Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)

Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)

Mkuu hujui nilivyokusubiri hii story yako uimalizie

Kwanza ilikuwaje mpk ukala ban mkuu
Kwanza hata hapa nahisi nina masaa 24 ya kuwa hewani Harafu baadaye ban nyingine tena.
 
Kwanini mkuu
Nahisi makosa yatajirudia maana nipo kwenye ulinzi maalum wa mods kwa kila comment, thread na hata reaction ninayo fanya inapitiwa na mods
 
Nahisi makosa yatajirudia maana nipo kwenye ulinzi maalum wa mods kwa kila comment, thread na hata reaction ninayo fanya inapitiwa na mods
Mkuu sema hii story iendeleze basi
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!

Sehemu ya Sita

#Ilipoishia: Nilimfokea Peter kwa ukali sana na kumuambia kama haamini niko na Careen, basi ajaribu kupiga simu ya Careen ili nimthibitishie.

Peter hakuamini nilichosema na kuamua kupiga kwenye simu ya Careen ili kuthibitisha kama ni kweli nimelala nae au namzingua tu.
Alivyopiga nikapokea, nikamsikiliza kwa dakika kadhaa anavyolalama, kisha nikamjibu kwa ukali "Bro acha usumbufu watu tumelala "- Nilivyomaliza kuongea tu nikakata na kuzizima simu zote, yangu na ya Careen.

#Inaendelea:
Moyo wangu ulijawa na amani sana, nikufurahia kwa kiasi kikubwa sana nikijua kuwa leo nimefanikiwa kumlaza na presha adui yangu.
"Wamenitesa sana, na kuanzia sasa itakua zamu yao"- nilijisemea kwa nguvu huku nikitabasamu.
Na mwisho nikalala nikiwa natabasamu kubwa sana.
.
Asubuhi nilipoamka, jambo la kwanza lilikua ni kuwasha simu yangu.
Mara message ikaingia, nikaifungua nikakuta ni Hasheem amenitumia, ilikua inasema "Oya njoo chuo mara moja, nimekutana na Careen hapa anakuulizia, tumekupigia hupatikani, we jamaa chenga sana".
.
Nikajua tu wazi Careen alikuja chuo kwaajili ya kufata simu yake, nikaamka haraka na kujiandaa ili kumpelekea simu yake.
Njiani wakati naelekea nikakumbuka kitu, sikufuta kumbukumbu ya simu aliyopiga Peter, "Najua Careen atakuja kutazama watu waliompigia, halafu tatizo mimi niliipokea"- nilijisemea kimoyo moyo.
"Na itakuwaje kama atakuta messages za peter akizungumzia mimi kulala na Careen? Endapo kama ametuma pindi nilipoizima.
Ngoja niwashe na kuhakikisha kabisa."- Nilijiuliza kwa sauti ya chini.
.
Nikaichukua simu ya Careen na kuiwasha, nikaingia upande "Call logs", na kufuta kumbukumbu ya simu ya Peter kwenye "Received calls".
Nilipomaliza, nikataka kuizima lakini ghafla ikapigwa simu hapo hapo.
Ilikua ni namba iliyoseviwa "Honey ", nikajua wazi huyu atakua ndiye boyfriend wake Careen ambaye nilishawahi elezewa na Careen.
.
Sikuipokea simu yake, nikaicha iite mpaka ikate, kisha nikaenda kufuta kumbukumbu ya simu hiyo iliyoingia kwenye "Missed calls " kwa kuhofia kuwa Careen asije gundua kuwa niliwasha simu yake wakati aliniambia niizime.
Nilipomaliza kufuta nikaizima.

Nilipofika maeneo ya chuo, nikakutana na Careen ambaye alipendeza sana, nahisi aliaga kwao anaenda kanisani, tukasalimiana.

Careen: Vipi hakupiga mtu yeyote jana?? (Aliuliza huku akiiwasha simu yake).

"Hapana hajapiga mtu, niliizima tu pale pale uliponitumia message kuwa niizime" (Nilizungumza kwa kujiamini japo nilijua kuwa nilikua nadanganya).

Kupiga jicho kwa mbali nililiona gari la Peter likiwa linaingia ndani ya chuo.
Nikajua wazi ni Peter na Abdulrahman wamekuja kuhakikisha kama ni kweli nililala na Careen usiku wa jana, au labda walitaka kuja kuulizia kwa marafiki zangu kuhusu mahali napoishi ili waje kunifanyia varangati.

