MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!
Sehemu ya Ishirini
.
#Ilipoisha:
Niliagana na Hasheem na Ramadhan na kupanda bus la kuelekea Ubungo.
Bus lilipoanza kuondoka, nilikua nikiitazama saa ambayo nilipewa na Careen kama ukumbusho.
.
Sikuona tena umuhimu wa saa hiyo kubaki mkononi mwangu wakati tayari mimi na Careen hatuna chochote kinachoendelea kati yetu.
.
Nilikumbuka sana siku ambayo alinivalisha saa hiyo siku ambayo nilimfurahisha sana, ilikuwa ni siku niliyomfanyia surprise ya birthday yake.
.
Nakumbuka alikuwa akimwaga machozi ya furaha mbele yangu, huku akiniambia kuwa saa hii iwe ukumbusho wa thamani yangu kwake.
Nilizidi kuumia moyoni na kuzidi kuitazama saa ya Careen.
.
Kwa huzuni kubwa nikaifungua mkononi mwangu, na kujiandaa kuirusha nje ya dirisha.
Lakini nikasita, nikataka kuirusha tena, lakini bado nikasita baada ya kuona mahala napotaka kurusha pana watu.
.
Ndipo nikajishauri niirushe barabarani ili gari liipitie na kuivunja.
Nikatupa jicho kwa nyuma na kumuona Ramadhan na Hasheem wakilikimbilia gari nililopanda.
.
Niliwatazama kwa mshangao, wakaanza kuita "Chris shuka Chris ".
Nikajiuliza kwanini wananiita, na wakati tayari tumeshaagana.
Kupiga jicho kwa mbele, ndipo nilipowaona Nasra akiwa na Ivan nao wanakimbilia.
.
Nilizidi kujiuliza wana nini hawa, wanahitaji nini kutoka kwangu.
Lakini Nasra alikua anaita huku akionyesha alama ya vidole.
Nikafata vidole vya Nasra vinakoelekea na kumuona Careen nae akikimbilia.
.
#Inaendelea:
Nilipatwa na nguvu ya ghafla, nilianza kuhisi kuwa huenda ukweli umejulikana na wanataka kunipatanisha na Careen.
Lakini wakati huu sikutaka kuwa dhaifu, nilitaka kuwavimbia.
Nikaingiza kichwa ndani ya gari na kujisemea "Shit, zamu yenu kuteseka.
Na kama kweli ananipenda na ana nia na mimi, basi atanifata hata nikienda China.
Na yeye ataabike kwanza."
.
Nilijikuta natabasamu baada ya huzuni yote niliyokuwa nayo mwanzo.
Gari lilienda na kusimama Kituo Kipya.
.
Nikaona Nasra na Careen wamechoka kukimbia, wakaanza kutembea.
Lakini wanaume wao hawakuchoka.
.
Pindi wanakaribia Kituo Kipya, ndipo gari nalo lilipomaliza kupandisha abiria na kuanza kuondoka tena.
Walilikosa kwa mara nyingine, nikaona Ivan ameshika kiuno kwa kuchoka.
Huku Ramadhan akiwa amesimama na kushangaa, nahisi alikua anajiuliza kwanini sikushuka.
Hasheem alikuwa akirusha rusha mikono kama mtu aliyechukizwa na nilichofanya.
Ramadhan akachukua simu na kuwa kama anampigia mtu, nikajua wazi itakua ananitafuta kwenye simu wakati simu yangu ilikuwa imeshazimwa.
.
Mdomoni nikawa nacheka kuona leo wanavyotaabika kunipata, lakini moyoni nilikua na wasiwasi itakuaje endapo wataghair kuja.
.
Walipotea kwenye macho yangu, nikahisi kuwa labda wameghairi tena kuja.
Sikumuona yeyote yule hadi gari lilipofika Mzambarauni.
