Mawazo na ushauri wako vitanisaidia.

Mawazo na ushauri wako vitanisaidia.

Nilijaribu kuwaza vile na nikatafuta mtu wa kununua lakini pesa niliyokuwa napatiwa haikuwa rafiki kwangu. Sijuwi ni kwa vile waliona nina tatizo 🤷
Siku ukienda kuuza ndo hapo hapo watakupiga spana....

Nikupe ushauri ndugu, utakuja kufa kwa mawazo, mtaji wa laki alafu una presha ya kufukuzia milion 12 ya watu hautatoboa kaka nikuambie tu ukweli

Tafuta watu wa busara huko kwenu, then urudi ukae na hao wanakikundi mpange njia rafiki ya kuwalipa, wakikataa acha waende mahakamani deni halifungi mtu, tena ukiona ni watata Katoe tahadhari ya usalama polisi na uwaambie kabisa chochote kitakachokupata watahusika

Fanya hustle ukiwa umerelax nyumbani uwatafutie hela Yao, ila hili la kufanya biashara roho juu juu unajificha kama digidigi huwezi kutoboa chief utaishia kua chizi tu
 
Nilijaribu kuwaza vile na nikatafuta mtu wa kununua lakini pesa niliyokuwa napatiwa haikuwa rafiki kwangu. Sijuwi ni kwa vile waliona nina tatizo 🤷
Pole sana mkuu,
Kama uliweza kukuza elfu 20 bas Pia Mungu akuwezeshe tena kukuza mtaji huo...

Kigenge tu ndio best (matunda
 
Daaah mii mwenzako niliachana na masomo ila huyo aunt aliyenifanya niache alikua na uhakika wa kunifanya niwe stable economically....

Ushauri
Rafiki kabla ya kuchukua maamuzi ya wewe kuondoka eneo hilo haukuweza kuongea nao ili uweze hata kuwalipa pesa zao kidogo kidogo?? Naamini ingekua ni njia nzuri ungeweza endelea na biashara yako hapo hapo
 
Sikulaumu kuondoka mkuu, kuna watu sio waelewa kabisa, mola akufanyie wepesi uweze kuwalipa!
Yaani we acha tu. Nilijaribu
Hata mimi naona kama kuna kitu anaficha japo sina uhakika. Huenda kuna mtu alimwambia kuna deal la kuingiza fedha chap chap, akatumia hizo fedha za chama ili afanye deal, achukuwe faida na fedha za chama zibaki, lakini mambo yakaenda sivyo. Watu wengi wanaotunza fedha za vyama huwa wanaangukia kwenye mtego kama huu. Yaani alilala na fedha nyingi namna hiyo na wezi wakaingia na kuchukuwa fedha tu bila yeye kusikia? Anyways, ni hisia zangu tu na anaweza kuwa anasema ukweli.
Penye wengi mambo ni mengi.
Hisia zako zisikilize ila sijawah kutumia pesa za mtu ninayemtunzia kwa maana muda wowote atazihitaji. Ila sina neno
 
Pole mkuu bahati nzuri unajituma Mungu atakubairiki.
Ulichokosea ni kukubali ukae na 12M ndani kirahisi sana wakati ulijua likitokea lolote hutaweza kuzilipa, hivyo ulivyoondoka wenye pesa zao ndo wanaamini kabisa umewaibia japo hata ungebaki wangeendelea kuamini ni mchongo.
We acha tu. Ila wengi wao nilikuwa nikiwatunzia mfano laki hamsini kwa wao kuogopa kuzitumia ila lilipotokea wapo waliosikitika ila kiukweli nilipata tabu sana
 
Kukimbia ndo itakua imechochea gadhabu ya wanakikundi japo wasiwasi ndo akili!fanya kuuza hata kiwanja uwapunguze na mathalani kama hata utauza 8milion,wape 6 au 7 zingne zungusha uwalipe taratibu,uzuri hata mkienda kisheria yanazungumzika,wakati mwingne usilale ndani na pesa ya watu kwan unaweza kuta kuna wanakikundi wanajua mchongo!
 
Daaah mii mwenzako niliachana na masomo ila huyo aunt aliyenifanya niache alikua na uhakika wa kunifanya niwe stable economically....

Ushauri
Rafiki kabla ya kuchukua maamuzi ya wewe kuondoka eneo hilo haukuweza kuongea nao ili uweze hata kuwalipa pesa zao kidogo kidogo?? Naamini ingekua ni njia nzuri ungeweza endelea na biashara yako hapo hapo
Maelewano duni ndiyo maana nikaamua kuondoka
 
Kukimbia ndo itakua imechochea gadhabu ya wanakikundi japo wasiwasi ndo akili!fanya kuuza hata kiwanja uwapunguze na mathalani kama hata utauza 8milion,wape 6 au 7 zingne zungusha uwalipe taratibu,uzuri hata mkienda kisheria yanazungumzika,wakati mwingne usilale ndani na pesa ya watu kwan unaweza kuta kuna wanakikundi wanajua mchongo!
Nitaufanyia kazi ushauri huu japo vitisho ninavyovipata mpaka sasa ni hatari tupu
 
Pole sana ndugu!! Pesa yoote iyo umekaa nayo ndani!! Ni hatari


KAZI ni kipimo cha UTU
 
Siku ukienda kuuza ndo hapo hapo watakupiga spana....

