Mkuu Safi Sana Kwa story na nimepata shauku ya kuendelea kuifatilia coz niliwahi ishi maeneo karibu na chuo cha Kampala...so maeneo kama ya legacy na migahawa ya Pepsi naisoma vizuri[emoji16]
#Ilipoishia: Careen alinitazama kwa hasira sana baada ya kupewa ukweli kuwa mimi ndiye niliyefanya boyfriend wake amuache, na bado nilijibu uongo kuwa sikuhusika.
Lakini pia nimempakazia kashfa kwa Peter kuwa nililala nae.
Alikasirika, alinitazama utadhani anataka kunivamia.
Nilibaki nimenyongea nisijue nini cha kujitetea.
Ndipo akanyanyua kinywa chake na kuzungumza kwa hasira.
**************
#Inaendelea: Careen: Nilikuheshimu sana, nikakuthamini na kukufanya kama rafiki chaguo la kwanza kwangu, nikaona haitoshi, nikakufanya kama ndugu wangu wa damu."
Akalia kwa uchungu kisha kuendelea tena "Chris siamini kama ni wewe ndiye uliyenifanyia haya yote...!!! Rafiki yangu wa dhati, kumbe ndiye mbaya kwangu.
Nilikueleza zima simu kwasababu fulani, lakini ukaona njia pekee ya kuniharibia ni kwa kuiacha on.
Na ukaona haitoshi, ukaamua kunipakazia"
Nilibaki nimeinamisha kichwa chini, aibu ilinijaa, nilitamani hata kukimbia lakini miguu ilikosa nguvu kabisa.
.
Nikamjibu "Careen, ni bahati mbaya tu, wala sikunuia kufanya yote hayo ".
Akanitazama kwa hasira zaidi, akafuta machozi kwa mkono wa kushoto, na kupandisha mafua yatokanayo na kulia.
Akanijibu "Bahati mbaya?? Kunipakazia nayo bahati mbaya??? Kuiwasha simu bahati mbaya???
Ulinidharirisha pale mgahawani Legacy, nayo ni bahati mbaya!??? Nilidhani yale maneno yalikutoka kwaajili ya hasira, kumbe Chris una lako una lako unalolitaka, nakuchukia kuanzia sasa "
.
Peter akasogea karibu na kumshika bega, Abdulrahman akachukua bag lake, wakimsisitiza waondoke waniache.
Careen akaniangalia kwa mara ya mwisho, na kusema "Naomba kuanzia leo, usinijue, nami sikujui, tusijuane, sitaki wanafki kwenye maisha yangu"- (Akazungumza kisha akasonya na kuanza kuondoka huku akiwa ameshikwa bega na Peter) .
.
Maneno yalinigusa sana, nilijihisi mkosaji, nilivyosikia tu ameanza kupiga hatua kuondoka ndipo nikapata nguvu ya ghafla na kunyanyuka kumfata kwa nyuma japo nimuombe msamaha.
Lakini Abdulrahman aliniekea mwili.
Na kwajinsi nilivyo kimbao mbao, Abdulrahman mwili nyumba, basi nilijikuta kama nimesombwa na fuso.
.
Nikadondoka chini, nikabaki nawatazama wanavyopotea mbele ya mboni ya macho yangu.
Tangia hapo ndipo ukawa mwisho wa urafiki wangu na Careen, nilijilaumu kwa mengi sana, niliumia sana.
Njiani tulikua tukipishana kama magari, tambo za kina Peter zilizidi na zilizidi kuniumiza zaidi.
.
Nakumbuka mitihani yangu ya CAT one sikuweza kuifanya vizuri kutokana na mawazo niliyo nayo, niliitwa kuhojiwa kuhusu maendeleo yangu, lakini pia nilihojiwa juu ya kesi yangu ya kupiga chabo, nikajitetea vya kutosha.
Nikapewa adhabu ya kufutiwa matokeo ya mtihani niliopiga chabo.
.
Kuna nyakati nilijitahidi kumtumia messages za kumuomba msamaha Careen, lakini hakuzijibu, simu hakupokea, njiani wala hakuwa na muda wa kunisikiliza.
.
Mwezi mmoja ulipita nikiwa mbali na Careen, nilirudisha majeshi upande wa kina Hasheem na Ramadhan, na nikabahatika kupata rafiki wapya wawili, mmoja wa kiTanzania aitwae Nasra, na mwingine wa Zambia aitwae Ivan.
.
Angalau walijitahidi kurudisha furaha yangu, walinifanya niamini kuwa "Sio kila mtu huja kwenye maisha yako ili kuwa nawe milele, wengine huja kwa muda mfupi tu ili kukupa funzo fulani".
Nami niliaamini Careen alikuja kunipa funzo kubwa sana.
Nasra alijitahidi kunisahaulisha maumivu yangu juu ya Careen, lakini alishindwa jambo moja tu "Kunifanya niache kumpenda Careen".
.
Siku moja maeneo ya nje ya geti za chuo, palisimama vijana kadhaa waliokuwa wakitoa vipeperushi kuhusiana na semina ya mahusiano kwa vijana kuhusu "Njia za kuepuka mateso ya hisia", semina itakayo fanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, siku ya Jumamosi, mchana.
.
Kwavile Nasra alijua kuwa napitia mateso ya kihisia juu ya Careen, basi alinialika twende wote labda naweza jifunza kitu kipya.
.
Mapema siku hiyo, majira ya saa 4 nikawahi na kukutana na Nasra katika ukumbi huo.
Na semina ikaanza, lilikua ni somo kuhusiana na "Jinsi ya kupambana na maumivu ya kutendwa "
.
Mwalimu wa siku hiyo alikua ni Dkt Leonard, na alikuwa akiendelea kutoa mafunzo, mada zake ziliwagusa watu wengi ndani ya ukumbi huo.
Nilimtazama Nasra ambaye alionekana yuko makini zaidi.
Nikarusha macho yangu pande zote na kuona jinsi watu walivyo busy kusikiliza kinachozungumzwa.
Lakini ghafla macho yangu yalikumbana uso kwa uso na macho ya Careen ambaye nae alinitazama na kugeuzia shingo mbele.
Nikatupa jicho pembeni yake, nikamuona Peter akiwa makini pia akifatilia mafunzo.
.
Nikajiuliza "Hadi nyinyi mpo?"
Lakini nilijua kuwepo kwao kwenye ukumbi mmoja na mimi kusingeleta mabadiliko yoyote yale, sababu tayari hawana muda wa hata kuongea na mimi.
.
Mwalimu wa mahusiano akazungumza jambo "Wengi wetu tunachukulia kuachwa kama adhabu ya kifo, kwamba ukiachwa hautakuja kupendwa tena.
Ngoja nikwambie kitu, kuna nyakati unaachwa ili uwe imara, ili umpate aliye bora zaidi yake, ili umpate aliyeumbwa kwaajili yako.
Achana na tabia ya kujiona kama una nuksi, huna thamani, hutopata mwingine...hizo ni fikra potofu.
Acha kujichukia, acha kuyachukia mapenzi, unapoachwa basi lia unavyoweza lakini mwisho wake jifute machozi na useme sitorudi nyuma kamwe maana nishapata funzo jipya juu ya mapenzi, nishapata nafasi mpya ya kumpata aliyeumbwa kwaajili yangu.
Be positive ".
.
Akakwama hapo na kututazama wasikilizaji wake, akaendelea "Kuna mtu unaweza ukajitoa kwake kwa kila kitu, ukaonyesha kumpenda, ukawa umewekeza muda wako, nguvu zako, pesa zako, na kila kitu ulichonacho kwaajili yake, lakini kwavile yeye ni limbukeni wa kupendwa basi akaanza kuzitesa hisia zako, akihisi kuwa huwezi ishi bila yeye kwahiyo anakufanya vile atakavyo."
Nilihema kwa nguvu, mada inanipa funzo kubwa sana.
Akaendelea "Mwingine anaingia kwenye mahusiano na wewe labda sababu ya upweke wake, au kwa tamaa zake za kimwili, mali zako.. kwakifupi haingii kwenye mahusiano na wewe sababu ya upendo wake kwako, no.
Sababu ya kile anachotaka kwako, akikipata tu basi huwa haoni sababu ya kuwa na wewe tena. Huanza kuleta visa mbalimbali, atakutesa, atakusaliti, atakutafutia visababu mbalimbali vya kukuacha, lakini kwavile wewe unampenda kwa dhati, unajikuta huwezi kumuacha, unateseka kila kukicha kwaajili yake".
.
"Wewe ni wathamani sana, huna haja ya kung'ang'ania unapoumizwa kila kukicha, usipopendeka.
Akitafuta sababu ya kukuacha, shukuru Mungu kwa kukuondolea uozo maishani mwako"
.
"Kuna nyakati Mungu anaweza mleta mtu yeyote yule ili aharibu mahusiano yako, ukaanza kumchukia mtu aliyeharibu, kumbe sio kosa lake, ametumika kuondoa nuksi kwenye maisha yako, na kuleta baraka kwako.
Iwe ni mchepuko wake, au wazazi, ndugu, rafiki, iwe ni yeyote yule ambaye ameharibu mahusiano yako na mtu ambaye hakupendi, anakutesa, anakusaliti, anakupiga, anakutafutia visababu vya kukuacha, hana malengo na wewe" mshukuru sana huyo mtu aliyeyaharibu."- Niliposikia maneno hayo nilijikuta napiga makofi sana baada ya kuona mada imegusa mahala husika.
Mwalimu aliendelea na somo, na lilipoisha sote tulitoka nje ya ukumbi.
Nilimvuta Nasra ili tusogee kwa mbele kidogo, tutoke kwenye msongamano wa watu.
Lakin ghafla nilisikia sauti ya mtu ikiniita.
Nilistushwa na sauti hiyo, ilikua ni ya mtu ninaye mfahamu, nikasimama na wala sikugeuke nyuma, shida yangu ilikua nisikilize kama ni kweli naitwa au masikio yananiletea maigizo.
Sikusikia tena, nikajua nimejidanganya tu, nikaanza kutembea tena.
Nikasikia naitwa tena "Chrisss" "Chriss".
Hapo ndipo nikagundua ni kweli naitwa, nikapata hamu ya haraka ya kugeuka nyuma ili kuthibitisha kwa macho yangu mwenyewe.
Kugeuka na kutazama, sikuamini macho yangu, nilibaki nimepigwa na bumbuwazi huku nafsi ikijiuliza maswali mengi.
Ananiita mimi kweli au anatania??? Au anataka anidharilishe mbele za watu??? Anataka kunieleza nini?! .
Je Chris anaitwa na nani?? Na kwanini??? Nini kitatokea.
#Ilipoishia: Nilisikia kama naitwa, sauti ya mtu ninaemfahamu, lakini sikuamini masikio yangu nikahisi kama yananidanganya, nikaanza kuchukua hatua kuelekea mbele.
.
Mara nikaitwa tena, "Chris, chris " hapo ndipo nikagundua kuwa sikua najidanganya, ni kweli nilikua naitwa.
Kutokana na sauti ya muitaji, nilipata shauku kubwa kutaka kuthibitisha kama ni kweli mwenyewe.
Nikageuza shingo haraka, kutupa macho mbele yangu nilimuona Careen ambaye alionekana anatembea mwendo wa haraka kuniwahi mahala nilipo.
.
#Inaendelea: Sikuamini kama ni kweli leo, baada ya mwezi, nakuja kuitwa na mrembo Careen.
Nilihisi kama naota, nikapata shauku ya kutaka kujua anataka kuniambia nini leo.
.
Lakini mawazo ya ajabu yakanijia akilini, kuwa huenda anataka kunifanyia jambo la udharilishaji mbele za watu.
Nikajiandaa kisaikolojia kwa lolote lile litakalo tokea.
