Mawazo na mbinu za biashara

Mawazo na mbinu za biashara

sawa mkuu nimekuelewa,kuna uzi nimekutag wa maswala ya mobile money...ukipitia ule uzi unaweza jifunza kitu...kama niliona umesema upo mbeya...ukipambana pale kabwe stendi ukapata chumba hii mitaa yenye mzunguko mkubwa wa watu or ukipata chumba huku mwanjelwa sehemu yenye mzunguko mkubwa wa watu utapiga hela...issue ni kupata chumba tu,and sehemu kama iyo unafungua duka kubwa sana la simu vikienda sambamba na hizo huduma..but hakikisha ofisi una i design inakuwa na muonekano classic wa pekee
JOKES...Hakikisha kwenye ilo duka kama utakuwa na wafanyakazi unaajiri vitoto vyakike vizuri but smart kichwani kwa ajili ya kukusaidia kwenye mauzo
Kwanza nikushukuri sana kwa kwa kunipa uzi wenye kunipanua mawazo zaidi..Naomba nikaupitie huo uzi then nitarudi kwako....

Kuhusu watoto wazuri na smart kaka siyo Jokes,, aiseee kwa biashara zinazohitaji issue ya marketing hao ni Muhimu hivyo pia umetoa mbinu mbadala ya ku catch minds za wateja..
 
Kazi gani ambayo huwezi kumove kirahisi? Endelea kuweka pesa afu omba uhamisho tu. Nasema hivyo kwa maana.. kuna Milengo miwili.. mlengo ambao hauamini kwenye ajira na ule unaoamini kwenye Ajira. Hivyo basi ili kujidhatiti lazima uanze biashara ungali kazini. Hii itakusaidia kupunguza usumbufu hasa kwenye ofisi kadhaa za umma as ww ni mtumishi pia. Mim nimeomba kuhamishiwa Mtwara au Lindi ili nijikite kwenye biashara hzo. Naamini nitahamishiwa kutoka hapa Dom nilipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hongera sana kwanza kwa hizo hatua ulizozichukua kwani ni moja ya hatua nzuri sana...
Kwakuwa umenipa kama wazo itabidi nikae kulifanyia kazi hili ili nione kama linawezekana...Mimi ni miongoni mwa wale wanaoamini Kuwa Ajira ni mtaji..hivyo imenisaidia kupata mtaji basi nikaona nikafie huko kwenye self employment ndo maana nikajituma kukusanya angalau haka ka myaji ili nisipate kuyumba sana...lakin wazo lako ni zuri pia nitalifanyia kazi mkuu..
Shukrani sana
 
kama upo kanda ya ziwa, kwa biashara ya nafaka inaweza kukulipa namtoa mfano hai uku kahama kw sasa bei ya mche per kilo 800-1200 kasababu ya msimu wa mavuno na gunia la mpunga ni sh 30000-35000 ukinunua gunia zako kadhaa ukaja kuuzia mwezi sept-january ni bei isiyo pungua 90000 na kilo ya mchele huwa inauzwa mpaka 1600 kwa huku.sasa unaweza ona ilivyo

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii kanda ya ziwa inasifika sana kwa biashara za nafaka na sijawahi fika huko..nimetenga mda wa kufanya research ya mikoa..hivyo nitafika kuona hali ipoje lakin hili wazo la biashara ya kuuza nafaka ni wazo ambalo skuwa nalo..

Lakini kupitia wadau wangu wa nguvu humu ndani nimeanza kuona ukuu wa hiyo biashara..nadhani hii inaweza nifaaa kwani pia si biashara rahisi kuanguka..
Shukran sana mkuu
 
Kiukweli niliangalia zaidi katika kupata experience ndo mana nikajiingiza kwenye ufugaji mdogo ili nipate japo la kujifunza..lakini pia aina ya ajira niliyonayo hainiruhusu kuwa mbali na mazingira ya kazi japo biashara kama ya duka ningeweza kuwa nayo lakin skufanya hivyo na badala yake nikapambana kupata hicho kiasi cha fedha ili hata nikitoka nikapatie uzoefu na mawazo mapya nikiwa katika motion...hivyo sijajiwekea mazingira ya hofu baada ya kutoka kwenye ajira

Mkuu nunua biashara inayo fanya vizuri na unaona vitabu vyake vinakueleza kwa mwezi inatengeneza faida ya sh fulani.

Kuanza biashara mpka isimame na huna uzoefu unaweza poteza pesa yote na ukawa bado huna uzoefu.



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu nunua biashara inayo fanya vizuri na unaona vitabu vyake vinakueleza kwa mwezi inatengeneza faida ya sh fulani.
Kuanza biashara mpka isimame na huna uzoefu unaweza poteza pesa yote na ukawa bado huna uzoefu.



Sent from my iPhone using JamiiForums
Hii ya kununua biashara inayofanya vizuri ni wazo mpya kabisa kwang mkuu naomba ufafanuzi kidogo
 
Kama upo mikoa kama Mwanza, Arusha...

Usi-Risk pesa zako, katika 34M weka 33.8M Bank, mkononi ubaki na 200,000 Cash then ingia PM kwangu nikueleze mbinu ya kutumia rasilimali watu kupata 300,000 Tzs kwasiku.
Mwaga nondo hapahapa ili kila mtu afaidike.....
#YNWA

Wrote from Anfield..!!
 
