Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,030
- 20,391
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!
.
Sehemu ya kwanza.
.
Mwaka 2016 ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia chuoni, ilikua katika chuo cha kimataifa cha Kampala.
Naikumbuka siku yangu ya kwanza nilikua naonekana mnyonge sana, hasa kutokana na ugeni wangu na kila mmoja ndani ya darasa alikua ameonekana kutokumzoea mwenzake.
.
Pindi lecture inaendelea, nilikua niko makini sana kusikiliza kile ambacho lecturer alikua akifundisha darasani, nikatupa macho yangu pembeni kuwatazama classmates wangu, kila mmoja alionekana yuko busy akimsikiliza.
Lakini pembeni yangu nilishangaa kumuona kijana mmoja akiwa ameduwaa, na wala hakuonyesha kufatilia kinachofundishwa. Nikapata shauku ya kutaka kujua kinachoendelea, anatazama nini hicho kiasi cha kumfanya aduwae kiasi kile, nikatupa macho kwa mbele zaidi kuelekea uelekeo wa macho yake.
.
Nilipigwa na bumbuwazi, nami niliduwaa zaidi ya yule kijana, macho yalinitoka huku nikiongeza umakini zaidi wa kutazama kile nilichokiona.
Macho hayana panzia, yalitua kwa msichana mmoja mrembo aliyefanya mimi na yule kijana tuduwae. Wala hakujua kama tunamtazama, alikua busy akifatilia lecture.
Nilitengeneza movie nyingi za mahaba kichwani mwangu juu ya yule msichana.
.
Ghafla nilishtushwa mawazoni mara baada ya lecturer kuuliza swali, na kuniomba mimi niliyeonekana sifatilii somo nilijibu swali hilo.
.
Lecturer: Differentiate between a manager and an entrepreneur???
.
Kwa mbwembwe zote, tena huku nikimtazama mtoto mkali, nikanyanyuka, nikamtazama lecturer na kujibu swali.
.
Siku ya kwanza ikapita kama hivyo, na ndiyo siku niliyoanza kumpenda.
.
Siku kadhaa zilipita, nikiwa tayari nimeshayazoea mazingira chuoni hapo, nikijulikana kama kijana mstaarabu na mcheshi ndani na nje ya darasa.
.
Siku moja nilipokuwa darasani nikifanya assignment kwenye laptop.
Ghafla ilisikika sauti nyororo yenye kumtoa nyoka pangoni, moyo ulinipiga Paaah, damu ikaanza kunichemka, nikapata shauku ya kutaka kujua ni nani huyu ananiongelesha.
.
Nikanyanyua uso ili nimtazame uso, macho yangu yalikutana na mavazi safi yenye kung'ara, zaidi ilikua ni harufu yake ya pafyumu iliyozidi kunivutia, nikapanda mpaka juu na kukutana uso kwa uso na msichana mrembo aliyekuwa akilini mwangu siku zote tangu nianze chuo.
.
Nilibaki nashangaa kwa sekunde kadhaa, ikabidi arudie salam yake.
Yeye: Hi.
Mimi: Hi, how umh how you doing?
Yeye: Doing great, sorry for disturbance, can you do me a favor?
.
Nikasikiliza jinsi anavyoteleza kwenye lugha ya kigeni, nikaona hapana, huku tunako endelea atanipoteza mwisho nipate aibu, mimi st.kayumba, English ilipanda ndege.
.
Nikamjibu: Bila samahani, wala hujanisumbua. Yes unaweza sema tu maybe naweza saidia.
Yeye: Onh asante kwa ukarimu wako, naomba unielekeze jinsi ya kuset hotspot kwenye iPhone, nataka niconnect na laptop yangu ".
.
Alizidi kunivutia kwa maneno yake matamu, nikajisemea kimoyo moyo "Haya ni maneno ambayo kina Mwajuma Ndalandefu uswazi hawawezi kuyasema, na leo ndo chance nzuri ya kujuana nae vizuri ".
Sikutaka kuchelewa nikachukua kiti, nikamsogeza karibu na kuanza kumpa maelekezo.
.
Nilipomaliza alishukuru sana, lakini alipotaka kuondoka tu akatupa jicho kwenye laptop na kugundua nilikua nafanya assignment.