Nikapiga hesabu za haraka, nikagundua kuwa roho yao itawauma sana wakinikuta nimesimama na Careen, sababu itathibitisha kuwa ni kweli nililala nae jana.

Nikaona huu ndio wakati muafaka wa kuzidi kuwaumiza roho, nilitaka wasinikute nimesimama nae tu, bali wanikute hata nafanya nae jambo ambalo litawaumiza zaidi.

Nikaona wamepark gari lao, wakashuka na kuanza kupapasa macho huku na huko kutazama kama wanaweza niona mimi au hata rafiki yangu.
Wakamuona Hasheem, wakamfata na kuzungumza nae, nikamuona Hasheem akiwaelekeza mahali ambapo tulipo.

Wakaanza kuchukua hatua na kujongea maeneo ya garden ambapo niliposimama na Careen.
Nikaona huu ndo wakati muafaka wa kuanza kumsogeza Careen karibu ili watukute tunafanya kitu chochote cha kumuumiza roho.

Wazo likanijia kichwani haraka, nikaichukua simu yangu na kuweka wimbo wa Marc Anthony uitwao "I need you".

Careen alipousikia huo wimbo akaacha kuchezea simu na kuanza kuuimba.
Nikamwambia "Unaweza kuuimba, unajua na kuucheza au? "

Akanijibu "Anh mie noma sana kwenye hiyo miondoko, au nikuonyeshe?" (Akaongea huku anajichekesha).
.
Nikamuambia "Unaonaje ukicheza nikuone?? "- (Nikamtupia swali la kiuchokozi).

Careen: Mmmh hapa?? Hadharani kama hivi?"
.
Nikamjibu "Yeah tena leo jumapili unajiachia tu, hakuna watu wengi, au unataka tucheze wote? "- (Nikaongeza uchokozi).
.
Akanitazama kwa sekunde kadhaa, kisha akajibu "Unaweza? "
Nikamjibu "Ndio, njoo tucheze "- (Nikaongea huku namsogerea kwa ukaribu zaidi).

Nikamshika kiuno kwa mkono mmoja na kukisogeza karibu yangu kabisa, mkono wangu mwingine ukiwa umeshikana na mkono wake wa kushoto.

Akanitazama usoni, nami nikamtazama usoni kwa jicho la mahaba, kisha nikamkonyeza, akatabasamu na tukaanza kucheza.

Careen alionekana mjuzi sana, lakini nami sikuwa nyuma kwenye kuonyesha umaridadi wangu.
Kutokana na miguso ya ukaribu, na jinsi nyimbo ilivyo ya hisia, na aina yetu ya uchezaji ilikua yenye uchokozi mwingi.
Tulijikuta tukiongeza ukaribu zaidi na zaidi.

Kutupia jicho kwa mbele, nikamuona Peter na Abdulrahman wakiwa hatua chache mbele yetu, walibaki wakiwa wameduwaa, na niliona machungu aliyonayo Peter moyoni mwake.

Macho yake yalionekana kuvimba kuashiria kuwa hakulala, na alilia usiku kucha.
Kwavile niliona wananitazama, na Careen hajagundua kama kuna watu, ndipo nilipozidisha utundu kwa kumsogeza karibu zaidi na kupeleka lips zangu kutaka kumbusu shavuni.

Ghafla nikakatishwa na sauti ya Peter akiita "Careen".
.
Careen akastuka, sote tukageuka na kuwatazama.
Wakatusogerea karibu, Careen alijihisi aibu, lakini mimi wala sikujali.
Nilikuwa mwenye furaha sana moyoni.

Wakatusalimia, kisha Peter akamvuta Careen kwa hatua kama kumi hivi pembeni yetu.
Nikawa nimebaki na Abdulrahman ambaye alionekana akinitazama kwa jicho la hasira, lililojaa uchu wa kunipiga hata ngumi ya uso.

Akanitazama kwa hasira, kwa sauti ya chini akauliza "Ulilala nae kweli?? ".
.
Nikaona sasa wakati wa kuanza kuwatambia umefika, nikamsogerea, kisha nikacheka kwa dharau na kumuambia "Ulitaka nirecord na video ili uamini?? Siwezi kufanya ujinga huo."

