Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)

Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)

Arafu uyo careen anauzuri gani??? Ata hurem mke wa sultan Suleiman hakuwa ivyo na ndiyo white dahh 😁
 
Hauna mk
Basi siku yako inakuja
Broo mm ni kijana mdogo sina mke na hio siku aisee naomba isije, iishie hukohuko
Human love is pure nonsense, it ain't everlasting, human love is based on frames of references(its conditional)
 
MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!

Sehemu ya Kumi na Tisa
.
#Ilipoishia:
Wakati Careen anarejea mahala nilipo, huku akiwa amebeba vinywaji.
Ghafla nilistukia nimekombatiwa kwa nyuma, nikageuza uso na kumtazama aliyenikombatia.
Sikuamini macho yangu, nilikombatiwa na mtu ambaye simjui na wala sijawahi kuonana nae mahala popote.
Pindi bado natafakari, ndipo alipoongea tena kwanguvu "Chris baby wangu, nilikumiss sana".
.
Sikutaka kumchelewesha, nikamsukumiza, akadondoka chini.
Kutazama mbele aliko Careen nilimuona akiwa anaondoka kwa hasira.
.
#Inaendelea:
Nikaanza kumkimbilia huku namuita "Careen, Careen "
Lakini kabla hata sijafika mbali nilistukia nimevutwa tena shati na mtu aliyekuwa akiongea kwa hasira "Nipe simu yangu, nataka simu yangu "
.
Sikuelewa huu mchezo uliotokea, nilishangaa haya yote anayo yafanya huyu msichana.
Nikamtoa mikono yake, na kumchapa kibao.
Wakati huo huo watu wakajaa na kutuzunguka.
.
"Dada vipi kwani? Kakuibia au?? Sema tumchezeshe kichapo"- Aliuliza mmoja wa watu waliozunguka.
Yule msichana akazungumza kwa sauti ya juu "Huyu bwana wangu, leo nimemfumania na demu mwingine.
Sasa kama anampenda huyo demu mwingine, basi anirudishie vitu vyangu nilivyo wahi kumuhonga" - (Alizungumza huku kanikunja kora).
.
"Mrudishie vitu vyake" - Mtu mwingine aliropoka.
"Mzee baba kumbe unalishwa!??? Hahahaha wenzako wanachepuka kiakili, we boya kweli yani.''- Mwingine akaongea.
Watu walizidi kutoa maneno ya kashfa, na wengine kuanza kutoa kelele "Mrudishie vitu vyake alivyokuhonga".
.
"Niachie'"- Nilizungumza kwa hasira na kuanza kukukuruka nae.
Sikutaka kumlazia damu, nikamtia vibao mfululizo.
.
Watu wakaniwahi na kunishika.
"Sister sema, huyu boya ulimuhonga nini na nini?? Tuvichukue sasa hivi'' - Aliuliza jamaa mmoja ambaye naye nahisi alikua ndani ya mpango mmoja na yule binti.
.
Nilizidi kupata aibu kwa kile kilichokuwa kinaendelea, lakini nilivyosikia hilo swali nikajua wazi nimeponyeka sababu yule msichana hajui vitu nilivyo navyo.
.
Akaropoka "Simu ", wengine wakaitika "Haya mpe simu yake".
Kwavile nilijiamini, nikajikuta nauliza "We umenipa simu??? Haya itaje ni simu ya aina gani?? "
.
Lakini nilijikuta nazidi kuuaminisha umati wa watu kuwa kweli nimehongwa, baada ya yule msichana kuitaja aina ya simu ninayo itumia.
Aliongea kwa kujiamini "Nimemuhonga Samsung J1 Ace, rangi ya Gold, ina cover jeusi".
.
Hakukosea hata kitu kimoja, hapo nilijikuta nazidi kushangaa haya yote yanayo nitokea.
"Haya itoe sasa umpe, usipende vya bure mtoto wa kiume utaolewa".
.
Sikukubali na nilisema hata wanipige sitoi kitu changu chochote.
Muda huo huo umati ukatawanyishwa na security guard.
Moyo ulisema "Afadhali nimeponyeka".
Walinikamata pamoja na huyo msichana na kwenda kutuhoji.
.