.
Nasra akajisogeza kwa pembeni ili kuacha nafasi Careen akifika niweze kuongea nae.
Alipofika Careen, akanisalimia.
.
Careen: Hi - (Alitoa salam kama mtu asiyejiamini hivi, nahisi labda alidhani nisingeitikia).
.
Nikamjibu "Hi" na wala sikutaka kuongeza neno lolote ili kumwacha aingie moja kwa moja kwenye alichotaka kusema.
.
Akaanza "Najua unashangaa kwanini leo aliyekuambia sikujui na usinijue, ndiye anayekuita leo." - (Akazungumza kwa kujihami mapema).
.
Sikutaka kuonyesha udhaifu wangu, ikabidi nionyeshe uanaume wangu.
Nikamjibu "Bado najiuliza hata jina langu umelijuaje??? Tulishawahi onana mahali? ". (Nikazungumza kwa kujiamini, na kumkazia macho).
.
Kauli ilimgusa sana, akainamisha kichwa chini kwa aibu huku akitafakari cha kunijibu.
Ikabidi nimuongeze mzinga "Dada sema ulichoniitia, rafiki yangu ananisubiria".
.
Nilizungumza maneno ya kujiamini huku nikijua kuwa nafsi yangu inaumia, nilitamani hata kumkombatia nimshukuru hata kwa kuniita jina leo.
Lakini sikutaka kuonyesha udhaifu wangu kwake, nilitaka nimuonyeshe jinsi gani naweza ishi bila yeye.
Ikabidi nitikise kibiriti baada ya kumuona anajifikiria sana kujibu, nikageuza mwili na kujifanya nataka kuondoka.
Ghafla akanishika mkono, "Chris, kwanza naomba usilichukulie hasira, usinichukie, nimekuita leo kwa nia njema tu ili tuyamalize yote yanayo tufanya tuchukiane." - (Alizungumza kwa utaratibu, na hisia zaidi).
.
Wahenga walisema "Hakuna mkate mgumu mbele ya chai", ndipo niliamini wakati huo, maana sauti nyororo iliyobeba hisia na utaratibu, ya kwake Careen, ilinifanya niwe mpole ghafla na kuanza kumsikiliza kwa makini.
Hapa ndipo nilipogundua kuwa kinywa cha mwanamke kina nguvu kubwa ya ushawishi kwa mwanaume.
Akanitazama usoni, kisha akashusha macho yake kwa aibu na kuendelea kuongea huku akinitazama kwa kuibia ibia, akaendelea "Siku zote nilihisi wewe ni mkosaji sababu uliniharibia kwa mwanaume ambaye nilimpenda kwa dhati.
Lakini leo nimejifunza, nimegundua umuhimu wako."
.
Nikamjibu "Careen sioni umuhimu wangu kwako, mimi mnafki, mimi nimekuharibia, mimi nimekupakazia, umuhimu wangu uko wapi??" - (Nilimuuliza kwa upole zaidi).
.
Akajibu "Chris naamini yale yote yalikua kwa makusudi maalumu.
Somo limenifanya niligundue hilo leo.
Umeniondolea uozo ndani ya maisha yangu, yule mwanaume alinitesa sana, kanifanyia visa vya kila aina, kanisaliti vya kutosha, na kuna siku niliwahi kumhoji kwanini, Chris huwezi amini alinipiga yule kaka". - (Alizungumza kwa machungu sana huku machozi yakianza kumlenga).
.
Akaendelea "Sio mara ya kwanza kunitafutia sababu ya kuniacha, lakini nilikua king'ang'anizi sababu nilimpenda sana, sikutaka aniache.
Lakini aliniacha kwasababu ndogo sana, nimeishi kwa mateso mwezi mzima, nimelia sana, Chris unaona hadi nimepungua." - (Nikaanza kuyaona machozi yanaanza kumtoka).
.
Sikutaka kupoteza point 3 muhimu, nikafanya kama wanavyofanyaga wazungu kwenye tamthilia, nikamvuta na kumkombatia kwa nguvu.
Nikamwacha alie kifuani mwangu, huku nazipapasa nywele zake kwa mkono mmoja, mkono mwingine ukiwa umemlaza vizuri kifuani.
Nikamwambia "Lia mamie, lia unavyoweza, lakini kamwe moyo wako haustahili kumpa asiyejua thamani yako."
.
Nikaendelea "Unastahili kupendwa, kumpata anayekujali, atakaye kufanya ujihisi kama Malkia, kwanini ujutie kuachwa na anayeutesa moyo wako.".
Nikaona Careen anaifunga mikono yake mgongoni mwangu kwa nguvu, nami nikaona nisichezee hii nafasi.
Nikahakikisha mwili wake unapata joto langu vizuri ili kuongeza misisimko kati yetu.
Nikamwambia "Naamini yale makosa yote, niliyafanya kwa kusudi maalumu, sababu hakuna hata moja nililowahi kulifanya kwa kukusudia. Nisamehe sana Careen, tusahau yote yaliyopita, tumshukuru Mungu kwakila jambo na tuanzishe maisha mapya".
.
Careen kwa sauti ya chini, akanijibu "Kaka Chris haina haja ya kuomba samahani, moyo wangu mweupe sasa, nimeijua thamani yangu na nimemjua rafiki bora aliye letwa na Mungu kwangu.
Nilikumiss, nilimiss vituko vyako". - (Akazungumza huku akitoa kicheko cha taratibu kilichochanganyika na hisia).
.
Ikabidi nimchekeshe "Twende mgahawani tukale leo, ila nitasahau wallet tena".
.
Careen akacheka, akanipiga kifuani na kuniambia "Nitaosheshwa vyombo leo, halafu wewe watakuacha na boxer tu"
Sote tukacheka kwa furaha, kisha kukombatiana kwa nguvu zaidi.
.
Kutupa jicho mbele, nilimuona Peter akiwa anatutazama kwa jicho la chuki, nilijua wazi kuwa hakufurahia kile alichokiona.
Kutazama upande wa Nasra, nako palionekana mabadiliko.
Niliona uso wa Nasra ukiwa hauna furaha, ameukunja, alionyesha kitu kama wivu ndani yake.
Nilihisi kuwa Nasra hakufurahishwa kuona mimi na Careen tunarudisha urafiki wetu, nilianza kuhisi kuwa labda Nasra alikuwa na hisia juu yangu.
.
Peter alisogea mahali tulipo, akakohoa kinafki "hnh hnh", Careen akastuka na kugeuka nyuma.
Peter akaongea kwa kingereza, akimaanisha "Nimeshangazwa kuona mpo pamoja".
.
Careen akajibu kwa lugha hiyo hiyo akimaanisha "Yeah nimeona ni vyema kumrudisha rafiki yangu aliyeletwa kwa kusudi maalumu, somo limenibadilisha leo". - (Akazungumza kwa tabasamu kubwa mno).
.
Peter akanitazama kwa jicho ambalo tafsiri yake ni kama alitaka kuniambia "Nakumaindi nikupige vichwa wewe".
.
Ikabidi nimuite Nasra, akasogea mahali tulipo na kumtambulisha kwa Peter na Careen.
Akampa mkono Peter kikawaida tu, lakini kwa upande wa Careen ni kama alitaka kumpa kisha akasita na kumpungia mkono kwa mbali kama anatoa "hi" vile, kisha akatoa tabasamu ambalo nilihisi halikua na ukweli ndani yake.
.
Careen akamwambia Peter, "Tumemrudisha Chris kwenye kundi, na chuki ziishe, mpeane mikono" - (Akazungumza huku amemshika bega Peter, ili kuonyesha msisitizo).
.
Peter akanyoosha mkono, nami nikamshika mkono wake, tukatupiana macho, kwavile Careen alikua akinitazama ilibidi nitoe tabasamu la kinafki.
Lakini Peter alizidi kuonyesha chuki yake kwenye macho yake, nami nikajisemea kimoyo moyo "Acha mechi ya wanaume iendelee".
.
Story mbili tatu zikaendelea, lakini Nasra na Peter walikua kama hawapo vile, lakin sikuwajali, nilichojali ni kuwa leo nimerudisha furaha yangu, na moyo wangu una amani sana.
Kwambali nilimuona Dkt Leonard, nikaona huu ni wakati muafaka wa kwenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kuirudisha furaha.
.
Niliwaomba nitoke mara moja, na kumfata Dkt.Leonard, nikazungumza nae mambo kadhaa na kumpa shukrani zangu, pamoja na kubadilisha nae namba za simu sababu nilihisi ana mengi zaidi ya kunisaidia.
Nilipomaliza tuakaagana na yeye akaendelea kusalimiana na watu waliokuja kwenye semina.
.
Nilipogeuka ili kurudi nilipowaacha kina Careen, nilishangaa kumuona Nasra na Careen tu ndio wamebaki, wala Peter hayupo.
.
Nikatafakari kidogo, kisha nikaanza kuchukua hatua kusogea mbele, nikasikia sauti nzito inaniita "Chris".
.
Nikageuka, kumtazama alikua ni Peter, nikagundua kuwa kumbe alikua akinifatilia kwa nyuma.
Akaniambia "Maamuzi uliyo yachagua leo, yana madhara makubwa sana kwako kwa hapo baadae. Acha kumfatilia Careen"
.
Nikamshangaa, nikajua wazi hilo ndilo lililokuwa linamkereketa.
Nikamuuliza "Maamuzi gani hayo niliyo yaamua mimi?? " - (Nilimuuliza swali huku nikijichekesha kwa dharau).
.
Peter: Maamuzi ya kumfata Careen na kumuomba msamaha.
.
Nikagundua kumbe Peter anahisi mimi ndiye niliyemfata Careen kumuomba msamaha.
"Aaanhaaa kumbe ndo unachowaza, habari mbaya kwako, Careen ndiye aliyenishobokea". - (Nikazungumza kwa kujiamini zaidi, huku nikimtazama kwa jicho la dharau).
.
Peter alistushwa na kauli hiyo, nikaona anatafakari na kunijibu "Sasa nakuamuru, vunja kabisa mazoea na Careen, yeye ni mchumba wangu mtarajiwa, kaa nae mbali" - (Alitoa kauli iliyojaa ukali na hasira).
.
Nikaona sasa muda wa kutambiana umeisha, huu ni muda wa kuonyeshana kwa vitendo, nikamjibu "Bro, siku zote hizo nilizokuwa mbali nae umeshindwa kumfanya awe wako??? Kweli wewe domo theeeeege hahaha" - (Nikazungumza kwa dharau na kuivuta "Theeege" huku nikicheka kwa dharau).
.
Akajisikia aibu sana, akakosa la kuongea.
Nikaona kama Peter ananipotezea muda, nilitaka niwahi mahali walipo Careen na Nasra.
Nikageuka chap na kuanza kuchukua hatua kadhaa.
.
Nikasikia tena "Chris" (Peter alikua akiniita).
"Shit" - (Nikajisemea kwa nguvu baada ya kuchukizwa na kupotezewa muda na Peter).
.
Sikugeuka, Peter akanifata na kunishika bega, kwa hasira nilizo nazo, nikageuza shingo na kumtazama kwa jicho la hasira.
.
Akaniambia "Wewe mwanaume, mimi mwanaume, sote tunataka kitu kimoja, ngoja tuone nani atakipata, na ambaye atakipata ndiye mwanaume. Atakaye kosa, atavalishwa dera na wigi" - (Akazungumza kwa kujiamini, na kwa hasira zaidi).
.
Niliposikia maneno hayo, nilijua wazi mchezo wa kuBet, Careen ndiye dau.
Nikakumbuka kauli moja "Mapenzi ni kama kamali, kuna kula au kuliwa".