Akaanza kupandisha hasira, nikamwongeza neno lingine, "Nahisi sasa ushaanza kuelewa Careen anahitaji nini maishani mwake, haitaji mwanaume tu, anahitaji mwanaume kamili aliyekamilika kama mimi, na sio Peter".

Akapandisha hasira zake na kutaka kunipiga ngumi ya uso, lakini ghafla akasita baada ya kusikia akiitwa na Careen ili wakajadili kitu pamoja na Peter.
Ikabidi azuge kama alikua anataka kunitoa sisimizi kwenye shavu.
.
Nikacheka kwa dharau, alipotaka kuanza kuondoka kuelekea kwa kina Careen, nikamuita, akasimama.
Nikamuwahi kwa nyuma na kumshika bega lake kwa dharau, huku nikimtamkia maneno ambayo yeye aliwahi nitamkia.

Nikamuambia "Kijana, hii ni mechi ya wanaume wa shoka, kuwa makini, huu mchezo hauhitaji hasira".
.
Maneno yalimgusa sana, nilimuona akikunja ngumi yake lakini hakufanya lolote zaidi akapiga hatua kuelekea mahali walipo kina Peter kwaajili ya majadiliano.

Nilisimama huku nikiwa mwenye furaha baada ya kuwanyoosha kisawa sawa, nikajisemea "Malipo hapa hapa duniani".
.
Mazungumzo yao hayakuonekana yenye kunipa wasiwasi kuendana na nyuso zao, lakini sikutaka kujihakikishia kwa nyuso tu, nilitaka kusikia japo kidogo ili kuthibitisha.
Nikatafuta sababu ya kunyanyuka na kujisogeza hatua kadhaa huku nikijifanya natafuta kijiti, nikaanza kusikia mazungumzo.
Peter alikua akijaribu kumficha Careen kuhusu sababu za kuvimba kwa macho yake, na kwanini mekundu.
.
Akamficha sana, ndipo nilipogundua kuwa sio mimi tu ambaye huwa hapendi Careen ajue hisia zangu juu yake, kumbe hata Peter hapendi kujulikana hisia zake juu ya Careen.

Nikaokota kijiti, na kujifanya nafungulia simu kisha nikarudi kupumzika kwenye benchi lililopo karibu.
Walipomaliza kuzungumza wakaja kuniaga, kwa mara ya kwanza Careen alinikombatia wakati wa kuagana.

Hii ilizidi kuwaumiza zaidi kina Peter, wakanitazama kwa jicho la chuki.
Tukaagana na wao wakaondoka kuelekea walikopark gari, nami nikarejea hostel.

Mchana Nilichat sana na Careen, na alikuwa mwenye wasiwasi sana kuhusu boyfriend wake.
Aliniambia kuwa boyfriend wake hapokei simu, wala hajibu message na anahisi ni kwasababu simu yake ilizimwa usiku kucha, ila mimi nilijua wazi kwavile sikumpokelea simu mida ile asubuhi, ndiomaana ameongeza hasira zaidi.

Majira ya saa mbili usiku, simu yangu iliita.
kutazama alikuwa ni Careen, kuipokea tu nikasikia sauti ya Careen akiwa analia.

Nikauliza "Careen nini? Mbona unalia?? "- (Niliuliza kwa hofu kubwa nikitaka kujua kwanini alikuwa analia).

Careen: Chri...chri...chris, Boyfriend wangu, ameni...(Alishindwa kumalizia na kubaki akilia sana).
.
Nikajitahidi kumbembeleza ili angalau anyamaze anieleze vizuri, hofu yangu kubwa ilikuwa huenda jambo nililofanya asubuhi ndio limeleta tatizo.

Careen Akanyamaza kidogo na kuanza kunielezea japo huku sauti inakwama kwama "Boyfriend wangu aligoma kupokea simu zangu leo kutwa nzima, wala kujibu message, nimemtumia message nyingi sana nikijaribu kumuelewesha kwanini simu yangu haikuwa hewani ".

Akagoma kidogo na kulia kwanza, kisha akaendelea
"Amenitumia sms za matusi, na bado akaniambia mimi malaya, ndiomaana jana nilizima simu usiku ili nilale na mwanaume wangu.
Nimejitetea sana, lakini akaniambia mbona asubuhi nimekupigia na hukupokea na bado ukanizimia simu".- (Akagomea hapo na kuanza kulia zaidi).