Kwa maelezo ya yake, iliwafanya security waamini kuwa ni kweli ni mpenzi wangu, sababu alizungumza utadhani ananijua.
Na kutaja vitu ambazo kweli ninavyo na hata walivyoomba wathibitishe, niliwapa na kujikuta naumbuka mimi.
.
Walitushauri twende nyumbani tukamalizane kimya kimya na kutuachia.
Nilitoka nje haraka na kumsubiri yule msichana ili nimuhoji vizuri.
Alionekana ni wa uswazi kutokana na dera alilovaa, wigi la bei rahisi, rangi yake aliyojichubua, na sauti yake kama radio mbovu.
Alionekana ni mtu anayependa shari muda wote na wala hana aibu, na inaonekana hii ndo kazi yake.
.
Alivyotoka tu akanisogerea na kuzungumza kwa sauti y chini "Mdogo wangu hapa mjini, tuliza ball. Usipende kushindana shindana na wenye mkwanja, utachezea chuma cha moto" - Alizungumza kwa dharau.
.
Nikamvuta mkono na kumuuliza "Nani kakutuma??? "
.
Akanitolea macho kama chura, na kunifokea "Wee weee wee babu tafa, tena unikome.. ooonh ushindwe babu kushika shika usivyo vijua.
Ndo unataka kunifanyia fujo?? Enh??? Nyoooo mxieeew.
Sasa kama hunijui mimi ndo Ashanti babu eenh.
Nipige nikuonyeshe " - (Alizungumza kwa haraka kama cherehani.)
.
"Sasa kama unataka kuchezeshewa kichapo na wanaume wa shoka, nipige uone.
Umewaona wale?? "- (Akazungumza huku akinionyesha kwa macho).
.
Nikageuza macho kuwatazama alionionyesha, nikaona kundi la wahuni watano.
Mmoja wao akaita "Oya Ashanti tusepe".
.
Nikamuachia mkono wake, akasonya na kuondoka huku akijitingisha japokuwa nyuma alikua kama kapigwa pasi.
.
Nilipatwa na wazo la kwenda kumtazama Careen maeneo yanapo egeshwa magari.
Nikidhani labda atakua bado hajaondoka, lakini sikumkuta.
Alikua tayari ameshaondoka, wazo likanijia na mimi niondoke.
.
Lakini ghafla nilistushwa na sauti ya mtu ikiniita kwa nyuma yangu.
"Chris"- Nikageuka haraka na kumtazama aliyeniita.
Sikuamini macho yangu, nilibaki nimeduwaa.
.
Nilikutana uso kwa uso na Peter akiwa na Ivan.
Niligundua kuwa kumbe mchezo wote huu ulisukwa na Peter na Ivan.
Nilipata ufumbuzi kuwa itakua Abdulrahman aliropoka kwa Ivan kuhusu safari yangu na Careen.
.
Peter akanitazama na kuongea "Najua unamtafuta Careen.
Usijali, yuko ndani ya mikono salama, Abdulrahman amemchukua na kumrudisha kwao.
Na kwajinsi navyomjua Abdulrahman, najua atamlisha maneno mengi Careen ili azidi kukuchukia.
Haha pole kwa kupokonywa tonge mdomoni". - Aliongea kwa dharau.
.
Nilitafakari kauli yake, nikajikuta najiuliza kimoyo moyo "Ina maana Abdulrahman naye yupo kwenye huu mchezo??''.
.
Ivan akaongea "Haya ni malipo ya kutuchezea akili mimi na Abdulrahman "
Peter naye akaongeza "Na ni mwendelezo wa ahadi yangu kwako kuwa hutashinda kamwe.
Na najua kuanzia sasa Careen hatokupenda tena, tukishamtumia picha na videos".
.
Nilistuka sana baada ya kusikia picha na videos, nikajua kuwa kuna mashambulizi zaidi yanakuja kwa hapo mbele.
Walipomaliza kuongea, wakaniacha na kuingia kwenye gari lao na kuondoka.
.
Nilibaki nimesimama na mawazo, sikujua la kufanya tena.
Niliwaza kumuomba Careen msamaha lakin bado nikawa nawaza "Je atanielewa kweli?? ".
.
Nilimuita dereva tax aliyenileta mwanzo, na kwavile sikuwa na pesa nyingi, akanirudisha mpaka Mbagala ambapo nilipanda daladala ya Gongo La Mboto kurejea Hostel.