Nilimtazama Peter kwa masaa, nikamtafakari muonekano wake, mali zake, nikagundua ana nguvu ya pesa tu, nikajitafakari nikasema nikikataa basi lazima nitaonekana boya.
.
Na je nikikubali, itakuwaje endapo nitashindwa?!
.
Akaniambia tena "Hizi ni mbio za wanaume, na ni mwanaume mmoja tu ndiye atakae ibuka mshindi"
.
Akaendelea "Chagua kupambana ili uibuke mshindi, au ushindwe na uvalishwe dera na wigi mbele za marafiki zetu??? "
.
Nikastuka sana, nikajua kuwa Peter hakuwa akitania, alimaanisha alichosema, na niliwaza kinachompa ujeuri ni pesa alizonazo.
Lakini amekaa na Careen mwezi mzima, lazima atakua anajua mengi kuhusu Careen, na amepata wakati mzuri wa kumjenga kihisia Careen.
.
Nikabaki na maswali mengi kichwani, "Nikubali mechi, au nikatae mechi"
Je Chris atakubali???"
. Usikose sehemu ya 10
#Itaendelea....
#Ilipoishia: Peter alitangaza mechi kati yangu na yake, na atakaeshindwa basi atavalishwa dera na wigi.
Nikajifikiria kwa mengi sana hasa kwa kuzingatia muonekano wa Peter, nguvu yake ya pesa, pamoja na ukaribu wake na Careen kwa kipindi chote hicho nilichokua siongei nae.
Nikabaki najiuliza sana, nikubali au nikatae?! .
.
#[COLOR]Inaendelea[/COLOR]: Nikafikria hii ni kamali, na naweza kushindwa, mwisho nitaaibika, najua hawatonivisha dera tu nakuniacha, lazima watanipiga picha na kuzisambaza.
.
Sura yangu nitaiweka wapi?? Wazazi, ndugu, na marafiki zangu watanifikiriaje??
Nilipofikiria hayo tu, ndipo nilipuuzia maneno aliyosema Peter na kupata nguvu ya kuanza kutembea kuelekea mbele.
.
Peter alibaki amesimama, akaanza kucheka kwa dharau.
Akaongea "Siku zote wanawake ndio huwa waoga, ila kumbe hata wanaume pia " - (Alizungumza huku akijichekesha kwa dharau).
.
Nikajikuta nimesimama ghafla, nikafikiria la kumjibu.
Akaongea tena "Kuna matokeo mawili tu, kushinda au kushindwa, na siku zote waoga ndio hujitabiria kushindwa hata kabla ya mechi".
.
Maneno yalinugusa sana na kunipandisha hasira, yakanichoma kisawasawa, nikageuka na kumtazama kisha nikamjibu "Wanaume huwa hawapambani kwa maneno kama waimba taarab, vitendo huwa ndo vinafata". - (Nilizungumza kwa msisitizo na kujiamini zaidi).
.
Akanitazama kama mtu anaetaka kunirukia, nikamwambia "Nimekubali mechi, nitashinda, na wewe njoo na make up kabisa, ili upendeze pindi umevaa dera na wigi". - (Nikamkejeli, na kugeuka nyuma na kuanza kuondoka).
.
Lakini nikapiga hatua mbili mbele, kisha nikasimama na kumtazama adui yangu, nikamwambia "Huu mchezo hauhitaji hasira" - (Nikazungumza na kuondoka huku nacheka).
.
Peter alinifata nyuma nyuma huku akiwa amenyongea, mpaka tulipofika mahala waliposimama Careen na Nasra.
Tuliwakuta wakizungumza mawili matatu, lakini Careen ndiye aliekuwa mzungumzaji zaidi, na Nasra msikilizaji huku akichangia moja moja.
.
Tulipofika wala hatukupoteza muda sana, tukaagana na Careena aliondoka na Peter.
Nami niliondoka na Nasra.
Njiani Nasra alionekana mwenye mawazo sana, nikajua kuna kitu Nasra anakiwazia kuhusu mimi na Careen.
.
Nikamuuliza "Mbona umenyongea hivyo?? "
.
Nasra: Mmh kwani naonekana nimenyongea!!!?! Mbona najiona niko sawa tu. - (Akajifanya kuruka ili nisijue kilicho mfanya anyongee).
.
Nikaona anaweza kunificha, nikaamua kumtupia mada za kiuchokozi.
"Leo nimefurahi sana kurudisha urafiki wangu na Careen". - (Nilizungumza huku natoa sauti iliyojawa na furaha sana).
.
Nasra akawa amegeukia upande mwingine huku akijifanya hajasikia nilichosema.
Nikaona bora ninyamaze, lakini nilijua wazi kuwa Nasra hajafurahishwa na uwepo wa Careen kwenye maisha yangu, na nilijua huenda akawa na hisia juu yangu.
.
Tulipofika Gongo La Mboto, tukaagana na kila mtu akaelekea kwenye hostel anayoishi.
Lakini kwajinsi tulivyoagana, nilizidi kupata wasiwasi juu ya hisia za Nasra juu yangu, nikahisi kuwa huenda zikaja kuniharibia mipango yangu ya kumpata Careen.
.
Jumatatu iliyofata kama kawaida ndani ya chuo, nikawa nimeketi maeneo ya Garden, pamoja na Hasheem na Ramadhan.
Tukawa tukipitia notes huku tukipiga story mbili tatu.
.
Ramadhan: Leo unaonekana hauko sawa??? - (Alinitupia swali mimi).
.
Nikamjibu "Yeah, kuna jambo linanisumbua kichwa na sijui nitalimaliza vipi".
.
Akaniambia "Jambo gani??? Kuhusu Careen tena au??? " - (Aliniuliza huku akinitazama kwa jicho la uchu wa kutaka kujua kiundani zaidi).
.
Nikatuliza nafsi kwanza, nikapoa, kisha nikaanza kumweleza kiundani zaidi kuhusu mechi niliyo ingia kati yangu na Peter.
.
Alinishangaa sana kwa maamuzi magumu niliyo chukua.
Akaniambia "Nadhani kwasasa una mambo mengi sana ya kufanya Chris, hukuwa na haja ya kuuthibitisha uanaume wako kwa Peter."- (Akazungumza huku akionekana mwenye kumaanisha anachosema).
.
Nikageuka na kumtazama usoni, akaendelea "Chris kumbuka umekuja chuo kwaajili ya kutengeneza maisha yako ya baadae, haya maswala ya kujiingiza kwenye mahusiano ni sehemu mojawapo ya kuharibu focus yako kwenye masomo".
.
Akahema kidogo kisha akaendelea, "Unakumbuka mitihani yako ya Cat one uliharibu??? Sababu ilikua ni mahusiano, Cat two umefanya vizuri, sababu ulikua mbali na yule unayempenda.
Hebu fikiria Chris, usikubali hisia ziendeshe maisha yako.
Leo hii umekua mtumwa, unafanya kila ambacho hisia zako zinasema, lakini laiti ungekua na control nzuri kwenye hisia zako, kwasasa usingeshindwa kuacha kusoma na kuwaza mahusiano".
.
Nikamsikiliza Ramadhan kwa umakini, lakin niliona kama ameanza kunioea wivu.
Ramadhan akatoa kauli za mwisho, akasema "Kwasasa chuo kinakufatilia kwa umakini na ukaribu zaidi tangu uharibu kwenye Cat one, wanajitahidi sana kukupa elimu bora wakidhani labda una uelewa mdogo darasani, kumbe tatizo tayari akili yako inaendeshwa kihisia.
Hebu zinduka Chris, huo mchezo ulio uingia haufai kwako.
Hebu fikiria siku ukija valishwa dera, nani atakaye aibika??? Ni wewe.
Kina nani wataaibika??? Wazazi wako.
Utawapotezea sifa kina nani!?! Chuo chako.
Hebu zinduka Chris". - (Akazungumza kwa msisitizo, kidogo maneno yaliniingia japo mwanzo nilihisi kama ana wivu na mimi).
Nikaanza kufikiria jinsi wazazi wangu walivyohangaika kunisomesha huko nyuma, nikawazia mkopo naopewa na serikali ili nisome, nikawazia chuo changu kinachojitahidi kunipa elimu bora, nikawazia rafiki zangu, nikajiwazia mimi mwenyewe na future yangu.
Nikajigundua nina mzigo mkubwa sana kwenye maisha yangu, kuna watu wengi wanategemea uwepo wangu, wanategemea matunda yangu ili waje kunufaika na kujivunia kupitia mimi.
.
Nikajisemea kimoyo moyo "Nahitajika kuwa balozi mzuri wa chuo changu, wazazi wangu, rafiki zangu, wote wananitegemea mimi".
.
Hasheem akanishika bega, akasema "Watu wengi wanapoingia vyuoni huwa wanasahau lile walilo lifata chuo, matokeo yake hujikuta wanajiingiza kwenye maswala ya mapenzi.
Wewe mtu mzima tayari, kwa umri ulionao hauwezi jizuia kupenda hasa katika mazingira kama haya yenye watu wengi wazuri.
Lakini ni vyema kabla ya kujifunza kupenda, ukajifunza kuzicontrol hisia zako ili usije changanya mapenzi na masomo, au mapenzi na maisha mengine.
Ukiishi kwa kuendeshwa hisia zako utakua mtumwa kwa unayempenda, utakuwa na wivu na kuzidi kuumia hata kwenye mambo madogo, na mbaya zaidi utajikuta unafanya maamuzi ya kijinga kama haya ambayo unayafanya."
.
Hasheem akanitazama na kuniambia "Fikiria kabla ya kutoa maamuzi yoyote maishani mwako, kuna wengi sana utawaumiza endapo ukitoa maamuzi kwa kufata hisia zako zinavyosema.
Cha kukushauri, ukimpenda mtu, usitake kushindana na mpinzani wako, wewe nenda wewe kama wewe na umweleze jinsi unavyompenda.
Najua hofu yako ni juu ya majibu yake, unahofu endapo atakukataa au laa, lakini huwezi jua saingine anakupenda pia, na kuchelewa kwako kukamfanya aone kama humpendi mwisho akamchagua mwingine.
Lakini itakuaje endapo utamwambia halafu akakukatalia??? Uzuri ni kuwa akikukataa, utaumia lakini tayari umeshapata ukweli ambao utakuweka huru.
Kuliko kusubiri miaka mingi na kuhofia atakukataa, mwisho unakuja kusikia anaolewa na mtu mwingine".
.
Maneno yaliniingia akilini, nikajihisi mjinga sana kwa kuchelewa chelewa kwangu, nimeumia vya kutosha, nimepoteza muda vya kutosha, na bado nimeteseka vya kutosha.
Nikasema "Nahitaji kuwa mwanaume, nahitaji kujitambua, nahitaji kujua kuzicontrol hisia zangu, na nahitaji kufaulu masomo yangu ili iwe furaha kwa chuo, rafiki, serikali, na wazazi wangu".
Hasheem akaniambia "Kuwa mwanaume, ishi kiume, kama kweli unampenda, jiandae kisaikolojia kwa jibu lolote utakalopewa, lakini nenda ukamweleze hisia zako leo.
Na mwambie Peter kuwa huna haja ya mechi yake, mapenzi sio mpira kusema mshindanie kombe". - (Akanisisitiza na kunitaka ninyanyuke niende).
Nilitamani kunyanyuka ili kumfata darasani, mahali ambapo Careen yupo, lakini miguu iliishiwa nguvu, nikaanza kutetemeka na miguu na mikono.
Mwili mzima ulikua kama kuna kitu kinanitembea, mapigo ya moyo yalizidi kunipiga.
.
Nikanyanyuka, nikaanza kutembea kama mtu ambaye haoni mbele vile.
Jasho lilikua likinimiminika utadhani nimetoka kumwagiwa maji, kwavile nilikua mwenye mawazo tani 1000, nilijikuta nimejikwaa ghafla.