Nilistuka sana kusikia maneno hayo ya mwisho, hasa ukizingatia mimi ndiye niliyeiwasha simu asubuhi halafu sikuipokea simu ya boyfriend wake.

Careen: " Kaka Chris kwani kweli uliiwasha simu leo na yeye akapiga simu??? Au ananitafutia sababu tu ya kuniacha? "- (Aliuliza swali kwa uchungu mno, huku akiendelea kulia).
.
Niliposikia hilo swali, nilibaki nimezubaa kama sanamu nisijue nini cha kujibu.

Nikajiuliza, itakuwaje nikijibu ndio, atanichukuliaje??? Na wakati yeye anampenda sana boyfriend wake.
Na nikikataa je itakuwaje???
Nilibaki nimenyamaza nisijue nini cha kujibu, nikaamini kweli "Mbio za sakafuni, huishia ukingoni.".
Mbwembwe zangu zote zimenipeleka kubaya.

Careen akauliza tena "Nijibu kaka Chris
"

"Je Chris atajibu nini???"

Usikose sehemu ya 7
#Itaendelea......


Sehemu ya Saba soma hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!

Sehemu ya Saba

#Ilipoishia: Careen aliniuliza swali tata huku akilia kwa uchungu, aliuliza kama ni kweli niliwasha simu yake, na kama ni kweli boyfriend wake alipiga.
Nilibaki najiuliza maswali mengi sana kichwani kuwa itakuaje endapo nitajibu NDIO, na itakuaje endapo nitakataa, hasa ukizingatia kuwa Careen anampenda sana boyfriend wake.

