa nimeng'ang'ania huku naomba msamaha.
Ghafla akaja Peter na akaunyofoa mkono wangu mikononi mwa Careen na Careen akaendelea na safari yake anakokujua mwenyewe.

Nilibaki nimeduwaa nisijue nini cha kufanya, moyo uliniuma sana.
Kugeuka pembeni yangu alikua amesimama Peter na Abdulrahman, kwa mbali nyuma yangu kulikua na wanafunzi kadhaa waliokuwa wakishuhudia picha ya kihindi niliyokua naicheza.

Machozi yalinitoka, ndio mara yangu ya kwanza kuona mwanaume anamwaga machozi.
Nilihisi kama mtu amenigusa bega langu la kushoto, nikageuza shingo ili kumtazama ni nani, nikakutana na uso wa Abdulrahman.

Akazungumza kwa kejeli maneno ya kingereza yenye maana ya "Kijana, huu mchezo hauhitaji hasira".
Kisha akacheka kwa dharau, Peter nae alikuwa akinitazama kwa dharau huku akijichekesha.

Nilijiona mjinga sana, nilitamani kuwapiga hata ngumi za uso, ila tatizo sheria za chuo zingeniandama, nikavumilia hivyo hivyo japo nafsi iliuma sana.
Nilirudi mgahawani na kuchukua begi langu, kisha kuondoka huku watu wakinitazama, wengine wakinicheka sana, na kina Peter walionyesha kufurahi baada ya mpango wao kutimia wa kunitoa kwenye reli ya Careen.

Nilizunguka chuo kizima, kila kona, kila darasa, kila faculty, lakini sikumuona Careen.
Nikajipa moyo labda atakuja darasani kwenye kipindi, lakini nako hakuonekana.
Nilikaa darasani kwenye kipindi, akili yangu haikuwa kwenye kile kinachofundishwa, kipindi kikaisha na sikutaka kubaki chuo, nikarudi hostel kupumzika.
Nilimpigia simu, hakupokea, sms hakujibu, Whatsapp aliniblock.
Na siku yangu iliisha vibaya kama hivyo.

Siku tatu mfululizo mambo yalikuwa tofauti kati yangu na Careen, hata darasani hatukukaa pamoja tena.
Hatukuwa na story wala salamu, alikuwa akinipita kama hanijui.
Alikua akitoka kwenye kipindi, basi lazima utamkuta yuko na Peter na Abdulrahman.

Nilikua naumia sana, nilimtumia message nyingi sana za kumuelewesha, na hata za kumuomba msamaha.
Kuna nyakati nilikua najaribu kumuongelesha ana kwa ana tukikutana, lakin alikua kama hanisikii.

Siku ya nne tangu aninunie, niliamua kushinda hostel tu pamoja na classmates wangu, Hasheem na Ramadhan, tukawa tukipiga story mbili tatu.
Hasheem: Kwani Chris vipi siku hizi na yule manzi? Mbona naona mnakwepana sana, au ndio umemtongoza kakuchomolea?!

Mimi: Anh hamna, nilimkorofisha kidogo, basi kanuna kabisa hataki hata tuzungumze.

Ramadhan: Umemfanyaje kwani?? Maana mpaka kakununia, basi ujue umemkera sana.

Ikabidi niwaelezee vizuri toka mwanzo mpaka mwisho.
Wote walionekana wakinisikiliza kwa umakini zaidi, na pindi nilipomaliza, Hasheem alinipa pole sana lakini akaniambia "Wewe kidume bwana huna haja ya kumnyenyekea mwanamke, mpige chini bwana, kwanza hana faida kwako ".

Lakini Ramadhan alizungumza maneno yaliyo niingia.

Ramadhan: Bro hilo sio tatizo dogo, ni tatizo kubwa sana.
Wanawake wameumbwa na aibu sana, hawajiamini sana, kwahiyo anapopata maneno yenye kumsifu huwa anapata uwezo wa kujiamini, anaua ile aibu yake na hujikuta anampenda sana yule mwenye tabia ya kumsifu, sababu ndiye anayempa nguvu".