Nikaanza kuwa na wasiwasi kuwa mchezo wangu utanifanya nimkose mwanamke ninaye mpenda kwa dhati.
Na nilijua tu wazi kuwa huu wasiwasi ninao pata ni kwasababu nampenda sana.
Lakini nikajipa moyo kuwa kama yeye ndiye aliyeumbwa kwaajili yangu, basi atajitoa kivyovyote vile ili kunifata mpaka nilipo.
.
Nikatulia huku najipa moyo "Atatokea tu".
Kipindi tunashusha kilima cha kuingia stand ya Mombasa, ndipo niliona bodaboda tatu zinakuja nyuma kwa kasi.
Kuzitazama vizuri, walikuwa wamepakizwa Ivan, Hasheem na Ramadhan.
.
"Daaaamn"- Nikasema huku natoa tabasamu kubwa nikijua kuwa mpango wangu umetimia.
Lakini bado kiu yangu ilikua ni kumuona Careen akinifata.
.
Bus lilipofika Mombasa, likasimama na kupakiza abiria.
Ndipo walipowahi haraka mpaka dirishani.
.
"Chris shuka man, manzi wako ana ana anakufata wewe" - Alizungumza Ramadhan huku anakwama kwama sauti.
.
"Achana nae, simtaki." - Niliwavimbia ili nisionekane dhaifu lakini moyoni nilikua natamani hata dereva asinzie ili niwavimbie halafu ndo nishuke kabla halijaondoka.
.
"Chris acha ujinga, hii ni nafasi uliyokuwa ukiota kuipata "- Hasheem akaongea huku akinitazama kama baba anavyozungumza na mwanae.
.
"Ndoto muda wake usiku, sahivi asubuhi nishaamka kiakili na kihisia.
Nishawaambia simtaki tena Careen, na kwanza nawahi usafiri nisije nikachelewa bus".- Nikazidi kuwavimbia.
.
Watu ndani ya bus wakabaki wananishangaa kuendana na aina ya maongezi tuliyokuwa tunazungumza.
.
Jicho langu likawa bado halikauki upande ambao magari ya Gongo la mboto yanatokea huku nikitamani nione japo sura ya Careen ikinifata.
.
Kwambali nilianza kuona bodaboda mbili zikija, na abiria walikua Careen na Nasra.
Nikaanza kupata moyo na kuanza kuijua thamani yangu kwenye moyo wa Careen.
.
Haraka nikaivaa saa aliyonipa ili akija nimtambie jinsi gani nampenda mpaka nashindwa tupa vitu vyake.
Ghafla nikasikia konda anagonga akiashiria dereva aondoshe gari.
Nikajikuta naita "Konda subiri nishuke".
.
Abiria waliokuwa wakinishuhudia nilivyokuwa najibu majibu ya kujiamini mwanzo wakacheka.
"Nyooo siulikua unajishaua hapa" - Aliropoka dada mmoja aliyekuwa seat ya nyuma yangu.
Nikamuona Ramadhan anacheka, alijua zote zile mbwembwe.
.
Niliposhuka tu, na Careen na Nasra nao walikua washafika.
Nasra akanifata na kunitia kikofi.
"Mjinga, hicho cha usumbufu "- Aliongea baada ya kunichapa kikofi.
.
Nikamuona Careen kama alikuwa anajiandaa kuja kunikombatia, nikaona nizidi kumvimbia.
"Haya semeni mlichoniitia maana mnazidi kunichelewesha, nisije ninakosa bus "- (Nikazungumza kwa kujiamini).
.
Careen akashusha uso chini.
Ivan akafikicha pua, na kunisogerea karibu.
Na kuanza kuelezea kuanzia mwanzo, siku ambayo alikunywa sana Whiskey na Hasheem.
Hali iliyomfanya Hasheem alewe na kujikuta akitoboa siri zote.