.
Usiku kucha nilimtafuta. Careen kwenye simu bila mafanikio, simu yake ilikua imezimwa kabisa.
Na hata kesho yake ilikua inapatikana ila hakunipokelea kabisa.
.
Juma lililoanza, lilikua ni Juma ambalo tulikua tunaanza mitihani ya mwisho wa semester maarufu kama U.F.E(University Final Exam).
Sikuwa na furaha kabisa siku hiyo, na hata sikuwa nimejiandaa kwaajili ya mitihani.
Kichwa kilikuwa kimezidiwa na mzigo wa jina la Careen.
Pindi nafika maeneo ya chumba cha mtihani, nilishangaa kuona watu mbalimbali wakiwa wananitazama na kucheka.
Sikuelewa, nikajitazama juu mpaka chini labda nimevaa vibaya, lakini hapana nilikua nimevaa vizuri tu.
.
"Chris" - Nilisikia sauti ya Ramadhan akiniita.
Tukasalimiana, na kunipa pole.
.
Nilishangazwa na pole yake, nikamuuliza "Pole ya nini??? "
.
Akaniambia "Pole kwa yaliyo kutokea juzi".
.
Nikastuka, nikaanza kujiuliza amejuaje, lakini kichwani nikapata jibu kuwa huenda Ivan ndiye aliyemwambia.
.
"Kakuambia Ivan?? " - Nimamtupia swali.
Hapo hapo akachukua simu yake na kunionyesha videos na picha mbalimbali nilizopigwa wakati wa varangati kule South Beach.
Kilichonishangaza ni vile vipande vya video viliwekwa vile vipande muhimu tu ambavyo mtu yeyote akitazama lazima atasema kuwa ni kweli yule Ashanti ni mpenzi wangu.
.
"Darasa zima wameona hizo picha na videos, na hata Careen ametumiwa pia" - Ramadhan alizidi kunieleza.
.
Hapo ndipo mwili wangu ulipozidi kukosa nguvu, nikapepesa macho kila kona na kuona watu wanavyonitazama na kucheka.
.
Niliumia sana, nikakosa amani.
Niliingia kwenye mtihani lakini sikuufanya kwa akili yangu, nilikua hata sijui nilichokuwa naandika.
Hata nilivyotoka nje ya chumba cha mtihani, Careen alinipita kama hanijui.
.
Hata nilipomuita ili nimuombe msamaha na kumuelewesha, wala hakutaka kunipa nafasi ya kunisikiliza.
Usiku nilijitahidi kupiga sana simu, na kutuma message za kuomba msamaha na kueleza hali halisi.
Wala hakujibu, wala hakupokea simu.
.
Siku ya Jumatano, ya juma tuliloanza mtihani.
Nilituma message nyingi kwa Careen.
Wala hakunijibu, nikakata tamaa kabisa kuwa sasa sitompata tena Careen
.
Baada ya masaa 8 kupita, simu yangu iliita mlio wa message.
Nikajua tu itakua ni message ya Tigo wakitangaza promotion zao.
Nikaidharau, lakini baadae akili ikanijia hebu itazame hiyo message.
Huenda ni ya mtu muhimu.
.
Nikaichukua simu, kutazama kwenye screen ilikua ni message moja kutoka kwa Careen.
Nikapata shauku ya kutaka kujua alichonitumia, nikaifungua.
Pindi tu nataka kuanza kuisoma, hapo hapo mama akapiga simu.
Ikabidi nipokee simu yake, tukaongea muda mrefu lakini nilikua natamani nimuambie mama subiri kidogo nitakupigia nikimaliza kusoma message, lakini nilisita kusema hivyo sababu mama ni wa muhimu kuliko hiyo message.
.
Nilipomaliza kuongea naye, nikakata simu na tayari kuanza kuisoma message.
Nilipoanza tu maneno ya kwanza "Hizi video" hapo hapo simu ikazima chaji.
.
Nikapiga kelele kwa hasira "Anhaa" na kuirusha simu kitandani kwa hasira.
Nilidhani itatua kitandani na kutulia, lakini ilidunda mara mbili na kwenda kudondoka upande wa pili wa kitanda.
Nikashika kichwa nikijua tayari nishavunja kioo ca simu.
Kwenda kuitazama ilikua tayari ishaweka ufa kwenye kioo.