Watu walio maeneo ya garden wakacheka, nikanyanyuka na kuanza kutembea tena.
Nilikua natembea kama kuna mtu ananisukuma, mapigo ya moyo yalikua yanadunda mpaka shati lilikua linadunda kama limebebea sabufa.
Nikaingia kwenye corridor ya kuelekea darasa alilo Careen, kila nilivyozidi sogea ndivyo nilivyozidi kupunguza mwendo, ghafla nilijistukia nimejigonga kwenye kiti kilicho kwenye corridor.
Nikainama na kutazama goti langu nililojigonga, nikawa naugulia lakini ndipo nilipogundua kuwa kumbe nilichafuka wakati nilipodondoka.
Nikachukua leso na kujifuta, lakini jasho nalo likawa linamwagika.
Nikaamka na kujifuta jasho pia.
nikajiweka sawa mavazi yangu na kuanza kupiga hatua kuelekea darasa alilo Careen.
Pindi nakaribia darasa mapigo ya moyo yalinizidi, lakini ghafla nilisikia sauti mbili zilizokuwa zikizungumza.
Sauti moja ilikua ni ya Careen, nyingine ya Nasra.
.
Nilistushwa na mazungumzo yao, nikahisi kama mipango yangu yote inataka kuharibiwa leo.
Careen alimuuliza Nasra, "inaonekana wewe na Chris mmekua marafiki wakubwa sana "
.
Lakini jibu la Nasra ndilo lililoniharibia siku yangu, alijibu "sio bestfriends tu, ni boyfriend wangu".
.
Careen aliye ndani alistuka, nami niliye nje nilistuka.
Nilitamani hata kumfata Nasra nimtie vichwa.
.
Pindi bado nafikiria jambo la kumfanya Nasra, ndipo Nasra alipo muongeza Careen maneno mengine yaliyo niacha mdomo wazi.
Je Nasra Alizungumza nini!!??
. Usikose sehemu ya 11
#Itaendelea
Sehemu ya Kumi Na moja
.
#Ilipoishia: Pindi nakaribia darasa alilo kuwepo Careen, ndipo nikasikia sauti mbili tofauti zikizungumza.
Moja ilikua ya Careen, na nyingine ilikua ya Nasra.
.
Mazungumzo yao yalizidi kunitisha hasa pale Careen alivyouliza kuhusu urafiki wangu na Nasra, kisha Nasra kujibu kuwa mimi sio bestfriend wake tu, bali ni boyfriend.
.
Nilistushwa sana na jibu hilo, nilihisi hasira zinanizidi kupanda, nilitamani niingie darasani nikamtie vichwa Nasra hasa baada ya kuona tayari keshaniharibia mipango yangu yote.
#[COLOR]Inaendelea[/COLOR]: Pindi bado natafakari cha kumfanya Nasra, ndipo nikasikia Nasra akizidi kumlisha maneno ya uongo Careen.
.
Nasra: Chris ni aina ya mwanaume ambaye mwanamke yeyote mwenye kuihitaji furaha ya kweli, upendo wa dhati, basi kamwe hawezi kumuacha.
Anaujua udhaifu wa kila mwanamke duniani, ni kuwa na mwanaume mwenye kujali, kuthamini, kupenda na kuheshimu. Hayo ni mambo ninayo jivunia kwake, nampenda sana na ananipenda pia" - (Alizungumza kwa kujiamini sana, huku akitoa sauti yenye kumaanisha anachosema, ni ngumu kwa Careen kudhani kuwa amedanganywa.).
.
Careen; Hilo ni kweli, Chris ni mwanaume mwenye kujali sana. Hongera sana Nasra.
.
Nasra: Asante sana best.
.
Careen: Ila Chris ana tabia mbaya sana, hajaniambia. - (Alizungumza kwa kuonyesha kukwazika).
Na kwanini sasa siku ile alikutambulisha kama rafiki tu???!!!
.
Nasra akabaki kimya kwa dakika kadhaa.
Nikagundua hana jibu la kutoa, nikaona huu ndo wakati muafaka wa mimi kwenda kumuumbua mbele za Careen.
Nikaanza kuchukua hatua, pindi naweka mguu tu kwenye mlango wa darasa, ndipo nilipoona Nasra amestuka kuniona, huku Careen akionyesha furaha kama aliyekuwa ananisubiri kwa hamu.
.
Nikasogea mpaka mahali alipo Nasra, nikawatazama wote wawili.
Nilitamani nianze na Nasra kumuuliza maswali mbele za Careen kuwa mimi na yeye tumeanza lini uchumba.
.
Nasra akaniwahi "Chris umechafuka, ulikuwa unafanya nini?? " - (Alizungumza kwa kuonyesha kushangazwa na kuchafuka kwa nguo zangu).
.
Ndipo Careen nae aliponitazama nguo zangu kwa mshangao, nae akauliza swali hilo hilo.
Nikaona kama maswali yao yanataka kunipotezea muda na kunisahaulisha nilichotaka kumuuliza Nasra.
.
Nikamuita "Nasra".
Akanitazama usoni, nahisi alianza kupata wasiwasi kuwa huenda nilisikia maongezi yao.
.
Nikaona nisichelewe, nikafungua kinywa na kutaka kumuuliza.
Ile nataka tu kumuuliza, ghafla nilikatishwa na sauti ya mtu mlangoni, aliyemuita Careen kwa nguvu sana "Careen nakuomba mara moja".
.
Nikapiga jicho mlangoni na kugundua kuwa alikua ni Madam Irene akimuita Careen.
Nikaona kama kaharibu inshu yangu, nilitaka nimuumbue Nasra mbele ya Careen.
.
Nikamtazama Nasra kwa jicho la hasira na kumuuliza ''Nani kakwambia umwambie Careen kuwa mimi ni boyfriend wako??? "
.
Hakuwa na jibu, akabaki anaona aibu baada ya kugundua kuwa nimesikia yote aliyo kuwa akizungumza.
Nikamwongeza "Hukuona watu wengine??? Kwanini iwe mimi??? Unataka kuniharibia sio??? Sasa akija umwambie ukweli, mbele yangu"
.
Nasra akastuka baada ya kumwambia atoe ukweli kwa Careen.
Akapatwa na wasiwasi na kujikuta akijibu "Lakini Chris nafanya yote kwa faida yako ".
.
Akaendelea "Chris ulitengwa tu na ukawa kama chizi, kumbuka niliko kutoa mpaka hapa ulipo, unadhani nafurahia kuona aliyewahi kuipoteza furaha yako anarudi tena?"
.
Nikamsikiliza Nasra, nikaona kama ananitibua tu.
Na kwa hasira nilizo nazo wala sikutaka kuendelea kukaa nae karibu, lazima ningefanya kitu kibaya.
.
Nikamuambia "Niwe napata furaha, niwe nateseka, hayo ni maamuzi yangu, akirudi Careen umwambie ukweli. Kama huwezi nitamuambia mimi mwenyewe " - (Nilizungumza kwa hasira na msisitizo).
.
Baada ya kumuambia hayo nikageuka na kuondoka, huku nikimuacha akinitazama kwa huzuni nyingi.
.
Majira ya saa 2 usiku pindi nikiwa hostel, nikapokea simu kutoka kwa rafiki yangu wa kiZambia, Ivan.
Tulizungumza mengi sana, lakini mwisho ikabidi aweke wazi kilichofanya anipigie.
.
Ivan: Chris kuna mchezo mbaya sana unaendelea kati yako, Nasra, na Peter.
.
Nikastushwa na kauli yake, na kupata shauku ya kutaka kujua kiundani mchezo wenyewe ni upi.
.
Akaendelea "Leo asubuhi nilimuona Peter akizungumza na Nasra, japo sikuelewa walichokuwa wanazungumza." - (Alizungumza na kuonyesha kuwa kuna kitu anahisi kinaendelea nyuma ya pazia).
.
Maneno yale yalianza kunifumbua macho juu ya kile alichokifanya Nasra pindi alipokuwa na Careen, nikagundua kuwa huenda Nasra ameanza kutumiwa na Peter ili kumvuruga Careen asiwe na mawazo yoyote kuhusu mimi.
.
Ivan hakuishia hapo, akaniambia "Na kuna muda leo mchana nilienda nae kula, akapokea simu ambayo nahisi ilikua ni Peter kuendana na mazungumzo yao. Walivyomaliza kuongea, Nasra hakumaliza kula, aliniaga na kuondoka.
Nikapata wasiwasi sana, ilibidi nianze kumchunguza anako elekea, ndipo nilipomuona anapanda kwenye gari la Peter, na ndani yake alikuwepo Careen na Peter pia". - (Ivan alinieleza kwa utaratibu na kuonyesha wasiwasi wake juu ya mwenendo wa Nasra).
.
Hapo akili yangu iliaanza kuvurugika, nikahisi kuwa tayari Peter ameshaongeza nguvu ya mashambulizi kwangu.
Njia wanayoitumia ni kujaribu kuweka umbali wa hisia kati ya Careen na mimi, ili iwe rahisi Peter kumpata Careen bila kipingamizi.
Na Nasra alijua kuwa Careen akiwa na Peter, basi nami sitakua na chaguo lingine zaidi yake.
.
Ivan akaniambia "Chris, kama unataka kufanya lolote, jua kwamba niko nawe bega kwa bega kama rafiki, lakini tafadhali naomba usifanye lolote litakalo muumiza Nasra, shida yangu ukimpata Careen, nami nitampata Nasra." - (Alizungumza kwa hisia, na kufunguka ya rohoni).
.
Hapo ndipo nilipostushwa zaidi baada ya kuujua urefu wa mnyororo uliopo kati yetu, "Ivan anampenda Nasra, Nasra anampenda Chris, na Chris anampenda Careen, Careen ambaye anawindwa na Peter" - Nikajisemea kimoyo moyo.
Kisha kuagana na Ivan, na kukata simu.
.
Nikawaza kumbe ukionacho cha nini, mwenzako anawaza atakipata lini.
.
Nilifikiria mbinu nyingi sana juu ya kupambana na Nasra na Peter.
Wazo la ghafla likanijia kuwa niwatumie messages Nasra na Careen, wote nikawauliza "Uko wapi".
.
Nasra akajibu "Nilikua na Careen kwao Tabata, ndo narejea hostel".
.
Nikajua kweli alichosema Ivan kuwa Careen alikua na Nasra, na Peter, nikakithibitisha hapo.
Pindi najiandaa kumuuliza maswali mengine ili kumuhoji zaidi, ndipo simu yangu ikaita hapo hapo.
.
Kutazama kwenye screen, ilikua ni simu kutoka kwa Careen, nikaipokea.
"Hallow Chris" - (Alisalimia Careen).
.
Nikamjibu salamu yake, na hapo hapo Careen akaanza kunishushia lawama "Kwanini Chris umepata girlfriend na hukuniambia rafiki yako??? "
.
Nikaona njia pekee ya kunisaidia ni kukana mashtaka, nikasema "Sina girlfriend mimi, yeyote aliyekueleza utumbo huo ni muongo".
.
Careen akajibu "Yani Chris bado unamkana Nasra, sio girlfriend wako yule??? "
Bado nikamjibu "Sio girlfriend wangu, ananipakazia uongo".
.
Careen ikabidi atoboe siri, akasema "Hata mimi nilidhani nadanganywa, ila akanithibitishia hadi kwa messages zenu mnazoitana itana majina ya mapenzi, ndio nikaamini".
.
Hapo sikuwa na lakujibu, nakumbuka ni kweli Nasra alikua akipenda kuniita "Baby, Sweetheart, honey, darling ", majina ambayo nilidhani labda tunataniana tu, kumbe alikua anajua anachokifanya.
.