Ivan aliumia sana baada ya kugundua kuwa nimemtumia yeye na Abdulrahman kwa manufaa yangu binafsi, na tangia hapo ndipo alipoamua kuwa anatoa siri kwa Nasra ili mipango yangu juu ya Careen ivurugike.
.
Ivan alivyoelezea mpaka hapo, nikagundua kuwa kumbe aliyefanya Abdulrahman agombane na Peter alikua ni Ivan.
.
Ivan akaendelea kusimulia jinsi alitumia mwanya wa kupanda gari moja na Abdulrahman ili ampe siri ya mchezo ambao nilikua nawafanyia kati yao.
Abdulrahman nae alikasirika na wote kurudi kwa Peter.
Hawakutaka kunistua mapema kinachoendelea, walitaka kunipa surprise ya maumivu kwa kuniharibia kwa Careen, ndiyo maana wakaamua kuuharibu mtoko wangu na Careen kwa kumkodisha mwanamke maarufu Manzese kwa kufanya vurugu, Ashanti.
.
Mpaka hapo nilimtazama Ivan kwa hasira, hasa nikikumbuka vurugu na aibu niliyoletewa na Ashanti.
Lakini akili yangu iliniambia "Chris tulia, haya yote uliyasababisha wewe mwenyewe ".
.
Ivan aliendelea kusimulia jinsi alivyompata Nasra na vile Abdulrahman alivyokubali matokeo ya kumkosa Nasra.
Na tangu hapo hakuona tena sababu ya kuendelea kupambana na mimi.
.
Ivan alinyamaza na kusimulia ""Leo nilipoamka nilimuambia Nasra azma yangu ya kuwarudisha Careen na Chris pamoja.
Nasra aligoma lakini baadae akaelewa, ndio tukaamua kumtafuta Careen asubuhi na kumweleza kila kitu.
Careen allilia sana na kujutia aliyokufanyia, na tukashauriana tuwahi asubuhi hii hii kuja kwako sababu tulisikia tetesi unataka kuondoka."
.
Ivan akahema kidogo, na kuendelea "Mimi na Nasra tuliwahi hostel, na Erick akatuambia umeshaondoka dakika tano zilizopita.
Tukawahi kituoni, bahati nzuri Careen nae alikuwa ndio ameshuka kwenye gari.
Na ghafla tulionana na Hasheem na Ramadhan.
Ona kiasi gani unapendwa Chris ".
.
Nikamtazama Ivan huku nikitafakari swali la kumpa, nikamuuliza "Nashukuru kwa yote uliyonitendea, lakini kwanini umegeuka msaliti kwa marafiki zako!?? "
.
Nasra akataka kujibu, lakin Ivan akamuwahi.
.
Ivan: "Chris sijatenda hili kwaajili yako, bali kwaajili ya Careen. "
.
Nikastuka, na kuuliza "Kwaajili ya Careen? "
.
Careen aliinamisha kichwa chini, na Ivan akaendelea kuongea "Chris ulikuwa unapendwa, unapendwa, na utazidi kupendwa zaidi ya ujuavyo ".
.
Nikaona kama anaongea taratibu, nilitamani azungumze haraka zaidi.
Ivan akazungumza "Siku ya birthday ya Careen nilichukua simu yake ili niwe napiga picha, huku nafanya kazi ya kukata simu za Peter kama tulivyo ahidiana."
.
Akanyamaza kidogo, na kuendelea "Ndiyo siku niliyogundua kuwa Careen anakupenda zaidi. Nilipekua sana simu yake na kukuta ameandika ujumbe mbalimbali za hisia zake juu yako, na alisave kwenye Notebook ya simu yake.
Nilitamani kukueleza siku hiyo hiyo lakini nilihisi ningekupagawisha akili mwisho uanze kumringia, nilitaka uhangaike mwisho useme wewe mwanaume kwa mdomo wako, ili iwe rahisi nyie kuwa pamoja.
Najua Careen asingeweza kukueleza hisia zake".