Nikakumbuka kweli Careen aliwahi niambia nifungukia kiasi gani ananikubali kwa kumjali na kumthaminisha kwangu, na vile ninavyomfanya amkumbuke boyfriend wake wa zamani.

Nikarudisha masikio yangu tena kumsikiliza Ramadhan, akaendelea kusema "Anapopitia mateso ya kihisia kwa kumpenda boyfriend ambaye hamjali, hamthamini, anamshusha hadhi, haonyeshi kumpenda, anatoa kauli za kejeli, basi hata kama yeye ni mzuri kiasi gani, hujikuta anaanza kujichukia, anajiona labda ana nuksi, labda mbaya, anakosa kujiamini, anakosa kujithamini.

Sasa anapokuja mwanaume mwingine hata kama ni rafiki, lakin anaonyesha kumjali, kumuheshimu, na kumthamini, basi hujikuta anapata mwanga mpya wa maisha yake.
Kosa baya ambalo humrudisha kwenye maumivu, ni pale huyu mwanaume anapokuja kutoa kauli za kejeli, basi hujikuta anarudia kuyakumbuka machungu yale yale ya mwanzo anayoyapata kwa boyfriend wake ".

Alinyamazia hapo, maneno yaliniingia kisawa sawa, mwanzo niliona kama Careen amenuna sababu ya kikosa kidogo sana, lakini sasa nikawa nimepata mwangaza wa ukubwa wa kosa langu.

Nikamuuliza "Dah man umenigusa sana, ila sasa unanishauri nifanyaje ili anielewe"

Akaguna kidogo, akakaa kimya kwa dakika kadhaa, kisha akazungumza "Kwasasa hapokei simu zako, hajibu sms zako, hataki kuongea na wewe ana kwa ana, anahisi aibu kuzungumza nae, anapata hasira kuonana na mtu kama wewe uliyeongeza donda lake lililosababishwa na boyfriend wake.".

Akatafakari tena kisha akaendelea "Kuna njia moja tu unayoweza mshawishi, nayo ni SMS. Sababu simu ukipiga hatojibu, ana kwa ana unaweza hata tukanwa au ukamzidisha hasira, lakini sms atake asitake kwa kiranga chake lazima atasoma tu.".

"Kaa chini tulia, andika sms moja nzito sana, weka hisia zako humo jinsi gani unauthamini uwepo wake, weka machungu yako humo jinsi gani unajutia kosa lako, na uweke ukweli halisi kwanini uliropoka yale maneno, sababu Careen haelewi bifu lililoko kati yako na kina Peter, muweke wazi vita inayoendelea, lakini chunga usionyeshe hisia zako kuwa unamtaka kimapenzi sababu kwasasa ana machungu ya boyfriend wake, lazima utamuongeza hasira."- Akaishia hapo.

Nilishusha pumzi nzito sana, nilijihisi kama niliyetua mzigo mzito kifuani kwangu, hakika sikujutia kutoa yaliyonisibu kwa hawa watu wawili, japo Hasheem alitoa ushauri mbaya, lakini nilipata Ramadhan aliyetoa ushauri wenye kunivua matatizo yangu.

Niliwashukuru sana, na kuamua kukaa chini kiutulivu na kuandika message iliyowakilisha machungu yangu na kumtumia Careen.
Ilikua ni message ndefu sana iliyojaa kila kitu alichonishauri Ramadhan.

Baada ya kama dakika 26 hivi nilistukia simu yangu inaita, kutazama mpigaji alikuwa ni Careen, niliruka ruka juu kwa furaha kama chizi nusura nivunje Laptop ya Hasheem.
Wote wakabaki wananishangaa, lakini ghafla nilipoa, nikaanza kujipa maswali ya kijinga kichwani kuwa itakuwaje endapo Careen ananipigia ili anichambe, lakini Ramadhan akanipa moyo na kusema "Pokea tu, jiandae kwa lolote utakaloambiwa, na kama amepanga kukutusi basi asingehangaika kukupigia"

Kipindi napokea ushauri huo, nikastuka simu tayari imeshakata, lakin baada ya sekunde kadhaa, akapiga tena na sasa nilikua tayari kumsikiliza.