Nasra alinizoesha kuchat kwa sms za mapenzi kipindi nimetengwa na Careen, kwavile nilikua mpweke basi sikupinga chochote zaidi ya kufurahia messages zake.
Lakini sasa ndio zimetumika kumthibitishia ukweli Careen kuwa mimi na Nasra tuwapenzi.
.
Nilikosa cha kujibu, nikaamua kukata simu na kuizima kabisa ili ionekane imezima chaji.
.
Nikawaza mengi sana, nikaanza kupiga picha jinsi dera na wigi litakapo valishwa mwilini mwangu.
Nikabaki na maswali mengi sana, ni kweli nimekosa mbinu madhubuti za kuwanyoosha hawa watu?? Kweli nakubali kushindwa kirahisi?? .
Nilianza kuona dalili za kushindwa mapema, lakini nikajisemea kuwa "Mwanaume huwa hachoki kupambana"
.
Pindi bado nipo kwenye dimbwi la mawazo, ghafla nilisikia mlango wa chumba changu unagongwa.
Kufungua ilikua uso kwa uso na Abdulrahman akiwa ameongozana na Ramadhan na Hasheem.
.
Nikajiuliza leo Abdulrahman amefata nini kwangu, anataka kuniambia nini.
Lakin kwajinsi alivyokuja, na kwavile amekuja na marafiki zangu, nikajua wazi kuwa leo hajaja kunifanyia vurugu bali amekuja kwa jambo lingine tofauti.
.
Ramadhan akanyanyua mdomo na kuniambia "Chris kuna kitu Abdulrahman anataka kukuambia".
.
Abdulrahman akanitazama kama mtu aliye na kitu anatamani kuniambia haraka, akaniambia kwa kingereza, akimaanisha "Usiniogope, leo nimekuja kwa wema, na ni kwa faida yako."
.
Nikapata shauku ya kutaka kujua anachotaka kuniambia, nikamwambia "Niambie nakusikiliza".
Lakini Hasheem akanikatisha na kuniambia "Atakwambia huku umetusimamisha hapa nje?? "
.
Ndipo nikagundua kuwa muda wote huo nilikua sijawakaribisha ndani, nikajisikia aibu na kuwaribisha ndani.
Kwavile nilikua na shauku ya kutaka kujua anachosema nikamuuliza kabla hata hajakaa chini.
.
"Enhee Niambie ulichotaka kuniambia" - (Nikazungumza kwa kuonyesha hamu yangu ya kutaka kujua).
.
Akakaa kwanza kwenye kitanda karibu yangu, na kuniambia "Nimeamua kurudi upande wako "
.
Nikastuka, "What?? " - (Nikauliza kwa mshangao mkubwa).
.
Akaendelea "Ndani ya mechi yenu, nami kuna kitu ambacho nakitaka, na najua kwa upande wa Peter siwezi kukipata.", akakwamia hapo, akashusha pumzi nzito na kunitazama.
.
Nikaanza kujiuliza maswali mengi kichwani, ni kitu gani hiko Abdulrahman anakitaka, kiasi cha kutaka kumgeuka rafiki yake Peter.
.
Akaniambia "Kama utampata Careen, nami nitafanikiwa kukipata nachotaka, niambie kama uko tayari kuungana nami ili tumpindue Peter??" - (Akaniuliza swali huku akionyesha anamaanisha anachosema).
.
Nikamtazama, na kumuona jinsi alivyo serious, uso wake ukiwa umebeba hisia juu ya kile alichokuwa anakisema.
Nikazidi kupagawa zaidi na zaidi, hamu ya kutaka kujua anachokitaka ikanipata.
.
Nikamtazama usoni, na kumkazia macho kisha nikamuuliza "Ni kitu gani hicho unachokitaka.??"
.
Kwa kuonyesha kuwa yuko serious na anachotaka, akazungumza "Namtaka Nasra".
.
Ndipo nilipobaki namshangaa bila kujua nijibu nini, hasa kwa kuzingatia naye Ivan amejiunga nami ili kumpata mtu mmoja huyo huyo.
.
Abdulrahman akaongeza "Kumbuka kuwa tayari Nasra ameshajiunga na Peter, kama ulikua hujui hilo.
Niunge kwenye team, nitakupa pesa, pamoja na mipango yote ya kwake Peter.
Kama utashinda, basi nami nimeshinda.
Na endapo utanikatalia, basi jiandae kukosa vyote".
.
Nikabaki na maswali kichwani, nimkubalie au nimkatalie??? lakini je itakuwaje endapo Abdulrahman amekuja kama mpelelezi wa mbinu zangu???, na vipi kuhusu Ivan, nitakuwaje na watu wawili kwenye team wenye nia moja??
.
Na hapo ndipo nilipobaki nimevurugwa akili, nisijue nini cha kujibu.
Abdulrahman akauliza tena "Umekubali au bado?? ".
. Je Chris atakubali???"
. Usikose sehemu ya 12
#Itaendelea
#Ilipoishia: Baada ya Abdulrahman kutoa ombi lake la kutaka kujiunga nami, huku akiwa na mawazo kuwa mimi nikimpata Careen, basi naye atapata urahisi wa kumpata Nasra.
.
#Inaendelea: Nilibaki na maswali mengi kichwani nisijue nini cha kumjibu Abdulrahman, nilikumbuka maneno aliyo niambia Ivan juu ya Nasra, nikaona kuwa wote wana nia moja hivyo inaweza leta ugomvi kwa hapo baadae.
.
Lakini nikimtazama Abdulrahman, naona kabisa ana msaada mkubwa sana kwangu endapo nitaamua kumtumia.
Nikaona nisitumie akili yangu peke yangu, nikawaomba Ramadhan na Hasheem tutoke nje kidogo tujadili.
.
Ramadhan: Wewe mkubalie, kuna kitu kimoja kinaitwa "Divide and rule", ukitaka kumshinda adui yako, lazima kwanza utumie akili kwanza kuitawanya nguvu yake, ili iwe rahisi kupambana nae.
.
Hasheem: Hapo naona mambo mawili, ukimkubalia itakusaidia kupata mipango yote ya Peter, utapata nguvu ya pesa, lakini pia utapata support kubwa itakayo fanya iwe rahisi kumshinda Peter".
.
Nikawasikiliza wote wawili, nikaona hoja zao zina mashiko ila tatizo zimeangalia upande mmoja.
Nikawauliza "Na vipi kuhusu Ivan??? Maana nae ana nia sawa na Abdulrahman ".
.
Wote wakanitazama kwa mshangao, "na Ivan pia??? ''- (Aliuliza Hasheem).
.
"Yeah" - Nikamjibu huku natikisa kichwa.
.
"Kheee...!!!!" Ramadhan alitoa mshangao na kubaki mdomo wazi.
.
Hasheem akafikiria kwa muda kidogo kisha akajibu "Naziona mechi mbili za wanaume, na wewe unatumika kama daraja kwenye mechi moja".
.
Akashusha pumzi kidogo, na kuendelea "Kama utakua makini kucheza na akili zao wote, badala ya wewe kutumiwa kama daraja, wewe ndio utawatumia'".
.
Nikageuza shingo kumsikiliza Hasheem kwa umakini, kisha macho yangu nikayatupa kwa Ramadhan ambaye nae alinyanyua kinywa chake.
Ramadhan: "Umesema kweli Hasheem, wakubaliwe wote, lakini akili itumike zaidi ili kuepusha migongano kwa hapo baadae".
.
Akatulia kidogo na kuendelea "Mwisho wa yote, Ivan na Abdulrahman watabaki na mechi yao ya kuwania kumpata Nasra, kipindi hicho wewe ushampata Careen".
.
Mawazo yao yaliniingia akilini vizuri, nikaona yana mashiko.
Tukamaliza mazungumzo na kurudi chumbani ambapo tulimwacha Abdulrahman peke yake.
.
Jibu kubwa nililotoa kwake, ilikua "Ndio, nimekubali".
Alifurahi sana na kuniambia sasa jiandae kurusha makombora kwa Peter.
.
Akanyanyuka, ili kuanza safari ya kurudi nyumbani kwake.
Tukamsindikiza mpaka nje ya nyumba ambapo alipo park gari lake.
Pindi tuna agana akaniambia "Unajua kama kesho kutwa ni birthday ya Careen??? Na umepanga kufanya nini siku hiyo".
.
Nilishangaa, maana siku zote tangu Careen awe rafiki yangu, sikuwahi kujua siku yake ya kuzaliwa.
.
Nikamwambia "Ulijuaje??? "
Akaniambia "Uko nyuma sana Chris, na hii mechi usinge iweza endapo vitu vidogo kama hivi na vyenye umuhimu kwenye maisha ya mwanamke, huvijui, sijui ulikua unashindana nini na Peter".
.
Nilibaki na tafakari maneno yake, nikajiona mjinga sana, nimekaa na Careen miezi mitatu mpaka sasa.
Tangu tuanze chuo mwezi wa 11, mwaka jana, mpaka leo hii mwezi wa kwanza, na sijajua vitu muhimu kama hivi.
Nikajiona niko nyuma sana kwenye kuwasoma wanawake.
.
Nikamuuliza "Kweli hata mimi nimejishangaa, utakua free kesho tuelekee mahali??? " - (Nilimuuliza kama atakua huru ili tuweze kuelekea kwa dkt Leonard ili kupata msaada wa kifikra juu ya wanawake).
.
Akanijibu "Niko huru, unataka twende wapi?? " - (Akaniuliza kwa mshangao).
.
"Posta, kwa Dr.Leonard " - (Nikampa jibu.).
.
Akanikubalia, na kuniaga na kuondoka na Hasheem na Ramadhan.
Nikachukua simu na kuweka appointment ya kuonana na Dr. Leonard majira ya saa 6 mchana, kwa siku ya kesho yake.
.
Kesho yake, Abdulrahman alinipitia mapema tu maeneo ya Gongo la mboto, nakuelekea wote hadi ofisini kwa Dr. Leonard.
.
Nilimwelezea mengi sana Dr. Leonard na akanipa majibu.
Akasema "Kumjua mwanamke inahitaji utulivu mkubwa sana, lasivyo unaweza kutoka kapa".
.
Akaendelea "Kuendana na jinsi ulivyo nieleza, unahitajika kuelewa mambo matatu makubwa.
1: Unahitajika kujijua wewe mwenyewe kwanza, unamtaka Careen kwa muda mfupi tu, au kwa kuwa nae milele?? Kama ni muda mfupi tu, basi huitaji mzunguko, acha kumfatilia, sababu siwezi kukushauri uende kumchezea mwanamke. "
.
Nilimtazama, nikagundua Dr. Leonard ni mwanaume mwenye kujali sana thamani za wanawake.
Akanywa maji kidogo, na kuendelea "Lakini kama unamuhitaji kwa kuwa nae milele, hapo nakushauri uwe mtulivu, utumie akili nyingi kuliko nguvu. Jijenge kihisia na ujue kujicontrol, ili kuepuka kuwa na maamuzi mabovu, unahitaji hekima na busara za hali ya juu".
.
Akaniangalia na kusema "Namba 2: Unahitajika kuwa na maarifa juu ya wanawake, nini wanapenda na nini hawapendi.
Vitu vidogo sana kama kujaliwa, kuthaminiwa, kuheshimiwa, kupewa kipaumbele, kufurahishwa, na kupenda kusikilizwa, humfanya mwanamke ajione mwenye bahati sana chini ya jua.
Lakin kuna mengine pia unahitajika kuyajua, kama mambo ambayo wanawake huvutiwa kwa wanaume. ''
.
"Mh" - Nikaguna, akaeleza mengi sana kwenye namba mbili.
Kisha akarukia namba 3.
.
Akaendelea "Namba 3: Unahitajika kumjua kiundani mwanamke unaye mtaka.