#Inaendelea :
Nikapiga hesabu za haraka haraka, nikakumbuka kuwa tumeambiwa tuishi na wanawake kiakili.
Nikaona njia bora ni kumdanganya, sababu nikimuambia ukweli basi atazidi kunichukia.
.
Nikamjibu "Hapana, sikuiwasha kabisa simu ".
.
Akanisisitiza kwa uchungu, "Kaka Chris niambie ukweli ".
Lakini bado nilisimama kwenye jibu langu lile lile.
.
Aliniamini nilichosema huku akisisitiza kuwa huenda boyfriend wake ametafuta tu sababu ya kumuacha.
Nilibaki nimenyong'onyea nisijue cha kuongea, akashindwa kuzungumza mwisho akakata simu.
.
Nilihangaika usiku kucha kutaka kujua anaendeleaje, niliogopa asije kuchukua maamuzi mabaya sababu ya kuachwa na ampendae.
Lakini sikufanikiwa kujua liendelealo, simu yake ilikua imezimwa muda wote.
Nilijihisi mwenye makosa sana, nilijilaumu kwa ujinga wangu wa kusahau kumkabidhi simu yake siku ile kwenye gari, lakini nilijilaumu zaidi kwa ujinga wangu wa kutaka kuwaoshea kina Peter, kumbe mwisho nimekuja kusababisha maumivu kwa mwanamke ninaempenda.
.
Kutokana na mawazo niliyo nayo, sikupata usingizi kabisa, na nilishindwa kabisa kusoma notes kujiandaa kwaajili ya mtihani wa kesho chuoni.
.
Mitihani ya kujipima maarufu kama C.A.T(Continuous Assessment Test) one, ilikuwa ndiyo inaanza kwa siku ya kesho yake Jumatatu, na mtihani wetu wa kwanza ulikua ni English And mmunications Skills, utakaofanyika majira ya saa mbili asubuhi.
Sikuwa na mawazo ya mtihani wa kesho, nilikua na mawazo juu ya Careen.
.
Nilipitiwa na usingizi majira ya saa 10 alfajiri, na kujikuta nimestuka usingizini majira ya saa 2 na dakika 6 asubuhi.
Nilistuka sana, niligundua kuwa nimeshachelewa dakika 6 tangu mtihani uanze.
Nikajiandaa tu haraka haraka, hostel mpaka chuo hapana umbali sana, lakini ilibidi nichukue bodaboda ili niwahi.
.
Nikafika chuo, nikashuka kwenye bodaboda na kulipa.
Pindi nataka niingie ndani mlinzi akauliza "Kitambulisho tafadhali? "
.
Nikaanza kukitafuta kitambulisho mifukoni, nikakikosa, nikatafuta kwenye begi na bado nikakikosa.
Ndipo nikakumbuka kuwa nilikiacha kwenye mfuko wa shati nililovaa siku iliyopita niliyokuja chuo.
.
Kutazama muda, nimechelewa kama dakika 12 tayari, na siwezi ingia ndani ya chuo, wala ndani ya chumba cha mtihani bila kitambulisho.
Nikaita boda boda haraka, nikarudi hostel na kukichukua.
Nilichanganyikiwa sana, lakini nilichelewa sana.
.
Nilihojiwa maswali kadhaa kwanini nimechelewa, nikajitetea kuwa naishi mbali sana na chuo.
Nikaruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha mtihani.
Nikatupa jicho, wanafunzi wote walikua busy kasoro Careen ambaye alionekana kama ametulia tu akiwaza.
.
Nikakaa kiti kilicho kando yake, nikayatazama maswali na kugundua hayakua magumu sana, na Careen anayajua vizuri sababu tuliwahi jadili wote hizi topic.
.
Ndani ya nusu saa nzima ya mtihani, Careen alikua ameinama tu akiwa mwenye mawazo, hakuonekana kujibu lolote.
Nikagundua kuwa bado ana mawazo ya kuachwa na boyfriend wake.
Nilijua hakuna chochote ambacho angeweza fanya kwa wakati huo.
.
Nikatazama mbele, nikaona msimamizi anazungumza na mkaguzi wa ledgers, nikaona huu ndio mwanya wa kuweza kumsaidia Careen.
Nikamuita kwa sauti ya kunong'ona "Careen "
.
Akanitazama, nikamuonyeshea ishara "Vipi?? Mbona huandiki".
Akabaki amenitazama tu, nikajua hajanielewa, nikarudia ishara zile zile.
.
Ghafla nilishtushwa na sauti ya msimamizi, aliyezungumza kwa kingereza akimaanisha "Chris na Careen mnazungumza nini??".
.
Sote tukamtazama tukijua kuwa tayari tuko matatizoni, na kweli kilichofata alituletea fomu tujaze namba ya usajili, jina, na sahihi kwa kosa la kukutwa tunapiga chabo.
.
"Chabo ni kinyume na sheria na kanuni za chuo chetu, ndiomaana tunajitahidi kuhakikisha mnapata elimu bora, tumewawekea mazingira bora, vifaa vya kutosha vya kujifunzia, walimu kuingia kwa wakati kwenye vipindi na kuhakikisha kuwa wanakufundisha mpaka unaelewa.
Hebu tuambie Chris, wapi unahisi tulishindwa kukupatia elimu bora, ili tujirekebishe??? "
.
Nikamtazama msimamizi, nikashindwa kujibu sababu elimu tunayopatiwa ni ya kiwango kikubwa sana.
Lakini nilijua tatizo lilikuwa hajaelewa kwanini tulikua tunazungumza.
.
Nilizidi kuiona siku yangu mbaya, hasa ukizingatia nilizidi kumuweka Careen kwenye wakati mgumu.
Nimemkosesha boyfriend wake, na sasa nimemkosesha mtihani wake na bado anasubiri adhabu ya chuo juu ya kosa la kupiga chabo.
.
Tulitoka nje na kuelekea maeneo garden, alizidi kulia sana.
Alijumlisha machungu yote aliyonayo.
Nilijitahidi sana kumbembeleza lakini hakutulia mpaka akaja kunyamaza mwenyewe.
.
Baada ya kama masaa 3 mbele, Peter na Abdulrahman walikuja kwa pamoja na kumkuta Careen akiwa kwenye majonzi.
Peter akauliza kwa kingereza akimaanisha "Mbona unaonekana umenyongea??? Unaumwa mpendwa?? "
.
Careen: Hapana. (Akajibu huku anaanzwa kulengwa na machozi)
Ikanibidi niwaombe wasimsumbue, ili apate mapumziko.
.
Peter akanitazama kwa jicho la kunitamani japo aning'ate, lakini akanistahi tu.
Akamshika Careen na kuanza kumhoji taratibu, Careen alianza kuficha ficha mambo, lakini baadae alijikuta akianza kufunguka.
Hofu yangu ilizidi, nilikua nawaza litakalo fata hasa akianza kugusia juu ya story ya simu.
.
Careen: Boyfriend wangu ameniacha.
.
Peter akajibu "Sikuwahi kuwaza kama una boyfriend, na kwanini amekuacha.??."
.
Kila maneno waliyozidi kuzungumza, yalizidi kunipa hofu, nikaropoka tena nikimtaka Peter aache kumsumbua Careen kwa maswali.
.
Careen akaniambia nisijali, akaanza kuelezea jinsi boyfriend wake alivyomnyamazia siku nzima, na jinsi alivyoanza kumtusi na maneno aliyomuambia.
Mwisho akamaliza "Anasema mimi nimelala kwa mwanaume mwingine na simu sijampokelea".
.
Peter na Abdulrahman wakastuka, nami pia nikastuka sababu nilijua kuwa kinachofata ni majanga kwangu.
Nikawaambia kina Peter ''Inatosha, mwacheni apumzike "