Akasema na yeye alikua bado hajafanya, nikamuomba tujumuike ili tufanye wote.
.
Shida yangu haikuwa tufanye wote assignment, shida yangu ilikua tuzidi kuzoeana ili hata kesho yake nisipate tabu tena kuanza kujitambulisha.
Nilizidi kumnogesha kwa story ambazo zilimfanya azidi kucheka huku tukifanya assignment.
.
Tulipomaliza wala hakunyanyuka kama mwanzo, aliendelea kukaa na tukazidi kupiga story.
Nikaona nisichelewe kutaka kumjua.
.
Mimi: Hahah yale makoti hayafai kwa Dar es salaam hii, labda utembee huku na feni pembeni.
.
Akacheka, kisha akatazama saa yake, nikastuka nikajua huu utakua muda wa lunch au kuondoka tayari.
Nikamuwahi "Btw nimefurahia sana uwepo wako, na umefanya niione assignment nyepesi pia.".
.
Akanijibu "Asante sana, tangu nianze chuo leo ndo nimefurahi sana, ndomana nimetazama saa hapa nikashangaa leo nimebaki hadi saa 7".
.
Mimi: Onh nimefurahi kusikia hivyo, kwani haujapata marafiki bado?!
.
Yeye: You know what, mahali kama hapa pana watu tofauti, waliotokea kwenye malezi tofauti. Na usipokua makini kwenye uchaguzi wa marafiki, ukawa unaparamia tu, basi unaweza jikuta unapata marafiki wa hovyo hovyo.
Najiheshimu sana, na napenda niwe na marafiki wanao jiheshimu pia, hata wewe nimekufata mpaka kukuomba unisaidie, sababu nilijua wewe mstaarabu na ni tofauti na vijana wengine darasani."
.
Nikashusha pumzi nzito sana, maneno yaliniingia sana akilini. Mwanzo nilikua na wazo la kumuomba namba leo leo, lakin nikaona hapana huyu nikienda nae haraka nitampoteza, anajithamini na kujiheshimu sana tofauti na nilivyofikiria.
.
Nikamjibu: Uko sahihi kabisa, hata mimi ndio maana unaona nakaa peke yangu sana sababu hiyo hiyo, naogopa kujiingiza kwenye makundi ya watu wasio na maadili.
Hata hivyo, nimefurahi kujua kama uko tofauti na wasichana wengine, naitwa Chris. "
.
Yeye: Nice to meet you Chris, naitwa Careen".
.
Mimi: "Damn, nice name''
.
Akafurahi sana, tukaagana na kuondoka. Nakumbuka nilijilaumu sana kwanini sikumuomba namba yake ya simu, lakini nilijipa moyo kuwa huo ni mwanzo mzuri sana kwangu, na pia ni jambo zuri kutokumuomba namba mapema kiasi hicho kutamfanya asihisi chochote kuhusu hisia zangu kwake.
.
Siku iliyofata mambo yalizidi kuwa moto darasani, nakumbuka alibadili sehemu yake ya kukaa na kuja kukaa karibu nami, alikua akipenda kuniita kaka Chris, japo sikupenda kuitwa "Kaka" lakini nililivumilia tu sababu sikupenda ahisi kuwa nina hisia juu yake.
.
Watu walikua wakitutazama sana, na wengine kuulizana hawa Wamezoeana saa ngapi, sababu hakua na mazoea na mtu yeyote yule zaidi yangu, na wengine aliishia kuwapa salamu na story mbili tatu pale inapobidi.
Nilifurahishwa sana na mwenendo wake, hasa ukizingatia hakuna mwanaume anayependa kuwa na mwanamke ambaye Mcharuko, au anajifanya ana mazoea na kila mtu.
.
Nakumbuka siku ya tatu ya urafiki wetu, majira ya saa 6, nilimuomba twende tukapate lunch wote, hasa ukizingatia nilitaka niwe rafiki yake wa karibu zaidi ambaye ataweza kula nae, kuongea nae, kuniambia jambo lolote hata lile lisilo ambikika kiurahisi, ambaye atamkumbuka wakati wa huzuni na furaha.