- Kama ana mtu, kuna vitu vya kufanya, ila hapa sitakushauri chochote, sitaki laana ya kuachanisha watu."
.
Akaendelea "Kuna wale wapweke, hawa huitaji nguvu sana wala kupoteza muda sana. Kuna wale waliotoka kuumizwa, hawa ndio kazi ilipo, ukimfata kichwa kichwa basi unaweza ambulia kukataliwa, au kama atakubali basi jiandae kuumizwa.
Unahitajika hekima, uvumilivu, busara ya hali ya juu sana kuubadilisha moyo wake ili kuja kupenda tena.
Na kufanya mwanamke akufungukie haya, basi uwe na akili ya kumfanya akuamini na kumjengea uwezo wa kukuambia lolote lile.
Na hii huletwa na urafiki mzuri, akikuamini, na ukiwa unaonekana una hekima ya kumshauri mambo mazuri".
.
Alizungumza mengi sana kuhusu wanawake ambayo yalinifumbua macho, na kujiona wapi nilipokuwa nakosea siku zote.
Nakumbuka aligusia umuhimu wa kukumbuka birthday ya mwanamke, na kuifanya siku nzuri sana kwake kwa kumtengenezea kumbukumbu nzuri kichwani kwake.
Hapo ndipo nilipoona umuhimu wa kuifanya tarehe 12, siku ya kuzaliwa Careen, kuwa siku bora ndani ya maisha ya Careen.
.
Nilitoka nje ya ofisi na kukutana na Abdulrahman ambae alikua akinisubiri kwa hamu, nilimueleza yote nae alipata mwangaza wa jambo la kufanya kwenye siku ya kuzaliwa ya Careen.
.
Akaniambia "Peter amepanga kumfanyia Surprise Careen, na amealika marafiki zake wengi tu. Na party itafanyika kesho mida ya saa 2 usiku, maeneo ya Kiota Jungle. "
.
Nikamsikiliza Abdulrahman kwa umakini zaidi na kumuambia, "Unadhani sisi tutafanyaje ili kumuharibia mipango Peter, na kuweza kumfanyia jambo kubwa Careen".
.
Abdulrahman akafikiria kwa muda kidogo, kisha akanipa majibu "Jiandae kwaajili ya kumfanyia surprise Careen kesho, usijali kuhusu pesa, ukumbi, keki, vinywaji, na zawadi."
.
Akazungumza kwa kujiamini huku akiingiza mkono mfukoni na kunipa $1000(dollar 1000).
Nikapokea huku nikiwa siamini nachokiona, akaniambia "Nenda kafanye maandalizi".
.
Tukaondoka maeneo ya ofisini mpaka kwenye gari, huku tukijadili mambo kadhaa.
Tukiwa ndani ya gari, tuliweka mipango yote sawa ya jinsi tutakavyo uendesha mchezo ili kumzidi kete Peter.
Kwavile Peter aliandaa Party saa 2, sisi tukaandaa party saa 12 jioni, maeneo ya hostel yetu, ili iwe rahisi kumtoa Careen kutoka chuo mpaka hostel kabla Peter hajamtuma Nasra na Abdulrahman kumfata Careen chuo.
.
Mipango ilikua hivi, Abdulrahman atakua na Nasra kwenye gari ili kumfata Careen chuo, Abdulrahman atafanya kila jambo ili kuchelewa kufika kumchukua Careen.
Atakitumia kipindi hiko kujenga ukaribu na Nasra.
Wakati Ramadhan akitumia kipindi hiko kumchukua Careen kumleta hostel.
Na zitatumika kila mbinu ili kumfanya Careen akose kuenda kwenye party aliyo andaa Peter.
.
Niliona mchezo utakua mwepesi sana, na nilijihisi kushinda mechi kabla ya yeyote yule.
Pindi bado tunajadili kabla gari haijaanza kuondoka, ndipo Peter alipopiga simu na kumuuliza Abdulrahman yuko wapi, na nani?!
.
Abdulrahman: Niko Posta Peter, peke yangu. - (Ikabidi adanganye).
.
Peter: " Niko maeneo hayo hayo, nimekuja kwa Dr. Leonard, nipo kwa nje hapa nimeona gari kama yako imepark."
.
Tukastuka wote, tukanong'onezana Abdulrahman adanganye sio gari lake, itakua amefananisha.
.
Pindi anajiandaa kumjibu, ndipo Peter alivyozungumza "Ndo lenyewe, nimeona plate number".
.
Sote tukabaki tunashangaa tusijue nini cha kufanya, kutazama huku na huko ndipo tulimuona Peter akiwa umbali wa hatua 10 kukaribia upande niliokaa mimi.
.
Tulichanganyikiwa ghafla, Abdulrahman akashika kichwa.
.
Mwisho nilibaki nimeduwaa nisijue cha kufanya.
.
*Je nini kitatokea?? Peter atajisikiaje kuwakuta Abdulrahman na Chris pamoja???
. Usikose sehemu ya 13
#Itaendelea
#Ilipoishia: Baada ya Peter kuliona gari la Abdulrahman, ndipo alipoaanza kupiga hatua kuelekea mahali gari lilipo.
Tulipagawa sana huku nikiwa natafuta mahali pakujifichia ndani ya gari.
Lakin sehemu zote nikaona kama Peter akiingia ndani ya gari itakua rahisi kuniona.
.
Nikabaki nimeduwaa, sikujua nini cha kufanya, wala Abdulrahman hakujua nini cha kufanya huku akiwa ameshika kichwa.
#Inaendelea: Pindi Peter anakaribia kama hatua 6 hivi kufika kwenye mlango nilipo mimi, ndipo simu yake ilipoita.
Nikaona amechukua simu na kuanza kuongea, nami ndipo nilipopata wazo la haraka kuwa Abdulrahman ashuke na kumfata huko huko alipo.
Abdulrahman alinielewa, na kwavile gari ilikua na tinted, tuliamini kuwa hakuweza kutambua Abdulrahman yuko na nani ndani.
Tukashauriana kuwa endapo wataondoka wote kuelekea kwa Dr Leonard, basi nami nitatumia hiyo nafasi kutoka ndani ya gari na kuelekea kwenye kituo cha daladala.
Abdulrahman akanielewa na kushuka ndani ya gari kumuwahi Peter.
Peter alipomaliza kuongea na simu, akawa akionekana akimuuliza maswali mengi Abdulrahman huku akiwa na wasiwasi na gari la Abdulrahman.
Lakini mwisho walielewana na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye ofisi ya Dr Leonard.
Nilipoona tu wameshaingia ndani ya mjengo, ndipo nami nikashuka na kuelekea kwenye kituo cha mabasi kurejea chuo.
Nilipofika chuo niliwakuta Careen na Nasra wanapiga story, nikajua leo ndo siku ya kumthibitishia Careen kuwa Nasra sio girlfriend wangu.
Nikawasalimia "Habari zenu wadada".
Careen: Mh hadi mama watoto nae unamwita dada - (Akimaanisha Nasra).
.
Nikamjibu "Sijapata bado, nikimpata nitamsalimia hivyo".
Careen akabaki ananishangaa sana, nikaona nisipoteze muda, nikaondoka hapo hapo kuelekea hostel.
Nilimuacha Careen akiwa na maswali mengi sana kichwani.
Niliporudi hostel nilikutana na Ivan, Ramadhan na Hasheem na kuwapa mipango ya kumfanyia surprise Careen kwa siku ya kesho.
Lakini nilificha kuhusu mpango wa Abdulrahman na Nasra, ili Ivan asijue kinachoendelea kwa upande mwingine.
Majira ya saa 6 usiku, ya usiku wa kuamkia tarehe 12.
Niliandika ujumbe mzuri sana, na wenye kubeba hisia.
Nakumbuka Dr Leonard aliniambia jitahidi sana uwe miongoni mwa watu wa tatu wa kwanza kumtakia kheri ya siku ya kuzaliwa, na ujumbe wako usiwe mfupi tu, jaza pilipili, chumvi na ndimu humo humo.
Ulipomfikia Careen, akausoma na kunipigia simu muda huo huo.
Alikuwa mwenye furaha sana, na kwajinsi nilivyompa sifa na maneno yaliyojaa hisia, alijiona mwenye thamani sana.
Akaniambia "Chris, wewe ndo mtu wa kwanza kunitakia kheri ya siku yangu ya kuzaliwa, na nashangaa umejuaje"
Nikapigwa swali, nikaona bora nijibu kiujanja ujanja "Anh ukiijua thamani ya mtu maishani mwako, kamwe huwezi shindwa kuijua siku yake muhimu kama hii".
Careen alifurahi sana, lakini akakumbuka kuniambia "Chris nimepata uthibitisho kuhusu wewe na Nasra kutoka kwa Abdulrahman, ameniambia ukweli kuwa yule sio girlfriend wako".
Nikajua kuwa tayari Abdulrahman ameshasawazisha mambo.
Nikamweleza kwa undani, kisha tukatakiana usiku mwema na kila mtu kulala.
Kesho yake, siku ya tarehe 12, tulianza maandalizi mapema asubuhi.
Na kumaliza mida ya mchana.
Sikwenda chuo kabisa, na ni Ramadhan pekee ndiye aliyekuwa chuoni akipeleleza kila hatua ya Careen.
Careen aliuliza kuhusu mimi, alipewa majibu kuwa najisikia homa ndomana sikuja chuo.
Alinijulia hali kwa simu, na kuniambia kuwa kabla ya kuondoka, atakuja kuniona hostel.
Nami nikaona mpango wetu wa kwanza wa kumpata Careen ushatimia.
Ilipofika majira ya saa 11, Abdulrahman akanitumia message kuwa Kiota Jungle mambo yako tayari, na Peter amemtuma yeye pamoja na Nasra kuenda chuo kumfata Careen.
Kwahiyo itumike mbinu ya haraka ya kumtoa Careen chuo ili wao wakienda wasimkute.
Na tutumie kila njia ili simu ya Careen aidha isipatikane au iite tu bila kupokelewa.
Tulipoona watu kadhaa tulio waalika kisiri tayari wameshafika kwenye party.
Papo hapo, tukamtumia message Ramadhan ajiandae kuigiza kuwa kapokea taarifa mbaya kunihusu mimi.
Kisha Hasheem akampigia simu Careen na kumuambia kuwa "Chris ana hali mbaya, wahi hostel tumsaidie".
Careen: "Mungu wangu, nakuja hapo haraka, ngoja nimfate Ramadhan anilete".
.
Akazungumza haraka na kukata simu, kisha kumuwahi Ramadhan ambaye nae alijifanya kachanganyikiwa.
Haraka haraka wakatoka nje ya geti, na kupanda bodaboda.
Kwavile walikua na haraka na purukushani za kuwahi hostel, Careen alipokea simu ya Abdulrahman kwa haraka na kumjibu "Nitakupigia, nitakupigia".
Abdulrahman hakutaka kuhoji maswali mengi sababu alijua kinachoendelea.
.
Ikabidi ajifanye anapiga piga kila mara, lakini Careen hakuweza kupokea.
Abdulrahman akanitumia message "Kazi nzuri, mipango inaenda vizuri, nami ndio nakaribia kwenye geti la chuo''.
.
Abdulrahman na Nasra wakaingia ndani ya chuo na kujifanya wakimtafuta Careen kila pande baada ya kuona simu yao haipokelewi.
Kipindi mimi na Hasheem tuliwaambia wageni waliokuja kwenye party wote waingie ndani, tukaondoa viatu vyao nje, tukafunga mlango, taa zikazimwa, na kuwaomba wote wanyamaze kimya ndani ili isijulikane.
Ghafla tulisikia mlango unagongwa, tukajua wazi itakua ni Careen na Ramadhan.
Hasheem alienda kuwafungulia mlango, akawakaribisha.