.
Hapo nilinywea, nikashusha pumzi nzito na kushusha uso wangu chini.
Ramadhan akazungumza "Siku ya birthday sote tulipanga tumdanganye unaumwa ili aje hostel, njiani Careen alikua kama chizi akizungumza peke yake "Chris nisubiri, pepo la homa lishindwe ".
Alikua akizungumza mengi, na nilijua kabisa kuwa Careen anaficha hisia zake juu yako".
.
Nasra akasema "Pindi nilipojenga nae ukaribu, alikua hachoki kukuzungumzia. Na siku niliyo mwambia wewe ni boyfriend wangu, ni kwasababu nilikua nakupenda na alikua ananikera na maswali yake kila mara kukuhusu... na nilijua ni kwasababu anakupenda ".
.
Nikawatazama wote, nilijikuta machozi yananitoka.
Nilikumbuka jinsi nilivyo hangaika kumpata Careen halafu leo naambiwa nilikua napendwa.
Nimepitia misukosuko yote ile, sikuwaamini.
Nikawaambia "Nyie wote mnasema mnachohisi, ila siri iko moyoni mwake. Acheni kunidanganya".
.
Careen akanitazama huku akidondosha chozi.
Watu walio pembeni walikua wakitutazama huku wakiwa hawaelewi kinachoendelea.
Careen akanisogerea na kunishika mkono ambao nilivaa saa yake.
.
Akaniambia "Nilikupa hii saa kama ukumbusho wa thamani yako kwangu.
Nilidhani ipo siku itaharibika na utaifungua na kukuta ujumbe niliouweka."
.
Maneno yake yalinifanya nifikirie kwa sekunde kadhaa, ndipo nilipo ichukua saa na kuifungua mfuniko kwa nyuma na kukuta kipande kidogo sana cha karatasi kilicho viringitwa na kuwa kidogo sana mpaka kutosha.
Nikakifungua na kukuta vimaneno vidogo sana kutokana na udogo kipande cha karatasi, vimaneno hivyo viliandikwa "I <3 u Chris".
.
Nilijikuta nalia sana, nikajisemea kimoyoni "Ndio maana nilishindwa kuitupa hii saa leo".
.
Akaichukua simu yake na kunipa mkononi na kuniambia nichore Pattern yake kwa vile naijua.
Nikachora, akaniambia pattern ni alama ya "C" inaamana ya jina lako.
Lakini sikuwahi kumpa mtu yeyote pattern yangu zaidi yako, na Ivan siku aliyotaka kupiga picha.
Kuna sababu moja tu kwanini nilikutajia pattern yangu, nilitaka uwe nayo huru simu yangu ili siku upekue na kukuta siri ya moyo wangu."
.
Akafungua App ya notebook na kunipa ujumbe mmoja aliowahi kusave, ulisomeka hivi "Chris amenifanya nimkumbuke Khalfan, mwanaume aliwahi kunijali.
Lakini Chris amezidi, ananijali zaidi na nazidi kuvutiwa nae kila siku".
Nilikwambia kusoma hapo, na kukumbuka Careen aliwahi niambia jinsi gani namkumbusha Khalfan, na akanipa sifa za Khalfan.
.
Nikafungua nyingine ambayo iliniliza zaidi, aliandika "Nampenda sana, ila siwezi kumwambia na wala sina nguvu ya kuzieleza hisia zangu wala kuzionyesha.
Anaonekana ananipenda pia, lakini naye ni mwoga wa kuniambia."
.
Ujumbe Mwingine "Leo amenitamkia jinsi gani ananipenda, lakini siwezi kumuambia kama nampenda pia.
Nilishindwa kumkubalia kwa kuhofia ataniona malaya, nilitamani kumjibu pale pale."
.
Kila ujumbe ambao Careen aliuandika ulinifanya nizidi kulia machozi ya furaha baada ya kujua jinsi gani alivyokuwa akinithamini siku zote hizo.