Tulisalimiana, lakini alikuwa akizungumza kama mtu mwenye kulia, aliniomba msamaha kwa kuninunia bila kujua sababu, lakini alinilaumu sana kwanini sikumuweka wazi mapema kuhusu bifu kati yangu na kina Peter.

Akaniambia kuwa hawezi kuwa na marafiki ambao wao kwa wao hawaelewani, hivyo kesho majira ya saa 10 jioni tukutane Mbalamwezi Beach Resorts, mimi, yeye, Peter na Abdulrahman, ili tuweze kuweka upatano kati yetu.
Nikakubali alilosema, mwisho na kuahidi kufika maeneo hayo mapema.

Kesho yake kama kawaida nilivunja kabati na kuwahi Mbalamwezi Beach, nilipofika niliwasubiri kama nusu saa kisha nilianza kuona Careen akija, baadae Peter na Abdulrahman wakija pamoja.

Tulikaa mahali tulivu tukipata vinywaji huku tukiyazungumza, tukayajadili sana mwisho tukafikia maelewano, tukaanza urafiki hapo hapo na Careen aliamuru tupeane na namba za simu ili tuwe tunachat, na bifu likaisha japo niliamini moyoni mwa kina Peter na kwangu bifu lilikuwa bado lipo.

Wakati wa kuondoka, tulipewa lift kwenye gari walilokuja nalo kina Peter, mpaka buguruni, wao walikua wakielekea Mbagala kwa siku hiyo.
Tulishuka na kwenda kugombania magari ya kwenda Gongo La Mboto.
Lakini cha ajabu Careen alinipa simu yake na mkoba nimshikie sababu anaogopa kuibiwa pindi tukitaka kugombania gari.
Nikaupokea mkoba wake, nikaushika mkononi, na simu nikaiweka mfukoni.

Daladala ikaja japo imejaa kiasi lakini wote tukaigombea mpaka tukapanda, nilisimama mbali kidogo na Careen.
Bus lilipofika njia ya panda segerea, Careen aliomba kushuka, akashuka na kuniomba mkoba wake dirishani, nikampa.
Lakini kwa bahati mbaya nilisahau kumpa simu, na kwa haraka aliyokuwa nayo Careen kwa siku hiyo, wala hakutazama kama simu ilikuwa ndani ya mkoba wake au laanh, aliondoka na huku bus letu liliendelea na safari.

Pindi nimefika hostel majira ya saa 3 usiku, nilistukia simu inaita mlio tofauti na wangu, nikapapasa na kushangaa kukuta ni simu ya Careen, ndipo nilipostuka kuwa sikumpa simu Careen.
Kutazama anayepiga ilikuwa ni namba iliyoseviwa "Mom", nikajua ni mama yake Careen anapiga, nikaogopa kupokea.
Simu ikakata, baada ya sekunde mbili ikaingia message.

Nikajaribu kuikumbuka Pattern lock ya Careen, sababu kuna siku aliwahi chora pattern mbele yangu.
Nilivyoikumbuka nikaijaribu na ikakubali.

Kuisoma message ilikuwa ni kutoka kwa "Mom", ilisema "Hi Chris, nimeshindwa kukutafuta kwenye namba yako sababu sijaikariri na iko humo kwenye simu. Najua unaijua Pattern yangu na message hii itakua umeisoma. Please, naomba uizime simu, ni kheri boyfriend wangu aikute simu haipatikani kuliko ikiwa haipokelewi. Na pls usipokee simu ya mtu yeyote ".

Nilimuelewa sana alichomaanisha, nikamjibu "Sawa usijali "
Kisha nikashika kitufe na kutaka kuizima simu yake.
Lakini ghafla wazo likanijia kichwani, kwanini nisisome kwanza message wanazotumiana kati ya Careen na Peter??
Nikafunga minara kwa kuweka "Airplane Mode ", kisha nikazama inbox na kuanza kusoma message Careen na Peter.