Nikupe ushauri ndugu, utakuja kufa kwa mawazo, mtaji wa laki alafu una presha ya kufukuzia milion 12 ya watu hautatoboa kaka nikuambie tu ukweli

Tafuta watu wa busara huko kwenu, then urudi ukae na hao wanakikundi mpange njia rafiki ya kuwalipa, wakikataa acha waende mahakamani deni halifungi mtu, tena ukiona ni watata Katoe tahadhari ya usalama polisi na uwaambie kabisa chochote kitakachokupata watahusika

Fanya hustle ukiwa umerelax nyumbani uwatafutie hela Yao, ila hili la kufanya biashara roho juu juu unajificha kama digidigi huwezi kutoboa chief utaishia kua chizi tu
Kabla ya kuondoka nilijaribu kutafuta njia ya kumaliza tatizo lakini sikupata ushirikiano nikaona nitakuwa matatani ndipo nikaamua kuondoka.
 
Kabla ya kuondoka nilijaribu kutafuta njia ya kumaliza tatizo lakini sikupata ushirikiano nikaona nitakuwa matatani ndipo nikaamua kuondoka.
Bora urudi mkuu, matatizo utakayopata ukirudi yatakua nafuu kuliko kulazimisha kujitafuta upya ukiwa na laki
 
Nitaufanyia kazi ushauri huu japo vitisho ninavyovipata mpaka sasa ni hatari tupu
kama vitisho vimezid toa taarifa kwenye mamlaka i.e polisi ili waitwe na kuonywa!mimi sion kwanin wanakutisha wakat unalitambua deni na uko tayar kulpa!ndugu kimfaacho mtu ni alichonacho,uza kiwanja walipe afu ingine walipe taratibu!
 
Kwanza nimetoa historia kwa ufupi sana.
Pili watu wana pesa tofauti na wengine tunavyofikiria.
Tatu ni pesa ambayo huwa tunapeleka benki kwa hiyo sikuwa na wasi wasi wowote ule. Kwa maana katika kikundi hiyo ilikuwa ni pesa ndogo tu. Ila kwangu mimi ni kubwa sana.

Halafu kama ni kuwapiga wenzangu ningewapiga pesa ndefu zaidi ya hiyo kwa maana wengi nilikuwa ninawatunzia na unapofika muda wa kuwasilisha nawapatia wanawasilisha.

Mimi siyo mtu wa maneno mengi sana ila kauli na vitisho vyao kiukweli havikuniacha na usalama wa nafsi. Hivyo niliamua kutoka na kuacha kila kitu changu.
"Kwa maana katika kikundi hiyo ilikuwa ni pesa ndogo tu. Ila kwangu mimi ni kubwa sana".

Hii hapa ni sababu kwanini hukupaswa kukimbia

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Nilijaribu kuwaza vile na nikatafuta mtu wa kununua lakini pesa niliyokuwa napatiwa haikuwa rafiki kwangu. Sijuwi ni kwa vile waliona nina tatizo 🤷
Ndivyo inavyokuwa, matatizo ni fursa na watu huyatumia sana kupiga hela.
Tuliza akili anza upya kwakuwa tayari unao uzoefu wa biashara mambo yatakuwa sawa.
 
Habari zenu wana jamvi!

Leo niko hapa ndugu zangu kwa ajili ya kuomba wenu ushauri ya kipi nifanye ili kuweza kukaa vyema kiuchumi.

Kisa changu kinaanzia hapa;
Tangu nilipoacha masomo yangu ya elimu ya chuo kikuu mambo yalikuwa ni magumu kwa upande wangu.
Sikuweza kujua nianzie wapi ili kujikimu kimaisha kwa kuwa sikuweza kuwa na usaidizi wa aina yoyote ile kutoka kwa mtu mwingine.

Kutokana na hali ile ilipelekea kuuza simu yangu ili nipate mtaji wa biashara. Nilipata shs20000 kisha nikatumia nusu ya pesa kununua jiko na wavu na nusu iliyobaki nilinunua mahindi na mkaa.
Kilichonishangaza katika biashara hiyo ni mara baada ya kurudisha pesa ya mtaji bidhaa ilikuwa haitoki; hali hii ilijitokeza kwa siku kadhaa hadi pale nilipochukua uamuzi wa kuachana nayo.

