demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Uchaguzi TFF unakaribia.
Ally Mayai Tembele na Jamal Malinzi wanaonekana washindani wenye nguvu zaidi wa nafasi ya Urais.
Ila napenda turudi nyuma,twende mbele. Miaka 4 haijawahi kumtosha na haitokuja kumtosha yeyote yule kwenye nafasi ya Uraisi wa TFF kufanya jambo ambalo linaweza kupendeza sana wapenda kandanda.
Ukizingatia watanzania tupendavyo short-cut ya Maendeleo, wengi wetu tunaona hakuna kitu chochote alichofanya JEM kwa kipindi chake chote cha Miaka 4.
Najua kunawengine tumezaa chuki mioyoni mwetu kutokana na Usimba na Uyanga tu.
Ila jambo muhimu ni kuwa JEM anahitaji miaka 4 zaidi muda wake uweze kupimwa na Maendelea aliyohusika nayo.
Kuna hii dhana ambayo tumejijenge kuwa soka la bongo linaposhndwa kupiga hatua kidogo, basi wa kulaumwa ni rais wa TFF. Hivi mmeshawahi kujiuliza vilabu vyenu vya Simba na Yanga vinafanya jitihada gani kukuza soka la bongo?
Au mnatarajia TFF iandae progamu za kukuza soka vilabuni vyenu humo?
Binafsi naipongeza TFF na rais wake kwa kuonyesha njia hasa kwenye suala la kukuza soka la vijana.
Ninaamini kuna mengi mno ambayo yapo kwenye mipango ya JEM kuhusu soka la Bongo....
Licha ya kuwa na muda mchache sana wa kutimiza hayo .....nimefurahia jitihada zake za kutokata tamaa na kuwania nafasi ya Urais kwa Mara nyingine tena ili kukamilisha yale makubwa zaidi aliyo yakusudia kwa ajili ya soka la Bongo.
Sina kinyongo kabisa na mdogo wangu Ally Mayay naye namtakia kila la kheri, ila akae akijua kuwa huu si wakati wake.
Na kwamba JEM amejipanga vilivyo kumgaragaza kwenye uwanja wa Uchaguzi.
Namshauri Ally Mayay ajipange upya kwa ajili ya Uchaguzi wa mwaka 2021.
Ninauhakika kuwa wajumbe wapiga kura watahakiksha ushindi wa kishindo kwa JeM
@TeamMalinzi
Ally Mayai Tembele na Jamal Malinzi wanaonekana washindani wenye nguvu zaidi wa nafasi ya Urais.
Ila napenda turudi nyuma,twende mbele. Miaka 4 haijawahi kumtosha na haitokuja kumtosha yeyote yule kwenye nafasi ya Uraisi wa TFF kufanya jambo ambalo linaweza kupendeza sana wapenda kandanda.
Ukizingatia watanzania tupendavyo short-cut ya Maendeleo, wengi wetu tunaona hakuna kitu chochote alichofanya JEM kwa kipindi chake chote cha Miaka 4.
Najua kunawengine tumezaa chuki mioyoni mwetu kutokana na Usimba na Uyanga tu.
Ila jambo muhimu ni kuwa JEM anahitaji miaka 4 zaidi muda wake uweze kupimwa na Maendelea aliyohusika nayo.
Kuna hii dhana ambayo tumejijenge kuwa soka la bongo linaposhndwa kupiga hatua kidogo, basi wa kulaumwa ni rais wa TFF. Hivi mmeshawahi kujiuliza vilabu vyenu vya Simba na Yanga vinafanya jitihada gani kukuza soka la bongo?
Au mnatarajia TFF iandae progamu za kukuza soka vilabuni vyenu humo?
Binafsi naipongeza TFF na rais wake kwa kuonyesha njia hasa kwenye suala la kukuza soka la vijana.
Ninaamini kuna mengi mno ambayo yapo kwenye mipango ya JEM kuhusu soka la Bongo....
Licha ya kuwa na muda mchache sana wa kutimiza hayo .....nimefurahia jitihada zake za kutokata tamaa na kuwania nafasi ya Urais kwa Mara nyingine tena ili kukamilisha yale makubwa zaidi aliyo yakusudia kwa ajili ya soka la Bongo.
Sina kinyongo kabisa na mdogo wangu Ally Mayay naye namtakia kila la kheri, ila akae akijua kuwa huu si wakati wake.
Na kwamba JEM amejipanga vilivyo kumgaragaza kwenye uwanja wa Uchaguzi.
Namshauri Ally Mayay ajipange upya kwa ajili ya Uchaguzi wa mwaka 2021.
Ninauhakika kuwa wajumbe wapiga kura watahakiksha ushindi wa kishindo kwa JeM
@TeamMalinzi