Kwakifupi, nilitaka niwe kila kitu kwake, ili hata pale nitakapo muhitaji tuwe wapenzi basi asiweze kukataa, yani niwe nimemtengeneza kihisia zaidi.
.
Tulielekea wote mpaka maeneo pakulia, maarufu kwa jina la PEPSI, sote tulichukua chakula na kuelekea mezani, story zilikuwa nyingi na chakula kilinoga.
Alikua akiniambia jinsi anavyojisikiaga aibu kula mbele za watu hasa wanaume, ila anashangaa leo hii ameweza kukubali kukaa meza moja na mimi.
Nilimshika mkono, nikamtazama usoni, nikamwambia ''Mimi ni rafiki yako, usiniogope, usinioneee aibu, jisikie huru kufanya lolote unapokua nami, ili tuwe marafiki bora basi inabidi tusioneane aibu."
.
Alitabasamu na chakula kiliendelea kuliwa, tulipomaliza tukaelekea mahali pakulipia, kwavile mimi ndiye niliyemualika, na ndiyo mwanaume, basi nikataka kuvimba ili nilipe bill.
.
Nikaingiza mkono mfukoni ili kuchukua wallet, nikastuka, nikaanza kupagawa baada ya kuikosa wallet kwenye mfuko wa nyuma wa suruali ninako wekaga.
.
Nikasearch na mifuko mingine sikukuta kitu.
Mwanadada ambaye ndiye mpokea malipo akaniongelesha tena "Nakusubiria wewe kaka".
.
Careen aliyekuwa kwa pembeni akageuka na kunitazama usoni, ikabidi nivunge nisionyeshe wasiwasi wangu.
Nikarudisha mikono mfukoni kuhakikisha kwa mara ya pili, mapigo ya moyo yalizidi kunidunda baada ya kugundua kuwa mfukoni ni kweupe, na dada mpokea malipo alikua akinitupia jicho.
.
Mawazo yakawa huyu binti, atanionaje??? Je atanisaidia kulipa??? Au nae hana hela?? Sindo mwanzo wa kuaibika huu??! .
_______________________________
Usikose sehemu ya pili
Itaendelea....
Soma Sehemu ya pili hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
.
Sehemu ya kwanza.
.
Mwaka 2016 ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia chuoni, ilikua katika chuo cha kimataifa cha Kampala.
Naikumbuka siku yangu ya kwanza nilikua naonekana mnyonge sana, hasa kutokana na ugeni wangu na kila mmoja ndani ya darasa alikua ameonekana kutokumzoea mwenzake.
.
Pindi lecture inaendelea, nilikua niko makini sana kusikiliza kile ambacho lecturer alikua akifundisha darasani, nikatupa macho yangu pembeni kuwatazama classmates wangu, kila mmoja alionekana yuko busy akimsikiliza.
Lakini pembeni yangu nilishangaa kumuona kijana mmoja akiwa ameduwaa, na wala hakuonyesha kufatilia kinachofundishwa. Nikapata shauku ya kutaka kujua kinachoendelea, anatazama nini hicho kiasi cha kumfanya aduwae kiasi kile, nikatupa macho kwa mbele zaidi kuelekea uelekeo wa macho yake.
.
Nilipigwa na bumbuwazi, nami niliduwaa zaidi ya yule kijana, macho yalinitoka huku nikiongeza umakini zaidi wa kutazama kile nilichokiona.
Macho hayana panzia, yalitua kwa msichana mmoja mrembo aliyefanya mimi na yule kijana tuduwae. Wala hakujua kama tunamtazama, alikua busy akifatilia lecture.
Nilitengeneza movie nyingi za mahaba kichwani mwangu juu ya yule msichana.
.
Ghafla nilishtushwa mawazoni mara baada ya lecturer kuuliza swali, na kuniomba mimi niliyeonekana sifatilii somo nilijibu swali hilo.
.
Lecturer: Differentiate between a manager and an entrepreneur???
.
Kwa mbwembwe zote, tena huku nikimtazama mtoto mkali, nikanyanyuka, nikamtazama lecturer na kujibu swali.
.
Siku ya kwanza ikapita kama hivyo, na ndiyo siku niliyoanza kumpenda.
.