Baadaye niliamua kujihusisha na kazi za migodini kwa kipindi cha mwaka mmoja lakini sikuambulia kitu maana pesa nilidhulumiwa hivyo sikuweza kuendelea kwa lolote lile.

Mwaka 2020 kwa msaada wa rafiki yangu, aliniazimisha shs20000 ambayo niliamua kuitumia kama mtaji na nikaanzisha genge la kuuza matunda.
Nashukuru mambo yaliweza kwenda vizuri kwa kuwa ndani ya mwezi mmoja niliweza kupata pesa ya kulipia eneo la biashara na sehemu ya kulala.

Baada ya mwaka mmoja niliweza kununua kiwanja cha cha thamani ya 700k na pia kukarabati genge langu.
Mambo yalikuwa ni mazuri sana japo changamoto za kibiashara hazijawahi isha ila niliweza kufanya vizuri tu.

Mwaka 2021 nilianza ujenzi na mambo yalikuwa sawia tu japo ni ujenzi wa kuunga unga ila nashukuru maana niliweza kufika kwenye usawa wa linta na niliishia hapo kwanza.

Mwaka 2022 kuna mtu alikuja kuchukua pesa kwangu kiasi cha 800k na kunikabidhi moja ya eneo lake kwa maandishi. Kwa kweli mambo yalikuwa ni mazuri tu. Pia kutokana na mwingiliano mzuri na watu vile vile niliweza kujiunga na kikundi cha kuwezeshana; ambapo kilichangia kwa kiasi kikubwa mimi kuboresha biashara yangu na kumjengea nyumba ya wastani mzazi wangu kabla ya kumalizia ya kwangu. Hii ni kutokana na nyumba ya mzazi wangu kuanguka kipindi cha mvua.

Mwaka 2023 miezi ya mwanzo mambo yalikuwa ni mazuri tu hadi ilipofika mwezi wa sita tarehe za mwanzoni ambapo nilipigwa na tukio zito. Katika kikundi cha kuwezeshana mimi nilikuwa ni mhasibu na kwa hiyo pesa zote nilikuwa nikitunza mimi kabla ya kupelekwa Benki.

Nilipokuwa nakaa na muda wa kukusanya pesa ili kuzipeleka benki havikuwa rafiki hivyo ilikuwa ni lazima nilale nazo na siku inayofuata asubuhi sana pesa ilikuwa ikipelekwa benki. Ila wiki ya kwanza ya mwezi Juni haikuwa nzuri kwa kuwa nikiwa nimelala niliamka mlango umeharibiwa kitasa na baadhi sebuleni hakukuwa na Tv yangu. Nilitahayari sana na ndipo nilipoangalia sehemu ya kutunzia pesa sikufanikiwa kukuta Chochote kile. Dah! Nilipiga ukunga maana nilichanganyikiwa ni kwa namna ipi nitawaaminisha wenzangu lakini haikusaidia Chochote kile.

Nilitoa taarifa kuhusu tukio ila hakuna aliyeweza kunielewa. Kila mmoja alisema zile ni njama za kutaka kuwadhulumu. Sikuweza kuwa na namna yoyote ile zaidi ya kunishinikiza nilipe pesa yao. Kiukweli nisingeweza kulipa maana pesa ilikuwa ni nyingi na mimi kwenye akiba yangu nilikuwa na pesa kidogo tu.

Kiukweli baada ya kuniandama sana sikuwa na chaguo zaidi ya kuamua kuondoka bila taarifa na kuacha kila kitu changu mpaka pale nitakapoweza angalau kupata hata nusu ya pesa ili niwapelekee na nirudi katika hali yangu ya kibiashara. Huku nilipo maisha nayaona ni magumu sana.

Nimejaribu kufanya shughuli katika mji Tunduma lakini hali imekuwa ni mbaya sana. Kwa sasa niko mji Dar Es Salaam na nina kiasi cha Shs100000 tu.

Kama mwana jamvi mwenzangu unaweza nishauri nifanye kitu gani ambacho kitanisaidia kuweza kuikuza pesa hii ili angalau nikuze mtaji na niweze kwenda kulipa pesa ya wanakikundi wenzangu? Nadaiwa shilingi milioni kumi na mbili(12,000,000).

Tafadhali; nimetoa historia kwa ufupi nilipotoka na nilipofikia na jinsi nilivyokwama kwa lengo la kuomba ushauri.
Sina amani ya moyo kabisa mpaka nitakapolipa pesa ya wenzangu maana hata nikisema kuuza mali zangu pesa hiyo haiwezi kufika kwa kuwa mimi mwenyewe nilikuwa najitafuta tu.

Uaminifu ni mtaji japo siaminiki tena ila sitodhulumu mtu.
Nisaidie kwa mawazo ya kunivusha.
Asanteni sana kwa muda wenu.🙏🙏
Sio fupi ndefu sana
Mie nataka kujua kama unakunywa wanzuki
 
Back
Top Bottom