Nakumbuka kilichowahi kunifanya nimpende zaidi ilikua ni misimamo yake, kujitambua kwake na kujithamini kwake.
Nilikumbana na mmoja "Ameniudhi jana, amekombatiwa na mpenzi wake mwingine mbele yangu.
Tena aliniacha niondoke wala hakunifata fata sana kunibembeleza.
Natamani nimpigie, natamani nipokee simu zake, ila acha tu ninyamaze, sitakiwi kuwa dhaifu kwake.
Nitamnunia na hata salamu yake nitajifanya sitaki. "
.
Mpaka hapo niliishiwa nguvu ya kusoma zaidi na kujikuta nikimkombatia kwa nguvu na kummiminia mabusu.
.
Pindi bado tumekombatiana, niliona wote wakitabasamu huku Nasra akitoa machozi ya furaha.
Lakini kwa mbele niliona Peter na Abdulrahman wakiwa wamesimama wakitutazama kwa mshangao.
.
Nikauliza "Nani kawaita wale?? "
.
Ivan akajibu "Usiogope, mechi tuliyoianzisha hatuwezi iacha hivi hivi.
Peter leo alikua airport anamsubiria mchumba wake wa kiNigeria.
Nikaona bora niwataarifu kuwa namaliza mechi yenu leo, na mimi ndo refa".
.
Niliwatazama Peter na Abdulrahman, nao wakatutazama kwa mshangao mkubwa.
Peter akasogea huku anakunja ngumi.
.
Nikawa nimejiandaa kuwa leo akizingua namchezesha kichapo.
Akaikunja ngumi yake na kutishia kama anataka kunipiga lakini akaipoza na kunipa ishara nipige tano.
Nikacheka na kupiga tano.
.
Peter akazungumza "Leo nimegundua kuwa mapenzi hayahitaji ushindani.
Kama unampenda mtu, usihitaji kutaka kupambana na mpinzani wako wala kuwekeana nae mchezo wa kubashiri."
.
Akahema na kusema "Umeshinda, sioni haja ya kuendelea kushindana na wewe wakati tayari mbingu na ardhi zinathibitisha kuwa Careen ni ubavu wako".
.
Nilimtazama Peter, nikamuuliza "Vipi umekuja na dera!!?? " kisha nikacheka.
.
Peter akacheka, akaniambia "Sijui nilikua nawaza nini wakati naweza adhabu hiyo".
.
Nikamshika bega na kumuambia "Hakuna atakaye vaa dera. Sababu kipindi mimi nimempata ninayempenda, wewe umempata unayestahili kuwa nae."
.
Akauliza "Umemuona??? "
Nikamjibu "Huyo nyuma yako".
.
Alipogeuka alikuta mchumba wake aliyechaguliwa na wazazi wake, amesimama nyuma yake.
Sote kwa pamoja tukasogereana na kutambulishwa kwa mchumba wake anayeitwa Emilie, na wote tukafurahi kwa story mbili tatu.
.
Abdulrahman: Mnaonaje wote tukienda kula bata siku tatu Zanzibar, tutembelee Changuu Island, na Sandbank.
.
Wote tukakubaliana na wazo la Abdulrahman
Ivan: Chris umesahau unatakiwa uende Arusha?? .
.
"Umenikumbusha chalii yangu"- Nikachukua simu na kumpigia mama na kumwambia nitakuja wiki ijayo.
.
Peter akaniambia subiri, akaenda kwenye gari lake na kuleta kimfuko.
Tulipotazama ndani yake tukakuta kuna Wigi, make up, na dera.
.
"Kumbe ulikua serious na mechi "- nikamuuliza Peter.
Abdulrahman akajibu "We acha tu, alikua nayo serious ila baadae aliachana nayo kabisa... alitaka akuache na maumivu tu, dera akasamehe".
.
