Mawasiliano ndio kigezo kikubwa kinachoonyesha kama kuna mapenzi au ndio yamejifia

Mawasiliano ndio kigezo kikubwa kinachoonyesha kama kuna mapenzi au ndio yamejifia

Copy and paste


Mambo 5 Muhimu Ya Kuyajua Kambla Hujaamua Kumchunia Mpenzi Wako Na Kuacha Kujibu Meseji Zake!

Unakaa wiki nzima hujibu hata meseji ya mpenzi wako, anakutumia meseji unaziona unajifanya uko bize, akipiga simu humpi nafasi unakuambia nitakutafuta kisha unampotezea! Unafanya hivyo halafu unajishaua sijui mke, mpenzi, mume au mchumba wangu! Kama una hii tabia naomba nikukumbushe mambo matano;

(1) Sio wewe peke yako mwenye simu, kuna watu kibao wanasimu, kama hujibu meseji zake uko bize unamuacha mpweke hajui kama ushamuacha au bado upo naye basi jua kuna siku atapata mwingine wakuchart naye na atasahau kuwa kuna mtu kama wewe.

(2) Huna chochote cha maana ulichonacho kaamua tu kukuvumilia; Wakasti mwingine unajiona keki labda kwakua anakutafuta kila siku yeye, ila nikuambie, huna cha maana chochote ulichonacho kuna mabaharia kibao wanavyo na kama ni wewe dada jua kuna wengine wanavyo siku akishtuka na kujitambua akaondoka ndiyo utaaanza kulalamika!

(3) Mawasiliano ni kitu cha muhimu, unapoaha kujibu meseji zake unamchanganya mwenza wako, anashindwa kujua kama bado upo naye, ushamuacha au unamiapngo gani, kama umemuacha muaambie aingie zake chooni alie mpaka basia kitoka amepona, na kama bado unampenda unatest kiberiti basi huo ni utoto, atakuvumilia wakati akitafuta mtu mwingine wa kuchukua nafasi yako.

(4) Kama wewe ulimuona ukamatamani basi jua kuwa kuna wengine watamatamani na usishani kwako kafika, kama alikutongoza ukakubali basi jua kuna wengine nao anaweza kuwatongoza wakakubali, anaweza kuwa anakuvumilia sikwakua una maajabu sana bali kwakua anajiheshimu tu hataki kuhangaika na leo huyu kesho yule.

(5) Mwisho hata kama uko bize namna gani basi mtumie meseji hata kumuambia Baby nimekumiss. Ule wakati unaingia chooni unakata gogo badala ya kufunga macho kusikilizia maisha basi mjibu meseji zako. Hakuna kitu kinaumiza kama kumtumia mtu meseji, unaona kabisa kaisoma halafu hata hajahangaika kuijibu na baadaye anaongea na wewe kawaida kama vile hakuna kilichotokea. Ndugu yangua cha kuringa hivyo hata huna maajabu yoyote ni kuvumiliana tu watu wanavumiliana!
Nimeipenda hii
 
Unaweza ukatafutwa ukawa hupendwi vilevile watu wako kimkakati zaid siku hizi usiamini sana simu za Mara kwa Mara wala msg mkajaa katika mifumo ya watu.watu wako kazini wanafanya kaz akijulia Hali mara moja inatosha. Ndio maana kila siku mnalia lia kwa kuingia kwa pupa katika mitego.Alafu mwanaume unaliaje kutokutafuwa Na mwanamke ??? Mwanaume ndio mtafute mwanamke mwanamke ndio Ana bembelezwa Na kudekezwa ili apate KUTII NA KUHESHIMU
 
Hisia zinashuka au kupotea kwasababu ya kuishi kwa mazoea,,mkiwa na tabia ya kuonyeshana upendo basi tambua hisia zitakuwepo siku zote
Ndugu, usichanganye hisia na upendo, mara nyingi hisia huondoka na kupotea kabisa hata uonyeshe upendo kiasi gani.