.
Ile kipindi Careen anaingiza uso tu, ndipo taa zikawashwa, kelele za watu waliomo ndani zikapigwa "Surpriseeeeeeee".
Careen alistuka sana, akawa amebaki ameshika mdomo wake, hakuamini alichokiona, alijikuta akianzwa kulengwa na machozi.
.
Watu wote ndani wakaanza kuimba "Happy birthday to you".
Nilimsogerea Careen, na kumkombatia, hakuwa akiamini alichokiona, nilibaki nimemlaza kifuani mwangu nikimwacha akiwa analia kwa furaha.
.
Kwavile tulijua kuwa Peter na Abdulrahman watapiga simu ya Careen mara kwa mara, ndipo mpango wa kuifanya simu ya Careen iwe busy ukafata.
Ivan alimuomba simu Careen ili aitumie kumpiga picha za ukumbusho, Careen alikubali na kuitoa.
.
Hasheem akamnong'oneza, yeyote atakaye piga, basi atakatiwa simu.
Sherehe ikaendelea, vinywaji vikagaiwa, picha za ukumbusho zikapigwa na wakati wa kukata keki ulipofika, kama kawaida mwenye siku yake akakata keki na kuwalisha wote.
.
Lakini kwangu siku hiyo ilikua tofauti, nililishwa na kupewa busu zito la shavu.
Na Ivan hakufanya makosa, alikumbuka kupiga picha pindi ananibusu.
Peter alihangaika sana kumtafuta Careen kwenye simu, lakini simu yake haikupokelewa, Ivan alikua anakata kila muda.
Abdulrahman nae alipiga simu za kinafki ili aonekane anamtafuta Careen, mwisho akajifanya amechoka na kwenda kupumzika kwenye gari na Nasra.
Akatumia muda huo kuyajenga na Nasra na baadae wakaondoka na kurudi Kiota.
Peter alivurugwa vya kutosha, alikua akituma messages kila sekunde kwa Careen na Abdulrahman.
Abdulrahman akanitumia message "Peter atakufa kwa presha, huko kwenye party yake ni aibu tupu".
.
Nikamjibu "Mwache ale keki yake mwenyewe".
Tulicheka sana na marafiki zangu.
Nakumbuka ile dollar 1000 niliyopewa na Abdulrahman niliitumia vizuri kwa bajeti, na mwisho kupata zawadi nyingi kwaajili ya Careen.
Na kiasi kingine niliwapa marafiki zangu ili nao wapate zawadi ya kumpa Careen ili sote kwa pamoja tuonekane tulijipanga.
Hii ilikua ni mbinu aliyotoa Dr Leonard, alisema itamfanya Careen ahisi kuwa hii party ilipangwa siku nyingi, hivyo itamfanya ajione mwenye thamani na kupendwa sana.
.
Wakati wa zawadi ulipofika, sote tulimtunza, Careen hakuamini yote yalikuwa yakitendeka, aliona kama ndoto.
Sherehe iliisha mida ya saa 3 usiku, na mwisho wageni wakaondoka, na kupata wasaa wa kuzungumza na Careen machache.
Tulijikuta tukizungumza mengi sana, Careen aliniambia kuwa katika maisha yake hakuwahi kulia machozi ya furaha kama siku hiyo.
"Ndio mara yangu ya kwanza kufanyiwa surprise kubwa kama hii, hakika umeifanya siku yangu kuwa yenye kumbukumbu kubwa sana maishani mwangu.
Nimejiona mwenye thamani maishani mwako, asante kwa kunijali na kunipa kipaumbele "- (Alizungumza kwa hisia, huku akiwa mwenye furaha mno).
Akafungua saa mkononi mwake, kisha akachukua mkono wangu wa kushoto na kunivalisha.
Akanitazama usoni na kunipa tabasamu mwanana, kisha kuniambia "Tunaishi ndani ya dunia kwa muda maalumu, naomba saa hii iwe ukumbusho kwako juu ya ahadi nitakayo iweka kwako ".
Nikaitazama saa, kisha kunyanyua macho kumtazama Careen, akasema "Nakuahidi nitakuthamini siku zote za maisha yangu. Na endapo nitasahau ahadi yangu, saa hii itumike kunikumbusha."
.
Moyo wangu ulizidi kupata amani sana, kwa upendo nilionao juu yake, nilijikuta namkombatia na kumwambia "Hakika wewe ni wathamani sana kwangu, saa hii pia itumike kunikumbusha umuhimu wako maishani mwangu".
.
Ivan alipiga picha ya ukumbusho tena tukiwa tumekombatiana.
Careen akaomba simu yake, na akawa anatazama picha.
Lakini ghafla simu ya Peter ikaingia, Careen akapokea.
Peter akawa anaongea kama mtu ambaye tayari ameshapanic, akamwambia Careen aende Kiota Jungle.
Careen akauliza "Saa 3 hii??"
Nikaona anatafakari lakini mwisho akakubali, na kukata simu.
.
Nikaona sasa Peter nae anaweza akapata nafasi kama niliyopata mimi, nikahisi kama mchezo wetu unataka kuharibika.
shida yetu ilikua Careen alale na mawazo ya surprise yangu tu.
Pindi bado atafakari.
.
Lakini ghafla simu ya Careen ikaita, kutazama kwenye screen ni baba yake.
Alipopokea tu akakumbana na sauti ya baba yake iliyojaa ukali, alifokewa vibaya sana kwanini amechelewa kurudi nyumbani mpaka sasa saa 3 na dakika 46 hajarudi.
.
Careen kwa uwoga wa ukali wa baba yake, akamtumia message Peter hapo hapo kuwa hawezi kwenda.
.
Na kuniaga kwa kunikombatia, na sasa sikutaka kufanya makosa, nikampiga busu la kwenye paji la uso.
.
Na kumtafutia usafiri wa kurudi wa kurudi kwao Tabata.
.
Wakati huo huo nikakumbuka kuchukua simu na kumtext Abdulrahman, "Kaka Tumefanikisha. Pongezi nyingi sana kwako".
.
Akanijibu "Nami nimefanikiwa kupata namba ya Nasra, na kujenga nae ukaribu zaidi".
.
Akaniongeza "Niko na Peter hapa, kama kaloweshwa maji tank zima, kwa jinsi alivyolowa jasho. Waliokuja kwenye party wamemcheka sana".
.
Nikacheka sana, na kuwachekesha kina Hasheem.
Ivan akatoa wazo, kwanini tusiharibu usiku wa Peter kwa kumtumia picha ya party.
.
Nikachukua simu, na kumtumia picha ya Careen akinilisha keki, na kumtumia maneno "I wish ungekuwepo".
.
Muda huo huo Abdulrahman akapiga simu, "Chris umefanya nini??? Mungu wangu" - (Akauliza kama aliye changanyikiwa)
.
Nikamuuliza "Vipi kwani??? ".
Akaniambia jambo ambalo lilinifanya nibaki mdomo wazi.
#Ilipoishia: Ivan alitoa wazo la kuufanya usiku wa Peter kuwa mbaya zaidi.
Kwavile aliandaa party kwaajili ya Careen, na hakufanikiwa kumpata Careen, hivyo kumtumia picha tukiwa na Careen kwenye party ingemfanya aumie zaidi.
Nikaona ni wazo zuri sana, nikachukua simu na kufungua WhatsApp, na kumtumia picha Peter nikiwa nalishwa keki na Careen.
Pamoja na ujumbe "I wish ungekuepo".
#Inaendelea: Baada ya dakika kadhaa, Abdulrahman akapiga simu na kuniuliza kama mtu aliyejawa na wasiwasi sana.
"Chris umefanya nini!?? Mungu wangu" - (Aliuliza Abdulrahman).
Nilishangazwa na swali la Abdulrahman, ikabidi niulize "Kwani vipi??? "
Tukatazamana na tusijue nini cha kufanya, tukabaki tukiulizana itakuaje endapo jambo hili litakuwa kubwa zaidi ya tujuavyo.
Ivan ambaye ndiye aliyetoa wazo, akaanza kuonyesha ameingiwa na uoga mkubwa, lakini Ramadhan akasema "Kuna njia za kupambana na tatizo".
Sote kwa pamoja tukamtazama kwa makini zaidi kutaka kujua yale atakayo yasema.
Akafikiri kidogo kisha kusema "1: Kulishinda au kushindwa na tatizo huanzia ndani mwako mwenyewe, ukilichukulia tatizo kama ni kubwa sana kwako basi lazima utashindwa, na ukilichukulia kama ni dogo sana, pia utashindwa sababu utadharau kufikiri sana jinsi ya kulitatua.
Kinachotakiwa tulichukulie tatizo kawaida tu, na tuwe na imani kuwa tunaweza kulitatua, na kwa imani tuliyo nayo juu ya kulishinda tatizo ukimjulisha na imani tuliyo nayo juu ya Mungu ambaye kamwe hashindwi kitu, basi hakuna tutakacho shindwa kwenye tatizo hili".
Tukawa tumebaki kimya tukitafakari maneno yake, na mwishowe akaendelea "2: Kuwa na utayari wa kulikabili tatizo, na kuanza kulitambua tatizo, tafuta njia za kulitatua tatizo, na pia chukua hatua za kulitatua tatizo, na uwe na njia za kuliepuka tatizo ili siku nyingine lisije jirudia".
Akanyamaza kidogo, ndipo sote kwa pamoja tukaanza kuondoa wasiwasi wetu na kuanza kujijenga kiimani kuwa haliwezi kuwa tatizo kubwa sana.
Ivan akazungumza "Njia pekee ya kulitatua tatizo, sio kwa kulikimbia, ni kwa kuwa tayari kulikabili haijalishi litakua kubwa kiasi gani, tufate vile Ramadhan amesema.".
Nikaona njia ya kwanza ni kumtafuta Abdulrahman atueleze vizuri kilichotokea, ili tuwe na utayari wa lolote litakalo tokea.
Nikampigia simu, lakini alikata.
Tukabaki tunawaza la kufanya, lakini ghafla ikaingia message kutoka kwa Abdulrahman akielezea tukio lililo tokea.
Alisema " Peter alikuwa kachanganyikiwa baada ya kumtafuta Careen bila mafanikio.
Akazidi kuvurugwa baada ya kuona watu waliokuja kwenye party wakianza kuondoka mmoja baada ya mwingine.
Kuna rafiki yake mmoja ambaye ni mtani wake sana, anayeitwa Hans, ambaye alilewa sana, akawa anamtania Peter kwa sauti ya juu "Wamekuibia wajanja, ona hajaja sasa."
Peter kwa hasira aliyonayo alijikuta anamtukana rafiki yake, na Hans kuamua kuondoka na marafiki wengine.
Baada ya muda kidogo Peter alirejesha furaha yake pindi Careen alipopokea simu yake na kujibu anakuja.
Aliruka ruka sana kwa furaha, wakati huo tulikua tumebaki watu wanne tu(Abdulrahman, Nasra, Magdalena(dada yake Peter), na Peter mwenyewe).
Tukarudi kuweka vitu vizuri, lakini ghafla furaha ilipotea tena baada ya Peter kutumiwa message na Careen kuwa hatofika kwenye party."
Message ya kwanza aliyotuma Abdulrahman iliishia hapo, tukawa bado tunatafakari.
Nilianza kuyahisi machungu ambayo Peter aliyapitia.
Pindi bado tunawaza na kuwazua, ikaingia message nyingine.
Ikisema "Peter alivurugwa kabisa, akawa kama aliyechanganyikiwa, akili yake haikumkaa sawa kabisa.
Alikua akizunguka zunguka, ghafla simu yake ikaita muito wa message.
Akachukua simu haraka akidhani labda ni Careen katuma, mwisho tulimuona kama amechanganywa na alichokiona, hali yake ilibadilika ghafla na kudondoka chini.