Nilichokiona kiliniumiza sana, Peter alikua amefikia hatua nzuri sana ya kumpata Careen, huku akionekana mwenye kumjali zaidi yangu, hata kumtumia mara kwa mara pesa za matumizi.
Niliumia sana, niliona kama nilishazidiwa kete.

Lakini kilichoniumiza zaidi, ni baada ya kuona message za Peter akizungumza kuhusu mimi, kiukweli ziliniumiza sana, Peter alikua ananipondea sana, akaniharibia vya kutosha, na hata kumshauri Careen aue urafiki na mimi.
Ilinichukua masaa mawili na nusu kusoma messages zao na zilinipa hasira sana.

Nilishtushwa na muito wa simu yangu, kuitazama alikua ni Peter akinipigia, kwa hasira nilizonazo nikaikata.
Hakuridhika akapiga tena, sikuipokea, akarudia tena kama mara 4 na wala sikuipokea.
Mwisho akaamua kutuma message kwa kingereza, yenye maana ya "Hey Chris, Umezungumza na Careen kama amefika?? Nampigia simu yake hapatikani."

Nikajisemea kwa nguvu "Ina maana huyu mwehu hakuwa ana nia na mimi, ila ana nia ya kujua kama Careen kafika??! Anachowaza ni Careen tu? Ndiomaana ananikandia kwa manzi ili ampate yeye, sasa ngoja nimuonyeshe".

Kwa hasira nilizonazo baada ya kuchefukwa na message zake alizochat na Careen, na sasa ananiuliza kuhusu Careen.
Nikamjibu message yake kwa kingereza, nikimaanisha "Bro acha usumbufu, Careen niko nae kalala "

Inaonekana message ilimstua sana, akapiga tena mara mbili, nikakata, nikamuongeza message nyingine "Nishakwambia acha usumbufu, Careen kalala, kwangu, kifuani kwangu, kama huamini piga tena kwenye namba yake ".

Nilivyomtumia hiyo message, nikaifungua minara haraka ya simu ya Careen, baada ya sekunde kadhaa Peter alipiga simu kwenye simu ya Careen, nikaipokea na kumsikiliza Peter alivyokuwa akilalama, kwa dharau na hasira juu nikamfokea kwa nguvu "BRO acha usumbufu watu tumelala "- Nikazungumza na kukata simu hapo hapo kisha kuzima simu ya Careen na simu yangu.

Nikacheka sana, sikujali kitakuja kutokea nini, nilichojali ni kuwa leo nimemnyoosha adui yangu, na lazima afe kwa presha leo "Sambaaf mxieeew"...!!!


Je, kitatokea nini kwa Peter?? Careen atajisikiaje akija kugundua yaliyotokea??

Usikose sehemu ya 6
Itaendelea....

Sehemu ya sita soma hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!!

Sehemu ya nne...

#Ilipoishia: Baada ya Abdulrahman kuniambia kuwa Careen na Peter wameelekea Bahari Beach, nilipatwa na hofu ya ghafla, hasa kwa kuzingatia nipo kwenye vita na Peter, ya kugombania kumpata Careen.

Nikamuomba anishushe, akakubali na kunishusha haraka.
Nilivyoshushwa, wala sikuwa na wazo lingine tena zaidi ya wazo la kupanda gari na kuelekea Bahari Beach.
Niliwahi haraka na kupanda daladala, lakini akili ikanijia kuwa daladala zinasimama simama sana hivyo zitanichelewesha, nikashuka haraka kabla halijaondoka, ikanibidi nitafute tax haraka sana.

#Inaendelea:
Mimi: Kanyaga mafuta, tembea fasta bro.

Dereva: Unakwenda wapi??
Mimi: Huko huko mbele bwana aanh.
Dereva: Mbele kwenye zipu au??
Mimi: Acha utani, niwahishe Bahari Beach.