Hisia zikiondoka na kufa kinachobaki ni upendo pekee ambao ndiyo utaamua huo uhusiano uendelee ama usiendelee.Hisia mara nyingi huwa ni jambo la kuja na kuondoka.
Ngoja nikuelimishe kwanini waislamu au wanaume wameruhusiwa kuwa na wake wengi tena na Allah ingawa wewe humuamini
Kwanza ni kutuliza kiu ya mwanaume ,wote tunajua sisi wanaume kutulia na mke mmoja ni mtihani sana labda uwe una ucha mungu na hofu ya Allah
Swali: Mtume wako hakuwa na hofu ya Mungu?? Alikuwa na kiu sana?? Si unafahamu alipitiliza idadi ya wanne??
Pili wanawake baadhi yao wanachangamoto sana katika swala zima la kujahamiana,,mwingine akiwa na mimba tu basi ujue unyumba utautafuta kwa tochi,
Hoja dhaifu sana, yaani Mungu yeye kipaumbele chake ni ngono na mapenzi, mwanaume yeye hana changamoto??
Tatu kuna watu wamejaaliwa nguvu ya matamanio yaani hao ni bakora kwa kwenda mbele haina kulala yaani kila siku lazima apige bakora,
Hao walijaaliwa ni wanaume tu?? Vipi wanawake hawana matamanio makubwa?? Hawapo kwenye jamii zetu??
Na nne huenda mke mmoja asiwe na kizazi basi sio ndio umuache laa! Ongeza mke mwingine na mambo yaendelee huku kizazi kinaendelea.
Vipi kama mwanaume hana kizazi?? Vipi kama wote wanne hawana vizazi?? vipi kama mume na mke hawana vizazi??

Nb: Kwa kutumia akili yako ya kuzaliwa na siyo kushikiwa, Mungu anaweza kuruhusu mwanaume aoe idadi fulani ya wanawake?? Unafahamu mila na tamaduni za kiarabu wakati huo?? Unaweza kutenganisha dini na utamaduni??
 
Ndugu, usichanganye hisia na upendo, mara nyingi hisia huondoka na kupotea kabisa hata uonyeshe upendo kiasi gani.

Hisia zikiondoka na kufa kinachobaki ni upendo pekee ambao ndiyo utaamua huo uhusiano uendelee ama usiendelee.Hisia mara nyingi huwa ni jambo la kuja na kuondoka.


Swali: Mtume wako hakuwa na hofu ya Mungu?? Alikuwa na kiu sana?? Si unafahamu alipitiliza idadi ya wanne??

Hoja dhaifu sana, yaani Mungu yeye kipaumbele chake ni ngono na mapenzi, mwanaume yeye hana changamoto??

Hao walijaaliwa ni wanaume tu?? Vipi wanawake hawana matamanio makubwa?? Hawapo kwenye jamii zetu??

Vipi kama mwanaume hana kizazi?? Vipi kama wote wanne hawana vizazi?? vipi kama mume na mke hawana vizazi??

Nb: Kwa kutumia akili yako ya kuzaliwa na siyo kushikiwa, Mungu anaweza kuruhusu mwanaume aoe idadi fulani ya wanawake?? Unafahamu mila na tamaduni za kiarabu wakati huo?? Unaweza kutenganisha dini na utamaduni??
Kupitia comment yako,,nahisi ubishani mbeleni usio na tija kwangu na utanipotezea mda wangu

Asante
 
Kuna husiano ninalo ila sijui linahusiana na nini maana asilimia kubwa kama sio mara nyingi mimi ndie huwa ninaanza kumtafuta.

Ingawa ndio tuko mwanzoni kabisa mwa husiano just to get to know each other😌ila hii ni red light🏮 nimeshaiona nisikaze fuvu.

Naona hisia zinashuka kabisa💔
 
We mtoto weweeeh..😀
Muambie Nampenda sana pia,
no mara waa am going through, aah' no mara waa, no mara how busy I am, aaam, no mara how many times anazurura, Lindi ni nyumbani atarudi tu..!!😂😂
 
Kuna husiano ninalo ila sijui linahusiana na nini maana asilimia kubwa kama sio mara nyingi mimi ndie huwa ninaanza kumtafuta.

Ingawa ndio tuko mwanzoni kabisa mwa husiano just to get to know each other😌ila hii ni red light🏮 nimeshaiona nisikaze fuvu.

Naona hisia zinashuka kabisa💔
Upo sahihi kabisa
 
Uzuri babez zangu wanajua mbilinge za kariakoo, muda wa kuwacheki ni night kali.!!
 
Back
Top Bottom