Nikaichomeka chaji na kuisubiria japo kwa dakika tano ili niiwashe.
Nilipoiwasha nikakutana na message mpya kutoka kwa mama akiuliza "Mitihani inaendeleaje??"
.
Nikamjibu message yake na kuendelea ya Careen.
.
Nikafungua message ya Careen, nikaanza kuisoma " Hizi video ni ushahidi tosha. Huyu dada hakuwa anaongopa. Vyote alivyosema ni vya ukweli.
Ishi maisha yako Chris, niache.
Nayajua machungu ya kusalitiwa, na kamwe siwezi vumilia kuwa na mwanaume msaliti.
Nilikupenda na kukuheshimu, lakini umejishusha CV. Achana na mimi".
.
Nilibaki nikiyatafakari maneno ya Careen, niliona machungu yake kupitia message yake.
Niliona jinsi gani bado ana kidonda cha kusalitiwa kwenye mahusiano yaliyopita, na sasa hataki rudia maumivu tena.
Moyo uliniuma sana, machozi yalinitoka hasa nilipowazia juu ya kumkosa Careen kwa kosa la kusingiziwa.
.
Nikaona nisipoteze nafasi hii, niombe msamaha navyoweza.
Akili yangu ilizidi kunivuruga.
.
Nikamtumia message mfululizo za kumuelewesha Careen kuwa hiyo ni mipango ya kina Peter.
Wala hakunielewa, tukawa tunabishana kwenye message, kipindi hicho nacho mama alikuwa akituma message na namjibu, huku akili ikiwa umevurugwa na Careen.
.
Baada ya muda nikastukia napigiwa simu tena na mama, kupokea nikasikia "Careen ndo nani!?? "
Nikashangaa Careen kamjuaje, akaniambia "Unanitumia message za mapenzi, unalia na kumuomba msamaha Careen.
Chris ukimaliza mitihani urudi nyumbani, dawa yako iko jikoni mpumbavu wewe ".
.
Alizungumza kwa hasira na kukata simu, nilibaki mdomo wazi.
Ikabidi nitazame messages, nikakuta nimechanganya za hovyo hovyo na nyingine zimeenda kwa mama.
.
Siku kadhaa zilipita bila kuzungumza na Careen, na marafiki zangu walibaki Ramadhan na Hasheem ambao pia sikuwaamini.
Siku ya mwisho ya mtihani, siku ya Ijumaa, kulikuwa kuna safari ya party baada ya mtihani.
Na party ilikuwa inafanyika Element Club.
Nilijua watu wengi wataenda, lakini sikutaka kwenda sababu nilijua kina Ivan pia watakuwepo.
Nilirudi zangu hostel kupanga vitu vyangu kwaajili ya safari kesho yake, nilitaka nirejee nyumbani kwa wazazi Arusha, nikajibu kesi yangu kwa mama.
.
Hakuna aliyejua kama naondoka kesho yake, zaidi ya Hasheem, Ramadhan, na Erick, mwanafunzi mwenzangu anayeishi chumba kinachofata hostel.
Ilikua ni siku ya huzuni kwangu, sikuwa na matumaini tena ya kuwa na Careen tena, nilijua nishampoteza.
.
Nikampigia simu Dr Leonard, na kumweleza jinsi marafiki zangu wanavyonizunguka.
Akaniambia "Chris una kasoro mbili.
Moja, hujiamini. Na pili, huna kifua. Na hivi ni vitu muhimu sana unavyotakiwa kuwa navyo.
Hujiamini ndomana unahitaji kuwa na backup, unahitaji watu wengi sana ili kumpata unayempenda, na hii ni hasara sababu penye watu wengi hapakosi unafki.
lakini kama ungejiamini na kubeba mahusiano yako kivyako vyako, wala usingekuwa na tabu ya kuwazia fulani kanigeuka.
Lakini pia kama ungekua na kifua, basi suala lolote kuhusu moyo wako, au mahusiano yako, basi lingebaki kuwa siri yako.
Marafiki zako hawahitajiki kujua linaloendelea kati yako na girlfriend wako. Unapowaambia siri za mahusiano yenu, basi inaweza leta madhara kama haya, aidha muachanishwe, au uibiwe mpenzi wako.
Awe ana madhaifu, muwe mnatoana out, au kufanyiana mambo mazuri, mipango yenu, kamwe usiyaseme kwa rafiki zako."
.
Maneno yaliniingia na kuona wapi nilipokuwa nakosea, nakujipa moyo mwenyewe kuwa sitarudia kwenye mahusiano yatakayofata.
Nilipokata simu, ikaingia message WhatsApp.
Kufungua ilikua ni picha imetumwa na Peter, akiwa na Careen, Abdulrahman, Nasra, na Ivan.
Na aliandika ujumbe "Natamani ungekuwepo".
.
Niliitazama sana, lakini sikuweza fanya lolote sababu tayari nilikua nishakata tamaa kuwa Careen hawezi kuwa na mimi tena.
.
Masaa mawili baadae, nikapokea message nyingine Whatsapp.
Kufungua ilikua ni Ivan aliyenitumia picha akiwa anampiga busu zito Nasra, na kunitumia maneno ya kingereza akimaanisha "Baada ya fitna zote ulizonifanyia... bado nimempata niliyemtaka.
Sina kinyongo na wewe tena, moyo wangu una amani".
.
Wakati huo huo Nasra akatuma nae picha na ujumbe "Siku zote kwenye maisha ni ngumu sana kukipata unachokitaka, utakipata kile unachostahili.
Asante kwa yote, siwezi kukuchukia, umenifunza kuwa maana halisi ya upendo ni kuthamini pale unapopendwa, sababu mara nyingi unapopenda huwa hupendwi."
.
Nilizidi kujiona mjinga sana, lakini tayari nilishakubali matokeo, nilishakubali kushindwa.
Nikaitazama saa ya ukumbusho aliyowahi kunipa Careen siku ya birthday yake, nilijikuta nalia sana.
Nilitamani usiku ungeisha haraka ili angalau niondoke ndani ya jiji hili la Dar es salaam, labda kumbukumbu za Careen zingefutika.
.
Kesho yake asubuhi nilifatwa na Hasheem na Ramadhan ambao walikuwa wamejiandaa kunisindikiza mpaka Gongo La Mboto.
Nikaagana na marafiki wengine pia niliokuwa nikiishi nao Hostel.
.
Tulipofika kituo cha ma-Bus cha Gongo La Mboto, nikaagana na Ramadhan na Hasheem kisha
Nikapanda bus linalo elekea Ubungo, na kwenda kutulia kwenye seat, na bus likaanza kuondoka taratibu.
.
Nikaitazama saa ya Careen, nikaona kuwa huu ndio mwisho wa kila kitu kati yangu na Careen.
Nikaivua saa, nikawa bado najishauri kuitupa dirishani.
Lakini ghafla kutupia jicho upande wa dirisha nililokaa, ndipo nilipowaona Hasheem, Ramadhan wakirudi kwa mbio kuliwahi bus nililopanda.
.
Moyo ulistuka, nikajua kuna kitu.
Kutupia jicho kwa mbele ndipo nilipoona Ivan na Nasra nao wanakuja kwa haraka.
.
Wote wakawa wanaita "Chris shuka, Chris"
Nikajiuliza kwanini wananiita.
Wakawa wanaita huku wanakimbia kuliwahi bus.
.
Nasra akawa anaita huku akionyesha ishara ya vidole, nikavifata vidole na kumuona Careen naye akija huku anakimbia
.
.
Je Chris atashuka!?? Na je, anaitiwa nini??