Akakanyaga mafuta kwa speed kali, lakin nilihisi kama anatembea taratibu.
Ghafla simu iliingia message, niliiwahi sana nilidhani ni Careen, kuitazama nikakuta missed call mbili na message moja, zote zimetoka kwa classmate wangu, Hasheem.
Alikua akiulizia niko wapi na party inakaribia kuanza chuo, nikaona ananipotezea muda, nikachukua simu nakuitia mfukoni.

Kichwa changu kilikuwa kizito sana, kilijawa na mawazo mengi sana juu ya Careen, kuna muda nilijiona mjinga sana, kwanini nafanya yote haya?? Hata huko nakoenda nitafaidika nini hasa?

Pindi gari lilinakaribia maeneo ya Mbezi Beach Tangi bovu, nilikatishwa kwenye mawazo baada ya simu yangu kuita.
Niliidharau sikuipokea, "Hasheem huyu anapiga piga kila mara hadi kero sasa ''- Nilijisemea kwa nguvu bila kuitazama simu kujua anapiga nani.

Simu iliita mpaka ikakata, lakini ikapigwa tena kwa mara ya pili, nikaona sasa Hasheem kazidisha fujo, nikaitoa simu mfukoni ili nifunge mtandao kwa kuweka "Airplane Mode".

Nilipoichukua na kuitazama, nilishangaa kukuta ni Careen ndiye ananipigia.
Sikuamini, nikaitazama simu mara mbili mbili mwisho nikaipokea.

Careen: Hallow.
Mimi: Hello, uko okay?

Careen: Niko poa ila umeniudhi, simu uliweka kwenye kibubu nini?? (Aliuliza huku akijichekesha).

Sikucheka wala nini, nikamjibu "Hapana, niliiweka mfukoni halafu ilikua na sauti ndogo. Bado uko na Peter?? " - (Ilibidi niulize kabisa adui yangu yupo au laanh.)

Careen: Hapana aliniacha tu mahali na kila mtu akaendelea na safari yake.

nikastuka kidogo, nilitamani kuuliza "Mbona Abdulrahman alisema mpo wote Bahari Beach ", ila ikabidi ninyamaze ili nipewe uhakika zaidi.
Nikauliza "Kwani uko wapi sasa hivi??".

Careen: Nipo Kinondoni sasa hivi, nitalala huku huku kwa dada yangu.
Hata hivyo nimekupigia nijue umefikia wapi??

"Kheee " nilitoa mshangao, nikajisemea kimoyoni "Sasa kwanini niliambiwa yuko Bahari Beach?"

Sikujibu swali la Careen, nikakata simu kwanza, na kumwambia dereva tax asimamishe gari "Oya broo, hebu simamisha mbele hapo kwenye zipu, tangi bovu " (Nikatumia utani wake).
Akaniuliza "Vipi mbona umekatisha safari? "

Nikamwambia "Anh nayemfata hayupo huko "
Akajibu "Basi niongeze mkwanja nikurudishe mpaka Simu 2000".
Nikamcheck, nikamjibu "Acha ujinga wewe, daladala nauli bei chee tu."

Akasimamisha gari, nikashuka na kumlipa hela yake.
Nikaelekea moja kwa moja mpaka kwenye kituo cha kusubiria daladala.

Nilijicheka sana, nikajiona boya, lakini nilijiuliza sana kwanini Abdulrahman alinidanganya, nikapata jibu kuwa huenda wanahisi kitu kati yangu na Careen, hivyo wanajaribu kunipima hisia, au kuniharibu kisaikolojia.

Kutokana na tabu ya usafiri, nilifika Gongo La Mboto majira ya saa 4 usiku, kwavile nilichoka sana, nilienda hostel tu kulala na wala sikuwa na hamu ya kwenda kwenye bhash chuoni.

