Mawasiliano ndio kigezo kikubwa kinachoonyesha kama kuna mapenzi au ndio yamejifia

Mawasiliano ndio kigezo kikubwa kinachoonyesha kama kuna mapenzi au ndio yamejifia

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Kuna siku nimekutana na post moja ambapo mwamba anasema anamtext mrembo halafu hujibu baada ya masaa mawili au matatu. Mwamba akawa anauliza, "Hivi imekaaje?"

Wakati unatafakari juu ya jambo hilo la mwamba, nami nimejikuta natafakari yangu. Kuna mrembo mmoja alikuwa anaitwa Zawadi. Hatukuwahi kuduu lakini tulikuwa very close, yaani kilichobaki ilikuwa ni kuunganisha viungo vyetu vya uzazi tu. Ila katika hili, mimi nilizingua, nilikuwa naleta mambo mengi kama ya kwenye movie, hahaha.

Inaelekea mrembo hakutaka mambo mengi. Mawasiliano yakaanza kupungua taratibu, na mwisho wa siku nilimuona Kariakoo ana mimba. Nikapata majibu kwanini alikuwa sio active katika mawasiliano.

Turudi kwenye mada. Iko hivi: hakuna ubize kwa mtu unayempenda. Hata uko bize kiasi gani, lazima utatafuta muda wa kuwasiliana naye. Ukiona mtu anakwambia yupo bize, basi fahamu yupo bize na mtu wake mwingine, period.

Kwahiyo, wakati mwingine jiongeze mwenyewe. Chap basi acha ujinga. Hata kama yupo bize, akipata muda atakucheki na kukufahamisha kuna moja mbili tatu, na hata kukuomba radhi anaweza ili mradi tu akuweke sawa. Lakini kama mtu hajibu simu kila mara na hata akipokea haonyeshi kujali wala kutoa sababu, ujue una mboa, jiongeze mapema. Hajibu meseji kwa wakati na mara nyingi haonyeshi kujali, jiongeze chap.

Mawasiliano ndio msingi mkubwa wa mapenzi. Anayekupenda atatafuta muda kwa ajili yako, iwe mvua iwe jua. Atahakikisha mnakuwa karibu siku zote.

Kwahiyo usipoteze muda wako kwa mtu ambaye hana muda na wewe. Tambua thamani yako. Kama yeye anasema "wa nini", wenzake wanasema "watakupata lini?"


Ni hayo tu!

Pia soma:Je, mapenzi yanaweza kuishi bila mawasiliano ya kimwili?
 
Kwenye urafiki na hata mapenzi hakuna ubize kwa best friend ama mtu unayempenda

Ukiambiwa yupo bize jua kwamba kuna mtu wake yupo tayari kuvuruga ratiba waonane.

Nipo bize = huna uzito kwangu na hata kampani yako ni ya kuivumilia ama maslahi tu.
 
Yeah man huo ndio ukweli

Mawasiliano ndio kigezo na msingi mkuu wa mahusiano

Ukiona mawasiliano yanayumbas basi jua ameshakuona humfai, huna hadhi ama wewe sio type yake yaani msumbufu, uwepo wako unavumiliwa tu Wala huitajiki tena

Hata ukiwa unafukuzia zigo ukiona ndani ya mwezi MMOJA mpk miwili hilo zigo mawasiliano yake ya kusuasua jua ajakuelewa usipoteze potezea na wewe

Mbna kawaida tu katika haya MAISHA huwezi kupendwa na Kila mtu hivyo kukataliwa makavu live kuonekana sio type yake au kupigwa kibuti ni kawaida mno 7bu katika haya MAISHA Uaweza ukajikuta unaibua ZIGO la ukweli kinomanoma mpk ukawa ujiamini kama kweli umeliopoa Hilo GOMA mana toto limekuelewa tangu first time amekupa namba halipoi kwa charting mpk siku unaenda kulicheda Bado moto mtoto macho kurembua

So yote hii nguvu ya mawasiliano

Hvyo ukiona Kuna kusuasua katika mawasiliano chukua hatua mapema kabla hujaonekana Bonge la fala
 
Aloo. Nmekaa naona binti mashaalah. Sura inavutia haswa, shepu iyo kimo icho moyo ukapiga pah .. haha
Nilimpenda kweli kumbe ye Hana time ya mapenzi anakitembeza TU , nami siachi Nala ila why akitembeze nngekaweka ndani.. ila dah. WA Ivi hawataki story we SEMA venue kale mzigo
 
Mawasiliano na muda wake kwangu ndivyo vilinifanya niamini ananipenda sana.

Kwa mwanaume aliye busy kama yeye kunitafuta kila aamkapo, breakfast, lunch, jioni, atokapo kazini na afikapo nyumbani kila siku bila kukosa ni zaidi ya yote!
Nampenda sana.

So yeah, mawasiliano imara ndiyo mahusiano imara.
 
Mawasiliano na muda wake kwangu ndivyo vilinifanya niamini ananipenda sana.

Kwa mwanaume aliye busy kama yeye kunitafuta kila aamkapo, breakfast, lunch, jioni, atokapo kazini na afikapo nyumbani kila siku bila kukosa ni zaidi ya yote!
Nampenda sana.

So yeah, mawasiliano imara ndiyo mahusiano imara.
Bongo kuna mtu yuko busy? Rais mwenyewe tuko nae jf humu muda wote.
 
Back
Top Bottom