Peter akamtazama Abdulrahman, Peter akaropoka "Kwani juzi jumamosi ulilala wapi??? Na kwanini ulizima simu?? "
.
Hapo ndipo presha ilipozidi kunipanda na kutamani ardhi ipasuke niingie.
Careen akajibu "Nililala nyumbani, na simu niliisahau kwa Chris pindi nilipokuwa kwenye gari "

Peter na Abdulrahman wakaguna kwa nguvu huku wakitazamana, lakini mimi nilikua nahisi nafsi inataka kupasuka nife hapo hapo.
.
Peter akachukua simu yake, na kumuonyesha Careen kumbukumbu za simu alizopiga na kupokelewa, Careen alikuta namba yake nayo ipo kwenye list.
Careen akanitazama kwa mshangao, akarudisha macho kwa Peter.
Abdulrahman akaongeza "Na Chris alisema tusiwasumbue, umelala nae, chumbani kwake, kifuani kwake "- (Alizungumza kwa msisitizo).
.
Peter akaongeza, "Na nadhani, Chris aliiwasha simu yako asubuhi, na hakuipokea simu ya boyfriend wako".
.
Careen aligeuka na kunitazama kwa hasira, nahisi alitamani hata kuninyonga, machozi yalimjaa machoni mwake.
Uso ulinijaa aibu, lakini hofu kubwa ilinizidi.

Nilijua leo ndio nampoteza Careen, nikageuka na kuwatazama, kwajinsi walivyokuwa wakiniangalia, nilitamani hata ningekimbia, au hata ningerudisha muda nyuma ili niyafute makosa yangu yote.

Careen alinitazama kwa hasira, kisha akazungumza maneno yaliyo nifanya nihisi moyo unataka kunitoka
.
.
Je Careen alizungumza maneno gani!!??? Chris atafanya nini???

Usikose sehemu ya 8
#Itaendelea


Sehemu ya Nane soma hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!

Sehemu ya Saba

#Ilipoishia: Careen aliniuliza swali tata huku akilia kwa uchungu, aliuliza kama ni kweli niliwasha simu yake, na kama ni kweli boyfriend wake alipiga.
Nilibaki najiuliza maswali mengi sana kichwani kuwa itakuaje endapo nitajibu NDIO, na itakuaje endapo nitakataa, hasa ukizingatia kuwa Careen anampenda sana boyfriend wake.