Weekend niliitumia vizuri sana kuchat na Careen, na ilizidi kunoga zaidi na zaidi, huku nikionyesha umahiri wangu kwenye kujali, kuheshimu , kumthaminisha na kumchekesha pia.
Alifurahia sana kuchat na mimi, na kuna nyakati alinipigia tukazungumza sana kwa muda mrefu mazungumzo ya maisha na mambo mbalimbali.

Lakini mwisho tulijikuta tumedondokea kwenye mazungumzo ya mahusiano.
Careen: Unajua kaka Chris tangu nikujue, unanifurahisha jambo moja.

Mimi: Jambo gani hilo mamie??

Careen: Unanijali sana, unanipa sana kipaumbele, na hata kunithamini pia. Kiukweli najisikia furaha sana kuwa na rafiki kama wewe.

Mimi: Asante sana, ni jukumu langu kuhakikisha rafiki yangu anajisikia yupo na rafiki anayejali uwepo wake.

Careen: Nashukuru sana kwa hilo, Mungu akuweke miaka mingi. Huwa unanikumbusha mbali sana.

Mimi: Mbali wapi tena mamie?

Careen akakaa kimya kidogo, kisha akaendelea maongezi "Leo ngoja nikupe siri moja maana umeshakua rafiki yangu, na ni zaidi ya rafiki, umekuwa kama ndugu kwangu.
Kaka Chris unanikumbushaga mwanaume ambaye sikuwahi kumpenda hapo zamani, alikua anaitwa Khalfan."

Akanyamaza kidogo, nikazidi kupata shauku ya kutaka kujua zaidi, maana nilijua nikijua madhaifu ya Careen basi lazima nitafanikiwa kumpata kiurahisi.

Akaendelea "Huyo kaka tulianza uchumba kipindi hicho niko form two, alinipenda sana ila tatizo mimi sikumpenda, nilimkubali tu sababu enzi hizo kundi langu wote walikua na maboyfriend kasoro mimi, halafu Khalfan alikua na vijisent kidogo "

Nikaguna "mmmh ", akaendelea "Sasa kipindi hicho nilikua sijui mapenzi nini, kwahiyo zile kuonyesha kunijali, mara message, mara anipigie simu, halafu alikua na wivu.
Basi nikawa naona kero sana, mpaka kuna muda nilikua namkatia simu, au naizima tu kwa makusudi "- (akazungumza huku anajichekesha).
.
Nikamuuliza "Kwahiyo bado mpo pamoja??? "

Akajibu "Hapana, tuliachana form 4. Aliniheshimu sana, na wala hatukuwahi kusex."

Nikamjibu "Duh kweli huyo alikupenda "
Akaniambia "Kweli kabisa, na najutia kumpoteza.
Sababu akili ilikuja kunijia pindi nilipokuwa form six, ndipo nilimpata huyu boyfriend wangu wa sasa "
Nikastuka sana kusikia neno "boyfriend wake wa sasa "

Akaendelea "Nilikuja kugundua mapenzi ni nini baada ya kumpenda huyu boyfriend wangu wa sasa, yani wala hanijali wala kunithamini, yani yeye kila kitu ni ubabe na kuniforce tu, najitajidi sana kujitunza kwaajili yake lakini yeye hajali, na ananisaliti mara kwa mara.
Nayatamani sana maisha yangu ya zamani, natamani ningekua na Khalfan"- (Alizungumza kwa hisia sana na kuonyesha akimaanisha kile anachosema)

Niliyapokea maneno hayo kwa masikitiko makubwa sana, nikamtia moyo, pia nikajaribu kumpa ushauri wa kinafki ili aone kama namsapoti.
Akanishukuru sana kwa ushauri wangu, na kumtia moyo, na mwisho akanitakia usiku mwema.

Jumatatu iliyofata niliamka nikiwa mwenye furaha sana, huku nikiwa na matumaini mapya ya kumpata Careen hasa ukizingatia nimeshajua madhaifu yake yako wapi, nini anakosa kwa boyfriend wake.

