Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu hujui nilivyokusubiri hii story yako uimalizieNimerudi
Kwanini mkuuKwanza hata hapa nahisi nina masaa 24 ya kuwa hewani Harafu baadaye ban nyingine tena.
Mkuu sema hii story iendeleze basiNahisi makosa yatajirudia maana nipo kwenye ulinzi maalum wa mods kwa kila comment, thread na hata reaction ninayo fanya inapitiwa na mods
Poa poa mkuuNgoja stori niendeleze Kabula rungu halijaja ila bado nipo nipo kwanza.
SubscribedMAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!
Sehemu ya Saba
#Ilipoishia: Careen aliniuliza swali tata huku akilia kwa uchungu, aliuliza kama ni kweli niliwasha simu yake, na kama ni kweli boyfriend wake alipiga.
Nilibaki najiuliza maswali mengi sana kichwani kuwa itakuaje endapo nitajibu NDIO, na itakuaje endapo nitakataa, hasa ukizingatia kuwa Careen anampenda sana boyfriend wake.
#Inaendelea :
Nikapiga hesabu za haraka haraka, nikakumbuka kuwa tumeambiwa tuishi na wanawake kiakili.
Nikaona njia bora ni kumdanganya, sababu nikimuambia ukweli basi atazidi kunichukia.
.
Nikamjibu "Hapana, sikuiwasha kabisa simu ".
.
Akanisisitiza kwa uchungu, "Kaka Chris niambie ukweli ".
Lakini bado nilisimama kwenye jibu langu lile lile.
.
Aliniamini nilichosema huku akisisitiza kuwa huenda boyfriend wake ametafuta tu sababu ya kumuacha.
Nilibaki nimenyong'onyea nisijue cha kuongea, akashindwa kuzungumza mwisho akakata simu.
.
Nilihangaika usiku kucha kutaka kujua anaendeleaje, niliogopa asije kuchukua maamuzi mabaya sababu ya kuachwa na ampendae.
Lakini sikufanikiwa kujua liendelealo, simu yake ilikua imezimwa muda wote.
Nilijihisi mwenye makosa sana, nilijilaumu kwa ujinga wangu wa kusahau kumkabidhi simu yake siku ile kwenye gari, lakini nilijilaumu zaidi kwa ujinga wangu wa kutaka kuwaoshea kina Peter, kumbe mwisho nimekuja kusababisha maumivu kwa mwanamke ninaempenda.
.
Kutokana na mawazo niliyo nayo, sikupata usingizi kabisa, na nilishindwa kabisa kusoma notes kujiandaa kwaajili ya mtihani wa kesho chuoni.
.
Mitihani ya kujipima maarufu kama C.A.T(Continuous Assessment Test) one, ilikuwa ndiyo inaanza kwa siku ya kesho yake Jumatatu, na mtihani wetu wa kwanza ulikua ni English And mmunications Skills, utakaofanyika majira ya saa mbili asubuhi.
Sikuwa na mawazo ya mtihani wa kesho, nilikua na mawazo juu ya Careen.
.
Nilipitiwa na usingizi majira ya saa 10 alfajiri, na kujikuta nimestuka usingizini majira ya saa 2 na dakika 6 asubuhi.
Nilistuka sana, niligundua kuwa nimeshachelewa dakika 6 tangu mtihani uanze.
Nikajiandaa tu haraka haraka, hostel mpaka chuo hapana umbali sana, lakini ilibidi nichukue bodaboda ili niwahi.
.
Nikafika chuo, nikashuka kwenye bodaboda na kulipa.
Pindi nataka niingie ndani mlinzi akauliza "Kitambulisho tafadhali? "
.
Nikaanza kukitafuta kitambulisho mifukoni, nikakikosa, nikatafuta kwenye begi na bado nikakikosa.
Ndipo nikakumbuka kuwa nilikiacha kwenye mfuko wa shati nililovaa siku iliyopita niliyokuja chuo.
.
Kutazama muda, nimechelewa kama dakika 12 tayari, na siwezi ingia ndani ya chuo, wala ndani ya chumba cha mtihani bila kitambulisho.
Nikaita boda boda haraka, nikarudi hostel na kukichukua.
Nilichanganyikiwa sana, lakini nilichelewa sana.
.
Nilihojiwa maswali kadhaa kwanini nimechelewa, nikajitetea kuwa naishi mbali sana na chuo.
Nikaruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha mtihani.
Nikatupa jicho, wanafunzi wote walikua busy kasoro Careen ambaye alionekana kama ametulia tu akiwaza.
.
Nikakaa kiti kilicho kando yake, nikayatazama maswali na kugundua hayakua magumu sana, na Careen anayajua vizuri sababu tuliwahi jadili wote hizi topic.
.
Ndani ya nusu saa nzima ya mtihani, Careen alikua ameinama tu akiwa mwenye mawazo, hakuonekana kujibu lolote.
Nikagundua kuwa bado ana mawazo ya kuachwa na boyfriend wake.
Nilijua hakuna chochote ambacho angeweza fanya kwa wakati huo.
.
Nikatazama mbele, nikaona msimamizi anazungumza na mkaguzi wa ledgers, nikaona huu ndio mwanya wa kuweza kumsaidia Careen.
Nikamuita kwa sauti ya kunong'ona "Careen "
.
Akanitazama, nikamuonyeshea ishara "Vipi?? Mbona huandiki".
Akabaki amenitazama tu, nikajua hajanielewa, nikarudia ishara zile zile.
.