"Ila leo tumejifunza, tulikua na akili za kitoto "- Peter alijibu na kumkabidhi Careen kama ukumbusho wa mechi ya kumpata yeye.
.
Akaipokea na mwisho tukaagana, na Abdulrahman, Peter na Emilie wakaondoka.
Na sisi wengine tukaenda tukaenda panda daladala turudi Gongo La Mboto.
.
lakini ghafla wakati tunasubiria abiria kadhaa washuke ili nasi tupande.
Nikastuka kumuona Careen akitoa mshangao kumuona kijana mmoja sharobaro akishuka kwenye daladala.
Nikazidi kuwatazama wanavyoshangaana.
.
Nikaona wanasalimiana, ikabidi nipande ndani ya daladala ili niwatazame vizuri.
Kina Ivan na Nasra nao waliokuwa seat ya nyuma yangu, wakanistua kwa mkono "Chris vipi huibiwi!? "
.
Mwisho wa kusalimiana kwao niliona Careen akimkabidhi yule mwanaume kile kifuko chenye dera, wigi na makeup ndani yani.
Na Careen kupanda ndani ya gari.
.
Kwa wivu nilionao, nikauliza "Yule nani na mbona umempa kile kifuko!?? "
Akaniambia "Yule anaitwa Andrew, ndiye yule boyfriend wangu aliyekuwa ananisaliti na kunitesa kihisia."
.
Nikakumbuka pindi Careen analalamika kuhusu boyfriend wake anavyomtesa na hata kumuacha kwasababu ya kijinga.
.
Careen akaendelea kueleza "Pale alikuwa ananilalamikia kuwa alinitania tuachane, bado ananipenda.
Nikamshangaa, mimi siwezi rudia takataka.
Na kuhusu kile kifuko nilichompa, hajajua ndani kuna nini, amedhani nimempa zawadi tu, na akienda kukifungua nadhani atalia mpaka basi.
Wewe na Peter ni wanaume wa shoka, yule ni limbukeni wa kupendwa, kwangu namuona kama ana tabia za kidada, sasa acha akavae hilo dera na wigi ili atongozwe vizuri mxieeeew".
.
Tukacheka sana huku tukigonga mikono.
Nikampa kombatio la nguvu.
Na akakilaza kichwa chake kifuani mwangu.
Nikaanza kukumbuka yote niliyopitia na kusema nimejifunza mengi sana kupitia Careen.
Nikaanza kukumbuka moja baada ya jingine.
.
Pindi nipo kwenye mawazo, simu ya Careen iliita namba ngeni.
Kupokea ni Andrew amepiga kwenye namba nyingine.
Careen alivyomsikia tu, akachomeka earphone na kunipa sikio moja nisikilize.
.
Alilalamika sana huku akilia, lakini nilijifunza kitu kimoja kupitia Andrew kuwa kumbe kuna watu ukiwaonyesha upendo huwa wanakua malimbukeni, wanaanza kukufanyia visa na vituko, na hata kukutishia kukuacha.
Anadhani akikuacha utateseka, hutaweza ishi bila yeye, anakufanya atakavyo.
.
Ila unapoamua kuachana nae na ukawa huna muda nae tena, ukazidi kuwa bora zaidi yake.
Ndipo huwa anakumbuka kuwa sio wewe ambae huwezi ishi bila yeye, bali ni YEYE ambaye hawezi ISHI bila WEWE.
.
Nilipoona bado Andrew anaendelea kulia lia, nikakaza sauti na kumkaripia kwa nguvu "NANI HUYU AMBAYE ANAZUNGUMZA NA MPENZI WANGU".
.
Hapo hapo akakata simu, gari zima walicheka.
Nikambusu na kumuambia "Umenipa tulizo la maumivu yangu yasiyo kwisha".
Akaniambia "Nimekupa tulizo darling, maumivu tumemuachia Andrew".
.
******MWISHO******