Habarini wanaJF,

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 32 ni mwajiriwa wa serikali na nipo katika ajira kwa miaka 10 sasa. Kutokana na changamoto na kero za ajira niliona kama sijiskii kubaki katika ajira yangu nikiwa natamani kujitegemea. Kwa hali hiyo nikaona njia pekee ya kuwa huru ni kuwa na self employment, yaani nijiajiri.

Nimeweza kuweka viakiba kujikusanya nikapata TSH. 34M (Milioni Thelasini na nne)

Naombeni ushauri wenu
(1) Je, hiki kiwango kinatosha kuamua kujitegemea?
(2) Je, ni biashara gani niifanye?
(3) Nitaweza kufanikiwa kimaisha kwa huo umri wa miaka 32?

Sijawahi kujishughulisha na biashara nyingine zaidi ya ufugaji kuku lakin si sana japo uzoefu ninao.. Msaada wa ushauri tafadhali.

Ushauri wako mzuri kwangu ndiyo pona pona yangu.
Mungu awabariki.
ASANTE
Do your hobby.
Mi binafsi hobby yangu ni kilimo na nimejiajiri humo.

#YNWA

Wrote from Anfield..!!
 
Kuwa makini na kitu kinachoitwa uaminifu.

Chukuwa mawazo ya wadau wanaotoa hapa hapa hadharani, kuwa makini na wanaokuita huko sijui pm ni hatari kubwa.

Nikupongeze kwa kukusanya kiasi hocho ukiwa kazini lakini ulikosea sehemu ndogo saana kuruhusu miaka kumi bila hata kufanya kitu chochote ambacho ulikitamani kukifanya ukiww hado kazini

Hakuna kazi ngumu kama ujasiriamali. Huku utajikuta unalia kiasi kwamba hutoamini. Tumia akili kubwa saana kuchagua aina ya biashara unayohitaji kuifanya.

Tafuta wazo la biashara, lifanyie kazi hata kwa kukugharimu ili hali ukiwa kazini. Usichomoke kazini kama tairi kwenye gari, hapana jiandae katika kutoka kwenye mzunguko w ajira.

Hii itakuwa na faida zifuatazo
1. Pamoja nakuwa una mtaji pia unahitaji rasilimali watu. Rasilimali watu ni kuhimu saana kwani itakusaidia kukupa mtandao huku ukiwa kazini.
2. Mtandao ulio imara. Ukishatengeneza rasirimali watu unahitaji kuwa na mtandao ambapo kwa kutumia watu ulionao utatengeneza huku wewe ukisoma makosa na mazingira na makosa pamoja na changamoto huku ukiwa mbali

3. Unajifunza kuwa msimamizi huku ukijifunza namna unavyosimamiwa wewe kazini kwako.

4.
 
Kuwa makini na kitu kinachoitwa uaminifu.

Chukuwa mawazo ya wadau wanaotoa hapa hapa hadharani, kuwa makini na wanaokuita huko sijui pm ni hatari kubwa.

Nikupongeze kwa kukusanya kiasi hocho ukiwa kazini lakini ulikosea sehemu ndogo saana kuruhusu miaka kumi bila hata kufanya kitu chochote ambacho ulikitamani kukifanya ukiww hado kazini

Hakuna kazi ngumu kama ujasiriamali. Huku utajikuta unalia kiasi kwamba hutoamini. Tumia akili kubwa saana kuchagua aina ya biashara unayohitaji kuifanya.

Tafuta wazo la biashara, lifanyie kazi hata kwa kukugharimu ili hali ukiwa kazini. Usichomoke kazini kama tairi kwenye gari, hapana jiandae katika kutoka kwenye mzunguko w ajira.

Hii itakuwa na faida zifuatazo
1. Pamoja nakuwa una mtaji pia unahitaji rasilimali watu. Rasilimali watu ni kuhimu saana kwani itakusaidia kukupa mtandao huku ukiwa kazini.
2. Mtandao ulio imara. Ukishatengeneza rasirimali watu unahitaji kuwa na mtandao ambapo kwa kutumia watu ulionao utatengeneza huku wewe ukisoma makosa na mazingira na makosa pamoja na changamoto huku ukiwa mbali

3. Unajifunza kuwa msimamizi huku ukijifunza namna unavyosimamiwa wewe kazini kwako.

4.
Mkuu nashukuru kwa wazo zuri..Suala la mtu kunambia nimfate PM siyo rahisi naelewa na ndo mana nikaleta mada hapa hadharani..Shukrani sana mkuu kwa mawazo nitayafanyia kazi
 
Mkuu
Mkuu kwanini usiiwekeze kwa Mr. KUKU...kule wanasema utapaga gawio la asilimia mia na wewe una passion na kukuz!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwanini usiiwekeze kwa Mr. KUKU...kule wanasema utapaga gawio la asilimia mia na wewe una passion na kukuz!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu moja ya miradi yangu ni kufuga kuku hivyo kuwekeza kwa Mr. Kuku hakunifanyi nikaendelea kujitanua kiuzoefu na kukuza soko. Mr Kuku huenda akawa temporary but maisha yanatakiwa kuendelea..Nadhan kwa mm kutanua mradi wangu wa kuku ni sahihi zaidi.
Ushauri wako ni mzuri nitafuatilia huyo Mr. Kuku anafanyaje ili niendelee kupata somo.
Shukran sana kwa ushauri mkuu
 
Back
Top Bottom