Ghafla nilishtushwa na sauti ya msimamizi, aliyezungumza kwa kingereza akimaanisha "Chris na Careen mnazungumza nini??".
.
Sote tukamtazama tukijua kuwa tayari tuko matatizoni, na kweli kilichofata alituletea fomu tujaze namba ya usajili, jina, na sahihi kwa kosa la kukutwa tunapiga chabo.
.
"Chabo ni kinyume na sheria na kanuni za chuo chetu, ndiomaana tunajitahidi kuhakikisha mnapata elimu bora, tumewawekea mazingira bora, vifaa vya kutosha vya kujifunzia, walimu kuingia kwa wakati kwenye vipindi na kuhakikisha kuwa wanakufundisha mpaka unaelewa.
Hebu tuambie Chris, wapi unahisi tulishindwa kukupatia elimu bora, ili tujirekebishe??? "
.
Nikamtazama msimamizi, nikashindwa kujibu sababu elimu tunayopatiwa ni ya kiwango kikubwa sana.
Lakini nilijua tatizo lilikuwa hajaelewa kwanini tulikua tunazungumza.
.
Nilizidi kuiona siku yangu mbaya, hasa ukizingatia nilizidi kumuweka Careen kwenye wakati mgumu.
Nimemkosesha boyfriend wake, na sasa nimemkosesha mtihani wake na bado anasubiri adhabu ya chuo juu ya kosa la kupiga chabo.
.
Tulitoka nje na kuelekea maeneo garden, alizidi kulia sana.
Alijumlisha machungu yote aliyonayo.
Nilijitahidi sana kumbembeleza lakini hakutulia mpaka akaja kunyamaza mwenyewe.
.
Baada ya kama masaa 3 mbele, Peter na Abdulrahman walikuja kwa pamoja na kumkuta Careen akiwa kwenye majonzi.
Peter akauliza kwa kingereza akimaanisha "Mbona unaonekana umenyongea??? Unaumwa mpendwa?? "
.
Careen: Hapana. (Akajibu huku anaanzwa kulengwa na machozi)
Ikanibidi niwaombe wasimsumbue, ili apate mapumziko.
.
Peter akanitazama kwa jicho la kunitamani japo aning'ate, lakini akanistahi tu.
Akamshika Careen na kuanza kumhoji taratibu, Careen alianza kuficha ficha mambo, lakini baadae alijikuta akianza kufunguka.
Hofu yangu ilizidi, nilikua nawaza litakalo fata hasa akianza kugusia juu ya story ya simu.
.
Careen: Boyfriend wangu ameniacha.
.
Peter akajibu "Sikuwahi kuwaza kama una boyfriend, na kwanini amekuacha.??."
.
Kila maneno waliyozidi kuzungumza, yalizidi kunipa hofu, nikaropoka tena nikimtaka Peter aache kumsumbua Careen kwa maswali.
.
Careen akaniambia nisijali, akaanza kuelezea jinsi boyfriend wake alivyomnyamazia siku nzima, na jinsi alivyoanza kumtusi na maneno aliyomuambia.
Mwisho akamaliza "Anasema mimi nimelala kwa mwanaume mwingine na simu sijampokelea".
.
Peter na Abdulrahman wakastuka, nami pia nikastuka sababu nilijua kuwa kinachofata ni majanga kwangu.
Nikawaambia kina Peter ''Inatosha, mwacheni apumzike "
Peter akamtazama Abdulrahman, Peter akaropoka "Kwani juzi jumamosi ulilala wapi??? Na kwanini ulizima simu?? "
.
Hapo ndipo presha ilipozidi kunipanda na kutamani ardhi ipasuke niingie.
Careen akajibu "Nililala nyumbani, na simu niliisahau kwa Chris pindi nilipokuwa kwenye gari "
Peter na Abdulrahman wakaguna kwa nguvu huku wakitazamana, lakini mimi nilikua nahisi nafsi inataka kupasuka nife hapo hapo.
.
Peter akachukua simu yake, na kumuonyesha Careen kumbukumbu za simu alizopiga na kupokelewa, Careen alikuta namba yake nayo ipo kwenye list.
Careen akanitazama kwa mshangao, akarudisha macho kwa Peter.
Abdulrahman akaongeza "Na Chris alisema tusiwasumbue, umelala nae, chumbani kwake, kifuani kwake "- (Alizungumza kwa msisitizo).
.
Peter akaongeza, "Na nadhani, Chris aliiwasha simu yako asubuhi, na hakuipokea simu ya boyfriend wako".
.
Careen aligeuka na kunitazama kwa hasira, nahisi alitamani hata kuninyonga, machozi yalimjaa machoni mwake.
Uso ulinijaa aibu, lakini hofu kubwa ilinizidi.
Nilijua leo ndio nampoteza Careen, nikageuka na kuwatazama, kwajinsi walivyokuwa wakiniangalia, nilitamani hata ningekimbia, au hata ningerudisha muda nyuma ili niyafute makosa yangu yote.
Careen alinitazama kwa hasira, kisha akazungumza maneno yaliyo nifanya nihisi moyo unataka kunitoka.
.
Je Careen alizungumza maneno gani!!??? Chris atafanya nini???
Usikose sehemu ya 8
#Itaendelea
Mkuu Safi Sana Kwa story na nimepata shauku ya kuendelea kuifatilia coz niliwahi ishi maeneo karibu na chuo cha Kampala...so maeneo kama ya legacy na migahawa ya Pepsi naisoma vizuri[emoji16]Usisahau kubonyeza alama ya kengele.
SUBSCRIBED[emoji348]