Maxence Melo: Tumkumbuke William (Lemutuz) kama Mtetezi wa Uhuru wa Kujieleza na Mtetezi wa uwajibikaji Nchini

Maxence Melo: Tumkumbuke William (Lemutuz) kama Mtetezi wa Uhuru wa Kujieleza na Mtetezi wa uwajibikaji Nchini

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo Mubyazi ametoa pole kwa familia ya Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela kwa msiba mzito wa mpendwa wao ambae yeye amefahamiana nae kwa takriban miaka 20.

Melo amesema ameshirikiana na Marehemu kwa mambo mengi, pamoja na watu wengi kumtambua kama Le Mubebez yeye anamtambua kama “Sauti ya Umeme”, mwanachama wa mwanzo kabisa wa JamiiForums na mtu aliyekuwa anaamini kuwa binadamu wanapaswa kusemezana bila kuoneana haya.

Ameongeza, “lakini zaidi kulipotokea sheria mbalimbali au kanuni, William alitoa ushirikiano mkubwa na alikuwa sehemu ya kuomba marekebisho yafanyike ili space hii ya digitali iwe rafiki kwa kila mtu. Kwa mantiki hiyo, pamoja na mambo mengine yote, tumkumbuke William kama mtetezi wa Uhuru wa Kujieleza na mtetezi wa uwajibikaji nchini”
 
Jamaa nilikua namkubali kitu kimoja, Kila kitu alikua anachukulia easy sana, Kuna thread hapa kipindi Iko Yuko active yaani anatukanwa na karibu wachangiaji wote jamaa anakula nao sahani Moja, jamaa alikua mbishi balaa, alifanya ligi karibu na member 70 wote wakapoteana
 
Jamaa nilikua namkubali kitu kimoja, Kila kitu alikua anachukulia easy sana, Kuna thread hapa kipindi Iko Yuko active yaani anatukanwa na karibu wachangiaji wote jamaa anakula nao sahani Moja, jamaa alikua mbishi balaa, alifanya ligi karibu na member 70 wote wakapoteana
Reaction yake ya kujibu kwa kuambatanisha picha za kula Bata ilikuwa inafurahisha sana.

Tangulia Lemutuz, na sisi tupo nyuma yako, njia ni moja tu
 
Jamaa nilikua namkubali kitu kimoja, Kila kitu alikua anachukulia easy sana, Kuna thread hapa kipindi Iko Yuko active yaani anatukanwa na karibu wachangiaji wote jamaa anakula nao sahani Moja, jamaa alikua mbishi balaa, alifanya ligi karibu na member 70 wote wakapoteana
Ile waliyoweka picha kajilaza sebleni kwa mshua kwenye kochi mitaa ya seaview
 
Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo Mubyazi ametoa pole kwa familia ya Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela kwa msiba mzito wa mpendwa wao ambae yeye amefahamiana nae kwa takriban miaka 20.

Melo amesema ameshirikiana na Marehemu kwa mambo mengi, pamoja na watu wengi kumtambua kama Le Mubebez yeye anamtambua kama “Sauti ya Umeme”, mwanachama wa mwanzo kabisa wa JamiiForums na mtu aliyekuwa anaamini kuwa binadamu wanapaswa kusemezana bila kuoneana haya.

Ameongeza, “lakini zaidi kulipotokea sheria mbalimbali au kanuni, William alitoa ushirikiano mkubwa na alikuwa sehemu ya kuomba marekebisho yafanyike ili space hii ya digitali iwe rafiki kwa kila mtu. Kwa mantiki hiyo, pamoja na mambo mengine yote, tumkumbuke William kama mtetezi wa Uhuru wa Kujieleza na mtetezi wa uwajibikaji nchini”
.Maxence anampa sifa ambazo William hakuwa nazo. William alikuwa street smart lakini hakuwa intelectually smart. Hakuna evidence ya chochote ambacho Maxence anadai William alikuwa mtetezi. William was just out after fame, money, and women: in no particular order. William alikuwa anapenda kula chakula kizuri na kuishi maisha ya kifahari. Wangemsifia kwa hayo wala isingekuwa mbaya maana ndiyo ukweli wenyewe.
 
Back
Top Bottom