Sote tukamuwahi kumtazama, na kuanza kumpa huduma ya kwanza.
Niliiwahi simu na kutazama alichokuwa akisoma Peter, nikakuta ni wewe umetuma picha, lakini kabla sijaifuta dada yake alinipokonya simu na kutazama kilichomfanya kaka yake azimie".
Message iliishia hapo, tulianza kupatwa na wasiwasi zaidi, niliwaza sana itakuaje endapo Magdalena(dada yake Peter) atalifanya tukio liwe kubwa zaidi.
Ivan akazungumza "Mh majanga haya "
Tulinyanyua macho yetu na kumtazama, Hasheem alishindwa kuvumilia na kuropoka "Unasema majanga wakati wewe ndo uliyesababisha, ona sasa ulilosema tufanye lishaleta madhara". - (Alizungumza kwa kulalamika na ukali zaidi).
"Eeeenheee hebu acheni kuanza kutupiana lawama, tunahitajika kuwa tayari kwa lolote lile. Kama Ivan alitoa wazo bovu, mbona wewe hukukataza lisitekelezwe, tena ukashabikia kabisa". - (Alizungumza huku akimtazama Hasheem).
Nikaona sasa kama wanaanza kutupiana lawama wote, nikawaambia "Tulieni tujue tunalimaliza vipi".
Mabishano yakaendelea kati yao, Hasheem alizidi kumshtumu Ivan kwa kutoa wazo bovu lililosababisha madhara makubwa.
Pindi bado mabishano yanaendelea.
Abdulrahman akatuma message nyingine "Peter ameshapatiwa huduma ya kwanza, amezinduka japo ameumia kiasi kwenye mkono wa kulia kutokana na kujigonga sehemu aliyodondokea.
Tunamuwaisha nyumbani, atakuwa chini ya uangalizi wa daktari wa familia.
Ila na wasiwasi na dada yake ambaye ndiye mwenye simu, nitakujuza zaidi".
Nikashusha pumzi nzito, nikasema afadhali Peter ameamka.
Nasi tukarejea hostel kupumzika, usiku niliwaza mengi sana, niliwaza jinsi papara zangu na hasira zangu zinavyoharibu mambo yangu kila siku.
Nikajiona kama mtu mwenye matumizi madogo ya ubongo, sababu kila siku navurunda mimi tu.
Kesho yake majira ya saa 2 asubuhi, nilipokea simu kutoka kwa Careen ambaye alikua ananiambia kuhusu afya ya Peter kuwa anasumbuliwa na tatizo la Hypertension(Presha ya kupanda), pamoja na maumivu ya mkono aliojipigiza wakati amedondoka.
Lakini ghafla akili yangu ilivurugika baada ya Careen kuniambia anataka twende wote Kunduchi Beach, nyumbani kwa kina Peter, tukamjulie hali.
Nikaona kama Careen anataka kunipeleka kwenye tanuri la moto.
Nikajitahidi kukataa lakini akanilazimisha na kuniambia "Urafiki gani huo Chris ambao mwenzako akipatwa na matatizo huendi??? "
Nilitamani kumweleza Careen kwanini nakataa kwenda, lakini nikaona itamfanya anichukie.
Nikakubali na akaniambia tukutane Simu 2000, kama tulivyo kutana siku ya birthday ya Peter.
Akakata simu, nami nikaona bora niwatumie message marafiki zangu kuwajulisha kuwa Careen amelazimisha niende nae kwakina Peter, na nimemkubalia.
Abdulrahman akajibu "Onh My God, You're dead".
Ramadhan nae akajibu "Mmmmh ulishindwa kukataa???!".
Ivan "Chris unajipeleka mwenyewe"
Hasheem "Mungu wangu"
Message zao wote zilizidi kunichanganya, nikajiona kama nimefanya kosa kubwa sana kukubali kwenda na Careen.
Lakini nikajipa moyo na kufanya kama Careen alivyosema.
Tulifika Kunduchi Beach majira ya saa 6 mchana, Abdulrahman alikuja kutupokea getini.
Akamuacha Careen ametangulia mbele na kunisimamisha kwanza tutete jambo.
Akazungumza kwa kingereza akimaanisha "Maamuzi uliyofanya leo ya kujileta mwenyewe kwenye mdomo wa mamba, ni mabaya sana.
Wamemwacha mpaka sasa apumzike, party ilikua ya siri na wazazi wake wameshagundua kilichotokea na wanajaribu kuchunguza kwanini mtoto wao alizimia, na party iliandaliwa kwaajili ya nani "
Maneno yake yalinitia uoga zaidi, nilizidi kujutia maamuzi niliyochukua ya kuja kwa kina Peter.
Abdulrahman akaniambia "Twende ndani, ila hakikisha unakaa mbali na Magdalena maana anajua wewe ndiye chanzo cha matatizo yote ya kaka yake.
Aliona picha yako uliyomtumia Peter na jina lako. "
Nikazidi kupata wasiwasi, Careen alisimama kwa mbele kidogo akitusubiri.
Abdulrahman akaniambia "Twende", lakini nilibaki nimesimama nisijue nini cha kufanya.
Mawazo yakawa mengi kichwani, niendelee kuwafata, au nikimbie hapo hapo.
.
Careen akanitazama na kuniambia "Chris tunakusubiri wewe", ndipo nilipostuka na kuanza kupiga hatua kuwafata nyuma.
Tulipofika ndani tuliwakuta wazazi wa Peter wakiwa sebuleni, tukatambulishwa na wazazi wao walifurahi sana kuona wanafunzi wenzake na mtoto wao, wamekuja kumjulia hali mtoto wao.
Mfanyakazi alikuja na kuuliza aina ya vinywaji tunavyotumia, tukaletewa.
Tukaombwa kusubiri kidogo tutaenda kumuona Peter pindi daktari akimaliza kumkagua ndani.
Ghafla daktari alitoka, na wazazi wa Peter wakatoka nae nje ili kuzungumza nae.
Pindi bado tumezubaa zubaa, kutupa jicho mbele ndipo macho yangu yalivyokumbana uso kwa uso na Magdalena.
Moyo ukanipiga "Paaah", nilianza kuliona joto la jiwe, sofa nililiona kubwa sana nikaanza kujisogeza karibu na alikokaa Careen.
Magdalena alinipiga jicho lililojaa chuki, kama mtu aliyekuwa akimaanisha "Nakutamani wewe nikung'ate ng'ate".
Abdulrahman akatuambia "Tayari twendeni mkamsalimie".
Nilizidi kuona nyumba ya moto, ndani aliko Peter nilijua hapafai kuonekana hata sura yangu.
Na hapa sebuleni tayari kashakuja Magdalena ambaye anaonekana ana chuki moyoni mwake juu yangu.
Nikawa bado nafikiria, nikatolewa kwenye dimbwi la mawazo na sauti ya Careen aliyeita "Chris, Chris, nyanyuka".
Ndipo nilipostuka kuwa wenzangu tayari walishanyanyuka.
Nami nikanyanyuka na kuanza kuwafata nyuma, lakini presha ilinizidi baada ya kugundua kuwa njia tunayopita kwenda chumbani kwa Peter, ndio njia hiyo hiyo aliyosimama Magdalena.
Nikaanza kuongeza speed ili kuwawahi kina Abdulrahman.
Nikawa nao sambamba, lakini tulipomkaribia Magdalena ndipo niliposhangaa sote kuona wenzangu wote wamesimama.
Abdulrahman akafanya utambulisho, akaanza na Careen.
na pindi alipohamia upande wangu, hali ilikua tofauti.
Abdulrahman: "Na huyu anaitwa..." - Kabla hata hajamalizia, Magdalena akamalizia "Chris".
Nikatetemeka, akanipiga jicho, akakunja uso wake.
Baada ya utambulisho safari ikaanza kuelekea chumbani.
Lakini nilipopiga kama hatua mbili mbele, ndipo niliposikia sauti iliyonitetemesha.
"Chris" - Aliita kwa nguvu magdalena.
Nikastuka, sote kwa pamoja tukageuka kama vile tuliitwa wote.
Tulivyomtazama, akatoa ishara ya vidole kuwa Careen na Abdulrahman waendelee na safari, ananitaka mimi peke yangu.
Nikazidi kupata presha, nilihisi kama mwili umeanza kutoka jasho jembamba.
Mikono na miguu ilikua ikinitetemeka mpaka nikahisi naweza jikuta nimejikojolea hivi hivi.
Damu ikanichemka, mapigo ya moyo yalizid kunienda mbio.
Abdulrahman alizidi kupata wasiwasi, sababu alijua kilichokua kinaendelea.
Lakini nae aliondoka akijua kuwa labda ninaweza kuumaliza huu msala mwenyewe.
Magdalena akanisogerea, na kuchukua simu ya kaka yake, na kunionyesha message na picha niliyomtumia Peter kwenye WhatsApp.
Akaninyooshea simu, nikaitazama, na kuzidi kupata wasiwasi.
Akaniambia "Nafurahi umejileta mwenyewe, na maswali zaidi ya elfu moja. Na yote unahitajika kunijibu vizuri ".
Akazungumza kwa sauti ya chini iliyojaa hasira.
Huku akinitolea macho na kunikazia.
Nikaona nimuepuke, nikamjibu "Na haraka nataka kumjulia hali mgonjwa".
Nikazungumza kwa haraka na kugeuka nikitaka kuondoka.
Akanivuta shati na kunigeuza, kisha kunishika kwa nguvu shati langu sehemu za vifungo, na kunibana ukutani.
Akanikazia macho na kuniambia "Utanijibu maswali yote kabla sijakufanya chochote kibaya".
Sikutaka kuwa dhaifu kwa mwanamke, nikaanza kuhangaika kuinyofoa mikono yake na mwili wake kwenye mwili wangu.
Nikahangaika navyoweza lakini Magdalena alikua na mwili mnene, na mwenye nguvu, ukichanganya na ukimbao mbao wangu, ikawa inanipa shida.
Nikafanikiwa kuinyofoa mikono yake kwenye shati langu, lakini nilistukia vifungo vyote vimeachia na kudondoka chini.
Nikabaki na singlendi ikionekana.
magdalena hakukubali, akanikamata kwenye mbavu na kunibinya, nami nikaona nimsukume kifua niweze kumtoa vizuri.
.
Ghafla ilisikika sauti iliyojaa hasira, iliyotamka maneno ya kingereza yakimaanisha "Mke wangu unafanya nini?? "
Ndipo nilipostuka, nikakumbuka kuwa mikono yangu ilikua kifuani kwa Magdalena, huku Magdalena akiwa ameshika mbavu zangu.
Tukastuka na kuachiana, niliona tayari msala mwingine ushatokea.
Magdalena alichanganyikiwa ghafla asijue cha kufanya.
Na kwajinsi mumewe Magdalena alivyoona shati langu lilivyokuwa wazi kutokana na kukatika kwa vifungo, mikono yangu kaikuta iko kifuani mwa mkewe.
Huku mkewe akiwa amenishika mbavu zangu.
.
Alijikuta anafoka kwa ukali kwa kingereza, akimaanisha "Yani unafanya mapenzi na mgeni??? Tena hadharani???"
.
Hapo ndipo nilipotamani ardhi ipasuke, nidumbukie niepukane na aibu hiyo.
Kupiga jicho pembeni, niliwaona Abdulrahman na Careen waliotoka chumbani haraka kuja kushuhudia.
.
Ghafla ikasikika sauti nyuma yangu, "What??? ".
Kugeuka nyuma alikuwa ni baba na mama yake Peter wakija kwa hasira.
.
Hapo nilisimama kama mstimu, nisijue nini cha kufanya.
. Je Chris atafanya nini??? Nini kitatokea???
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.