MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!
Sehemu ya Kumi na Tano...
.
#
Ilipoishia: Baada ya purukushani za hapa na pale kati yangu na Magdalena ndipo mumewe alipotukuta na mawazo yake yakamfanya ahisi kuwa tulikua katika dimbwi zito la mapenzi kuendana na jinsi alivyotukuta.
.
Alifoka kwa nguvu kwa kingereza akimaanisha "Unafanya mapenzi na mgeni??? Tena hadharani???" - (Aliuliza kwa hasira sana huku akitutazama).
.
Nilistuka sana nikijua tayari msala mwingine umeshanikuta, kutazama pembeni ndipo nilipowaona Careen na Abdulrahman wakiwa nao wametoka chumbani kwa Peter baada ya kusikia kelele.
Nyuma yangu nako ilisikika sauti nzito iliyojawa hasira, "What?? "
.
Kutazama nyuma sauti inakotoka, ilikua ni baba yake Peter akija na mama yake Peter.
Hapo ndipo nilipotamani dunia ipasuke nidumbukie labda ningeweza kuuepuka msala huu.
Nilizidi kujilaumu kwa maamuzi yangu mabovu kila wakati, nilizidi kuziona athari za kuendeshwa kihisia, sababu nimekua mtumwa kwa Careen na sasa matatizo yote haya yananikumba kwasababu yake.
Nashindwa kuwa na maamuzi binafsi na matumizi mazuri ya ubongo, yote kwasababu yake.
#
Inaendelea:
Mumewe Magdalena alipandwa na hasira sana, hakutaka kunilazia damu, akanirukia na kunitwanga ngumi ya shavu.
Akaniongeza makonde lakini ilibidi niweke gadi ya mikono ili yasinipate usoni.
Wakati huo huo Abdulrahman na Magdalena walimuwahi na kujaribu kumzuia.
Tukawa ndani ya vuta nikuvute, Careen nae akaja kuongeza nguvu.
.
Baba Peter alikua na hasira, wala hakuja kutoa msaada, alikuja haraka na kuanza kunipiga mateke huku akifoka kwa kingereza, alimaanisha
"Umekuja kuharibu amani ya nyumba yangu".
.
Ikabidi mama Peter na Magdalena wapambane kumzuia baba Peter, na Careen na Abdulrahman wapambane kumnyofoa mumewe Magdalena.
.
Baada ya purukushani wote walifanikiwa kushikwa vizuri, Careen akamuachia mumewe Magdalena na kuja upande wangu.
.
Nilitamani upenyo nilioupata niutumie kukimbia, lakini nikahisi kuwa nikikimbia watahisi kuwa ni kweli.
Nikabaki naomba Mungu tu.
.
Mabishano yakawa yanaendelea kwa lugha ya kingereza yakiwa na maana ifuatayo:
Magdalena akaongea kwa nguvu akijaribu kumuelewesha mumewe "Unachohisi sicho, wala sikuwa nafanya nae ulichokuwa ukidhani".
.
Mumewe kwa hasira akajibu "Nachohisi sicho?!! Mikono yake ilikua inakushika nini??! Na wewe ulimshika nini? Na mlikua mnakombatiana kombatiana, unadhani mimi ni mjinga?? " - (Alizungumza kwa hasira kama mtu aliyetamani kumrukia mkewe).
.
"Haukuelewa kilicho kuwa kinaendelea, nilikua nimembana anieleze ukweli kuhusu Peter, hakutaka kuniambia, ndomana tukawa tunakunjana, hukuona shati yake nimekata vifungo??" - Alizungumza Magdalena kwa ukali huku kama anataka kulia.
.
Baba yake Peter akadakia "Hivyo vifungo vimekatika sasa hivi hapa" - (Akazungumza kwa kukanusha kauli ya Magdalena).
.
Sikutaka kuchelewa nami nikatetea "Vilikatwa na Magdalena "
Ghafla nikazimwa "Nyamaza mwana haramu mkubwa" - (Alikua ni mama yake Peter aliyetoa sauti ya ukali).
.
"Ni kweli mama, vilikatwa tangu mwanzo" - (Abdulrahman nae akatetea upande wa Magdalena).
.
"Havikukatwa kwa ugomvi, wamevikata kwenye mahaba, nimeshuhudia kwa macho yangu mawili" - (Alizungumza mumewe Magdalena).
.
Akataka kuruka ili amfate mkewe amshindilie japo makofi ya uso, lakini Abdulrahman alisimama vizuri kumzuia.
.
"Kama ni kweli mlikua mnagombana. Ulikua unamuuliza kuhusu Peter ili iweje? " - (Aliuliza Mama Peter).
.
Magdalena akamtazama mama yake, na kuamua kutoboa siri kuwa Peter alizimia baada ya kupokea message na picha kutoka kwa Chris.
.
''Kuna uwezekano Chris anajua kila kitu kuhusu Peter, na kuna siri kubwa kati ya Chris na Peter.
Na nilimbana ili anieleze, lakini hakuniambia chochote ndiomaana tukabaki tukigombana" - (Alimaliza kama hivyo Magdalena, kisha kuchukua simu ya Peter, na kufungua message niliyomtumia Peter na kumuonyesha mama yake, na mama yake akamuonyesha baba yake.
.
Kipindi hicho chote nilikua nimebaki kama msukule, sikujua nini cha kufanya, kila sekunde zilivyozidi kwenda nilizidi kutamani hata ningekua na mabawa nipeperuke, au hata ningekua mchawi niyeyuke.
Lakini haikuwezekana, kutazama mlango wa kutokea ulipo, ulikua umerudishiwa, nikapiga hesabu za haraka haraka kutoka niliposimama mpaka mlango wa kutokea, na kutoka mlangoni mpaka geti la fensi, nikaona hii ndio chance ya kutokea.