#Inaendelea :
Nikapiga hesabu za haraka haraka, nikakumbuka kuwa tumeambiwa tuishi na wanawake kiakili.
Nikaona njia bora ni kumdanganya, sababu nikimuambia ukweli basi atazidi kunichukia.
.
Nikamjibu "Hapana, sikuiwasha kabisa simu ".
.
Akanisisitiza kwa uchungu, "Kaka Chris niambie ukweli ".
Lakini bado nilisimama kwenye jibu langu lile lile.
.
Aliniamini nilichosema huku akisisitiza kuwa huenda boyfriend wake ametafuta tu sababu ya kumuacha.
Nilibaki nimenyong'onyea nisijue cha kuongea, akashindwa kuzungumza mwisho akakata simu.
.
Nilihangaika usiku kucha kutaka kujua anaendeleaje, niliogopa asije kuchukua maamuzi mabaya sababu ya kuachwa na ampendae.
Lakini sikufanikiwa kujua liendelealo, simu yake ilikua imezimwa muda wote.
Nilijihisi mwenye makosa sana, nilijilaumu kwa ujinga wangu wa kusahau kumkabidhi simu yake siku ile kwenye gari, lakini nilijilaumu zaidi kwa ujinga wangu wa kutaka kuwaoshea kina Peter, kumbe mwisho nimekuja kusababisha maumivu kwa mwanamke ninaempenda.
.
Kutokana na mawazo niliyo nayo, sikupata usingizi kabisa, na nilishindwa kabisa kusoma notes kujiandaa kwaajili ya mtihani wa kesho chuoni.
.
Mitihani ya kujipima maarufu kama C.A.T(Continuous Assessment Test) one, ilikuwa ndiyo inaanza kwa siku ya kesho yake Jumatatu, na mtihani wetu wa kwanza ulikua ni English And mmunications Skills, utakaofanyika majira ya saa mbili asubuhi.
Sikuwa na mawazo ya mtihani wa kesho, nilikua na mawazo juu ya Careen.
.
Nilipitiwa na usingizi majira ya saa 10 alfajiri, na kujikuta nimestuka usingizini majira ya saa 2 na dakika 6 asubuhi.
Nilistuka sana, niligundua kuwa nimeshachelewa dakika 6 tangu mtihani uanze.
Nikajiandaa tu haraka haraka, hostel mpaka chuo hapana umbali sana, lakini ilibidi nichukue bodaboda ili niwahi.
.
Nikafika chuo, nikashuka kwenye bodaboda na kulipa.
Pindi nataka niingie ndani mlinzi akauliza "Kitambulisho tafadhali? "
.
Nikaanza kukitafuta kitambulisho mifukoni, nikakikosa, nikatafuta kwenye begi na bado nikakikosa.
Ndipo nikakumbuka kuwa nilikiacha kwenye mfuko wa shati nililovaa siku iliyopita niliyokuja chuo.
.
Kutazama muda, nimechelewa kama dakika 12 tayari, na siwezi ingia ndani ya chuo, wala ndani ya chumba cha mtihani bila kitambulisho.
Nikaita boda boda haraka, nikarudi hostel na kukichukua.
Nilichanganyikiwa sana, lakini nilichelewa sana.
.
Nilihojiwa maswali kadhaa kwanini nimechelewa, nikajitetea kuwa naishi mbali sana na chuo.
Nikaruhusiwa kuingia ndani ya chumba cha mtihani.
Nikatupa jicho, wanafunzi wote walikua busy kasoro Careen ambaye alionekana kama ametulia tu akiwaza.
.
Nikakaa kiti kilicho kando yake, nikayatazama maswali na kugundua hayakua magumu sana, na Careen anayajua vizuri sababu tuliwahi jadili wote hizi topic.
.
Ndani ya nusu saa nzima ya mtihani, Careen alikua ameinama tu akiwa mwenye mawazo, hakuonekana kujibu lolote.
Nikagundua kuwa bado ana mawazo ya kuachwa na boyfriend wake.
Nilijua hakuna chochote ambacho angeweza fanya kwa wakati huo.
.
Nikatazama mbele, nikaona msimamizi anazungumza na mkaguzi wa ledgers, nikaona huu ndio mwanya wa kuweza kumsaidia Careen.
Nikamuita kwa sauti ya kunong'ona "Careen "
.
Akanitazama, nikamuonyeshea ishara "Vipi?? Mbona huandiki".
Akabaki amenitazama tu, nikajua hajanielewa, nikarudia ishara zile zile.
.
Ghafla nilishtushwa na sauti ya msimamizi, aliyezungumza kwa kingereza akimaanisha "Chris na Careen mnazungumza nini??".
.
Sote tukamtazama tukijua kuwa tayari tuko matatizoni, na kweli kilichofata alituletea fomu tujaze namba ya usajili, jina, na sahihi kwa kosa la kukutwa tunapiga chabo.
.
"Chabo ni kinyume na sheria na kanuni za chuo chetu, ndiomaana tunajitahidi kuhakikisha mnapata elimu bora, tumewawekea mazingira bora, vifaa vya kutosha vya kujifunzia, walimu kuingia kwa wakati kwenye vipindi na kuhakikisha kuwa wanakufundisha mpaka unaelewa.
Hebu tuambie Chris, wapi unahisi tulishindwa kukupatia elimu bora, ili tujirekebishe??? "
.
Nikamtazama msimamizi, nikashindwa kujibu sababu elimu tunayopatiwa ni ya kiwango kikubwa sana.
Lakini nilijua tatizo lilikuwa hajaelewa kwanini tulikua tunazungumza.
.
Nilizidi kuiona siku yangu mbaya, hasa ukizingatia nilizidi kumuweka Careen kwenye wakati mgumu.
Nimemkosesha boyfriend wake, na sasa nimemkosesha mtihani wake na bado anasubiri adhabu ya chuo juu ya kosa la kupiga chabo.
.
Tulitoka nje na kuelekea maeneo garden, alizidi kulia sana.
Alijumlisha machungu yote aliyonayo.
Nilijitahidi sana kumbembeleza lakini hakutulia mpaka akaja kunyamaza mwenyewe.
.
Baada ya kama masaa 3 mbele, Peter na Abdulrahman walikuja kwa pamoja na kumkuta Careen akiwa kwenye majonzi.
Peter akauliza kwa kingereza akimaanisha "Mbona unaonekana umenyongea??? Unaumwa mpendwa?? "
.
Careen: Hapana. (Akajibu huku anaanzwa kulengwa na machozi)
Ikanibidi niwaombe wasimsumbue, ili apate mapumziko.
.
Peter akanitazama kwa jicho la kunitamani japo aning'ate, lakini akanistahi tu.
Akamshika Careen na kuanza kumhoji taratibu, Careen alianza kuficha ficha mambo, lakini baadae alijikuta akianza kufunguka.
Hofu yangu ilizidi, nilikua nawaza litakalo fata hasa akianza kugusia juu ya story ya simu.
.
Careen: Boyfriend wangu ameniacha.
.
Peter akajibu "Sikuwahi kuwaza kama una boyfriend, na kwanini amekuacha.??."
.
Kila maneno waliyozidi kuzungumza, yalizidi kunipa hofu, nikaropoka tena nikimtaka Peter aache kumsumbua Careen kwa maswali.
.
Careen akaniambia nisijali, akaanza kuelezea jinsi boyfriend wake alivyomnyamazia siku nzima, na jinsi alivyoanza kumtusi na maneno aliyomuambia.
Mwisho akamaliza "Anasema mimi nimelala kwa mwanaume mwingine na simu sijampokelea".
.
Peter na Abdulrahman wakastuka, nami pia nikastuka sababu nilijua kuwa kinachofata ni majanga kwangu.
Nikawaambia kina Peter ''Inatosha, mwacheni apumzike "