Siku kadhaa zilipita, nikiwa tayari nimeshayazoea mazingira chuoni hapo, nikijulikana kama kijana mstaarabu na mcheshi ndani na nje ya darasa.
.
Siku moja nilipokuwa darasani nikifanya assignment kwenye laptop.
Ghafla ilisikika sauti nyororo yenye kumtoa nyoka pangoni, moyo ulinipiga Paaah, damu ikaanza kunichemka, nikapata shauku ya kutaka kujua ni nani huyu ananiongelesha.
.
Nikanyanyua uso ili nimtazame uso, macho yangu yalikutana na mavazi safi yenye kung'ara, zaidi ilikua ni harufu yake ya pafyumu iliyozidi kunivutia, nikapanda mpaka juu na kukutana uso kwa uso na msichana mrembo aliyekuwa akilini mwangu siku zote tangu nianze chuo.
.
Nilibaki nashangaa kwa sekunde kadhaa, ikabidi arudie salam yake.
Yeye: Hi.
Mimi: Hi, how umh how you doing?
Yeye: Doing great, sorry for disturbance, can you do me a favor?
.
Nikasikiliza jinsi anavyoteleza kwenye lugha ya kigeni, nikaona hapana, huku tunako endelea atanipoteza mwisho nipate aibu, mimi st.kayumba, English ilipanda ndege.
.
Nikamjibu: Bila samahani, wala hujanisumbua. Yes unaweza sema tu maybe naweza saidia.
Yeye: Onh asante kwa ukarimu wako, naomba unielekeze jinsi ya kuset hotspot kwenye iPhone, nataka niconnect na laptop yangu ".
.
Alizidi kunivutia kwa maneno yake matamu, nikajisemea kimoyo moyo "Haya ni maneno ambayo kina Mwajuma Ndalandefu uswazi hawawezi kuyasema, na leo ndo chance nzuri ya kujuana nae vizuri ".
Sikutaka kuchelewa nikachukua kiti, nikamsogeza karibu na kuanza kumpa maelekezo.
.
Nilipomaliza alishukuru sana, lakini alipotaka kuondoka tu akatupa jicho kwenye laptop na kugundua nilikua nafanya assignment.
Akasema na yeye alikua bado hajafanya, nikamuomba tujumuike ili tufanye wote.
.
Shida yangu haikuwa tufanye wote assignment, shida yangu ilikua tuzidi kuzoeana ili hata kesho yake nisipate tabu tena kuanza kujitambulisha.
Nilizidi kumnogesha kwa story ambazo zilimfanya azidi kucheka huku tukifanya assignment.
.
Tulipomaliza wala hakunyanyuka kama mwanzo, aliendelea kukaa na tukazidi kupiga story.
Nikaona nisichelewe kutaka kumjua.
.
Mimi: Hahah yale makoti hayafai kwa Dar es salaam hii, labda utembee huku na feni pembeni.
.
Akacheka, kisha akatazama saa yake, nikastuka nikajua huu utakua muda wa lunch au kuondoka tayari.
Nikamuwahi "Btw nimefurahia sana uwepo wako, na umefanya niione assignment nyepesi pia.".
.
Akanijibu "Asante sana, tangu nianze chuo leo ndo nimefurahi sana, ndomana nimetazama saa hapa nikashangaa leo nimebaki hadi saa 7".
.
Mimi: Onh nimefurahi kusikia hivyo, kwani haujapata marafiki bado?!
.
Yeye: You know what, mahali kama hapa pana watu tofauti, waliotokea kwenye malezi tofauti. Na usipokua makini kwenye uchaguzi wa marafiki, ukawa unaparamia tu, basi unaweza jikuta unapata marafiki wa hovyo hovyo.
Najiheshimu sana, na napenda niwe na marafiki wanao jiheshimu pia, hata wewe nimekufata mpaka kukuomba unisaidie, sababu nilijua wewe mstaarabu na ni tofauti na vijana wengine darasani."
.
Nikashusha pumzi nzito sana, maneno yaliniingia sana akilini. Mwanzo nilikua na wazo la kumuomba namba leo leo, lakin nikaona hapana huyu nikienda nae haraka nitampoteza, anajithamini na kujiheshimu sana tofauti na nilivyofikiria.
.