Usikose sehemu ya 20
#Itaendelea
...

Sehemu ya 20 soma hapa https://www.jamiiforums.com/posts/4..._id_internal=925946837445621;AfoblHfy8hy3A6gm
 
QuentinTarantino Isije ikatokea kumpenda mtu sana hata siku moja
Huwez kujizuia kumpenda mtu broo, Bali mm najijua moyo wangu ulivyo na baadhi ya wanaume tulivyo, ukiona unaanza kumpenda mtu punguza mazoea haraka na punguza kumwangaliaangalia na usitake ukae karibu nae, jaribu kuziwahi feelings zako kabla hazijawa intense
ILA BHANA HAYA MAMBO HAYANAGA UFUNDI, UKIPATIKANA UMEPATIKANA😊😊😊
 
Haya mambo yote(maumivu, chuki,wivu, unafiki kati ya marafiki) yameanza pale ambapo Chris aliamua kumzingatia careen siku ya kwanza kabisa darasani, kumbe Siri ipo hapo, kwamba usizingatie Mali yeyote
OKAY LESSON TAKEN😅😅😅
 
Kasomi wewe ni noma kwa story yenye kuburudisha, kuelimisha na kuonya
 
Haya mambo yote(maumivu, chuki,wivu, unafiki kati ya marafiki) yameanza pale ambapo Chris aliamua kumzingatia careen siku ya kwanza kabisa darasani, kumbe Siri ipo hapo, kwamba usizingatie Mali yeyote
OKAY LESSON TAKEN😅😅😅
🤣🤣🤣Kuna mali zingine inakupasa uzingatie tu maana zinavutia
 
Back
Top Bottom