Nilimtumia message, akaniambia yuko anapata kifungua kinywa kwenye mgahawa wa kifahari wa Legacy, uliopo ndani ya chuo.
Nikawahi mpaka mahali hapo, lakini sikufurahishwa na nilichokiona, nilimkuta Careen akiwa anapata breakfast pamoja na Peter na Abdulrahman.

Nikasonya kwa mbali.
Nikawasogerea, nikatoa salamu, kisha nikaagiza chakula na kujumuika nao.
Story zilinoga, tukamaliza kula, tukanyanyuka na sote tukaelekea mahali pakulipia bills.
Kimbembe kilianza wakati wakulipa bill.

Muhudumu: Jumla Tsh.9500.
Nikamtazama muhudumu, nikajisemea kimoyo moyo "Leo lazima niwavimbie hawa watu ".
nikaingiza mkono mfukoni na kutoa noti ya Tsh elfu 10 na kumpa muhudumu, nikamwambia "kata yote".
Peter kwa kutaka sifa nae, akasema "Bro, don't worry, i'll pay(Kaka usijali, nitalipa mimi)".

Nikamtazama Peter, nikamsisitizia muhudumu "Kata yote humo humo tu "
Abdulrahman akanitazama, aliniona pindi naichungulia pesa mfukoni, alijua wazi sina hela nyingine zaidi ya hiyo elfu 10 niliyotoa.

Akamtazama muhudumu, na kumwambia kwa kingereza maneno yaliyo maanisha "Utaniletea juice ya elfu 3 ya Azam Mango kwaajili ya Careen, na maji ya kilimanjaro lita moja kwaajili yangu, atalipa Chris."

Nikashangaa sana kauli alizotamka Abdulrahman, nilihisi huyu jamaa ana nia ya kuniua kwa presha.
Nilianza kuvurugwa akili, nikajihisi kama mwenye bahati mbaya siku zote, kila siku niaibike mimi tu.

Careen aliustukia mchezo na kutamka maneno yaliyonipa nguvu, akasema "No, sihitaji juice, nitachukua maji tu, na Peter utalipia bill yote."
Akageuka na kuelekea kwenye fridge la kuchukulia maji.

Peter akatoa hela na kulipa, kipindi Abdulrahman akinisogerea karibu, akanong'ona "Hey young man, did you really follow her that day?? (Hey kijana, ulimfata kweli siku ile???).

Nikajua sasa bifu la mafahari wawili, ndipo linapoanzia.
Nikamjibu, "Its none of your damn business bro"(Haikuhusu kaka).

Akacheka kinafki, akaongeza sauti na kusema kwa kingereza maneno yaliyo maanisha "Hahah kumbe unampenda sana eenh??!! Hujaona wasichana wengine? Wewe sio wa aina yake, anahitaji mwanaume, sio mvulana kama wewe."

Nilipandwa na hasira, nikasahau niko maeneo gani, sikutazama nyuma yangu kuna nani, nikaropoka " Kwa uzuri gani hasa aliokua nao, nimpende yeye nani?? Wewe kula kulala ndio unajiita "Mwanaume ", unachekesha sana, sina shida na huyo kinyago wenu, Careen Careen, kwanza sio type yangu. Kimwanamke kimechongoka kama spoku, mxieeeeew.
Nikasonya ".

Wote wakabaki wananitazama, sikuelewa kwanini hawakujibu walibaki wameduwaa, niligeuza macho pembeni nikaona jinsi wengine pia wanaokula kwenye meza wakinitazama.
Nilijistukia, lakini nilishangaa zaidi kuona Peter na Abdulrahman wakiwa wameduwaa kuelekea upande mmoja, ikanibidi nigeuze macho yangu kutazama wanachotazama.

Uso kwa uso, macho yangu yalikutana na ya Careen aliyekuwa amebaki ananishangaa huku akilengwa na machozi
.

Je nini kitafuata??! Careen atamchukuliaje Chris???.

******Usikose sehemu ya 5*****
#Itaendelea...

Sehemu ya 5 soma hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
Eti mbele kwenye zipu[emoji1787]
 
Back
Top Bottom