Peter akamtazama Abdulrahman, Peter akaropoka "Kwani juzi jumamosi ulilala wapi??? Na kwanini ulizima simu?? "
.
Hapo ndipo presha ilipozidi kunipanda na kutamani ardhi ipasuke niingie.
Careen akajibu "Nililala nyumbani, na simu niliisahau kwa Chris pindi nilipokuwa kwenye gari "

Peter na Abdulrahman wakaguna kwa nguvu huku wakitazamana, lakini mimi nilikua nahisi nafsi inataka kupasuka nife hapo hapo.
.
Peter akachukua simu yake, na kumuonyesha Careen kumbukumbu za simu alizopiga na kupokelewa, Careen alikuta namba yake nayo ipo kwenye list.
Careen akanitazama kwa mshangao, akarudisha macho kwa Peter.
Abdulrahman akaongeza "Na Chris alisema tusiwasumbue, umelala nae, chumbani kwake, kifuani kwake "- (Alizungumza kwa msisitizo).
.
Peter akaongeza, "Na nadhani, Chris aliiwasha simu yako asubuhi, na hakuipokea simu ya boyfriend wako".
.
Careen aligeuka na kunitazama kwa hasira, nahisi alitamani hata kuninyonga, machozi yalimjaa machoni mwake.
Uso ulinijaa aibu, lakini hofu kubwa ilinizidi.

Nilijua leo ndio nampoteza Careen, nikageuka na kuwatazama, kwajinsi walivyokuwa wakiniangalia, nilitamani hata ningekimbia, au hata ningerudisha muda nyuma ili niyafute makosa yangu yote.

Careen alinitazama kwa hasira, kisha akazungumza maneno yaliyo nifanya nihisi moyo unataka kunitoka
.
.
Je Careen alizungumza maneno gani!!??? Chris atafanya nini???

Usikose sehemu ya 8
#Itaendelea
Subscribed
 
Usisahau kubonyeza alama ya kengele.
SUBSCRIBED[emoji348]
Mkuu Safi Sana Kwa story na nimepata shauku ya kuendelea kuifatilia coz niliwahi ishi maeneo karibu na chuo cha Kampala...so maeneo kama ya legacy na migahawa ya Pepsi naisoma vizuri[emoji16]
 
Back
Top Bottom