.
Nikapata akili ya haraka kuwa nikimbie, sababu hata nikibaki bado nitapata shida ya kuingizwa kwenye kesi ya kumsababishia Peter matatizo.
Nikahesabu kimoyo moyo, 1, 2, 3, lakini nikasita baada ya kukumbuka kuwa nisingeweza kupita getini wala nisingeweza kuruka ukuta kwajinsi ulivyo mrefu.
Nikabaki nimesimama pale pale huku nikisubiri kama mfungwa anaye ngojea msamaha wa Rais.
.
Wakahoji mengi sana kuhusu message zangu kwenye simu ya Peter, lakini niligoma kueleza chochote na kusema kuwa "Peter ni rafiki yangu, na Careen ni rafiki yangu, ndio maana nilimtumia Peter picha ya birthday ya Careen na ndio maana nikamwambia "I wish ungekuepo" sababu hakuwepo."
.
Careen alistuka baada ya kusikia nimemtumia picha Peter.
Lakini Magdalena akawa tayari ameshapata jambo.
.
Akasema "Kama nyinyi ni marafiki, kwanini wewe uliandaa party kwaajili ya Careen, na Peter aliandaa kwaajili ya Careen???!!! Kwanini hamkuandaa wote kwa pamoja.
Na iweje Peter azimie baada ya kuona picha uliyo mtumia.??"
.
Nilishindwa kujibu lolote, nilihisi kuna kitu Magdalena anajaribu kuchimba.
.
Hapo ndipo Careen alipo gundua kuwa kumbe Peter alimuambia aende Kiota kwaajili ya kumfanyia surprise.
.
Baba yake Peter akamtazama Abdulrahman na kumuuliza swali, "Chris na Peter ni marafiki??? "
.
Abdulrahman akajibu "Ndio".
.
Mama yake Peter akasema "Nadhani majibu ya maswali yetu kichwani, yako kinywani mwa Peter
Na hatuwezi kumuuliza chochote Peter kwasasa mpaka presha yake itakapo kaa sawa".
.
Sote tukatazamana, nikaanza kupata mwanga mwa matumaini, nikajua wazi kuwa sasa naweza kutoka salama.
.
Baba yake akanitazama na kunikazia macho, akasema "Uko huru leo, ila tambua lolote tutakalojibiwa na Peter, ndilo litakalofanya uwe huru zaidi au laanh".
.
Nilinywea sana ila nikaona afadhali, nilishukuru Mungu sana.
Abdulrahman akaniambia tuondoke, Careen akawa tayari na tukaanza kuondoka.
Ghafla mumewe Magdalena akaniita, nilipomgeukia akanisogerea na kuniambia "Usidhani umeponyeka, ukweli ukijulikana ndio nitajua cha kukufanya. Hizi sababu bado hazijanifanya niamini kuwa hauna mahusiano na mke wangu".
.
Nilibaki nikimuangalia tu, Abdulrahman akamfokea "Michael inatosha".
.
Nikageuka na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye gari la Abdulrahman.
Tulipanda na kuondoka, njia nzima tulikua mabubu na wala hakuna aliyemsemesha mwenzie.
Tulimshusha Careen Tabata, nami nikaletwa mpaka Hostel.
.
Pindi nataka kushuka kwenye gari, Abdulrahman akaniambia "Subiri Chris".
.
Akazungumza huku akichukua simu yake na kufungua Gallery, na kunionyesha picha ya msichana na kiNigeria.
.
Niliitazama ile picha na kumuona msichana mzuri tu.
Nikamtazama Abdulrahman, kiukweli sikuwa kwenye mood ya kuzungumza chochote.
Abdulrahman akaniambia ''Chris usijutie ulichotenda jana na rafiki zako, na hata kilichotendeka leo nyumbani kwa kina Peter".
.
Nikamtazama usoni kwa makini, nilihisi labda anataka kunipa moyo tu kwa maneno matamu, lakini nilitamani kumuuliza swali kuhusu picha ya msichana wa kiNigeria niliyeonyeshwa.
.
Akaniambia "Japo umepitia magumu, ila naona dalili zako za ushindi zinakaribia.
Sababu wazazi wa Peter wakishajua kuhusu jambo linalo endelea kati ya Peter na Careen. Basi jua kuwa mchezo umeshaushinda.".
.
.
Maneno yake yaliniachia maswali kichwani, nikawa bado natafakari, akaniambia "Na usidhani Magdalena anakuchukia, wala hakuchukii, Anataka kuujua ukweli kama Careen na Peter wana mahusiano au vipi.
Na hata alivyo alikwa kwenye party, alikuwa akihoji maswali mengi kuhusu Careen na Peter, na kuna sababu kwanini anahoji''.
.
Nilianza kupata shauku ya kutaka kujua kwanini Abdulrahman anayasema yote hayo, ikabidi nimwambie "Sijakuelewa bado, hebu nieleze vizuri"
.
Akaniambia "Peter anampenda Careen, lakini....wazazi wake Peter wa...wa...." - (Akakwamia hapo).
.
Nikapata shauku ya kutaka kujua wazazi wake Peter "Wa" wamefanyaje.?!
Nikarudia alikomwamia "Wa..???"
.
Akanipa jibu ambalo lilinifanya nisiamini masikio yangu, nilipata furaha ya ghafla, na kutamani hata niruke ruke ndani ya gari.
Je Chris amepewa jibu gani!??! Na hiyo picha ni ya nani!?? Na Magdalena ana sababu zipi za udadisi wake???
Usikose sehemu ya 16
#Itaendelea
Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)