Nikamjibu: Uko sahihi kabisa, hata mimi ndio maana unaona nakaa peke yangu sana sababu hiyo hiyo, naogopa kujiingiza kwenye makundi ya watu wasio na maadili.
Hata hivyo, nimefurahi kujua kama uko tofauti na wasichana wengine, naitwa Chris. "
.
Yeye: Nice to meet you Chris, naitwa Careen".
.
Mimi: "Damn, nice name''
.
Akafurahi sana, tukaagana na kuondoka. Nakumbuka nilijilaumu sana kwanini sikumuomba namba yake ya simu, lakini nilijipa moyo kuwa huo ni mwanzo mzuri sana kwangu, na pia ni jambo zuri kutokumuomba namba mapema kiasi hicho kutamfanya asihisi chochote kuhusu hisia zangu kwake.
.
Siku iliyofata mambo yalizidi kuwa moto darasani, nakumbuka alibadili sehemu yake ya kukaa na kuja kukaa karibu nami, alikua akipenda kuniita kaka Chris, japo sikupenda kuitwa "Kaka" lakini nililivumilia tu sababu sikupenda ahisi kuwa nina hisia juu yake.
.
Watu walikua wakitutazama sana, na wengine kuulizana hawa Wamezoeana saa ngapi, sababu hakua na mazoea na mtu yeyote yule zaidi yangu, na wengine aliishia kuwapa salamu na story mbili tatu pale inapobidi.
Nilifurahishwa sana na mwenendo wake, hasa ukizingatia hakuna mwanaume anayependa kuwa na mwanamke ambaye Mcharuko, au anajifanya ana mazoea na kila mtu.
.
Nakumbuka siku ya tatu ya urafiki wetu, majira ya saa 6, nilimuomba twende tukapate lunch wote, hasa ukizingatia nilitaka niwe rafiki yake wa karibu zaidi ambaye ataweza kula nae, kuongea nae, kuniambia jambo lolote hata lile lisilo ambikika kiurahisi, ambaye atamkumbuka wakati wa huzuni na furaha.
Kwakifupi, nilitaka niwe kila kitu kwake, ili hata pale nitakapo muhitaji tuwe wapenzi basi asiweze kukataa, yani niwe nimemtengeneza kihisia zaidi.
.
Tulielekea wote mpaka maeneo pakulia, maarufu kwa jina la PEPSI, sote tulichukua chakula na kuelekea mezani, story zilikuwa nyingi na chakula kilinoga.
Alikua akiniambia jinsi anavyojisikiaga aibu kula mbele za watu hasa wanaume, ila anashangaa leo hii ameweza kukubali kukaa meza moja na mimi.
Nilimshika mkono, nikamtazama usoni, nikamwambia ''Mimi ni rafiki yako, usiniogope, usinioneee aibu, jisikie huru kufanya lolote unapokua nami, ili tuwe marafiki bora basi inabidi tusioneane aibu."
.
Alitabasamu na chakula kiliendelea kuliwa, tulipomaliza tukaelekea mahali pakulipia, kwavile mimi ndiye niliyemualika, na ndiyo mwanaume, basi nikataka kuvimba ili nilipe bill.
.
Nikaingiza mkono mfukoni ili kuchukua wallet, nikastuka, nikaanza kupagawa baada ya kuikosa wallet kwenye mfuko wa nyuma wa suruali ninako wekaga.
.
Nikasearch na mifuko mingine sikukuta kitu.
Mwanadada ambaye ndiye mpokea malipo akaniongelesha tena "Nakusubiria wewe kaka".
.
Careen aliyekuwa kwa pembeni akageuka na kunitazama usoni, ikabidi nivunge nisionyeshe wasiwasi wangu.
Nikarudisha mikono mfukoni kuhakikisha kwa mara ya pili, mapigo ya moyo yalizidi kunidunda baada ya kugundua kuwa mfukoni ni kweupe, na dada mpokea malipo alikua akinitupia jicho.
.
Mawazo yakawa huyu binti, atanionaje??? Je atanisaidia kulipa??? Au nae hana hela?? Sindo mwanzo wa kuaibika huu??! .
_______________________________
Usikose sehemu ya pili
Itaendelea....
Soma Sehemu ya pili hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)